Rais wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi afikisha miaka 95. Heri ya kuzaliwa Mzee Ruksa!

Rais wa Awamu ya Pili, Mzee Ali Hassan Mwinyi afikisha miaka 95. Heri ya kuzaliwa Mzee Ruksa!

Informer

JF-Expert Member
Joined
Jul 29, 2006
Posts
1,606
Reaction score
6,672
2A7C4885-29D7-4E8C-8F85-4DE3025B03AF.jpeg

Ali Hassan Mwinyi (amezaliwa 8 Mei 1925) alikuwa Rais wa Pili wa Tanzania kuanzia 1985 hadi 1995.

Aliyemtangulia ni Mwalimu Julius Nyerere, na aliyemfuata ni Benjamin Mkapa.

Pia, Mwinyi alikuwa mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kuanzia 1990 hadi 1996.

Mzee Mwinyi aliwahi pia kuwa Rais wa Zanzibar, Makamu wa Rais na Waziri wa Mambo ya Ndani.

Wakati wa utawala wake wa mihula miwili, Mwinyi alichukuwa hatua za mwanzo kubadilisha sera za ujamaa za Mwalimu Nyerere. Alilegeza vikwazo vya manunuzi ya nje na kuhamasisha watu kuanzisha biashara.

53D54469-6FA8-4314-811A-F0188019B078.jpeg

Picha ya Rais iliyokuwa ikibandikwa katika ofisi wakati wa utawala wake

Ni katika muhula wake wa pili ambapo mfumo wa vyama vingi nchini Tanzania ulianzishwa kufuatia shinikizo kutoka kwa wafadhili wa kigeni.

Akifahamika zaidi kama Mzee Ruksa (Kila kitu ruksa), aliwapa watu ruksa ya kufanya kile wakitakacho pasipo na kuvunja sheria.

Baada ya kustaafu, Mwinyi huonekana kwa nadra hadharani na anaendelea kuishi jijini Dar es Salaam.
 
Bado mpaka leo natamani kufahamu ilikuwaje Mwinyi ajiiuzulu uwaziri wa Mambo ya Ndani mpaka tena akaja kuwa President wa hii nchi?

Alivyojiuzulu aliendelea kubaki serikalini kwa kupangiwa kazi nyingine, au alitoka kabisa kwenye madaraka ya serikalini? ilikuwaje mpaka yeye ndie aonekane tena anafaa wakati taswira yake ni kama ilishachafuka kutokana na kujiuzulu kwake uwaziri wa Mambo ya Ndani.

Mliokula chumvi msaada tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado mpaka leo natamani kufahamu ilikuwaje Mwinyi ajiiuzulu uwaziri wa Mambo ya Ndani mpaka tena akaja kuwa President wa hii nchi?

Alivyojiuzulu aliendelea kubaki serikalini kwa kupangiwa kazi nyingine, au alitoka kabisa kwenye madaraka ya serikalini?

Mliokula chumvi msaada tafadhali.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu, hizo zilikuwa ni Siri za Mwl , naye huenda alikuwa hapangiwi!
 
Nadhani alibaki Serikalini, baadaye akateuliwa kuwa balozi moja ya Nchi za kiarahu nadhani ni Misri.
 
Bado mpaka leo natamani kufahamu ilikuwaje Mwinyi ajiiuzulu uwaziri wa Mambo ya Ndani mpaka tena akaja kuwa President wa hii nchi?

Alivyojiuzulu aliendelea kubaki serikalini kwa kupangiwa kazi nyingine, au alitoka kabisa kwenye madaraka ya serikalini? ilikuwaje mpaka yeye ndie aonekane tena anafaa wakati taswira yake ni kama ilishachafuka kutokana na kujiuzulu kwake uwaziri wa Mambo ya Ndani.

Mliokula chumvi msaada tafadhali.

Kwa ufafanuzi wake mwenyewe:

Rais mstaafu wa awamu ya pili, Ali Hassan Mwinyi anataja sababu za kujiuzulu kwake nafasi ya Waziri wa Mambo ya Ndani kuwa kulitokana na “kulinda heshima ya Taifa na ya Rais wa awamu ya kwanza”.

Hata hivyo anasema anasikitika kuona chanzo cha kujiuzulu kwake bado hadi sasa kipo ambacho ni mauaji ya vikongwe jambo ambalo anadai ni fedheha kubwa kwa Taifa kama Tanzania.

Mzee Mwinyi anasema hakuna haja kwa sasa kiongozi kujiuzulu kutokana na mauaji bali Serikali inapaswa kupambana na wauaji wote ili kutoruhusu hali hiyo kuendelea.

Mwaka 1976 akiwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwinyi alilazimika kujiuzulu nafasi yake baada ya kutokea mauaji katika Mkoa wa Shinyanga lakini miaka tisa baadaye akawa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kipindi cha miaka kumi.

"Hali ya kuongezeka kwa wazee ni jambo jema linaloonyesha Taifa linapata maendeleo lakini hili kuwaua vikongwe ni aibu na fedheha kubwa sana, naomba likomeshwe," anasema Mwinyi.
 
HBP Mwinyi, mwaka jana akizungumzia siri ya maisha yake ni kufurahi, kuto kukasirika, na kufanya mazoezi.

Alisema hata kama kutatokea jambo la kukukasirisha, usiliruhusu, samehe

Hata yule jamaa aliye wahigi kumpiga kibao, alimsamehe pale pale na kuwasisitiza wale jamaa wa usalama wamwache, ila jamaa walimngangania ili tuu kujiridhisha he was real insane and was acting alone na hajatumwa !.
P
 
Hongera sana Mzee Mwinyi kwa kufikisha umri huo, Mwenyezi Mungu azidi kukujalia afya njema ya roho na mwili. Happy birthday Mzee wetu
 
heri ya kuzaliwa mzee baba,
bado yuko fiti sana.hapa ndio watu wenye maumbo madogo wanapotuzidi warefu.

nikiiona hiyo sura picha ya pili naikumbuka miambili ya noti tu.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakati wa utawala wake wa mihula miwili, Mwinyi alichukuwa hatua za mwanzo kubadilisha sera za ujamaa za Mwalimu Nyerere. Alilegeza vikwazo vya manunuzi ya nje na kuhamasisha watu kuanzisha biashara.
ALLAAH AKUPE AFYA NA AKULINDE NA MABALAA NA HASAD NA AKUPE UMRI WENYE BARAKA. UMUHIMU WAKO UNAJULIKANA.

AAMIYN.
 
Back
Top Bottom