Rais wa Chile anusurika kuondolewa madarakani

Rais wa Chile anusurika kuondolewa madarakani

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
IMG_336E30-702EDC-6B12E0-05ED77-E08189-CA903C.jpeg

Picha: Raiswa Chile Sebastian Pinera

Baraza la senate la Chile limepinga mchakato ulioanzishwa na upinzani uliolenga kumuondoa madarakani Rais Sebastian Pinera.

Upinzani ulitaka Pinera ang’olewe madarakani kufuatia sakata lililofichuliwa kwenye nyaraka za Pandora na pia kutokana na hatua yake ya kutoshirikiana na bunge wakati mchakato huo dhidi yake ulipoanzishwa.

Waliopiga kura ili rais huyo ambaye ni bilionea aondolewe mamlakani walikuwa 24, idadi ambayo ni chini ya kura 29 zinazohitajika ili mchakato kama huo ufaulu. Na waliopinga kuondolewa kwake walikuwa 18.

Endapo mchakato huo ungefaulu, basi huenda angekabiliwa na kifungo cha hadi miaka mitano gerezani.
 

Hii rangi nyekundu ya wino naipata wapi ndugu? Naomba mwongozo tafadhali.​

Unaandika hivii

[color=jina la rangi unalotitaka kwa english]then andika sentensi yako mbele ya mabano ya kufunga bila kuacha nafasi

NB; io jina la rangi unayotaka kuiweka nimeiandika kwa kiswahili ili uelewe format ya kuandika. Jina la rangi linaandikwa kwa english kama ni red blue ninwewe tuuu

NADHANI UTANIELEWA MI SIJUI KUELEWESHA SANAAA ILA NIMEJARIBU TUUU.
 
Amenusurika kupitia mchakato halali (impeachment). Kuna wenzetu kule pande fulani ukisikia 'kunusurika' mara nyingi ni kuponea kifo (assassination) au mapinduzi.
Nchi za kiafrika nyingi ukiitoa South Afrika , marais wanatolewa madarakani kwa kupinduliwa na wengine kwa maigizo ya uchaguzi kama hapa Tanzania

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom