Inside10
JF-Expert Member
- May 20, 2011
- 29,909
- 32,414
Rais wa Colombia, Gustavo Petro, amesema biashara ya kokeini inaweza kudhibitiwa kwa urahisi ikiwa dawa hiyo itahalalishwa duniani kote, kwakuwa dawa hiyo si mbaya zaidi kuliko whisky.
Katika mkutano wa mawaziri uliorushwa moja kwa moja, Petro amesema Kokeini ni haramu kwa sababu inatengenezwa Amerika ya Kusini, si kwa sababu ni mbaya zaidi kuliko whisky, akiongeza kuwa wanasayansi wamechambua suala hilo.
Kiongozi huyo aliyeingia madarakani mwaka 2022, ameahidi kupambana na biashara ya dawa za kulevya na kudhibiti matumizi ya dawa haramu. Hata hivyo, tangu aingie madarakani, uzalishaji wa kokeini nchini Colombia umeongezeka.
Katika mkutano wa mawaziri uliorushwa moja kwa moja, Petro amesema Kokeini ni haramu kwa sababu inatengenezwa Amerika ya Kusini, si kwa sababu ni mbaya zaidi kuliko whisky, akiongeza kuwa wanasayansi wamechambua suala hilo.
Kiongozi huyo aliyeingia madarakani mwaka 2022, ameahidi kupambana na biashara ya dawa za kulevya na kudhibiti matumizi ya dawa haramu. Hata hivyo, tangu aingie madarakani, uzalishaji wa kokeini nchini Colombia umeongezeka.