Rais wa Guinea Ikweta, amteua Zenón Avomo kurithi Mikoba ya Baltasar Engonga, aliyeng’olewa kufuatia kashfa ya video za ngono 400

Rais wa Guinea Ikweta, amteua Zenón Avomo kurithi Mikoba ya Baltasar Engonga, aliyeng’olewa kufuatia kashfa ya video za ngono 400

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
2,060
Reaction score
5,648
Zenón Avomo ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu mpya wa Shirika la Kitaifa la Upelelezi wa Fedha (ANIF) akichukua nafasi ya Baltasar Engonga, aliyeng’olewa kufuatia kashfa ya ukiukaji wa maadili katika ofisi ya umma. Kashfa hiyo iliibuka baada ya uchunguzi kubaini uwepo wa video zaidi ya 400 zilizorekodiwa ndani ya ofisi ya Engonga, zikionesha wake, jamaa, na maofisa wakuu wa serikali, wakiwemo mawaziri na polisi, katika mazingira ya utata.

Pia, Soma: Guinea: Kigogo Baltasar Ebang Engonga anaswa na video 400 za ngono na wake wa viongozi mashuhuri, mwanasheria Mkuu aingilia kati

1731068328180.png

Kusambaa kwa video hizo kumesababisha wasiwasi mkubwa serikalini, na hatua za kinidhamu zimeanza kuchukuliwa dhidi ya wale waliohusika. Ili kuimarisha uadilifu, Serikali ya Guinea Ikweta imeagiza kufungwa kwa kamera za ulinzi katika taasisi zote za umma, lengo likiwa ni kudhibiti tabia za maofisa na kurejesha imani ya wananchi kwa serikali.

Zenón Avomo, akiwa na utaalamu wa sheria na fedha, anatarajiwa kuleta mabadiliko muhimu katika ANIF. Amewahi kushika nyadhifa za juu, ikiwa ni pamoja na Jaji wa Mahakama ya Malabo, Mkurugenzi Mkuu wa Masomo ya Mikataba na Masoko ya Serikali katika Wizara ya Fedha, na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha pamoja na Wizara ya Madini, Viwanda, na Nishati.

Soma:
 
Naamini DNA ikipimwa watanzania wengi asili yao ni Equatorial Guinea! Hao jamaa (picha hapo juu) wanafanana sana na wabongo.

Huyo black resembles Makete ndani ndani huko kwa akina Lutengano, Haule, Sanga and the like. Huyo white judge yourself.
 
Baltasar Engonga, ambaye amekuwa akitawala vichwa vya habari siku za hivi karibuni kuhusu kashfa ya ngono iliyohusisha zaidi ya Wanawake 400 nchini Equatorial Guinea, amefukuzwa kazi yake kama Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kitaifa la Uchunguzi wa Fedha (ANIF).

Ripoti za vyombo vya habari nchini humo zinaonyesha kuwa Engonga alifukuzwa kazi kwa makosa na tabia isiyofaa chini ya amri iliyotolewa na Rais wa Equatorial Guinea Teodoro Obiang Nguema Mbasogo.

Engonga amekuwa akivuma kwenye mitandao ya kijamii kwa muda wa wiki nzima baada ya uchunguzi wa hivi majuzi kufichua zaidi ya video 400 za utupu zinazomhusisha na Wanawake wengi, wakiwemo jamaa na wake za Viongozi wa ngazi za juu akiwemo dada yake Rais.

Video hizo zimezua mtafaruku kwenye mitandao ya kijamii, huku Makamu wa Rais wa Equatorial Guinea, Teodoro Mangue, akiapa kuchukua hatua kali dhidi ya maafisa wanaohusika na vitendo vya ngono katika ofis
i zao.
 
Nchi hiyo imeoza. Video zisingetrend wasingemfanya chochote, wanaona aibu kwa AU kwa kuwa hicho ni kitendo cha aibu kiafrika. si rahisi kuwa vitendo vyake havikuwa vikijulikanaz hata tetesi tu?
 
Baltasar Engonga, ambaye amekuwa akitawala vichwa vya habari siku za hivi karibuni kuhusu kashfa ya ngono iliyohusisha zaidi ya Wanawake 400 nchini Equatorial Guinea, amefukuzwa kazi yake kama Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kitaifa la Uchunguzi wa Fedha (ANIF).
Hapa Tz na East Africa nzima nani anaweza kumfikia huyu jamaa au hata nusu yake tu
 
Hata henry kissinger alikichafua sana enzi zake. Totoz zilipata sana dozi.
 
Anamuonea jamaa...
Waliovujisha picha zake ndio wa kufukuzwa kazi .... Na hao wake za watu waliutaka... Jamaa hana kosa...
Ana makosa ama ifuatavyo

* Kutumia ofisi ya selikali kufanya mambo ya kuzalilisha selikali.

* Amefanya mapenzi mbele ya bendera ya nchi, ameizalau bendera.

*Kutembea na wake za watu huku akijuwa ni wake za watu..
 
Back
Top Bottom