Raisi mpya wa Iran na kiongozi mpya wa Hamas ni wakali zaidi kuliko wenzao waliotangulia.

Raisi mpya wa Iran na kiongozi mpya wa Hamas ni wakali zaidi kuliko wenzao waliotangulia.

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Ile kampeni ya kuua viongozi na makamanda wa makundi pinzani kwa utawala wa Israel bado haijaonekana kufanya kazi kama ilivyokusudiwa.
Raisi Ibrahim raisi wa Iran alifariki kwenye ajali ya ndege miezi 2 iliyopita.Katika uhai wake hakuwa na mzaha na utawala wa kiyahudi huko Israel.Yeye ndiye aliyeamrisha jeshi la nchi yake kuipiga Israel baada ya ubalozi wake kushambuliwa huko Israel.
Kifo cha raisi huyo na waziri wake wa mambo ya nje ambao wote walitajwa wenye misimamo mikali ilitarajiwa kupatikana viongozi ambao wangekuwa baridi dhidi ya utawala huo.Wote wawili waliofuatiia siku za mwanzo tu za uongozi wao wameonekana kuwa na misimamo mikali kuliko waliowatangulia.
Kwa upande wa Hamas,kiongozi aliyechaguliwa kushika nafasi ya Ismail Haniya ndiye kabisa ni mtua asiyetamani hata kukenua meno kwa Israel.Yahya Sinwar ni kiongozi wa Hamas ambaye amesota magereza ya Israel kuliko wote waliomtangulia.Na ndiye anayetajwa na Israel kuwa ni maiti anayetembea na bado amepokea kijiti cha uongozi wa Hamas akiwa na hamasa tele.
Mtu anaweza akajiuliza kwa kuwaua viongozi hao jee Israel imejipatia usalama wake au imejiongezea hasira za maadui zake ?
 
Hakuna tofauti kati ya İsmail Haniyeh wala Sinwar. Wote ni magaidi ambao lengo lao ni kuwaangamiza Waisraeli.

Na baada ya Oct 7 Netanyahu aliagiza kusakwa na kuuwawa kwa magaidi wote waliohusika kwa namna moja ama nyingine
 
Palestina na Wapalestina, hatma yao nzuri ipo mikononi mwa viongozi watakaokuwa na hekima, na siyo kwa haya makundi ya kigaidi. Kama viongozi wa Wapalestina wangekuwa angalao kama alivyo Mahmoud Abbas, hakika Wapalestina wasingekuwa kama walivyo leo.

Haya makundi ya kigaidi yaliyoundwa na Iran, na Iran yenyewe wanachukiwa karibia na mataifa yote ya kiarabu. Ndiyo maana hata wakati ule Iran ilipoamua kurusha makombora kuelekea Israel, mataifa kama Saudia, Bahrain, Qatar, UAE, yaliamua kushirikiana na Marekani, Uingereza na Ufaransa, kuyadungua makombora ya Iran. Yaliyofika kwenye anga la Israel hayakufika hata 50%.

Haya makundi ya Kigaidi ni tishio kwa amani ya mataifa yote ya Kiarabu.
 
Ni kipigo tu,kesho mkisema alahu akibaru mpaka jumatatu mtajua kuimba tumsifu Yesu kristo.
 
Ile kampeni ya kuua viongozi na makamanda wa makundi pinzani kwa utawala wa Israel bado haijaonekana kufanya kazi kama ilivyokusudiwa.
Raisi Ibrahim raisi wa Iran alifariki kwenye ajali ya ndege miezi 2 iliyopita.Katika uhai wake hakuwa na mzaha na utawala wa kiyahudi huko Israel.Yeye ndiye aliyeamrisha jeshi la nchi yake kuipiga Israel baada ya ubalozi wake kushambuliwa huko Israel.
Kifo cha raisi huyo na waziri wake wa mambo ya nje ambao wote walitajwa wenye misimamo mikali ilitarajiwa kupatikana viongozi ambao wangekuwa baridi dhidi ya utawala huo.Wote wawili waliofuatiia siku za mwanzo tu za uongozi wao wameonekana kuwa na misimamo mikali kuliko waliowatangulia.
Kwa upande wa Hamas,kiongozi aliyechaguliwa kushika nafasi ya Ismail Haniya ndiye kabisa ni mtua asiyetamani hata kukenua meno kwa Israel.Yahya Sinwar ni kiongozi wa Hamas ambaye amesota magereza ya Israel kuliko wote waliomtangulia.Na ndiye anayetajwa na Israel kuwa ni maiti anayetembea na bado amepokea kijiti cha uongozi wa Hamas akiwa na hamasa tele.
Mtu anaweza akajiuliza kwa kuwaua viongozi hao jee Israel imejipatia usalama wake au imejiongezea hasira za maadui zake ?
Sasa kwa akili yako Sinwar atapona kweli kwenye mikono ya mossad wanavyomsaka kwa udi na uvumbi
 
Sasa kwa akili yako Sinwar atapona kweli kwenye mikono ya mossad wanavyomsaka kwa udi na uvumbi
Mossad wana nguvu gani mbele ya muumba mbingu na ardhi.Akipenda kumlinda Yahya hata Mossad washirikiane na CIA na KGB hawawezi kumpata.
Anaweza akaondoka Netanyahu mwanzo kabla ya Sinwar
 
Mossad wana nguvu gani mbele ya muumba mbingu na ardhi.Akipenda kumlinda Yahya hata Mossad washirikiane na CIA na KGB hawawezi kumpata.
Anaweza akaondoka Netanyahu mwanzo kabla ya Sinwar
Mbona mnamuingiza Mungu kwenye maugaidi yenu mbona huyo ismail haniyeh na mohamed deif hawakulindwa na Allah wameuawa?
 
Mossad wana nguvu gani mbele ya muumba mbingu na ardhi.Akipenda kumlinda Yahya hata Mossad washirikiane na CIA na KGB hawawezi kumpata.
Anaweza akaondoka Netanyahu mwanzo kabla ya Sinwar
kwahiyo Sinwar yeye hazitaki bikra 72 ?! Anawachochea wengine wajilipue na nyie mazuzu mnapayuka alauakibaru na kujilipua ila yeye anajificha kwenye mashimo kama panya buku akisikia risasi ni mbio kisigino kinagusa kisogo, yeye vipi hazitaki bikra 72 na mifereji ya konyagi ?
 
Mods bado tunaomba Ombi la kuongezea emoji ya 🚮 kwenye eneo la Thanks

Natanguliza Shukrani

Moderator
 
Back
Top Bottom