Elections 2010 Rakesh Rajani Kuukwaa Uwaziri? Elimu..?

Elections 2010 Rakesh Rajani Kuukwaa Uwaziri? Elimu..?

Mwalimu alisema ili nchi iendelee inahitaji ardhi, watu, siasa safi na uongozi bora. Naona tumejikita katika kutafuta watu tunaoona kuwa ni bora - Rakesh Rajani, Anna Tibaijuka n.k. Ila hata uwe na watu makini na waliobebea kiasi gani kama huna siasa safi na uongozi bora huwezi kufika popote. Sana sana utaishia kuwatibua tu watu hao wenye uwezo. Historia yetu haidanganyi - rejea yaliyomkuta John Magufuli!

Lakini yawezekana kuwa na siasa safi na uongozi bora bila ya watu wenye siasa safi na wenye kuleta uongozi bora?
 
Lakini yawezekana kuwa na siasa safi na uongozi bora bila ya watu wenye siasa safi na wenye kuleta uongozi bora?

MM mie nashindwa kuelewa ni vipi hawa wabunge wa viti maalum wanafanya kazi kwa malengo gani. Ila kama ni kuwaweka watu wanaowataka katika uwaziri ni sawa tu na ufisadi kwani hao wabunge waliopo hawafai kuwa mawaziri wa elimu? RR anaweza kuwa waziri mzuri wa elimu but kwanini alazimishwe kuwa waziri kama yeye mwenyewe hakuonyesha nia hiyo? Binafsi naona kama ni kuchochea mgongano wa kimaslahi na kizunguzungu hichi cha wabunge wa viti maalum
 
Ni vema viongozi ikiwa ni pamoja na wawakilishi na wabunge wawe wazalendo na wazawa, tunamifano tosha ya kuhofu majina kama hayo. Hata kama akiwa msafi kiasi gani jina lake linaweza kuwa na dosari, kuna wakati naweza kusema Masanja mwizi ni bora kuliko Kanjibahi mwizi, japo wote ni wezi.
 
Mwalimu alisema ili nchi iendelee inahitaji ardhi, watu, siasa safi na uongozi bora. Naona tumejikita katika kutafuta watu tunaoona kuwa ni bora - Rakesh Rajani, Anna Tibaijuka n.k. Ila hata uwe na watu makini na waliobebea kiasi gani kama huna siasa safi na uongozi bora huwezi kufika popote. Sana sana utaishia kuwatibua tu watu hao wenye uwezo. Historia yetu haidanganyi - rejea yaliyomkuta John Magufuli!

Ili tuendelee tunahitaji wavumbuzi wa kuvumbua vitu....
 
Mkwere anakuambia uwaziri hausomewi. So anyone anaweza kuwa waziri hata asiye na uwezo.
 
Kama vile unampigia ndogo ndogo rafiki yako....!:director:

Kama vile una majungu hili ni jamvi na huo ni mtazamo wake tu na watu wanachangia kulingana na record ya RR. Na haki elimu kwa ujumla
 
Kama tetesi zinazotembea taratibu zina ukweli utakuwa ni mojawapo ya mambo ambayo yanaweza kuleta matumaini katika wizara hii nyeti.. kwanza kwa sababu amejithibitisha kuwa ana uwezo, ni jasiri, na yuko tayari kuchukua maamuzi magumu. Pingamizi kubwa ni kutoka kona fulani fulani ambazo zinaona kuwa Bw. RR amekuwa anti-govt or anti-CCM. Watetezi wake wanadokeza kuwa kama mambo anayosema (kupitia taasisi zake) yana ukweli na ana mawazo ya kuboresha elimu.. give it to him...

BIO YA RAKESH KWA UFUPI


Kwangu mimi.. namuunga mkono na miguu!!!


What do you think?

Watamuumiza kwa sababu uozo uliopo kwenye elimu si wa kurekebishwa ndani ya muda mfupi; pia system ilivyo ataonekana bogus. Hayo yatakuwa ni maandalizi ya kumwondoa kwenye medani za uhanaharakati. Mbona Margareth Sitta aliwekwa hapo kwa sababu alikuwa kwenye umoja wa walimu na kuwa mbele sana kwenye kupigania haki na hajafanya chochote zaidi ya kuajili voda fasta na output kuwa wanaomaliza std 7 ni sawa na std 3.
 
Ili tuendelee tunahitaji wavumbuzi wa kuvumbua vitu....

Hao kina Erasto Mpemba tunao wengi tu ila wanarudishwa nyuma na siasa chafu na uongozi mbovu unaoua mianya ya uvumbuzi - aisee umemcheki yule dogo wa Kenya aliyevumbua taa ya sola kwa ajili ya vijiji vyetu?
 
Lakini yawezekana kuwa na siasa safi na uongozi bora bila ya watu wenye siasa safi na wenye kuleta uongozi bora?

Hapo ni swali na kuku na yai; unaanza kwanza kuwa na uongozi bora utakaohakikisha uozo hauendekezwi kisha ndio unasimika viongozi bora - au umesahau methali ya Kiswahili isemayo samaki mmoja akioza...?
 
mhh sidhani ..huyu jamaa alivyo radical kwenye issue za msingi sijui kama kwenye hilo baraza la mawaziri kutakalika ..By the way it is too late for Jk to appoint such a person kushika wizara hiyo maana miaka 5 sidhani kama inatosha
 
mhh sidhani ..huyu jamaa alivyo radical kwenye issue za msingi sijui kama kwenye hilo baraza la mawaziri kutakalika ..By the way it is too late for Jk to appoint such a person kushika wizara hiyo maana miaka 5 sidhani kama inatosha



duh Rakesh ninayemjua mimi hawezi kufanya kazi na wana Chama Cha Majambazi....
he is too smart for them lol!
CCM hata wakiingia maprofsa upembuzi wao wa mambo unarudi mpaka kwa level ya Mtoto wa Chekechea...
Rakesh Hawezi kukubali labda kama ataenda kum join Mwakembe...

Rakesh please ur my role model hawa watu wasijewakachahachua umakini wako....
 
Kwani ni mbunge tayari ??? Naipongeza haki elimu kwa kusaidia kuelimisha wadanganyika.
 
Kwa sasa hivi si Mbunge lakini wakitaka kumpa uwaziri itabidi wampe Ubunge kwanza.. uzuri wake once wakimpa Ubunge hata wakimuondoa Uwaziri hawezi kuachilia Ubunge hadi miaka yake mitano iishe!

kama si mbunge, basi aendelee kuikosoa serikali akiwa nje, akingia serikarini yatamkuta ya mama sita
 
Sounds interesting. But who can dare to do that in CCM. Remember we have said it many times and we say it again that, to these guys, 'capacity and being able' to deliver is a disqualification. If JK appoints RR, he will be signaling the unthinkable that he intends to do things differently and in a better way. But the unnecessary change of speaker does not make me believe that this can happen! It's a nice dream and is likely to remain so!

I would like to challenge your thinking kaka on two fronts. 1) When you say that for our President, he disqualify people who are able to deliver--you are being overly mshabiki. I think Kikwete love this country, despite of his incompetence, and it is a lie kwamba they guy, purposely choose folks who are incompeteny. But again he put Mustapha Mkullo on finance, which does not make sense. 2) Change of speakership was necessary, Sitta is an id!0t who pursued Richmond for his own umaarufu and not kwa maslahi ya taifa. He used speakership as a tool to punish his political enemies and advance his personal agenda, folks like him do not deserve the speakership.

I would also like to add that CCM wanasoma nyakati na upepo wa siasa. You will all be pleasantly surprised by their performance in the next 5 years. In a way, we needed DR. SLaa to provide changamoto, and he did just that. So do not be surprised when the cabinet will be shrunk, folks like Rakesh taking over Elimu and given mandate to transform the ministry. More than ever CCM want to show folks what they are capable of.
 
Guys i think i need to remind that in this country we don't have only corrupt individuals but also a corrupt system. Unless we do a significant overhaul of the system there is no hope for the cure. Hata uwe mwadilifu vipi ukishaingia kwenye system inayoongozwa na CCM lazima utazimwa tu au system itakutapika kama ukiwa mgumu kuzimwa (kama walivyofanya kwa spika Sita). Ni sawa na wewe uwe wa moto halafu ujidanganye kuwa ukiwekwa ndani ya fridge utaifanya iwe ya moto. Fridge ina system ya kupozea na hivyo hata ukiwa wa moto vipi ni suala la muda tu utaganda na kuwa barafu. Hiyo ndiyo nguvu ya system. Nyie wenyewe mmesikia tetesi za namna Pinda alivyosaidia uchakachuaji wa ubunge wa sumbawanga mjini. Unbelievable!!! tulidhani jamaa ni mwadilifu

La msingi ni kuing'oa CCM madarakani ili chama kitakachoshika hatamu kifanye overhaul ya system. CCM yameshawashinda na hili wanalijua.
 
Ikiwa watampa Rakesh uwaziri wa Elimu, wampe na mamlaka ya kutimua madubwana yote pale wizarani ndipo atafanya kazi vizuri otherwise ni sawa na kumtwisha gunia lililojaa mavi.
 
Kazi anayoifanya kupitia hizo taasisi zake ni kubwa sana na mara nyingi serekali imekuwa ikipingana naye,kumpa uongozi ni namna ya kudhoofisha utendaji wake kwani ndani ya serekali hataweza kukosoa na kuleta changamoto za msingi kama afanyavyo sasa hivyo ni bora abaki na nafasi yake na tunaukubali mchango wake.
 
duh Rakesh ninayemjua mimi hawezi kufanya kazi na wana Chama Cha Majambazi....
he is too smart for them lol!
CCM hata wakiingia maprofsa upembuzi wao wa mambo unarudi mpaka kwa level ya Mtoto wa Chekechea...
Rakesh Hawezi kukubali labda kama ataenda kum join Mwakembe...

Rakesh please ur my role model hawa watu wasijewakachahachua umakini wako....

Haya ndio matatizo ya ushabiki. U want a country to move forward, but you do not wish to see competent folks working for government--just because you hate CCM. Mshkaji, this kind of thinking won't take us anywhere!
 
Kazi anayoifanya kupitia hizo taasisi zake ni kubwa sana na mara nyingi serekali imekuwa ikipingana naye,kumpa uongozi ni namna ya kudhoofisha utendaji wake kwani ndani ya serekali hataweza kukosoa na kuleta changamoto za msingi kama afanyavyo sasa hivyo ni bora abaki na nafasi yake na tunaukubali mchango wake.

Taasisi yake has no ability to change the system. As a minister he can.
 
Back
Top Bottom