Ramadhan Special Thread

Waislamu wenzangu tusiwe wanafiki :
Kama tunafunga,tuache dhambi,tuwe na mke mmoja,tusinywe pombe,sigara,Kufanya mapenzi kwa nyuma na mambo kama hayo ,ili alah atupe pepo na mabikra 70
 
Waislamu wenzangu tusiwe wanafiki :
Kama tunafunga,tuache dhambi,tuwe na mke mmoja,tusinywe pombe,sigara,Kufanya mapenzi kwa nyuma na mambo kama hayo ,ili alah atupe pepo na mabikra 70
Waislam wanaume wameruhusiwa kuanza na wawl hadi wanne, sio dhambi kua na mke zaid ya mmoja. Mengine sawa.
 
Assalaam alaykum. Ndugu zangu, kuswali na viatu ni katika sunna zilizohamwa. Na ndio maana mpaka leo waislamu wengi hawaijui lakin ni sunna iliyothibiti kutoka kwa mtume wetu sala na salamu ziwe juu yake, na miongoni mwa mafunzo ya kuswal na viatu anasema mtume, "atakapoingia mmoja wenu katika msikiti basi na aswali na viatu vyake na asiposwali navyo basi aviweke upande wake wa kushoto na ikiwa upande wake wa kushoto kuna mtu basi aviweke baina ya miguu yake" hadith kwa maana. Na katika sunna hii kuna faida nying: kutulizana katka swala, kupunguza ufisadi na mengine mengi...
Ama ukisema mtume Musa aliambiwa avue viatu vyake! ile ni sheria yake na umma wake na hakituhusu sis isipokuwa kile kilicho wafikiana na sheria yetu ya umma wa Muhammad sala na salamu ziwe juu yake, na amesema Allah "kwa wote hao tumejaalia kwao sheria zao na mienendo yao" surat maida.
Na kitu ambacho hukuwahi kukisikia sio dalili ya kutokuwepo kitu hicho. Alhamdulilah umepewa dalili sahih(kama unashaka fatilia usahihi) baada ya hapo huna budi kusema 'nimesikia na kutii'...
 
jr boy. ndio, zama hizi na zile ni tofauti kidunia ama kidini hali ni ile ile, na Allah hakuwa ni mwenye kusahau kuwa kuna zama zitakuja kuwa hivi zilivyo, lakin alimtuma mtume atufundishe dini hii ambayo ni yenye kuenea mazingira yote na itafanyiwa kaz mpaka kitakapokaribia kiyama. Na kama tutazisingizia zama! Basi ni bora kutoa hizo carpet mpya ambazo ndio kisingizio cha wengi kuliko kukanusha au kupinga sunna za mtume, kwasababu sunna ni zenye kupendeza zaidi mbele ya Allah na kwetu pia kuliko hayo mabusati. Au kuna anayeweza kusema kuwa Allah alisahau au hakujua kuwa zitakuja zama kama hizi?! Bila ya shaka hakuna ambae anayeweza kusema hivyo. Na ametakasika Allah kutokana na yale wanayomsemea kutakasika kuliko mbali. Amesema Allah "pindi zitakapotamka ndimi zenu na itakaposema midomo yenu yale ambayo hamna elimu nayo na mnadhania ni jambo jepesi hali ya kuwa mbele ya Allah ni jambo kubwa" surat Nuur. Jambo ambalo hujui basi fanya research ya kina wala usitoke mbele kupinga ikawa ni sababu ya kuangamia..
 
jr boy. ndio, zama hizi na zile ni tofauti kidunia ama kidini hali ni ile ile, na Allah hakuwa ni mwenye kusahau kuwa kuna zama zitakuja kuwa hivi zilivyo, lakin alimtuma mtume atufundishe dini hii ambayo ni yenye kuenea mazingira yote na itafanyiwa kaz mpaka kitakapokaribia kiyama. Na kama tutazisingizia zama! Basi ni bora kutoa hizo carpet mpya ambazo ndio kisingizio cha wengi kuliko kukanusha au kupinga sunna za mtume, kwasababu sunna ni zenye kupendeza zaidi mbele ya Allah na kwetu pia kuliko hayo mabusati. Au kuna anayeweza kusema kuwa Allah alisahau au hakujua kuwa zitakuja zama kama hizi?! Bila ya shaka hakuna ambae anayeweza kusema hivyo. Na ametakasika Allah kutokana na yale wanayomsemea kutakasika kuliko mbali. Amesema Allah "pindi zitakapotamka ndimi zenu na itakaposema midomo yenu yale ambayo hamna elimu nayo na mnadhania ni jambo jepesi hali ya kuwa mbele ya Allah ni jambo kubwa" surat Nuur. Jambo ambalo hujui basi fanya research ya kina wala usitoke mbele kupinga ikawa ni sababu ya kuangamia..
 
Alhamndulillah, tumshukuru Allah kwakutupatia kheri ya kutekeleza swala 5, hakika si kwa ujanja wetu, Bali ni mapenzi ya Allah.

Tuwaombea dua njema wale ambao hawatekelezi swala 5 Allah awafanyie wepesi.

Allah tunakuomba pepo na mwisho mwema.


Ramadhani kareem.
 
ndio mkuu ume gusia pale pale kabisa sasa hv najisi kila kona.
 
Asalaam Aleikum!

Ndugu yetu thatsit aliwahi kuhoji inakuwaje mwezi mtukufu kama huu,waislamu katika huu uzi wapo wachache ukilinganisha na wingi wao humu jf?
Wengine ni kweli Maalim Shewedy wapo busy na maisha na anakosa mda wa kuingia humu
na ndivyo hivyo anavyotufundisha Mtume (saw) tudhaniane dhana njema

Ila sisi ambao tumeendelea kupita katika huu uzi,( na wengine ambao wapo busy na mada mfano wa hizi katika mitandao mbalimbali ya kijamii) wajue wapo katika ibada, ni kama vile watu wanavyosikia adhana na kwenda msikitini waweza kuta msikitini watu wachache lakin katika mambo ya anasa mfano disco wakajaa sana.Ndivyo dunia ilipofika hapo leo hii!
Jichunge tu usije kuukataa msikiti kwa vile una wachache ukakimbilia disco utapotea!!!

Huu umma wetu umeitwa umma bora sababu ya jambo hili la "nasaha" na tusichoke kukumbushana haya mambo ya heri, ndivyo Mtume (saw) alivyokuwa na sisi tunaosema tunamfata Mtume (saw) yatupasa tuwe hivyo.

Kwako wewe unayetoa nasaha, unayepita mara kwa mara hapa na kusoma yaliyomo,
kwa niaba ya Hance Mtanashati na wengine wote tulioweka nia ya kuendelea kuwepo katika huu uzi, tunasema.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…