Ramadhan Special Thread

Usiwe mwehu kijana, hakuna aliyekukataza kula....kufunga si lazima.....usipende kuendekeza hizi dini za kuletewa na maboti. jiulize, uache kula ili iweje, inakuja kichwani mwako kweli? Amini Mungu wako tu.
Mkuu vitu kama havikuhusu pita kimya. Sio lazima ucomment.
 
Mungu gani ambae ww unamuamini,mpaka ukataka mwengine amuamini?!
Usiwe mwehu kijana, hakuna aliyekukataza kula....kufunga si lazima.....usipende kuendekeza hizi dini za kuletewa na maboti. jiulize, uache kula ili iweje, inakuja kichwani mwako kweli? Amini Mungu wako tu.
 
Waalaykumu Salaam Warahmatullah Wabarakaatuh

Funga yako inaswihi ndg
Ila,lililobora ni kula Daku,kwakule kupatikana kwa Baraka ndani yake,kisha kuupa mwili nguvu

Ila Daku
si jambo la lazima

Shukran

Assalam aleykm warahmatullah wabatakatul! Naomba kujuzwa juu ya ulaj/ kutokula daku.Je nikiacha kula daku funga yangu itaswih?
 
Naomba kuuliza kufunga swaumu bila kuswali ni sawa na kushinda na njaa?
Naam ndugu Kizinga mpemba sala ni katika nguzo za kusihi amali zote,ni funguo ya kusihi amali zote.baada ya shahada ni sala kisha saumu zinakuja mbele.

Mtu akifunga hali ya kuwa hasali basi saumu yake haimfai chochote kwa sababu ameacha ufunguo wa ibada(sala)wapo wanaosema inasihi saumu lakini kauli ya sawa ni kwamba saumu yake haisihi mpaka atakapoanza kusali.

Anasema Mtume wa Allah salama na sala ziwe juu yakee.

أول ما يحاسب عليه العبد يوم القيامة الصلاة،فلإن صلحة صلحة سائر عمله.وإن فسدت فسدت سائر عمله

"jambo la mwanzo ambalo atahesabiwa mja siku ya kiama ni SALA ikiwa sala itatengenea basi yatatengenea matendo mengine yaliyobakia,na ikiwa sala ikawa imefisidika(imeharibika)basi yataharibika matendo yaliyobakia"

Mtume kasema ikifisidika au kuharibika sala basi yanaharibika na matendo mengi,je ikiwa mtu jakusali kabisa tutasema kaiharibu sala ama hakusali kabisa?

Ikiwa yule ambaye alisali lakini akaiharibu yanafisidika matendo yaliyobaki,vipi kwa yule ambae hakusali kabisa je matendo Mengine yatahesabiwa kweli?

Hivyo kwa mtu ambae hasali basi tunahofia saumu yake kutokubaliwa na kutoandikiwa thawabu.

والعلم عند الله
 
Taarifa kwa waislam. (Ofisi ya mufti wa tanzania) kamati ya kitaifa ya masuala ya mwezi inawajulisha waislamu wote kuwa Leo tarehe 5/5/19 kuonekana kwa mwezi hakujathibiti mbele ya mh mufti wa tanzania shk abubakar zuber mbwana.wala mbele ya kadhi mkuu tanzania bara shk abdallah mnyasi.wala hakujathibiti mbele ya mufti wa zanzibar shk swaleh kaab.wala mbele ya kadhi wa znz shk haji khamis. Wala hata jirani zetu kwa kauli ya kadhi wa kenya.hivyo mnatangaziwa rasmi kuwa huu ni usiku wa wa mwezi 30 shaaban. Kesh tunatimiza shaaban 30.hivyo basi ramadhan tutaanza rasmi siku ya jumanne 7/5/2019.ofisi ya mufti ya wa tanzania na mufti wa zanzibar.inawatakia waislam wote ramadhan mubaarak. (Shk alhad mussa salum)katibu wa kamati ya kitaifa ya mwezi muandamo na shk wa mkoa wa dsm)والسلام عليكم ورحمة الله وبركاته
 
Wale wa kuangalia mwezi wa uarabuni kuna update zozote??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…