Hance Mtanashati
JF-Expert Member
- Sep 7, 2016
- 20,137
- 26,189
Asalaam Aleykum ndugu zangu wote katika imani,
Kuelekea mfungo mtukufu wa mwezi wa Ramadhan, waislamu wote ninawaomba tukutane humu ili tuelimishane mawili matatu kuhusu mwezi huu.
Lengo kuu ni kuweza kufahamu yale yote aliyotufunza kipenzi chetu mtume Muhammad S.A.W kuhusu mwezi huu.
Vitu gani tukifanya vitaharibu swaumu zetu, vitu gani tukifanya vitaongeza thawabu zinazopatikana katika kufunga, ipi hukumu kwa wale wasiofunga na yapi malipo anayopewa mja ambaye anafunga swaumu kikamilifu.
Pia tuweze kujifunza neema zinazopatikana kwenye usiku wa lailatul qadr, usiku ambao umebarikiwa kuliko siku elfu moja.
Kwa haya machache ninapenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa muumba wa mbingu na ardhi ambaye si mwingine bali ni Allah S.W. T na kipenzi chake, Mtume Muhammad S.A.W.
Karibuni.
Kuelekea mfungo mtukufu wa mwezi wa Ramadhan, waislamu wote ninawaomba tukutane humu ili tuelimishane mawili matatu kuhusu mwezi huu.
Lengo kuu ni kuweza kufahamu yale yote aliyotufunza kipenzi chetu mtume Muhammad S.A.W kuhusu mwezi huu.
Vitu gani tukifanya vitaharibu swaumu zetu, vitu gani tukifanya vitaongeza thawabu zinazopatikana katika kufunga, ipi hukumu kwa wale wasiofunga na yapi malipo anayopewa mja ambaye anafunga swaumu kikamilifu.
Pia tuweze kujifunza neema zinazopatikana kwenye usiku wa lailatul qadr, usiku ambao umebarikiwa kuliko siku elfu moja.
Kwa haya machache ninapenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa muumba wa mbingu na ardhi ambaye si mwingine bali ni Allah S.W. T na kipenzi chake, Mtume Muhammad S.A.W.
Karibuni.