Ramadhan Special Thread

Ramadhan Special Thread

SAUDIA ARABIA MWEZI WALIUTAFUTA KWA DARUBINI

tarehe 23 kulikuwa hakuna uwezokano wa kuuona mwezi kwa macho ya kawaida japo ni kweli mwezi ulikuwa umeandama

Tarehe 23 mwezi umeandama sa 11:25 asubuhi

Kwakuwa mwezi mpya umechomoza sa 11:25 asubuhi ina maana hu mwezi utazama saa 11 jioni kabla jua halijazama hivyo ukisubiri jua lizame hauwezi kuuona ila ukitumia darubini kuutafuta mida ya mchana utauona ndicho walichofanya Saudi Arabia

Kwa hiyo hata sisi hapa Tanzania tarehe 23 mida ya mchana mwezi ulikuwepo katika anga letu kama tungetumia darubini kuutafuta kabla ya saa 11 jioni tungeweza kuuona

Sasa kama kuutafuta mwezi kwa njia hii inaswihi au haishihi mimi sijui

Sent using Jamii Forums mobile app
Ni kweli hata Mimi Jana nilijiuliza maswali mengi kama tupo masaa sawa na Saudia kwa nini kila siku watangilie wao

Ikabidi nianze Ku Google kuhusu mwenendo wa mwezi nimeona kitu hicho hicho tarehe 23 mwezi mpya ulikuwepo ila ulikuwa unazama kabla ya jua kuzama hivyo huwezi kuuona kwa macho

Hawa Saudia hili jambo wasipo liacha litawatesa sana na ndio maana mahakama kuu ya Saudi Arabia ndio ilitoa amri mwezi utafutwe na utangazwe maana ingekuwa kituko wamekamilisha 30 bila ya mwezi kuonekana

Pia nimeona mwezi mpya utaandama tarehe 22 May saa 2:38 asubuhi ina maana hu mwezi utazama mida ya saa 2 usiku kwa hiyo kuna uwezo kano mkubwa tukala idi pamoja wao itakuwa 30 sisi 29

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haina noma mkuu.

Muhimu haya mas'ala ni khilaafiyyah..

Wanachuoni wametofautiana mnoo juu ya mambo ya mwezi.

Kwa hyo haitakiwi kukinzana na kugombana.

Watu wa fiqhi wanasema..

لا ينكر في ما يختلف فيه ، لاكن ينكر في ما يجمع عليه.

Hapakatazwi kufanya moja kati ya yale ambayo wametofautiana ulamaa,lakini panakatazwa kwenda kinyume na waliyokubaliana maulamaa.
swadakta
 
Acha Uongo wewe....

Ukiambiwa lete ushahidi wa Saudia kuomba Radhi....ninahakika hutoleta

Hizo zilikuwa ni habari za Mitandao tu,na si uhalisi...

Sent using Jamii Forums mobile app
Acha kujipa uhakika bila kujua anaeongea amejipanga vipi. Acha kabisa, hata mwezi wa muandamo kwa juzi haukuwepo, ubaya ni kwamba tayari walikuwa wako ndani ya Shaaban 30 sasahapo utaona ni jindi gani wametangaza mwezi kuepusha madhara na kwa vile hakuna Shaaban 31, miezi yote ya kiislam muandamo wake ni kuanzia 29 hadi 30. Bado unataka ushahidi? Na vile vile mwezi wa muandano kiusahihi ni ule ambao utaonekana kwa macho ya kawaida na sio kwa kifaa kama telescope. Saudi Arabia wametumia twlescope hatima yake sawa wameuona lakini jinsi ulivyokuwa katika ukuaji wake ulikuwa ndio kwaknza upo katika asilimia 0.2 ya ukuaji wake kitu ambacho ni vigumu kuonekana. Kwa sisi ambao tumeanza kufunga leo tar 25 ambapo tar 24 ndio tumetizama mwezi, mwezi ulikuwa kwenye asilimia 3.5 ya ukuaji wake kitu ambacho unaweza kuonekana kwa macho ya kawaida. Saudi wanasababisha Controversy. IN SHAA ALLAH atujaalie tuwepo hadi mwisho wa Ramadhan ili tuje kushuhudia itakavyokuwa.

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Sifa njema zote Anastahiki Allaah Mola wa viumbe vyote na Swalah na salamu zimfikie Mtume wetu na kipenzi chetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) na aali zake na sahaba zake wote.



Ama kwa hakika katika mwezi wa Ramadhwaan kuna fadhila nyingi ambazo mimi nitazitaja kwa uchache namuomba Allaah Aniwafiqishe 'asaa yawe na manufaa katika Duniya na Akhera.



1) NI MWEZI WA QUR-AAN

Kama Alivyosema Allaah Mtukufu:

"Mwezi wa Ramadhwaan ni mwezi ambao imeteremshwa Qur-aan ili iwe uongozi kwa watu na hoja na upambanuzi (Baina ya haki na batil)” [Qur-aan 2:185]



Vilevile kama ilivyopokewa na Ibn 'Abbaas (radhiya Allaahu 'anhu) kuwa makusudiyo yake kwa hakika kuteremshiwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) Qur-aan mwanzo ni katika mwezi wa Ramadhwaan na vilevile Qur-aan mwanzo wa kuteremka ni usiku wa Laylatul-Qadir na Laylatul-Qadir iko katika mwezi wa Ramadhwaan.



Hivyo basi ni juu yetu kufanya juhudi katika mwezi huu kukithirisha sana kusoma Qur-aan. Walikua Salafus-Swaalih (Wema Waliotangulia) wakikilinda kitabu cha Allaah kwa kukisoma na kuyafanyia kazi yaliyokuwemo kwa mazingatiyo. Pia Tunaambiwa kuwa Sayyidnaa Jibriyl (‘Alayhis-Salaam) akimfundisha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) Qur-aan katika mwezi wa Ramadhwaan, na alikuwa 'Uthmaan bin 'Afaan (Radhiya Allaahu 'anhu) kila siku akisoma Qur-aan yote yaani anakhitimisha mara moja kwa siku, kwa maana, msahafu mzima anausoma kwa siku moja. Na walikuwa baadhi yao katika wema wakisoma Qur-aan yote kwa siku tatu, wengine kwa wiki moja na wengine kwa siku kumi. Walikuwa wakisoma Qur-aan ndani ya Swalah na nje ya Swalah.



Allaah Atuwafiqishe mimi na wewe tuisome Qur-aan na kwa mazingatio khasa katika mwezi huu tufanye juhudi sana ili tuweze kupata fadhila za mwezi huu mtukufu.



2) NI MWEZI WA SUBIRA

Subira ni katika jambo gumu na halipati ila kwa mtu mchaji Allaah na mnyenyekevu kwa Allaah. Na katika kufunga kunatakiwa subira pale mtu anapojizuilia kutokana na kutokula, kunywa, matamanio na mengineyo. Imekua Swawm ni nusu ya subira na subira malipo yake ni pepo kama alivyosema Allaah Mtukufu:

"Kwa hakika (Allaah) Atawapa wenye kusubiri malipo bila ya hisabu" [Qur-aan 39:10]



3) MILANGO YA MOTO INAFUNGWA, MILANGO YA PEPO INAFUNGULIWA NA MASHETANI WANAFUNGWA

Kama ilivyokuja katika Hadiyth iliyopokelewa na Maimamu wawili:

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) amesema, "Pindi inapokuja Ramadhwaan inafunguliwa milango ya pepo, na hufungwa milango ya moto, na mashetani wanafungwa kwa Minyororo." [mesimuliwa na Al-Bukhaariy na Muslim]



Kwa hakika utaona katika mwezi huu watu wengi wanajitahidi kujiepusha na maasi, watu wanajaa misikitini kwa kufanya ibada ya mwezi huu hii ni kwa sababu mashetani wamefungwa na shetani juu ya uasi wake lakini anauogopa mwezi wa Ramadhwaan na vitimbi vyake vinakuwa dhaifu ndio mana wengi nyoyo zinabadilika wanaswali na kujitahidi kufanya kheri. Lakini ikimalizika Ramadhwaan tu basi Swalah imekwisha kama vile Allaah yupo Ramadhwaan tu. Huu ni msiba ndugu zangu Waislamu Allaah Asitujaalie katika hao.



4) LAYLATUL QADR

Katika mwezi huu kuna siku ya Laylatul-Qadr siku ambayo ni bora kuliko miezi elfu kama Alivyosema Allaah:

"Huo ni usiku wa hishima ni bora kuliko miezi elfu.

Huteremka Malaika na roho (za viumbe watakatifu) katika (usiku) huo

kwa idhini ya Mola kwa kila jambo.

Ni amani (usiku) huo mpaka mapambazuko ya alfajiri"

[Qur-aan 97:3-5]



Imehisabiwa mtu atakapofanya ibada katika usiku huo mmoja ni kama amefanya ibada sawa na miaka 83 na hii ni katika fadhila kubwa kabisa. Na katika kitabu Muwatwaa, Imamu Maalik amesema.



Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) ameona umri wa ummah za mwanzo ni mrefu, na umri wa ummah wake ni mfupi akapewa usiku wa Laylatul-Qadr uwe ni bora kuliko miezi elfu.

[Muwatwaa, 1/321]



Hakuna siku tukufu na kubwa kama siku hii ni wajibu kwetu kuutafuta usiku huu katika kumi la mwisho kufanya ibada ili tupate fadhila hizo. Ninamuomba Allaah atuwezeshe kwa hilo, Aamiyn.



5) DU'AA NI ZENYE KUKUBALIWA

Katika hadiyth iliyopokewa na Imaam Ahmad:

Kutoka kwa Jaabir (Radhwiya Allaahu 'anhu) kwa isnadi iliyo nzuri

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) Amesema: "Kila Muislam du'aa zake ni zenye kukubaliwa atapomuomba katika mwezi wa Ramadhwaan"

Na imepokewa katika Hadiyth kuwa du'aa ya mwenye kufunga pia ni yenye kukubaliwa. Basi mtu ajipinde katika kumuelekea Allaah kumuomba mambo ya kheri ya dunia na akhera aombe pepo ya Jannaatul Firdaus na alete maombi mengine, Allaah Atayapokea maombi yetu, AAMIYN.



La mwisho ambalo nitakua nimekamilisha maudhui yangu:



6) MWEZI HUU NI MWEZI WA KUTOA

Na alikua Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) akizidisha kheri nyingi katika mwezi wa Ramadhwaan.



Imepokewa na At-Tirmidhiy kutoka kwa Anas (Radhiya Allaahu 'anhu) Kasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) "Bora ya (wakati wa) kutoa sadaqa ni kutoa katika mwezi wa Ramadhwaa.n"



Na imepokewa na Zayd bin Aslam kutoka kwa babake, amesema nimemsikia 'Umar bin Al-Khattwaab (Radhiya Allaahu 'anhu) anasema, "Ametuamrisha Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) tutoe sadaqa nikatoa mali yangu nikasema leo nimemtangulia Abu Bakr nimekwenda na nusu ya mali, akasema Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) kuniambia, "Umewabakishia nini watu wako?" Nikasema, nusu kama hii, na akaja Abu Bakr na kila mali yake Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) akamuuliza, "Umewabakishia nini watu wako? Akasema, nimewabakishia Allaah na Mtume wake. Nikasema huyu Abu Bakr hapitiki na kitu chochote abadan"



Kuonyesha wema waliotangulia walikua wakishindana katika kheri lakini tofauti kubwa katika zama zetu hizi watu wanashindana katika mambo ya kidunia na kujifakharisha nayo.

Tunamuomba Allaah Atuonyeshe mema tuyafuate na mabaya tuyawache na tushindane katika kila kheri ili tuwe ni wenye kufuzu na kupata daraja ya juu ya Pepo.

Aamiyn.



Sent using Jamii Forums mobile app
جزاك الله خيرا
 
SAUDIA ARABIA MWEZI WALIUTAFUTA KWA DARUBINI

tarehe 23 kulikuwa hakuna uwezokano wa kuuona mwezi kwa macho ya kawaida japo ni kweli mwezi ulikuwa umeandama

Tarehe 23 mwezi umeandama sa 11:25 asubuhi

Kwakuwa mwezi mpya umechomoza sa 11:25 asubuhi ina maana hu mwezi utazama saa 11 jioni kabla jua halijazama hivyo ukisubiri jua lizame hauwezi kuuona ila ukitumia darubini kuutafuta mida ya mchana utauona ndicho walichofanya Saudi Arabia

Kwa hiyo hata sisi hapa Tanzania tarehe 23 mida ya mchana mwezi ulikuwepo katika anga letu kama tungetumia darubini kuutafuta kabla ya saa 11 jioni tungeweza kuuona

Sasa kama kuutafuta mwezi kwa njia hii inaswihi au haishihi mimi sijui

Sent using Jamii Forums mobile app
Niliandika kwenye uzi huu huu, lakini bado kuna wengine wamepinga, hivi mwezi ukiwa katika 0.4% ya ukuaji wake utaonekana wapi. Kwasisi ambao tuliangalia mwezi tar 24 tayari ulikuwa katika 2.5% ya ukuaji wake hivyo ni rahisi kuonekana, ila wengine wana ubishi wa kiadili kwa vile tu Saudi Arabia katangaza kuuona.

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Nimefurahi sana Ramadhan ya mwaka huu naskia wanyamwezi wote wamerudi kwao. Zanzibar hotel zote za kitalii zimefungwa kwaio kutokuwepo kwa hawa majamaa wa kibara kumeifanya zanziba kuwa shuari kabisa i wish ningekueko Zenji ramadhani ya mwaka huu
[emoji848][emoji848][emoji848]

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Jazzakhallàh khàigr

Ahsante kwa ukumbusho Mwenyez Mungu atufanyie wekepes katik hili
In shaa Allah
السلام عليكم

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Acha kujipa uhakika bila kujua anaeongea amejipanga vipi. Acha kabisa, hata mwezi wa muandamo kwa juzi haukuwepo, ubaya ni kwamba tayari walikuwa wako ndani ya Shaaban 30 sasahapo utaona ni jindi gani wametangaza mwezi kuepusha madhara na kwa vile hakuna Shaaban 31, miezi yote ya kiislam muandamo wake ni kuanzia 28, 29 hadi 30. Bado unataka ushahidi? Na vile vile mwezi wa muandano kiusahihi ni ule ambao utaonekana kwa macho ya kawaida na sio kwa kifaa kama telescope. Saudi Arabia wametumia twlescope hatima yake sawa wameuona lakini jinsi ulivyokuwa katika ukuaji wake ulikuwa ndio kwaknza upo katika asilimia 0.2 ya ukuaji wake kitu ambacho ni vigumu kuonekana. Kwa sisi ambao tumeanza kufunga leo tar 25 ambapo tar 24 ndio tumetizama mwezi, mwezi ulikuwa kwenye asilimia 3.5 ya ukuaji wake kitu ambacho unaweza kuonekana kwa macho ya kawaida. Saudi wanasababisha Controversy. IN SHAA ALLAH atujaalie tuwepo hadi mwisho wa Ramadhan ili tuje kushuhudia itakavyokuwa.

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"


Mkuu kwanza tambua kuwa ukiwa mwezi thelathini hata kama hukuuona mwezi basi kesho yake ni mwezi mosi ya mwezi unaokuja

Unatakiwa ujue kuwa kuingia mwezi mosi ni eidha uonekane mwezi au itimie mwezi thelathini.

Kiislamu hakuna mwezi 28 kama ulivyosema,sijui umeetoa wapi mwezi 28 kiislamu jamaa ?

Mwaka 93 kama sikosei mwezi ulionekana tarehe 29 ya waliotangulia huku bakwata ikiwa ni tarwhe 28,mufti akatangaza watu wasali iddi na wailipe siku ile.

Lau kama ingekuwa kuna siku 28 za mwezi kiislamu basi mufti asingetangaza watu walipe.

Kwa hiyo mkuu hata kama saudia wasingeuona mwezi hiyo juzi bado kesho yake lazima ingekuwa ramadhani kwa sababu ilishatimia tarehe 30 shaabani tayari kwa hiyo hapo unatoa madai ambayo kimsingi yanaonesha kwamba wewe unadhani kuwa kama hukuuona mwezi basi uende hata tarehe 32 huko jambo ambalo sio sawa.

Unaposema mwezi sahihi ni ule unaoonekana kwa macho ya kawaida unamaanisha kuwa wanaotumia telescope kuangalia mwezi wanatumia macho yasiyo ya kawaida sio ?

Sasa kama unakataa telescope kuutafuta mwezi kwa madai ya kuwa ati mwezi utafutwe kwa macho ya kawaida basi hata simu usipige kumpigia mtu wa zanzibar wewe ulieko dar kumuulizia mwezi kwa sababu..

Unapopiga simu kumpigia mtu wa zanzibar unatumia kifaa kumsikia mtu wa zanzibar akikupa taarifa za mwezi wakati ambao kwa macho ya kawaida huwezi kumsikia kabisa bila simu mtu aliyeko zanzibar.

Kwa hiyo hata simu tusitumie kuwapigia watu kuwauliza taarifa za mwezi kwa sababu kutumia simu sio njia locally ambayo inahusisha masikio peke yake kama ambavyo kutumia telescope sio njia locally inayohusisha macho peke yake.

Ukipinga telescope kuangalia mwezi pia unatakiwa upinge kutumia simu na tv kusikiliza habari zamwezi.

Ukiikubali simu itumike basi unataka kuingiza vifaa ambavyo havikutumika enzi hizo kuutafuta mwezi kabisa.

Alafu jee ukitumia telescope kuangalia mwezi siku ya 25 utauona japo kwa 0.1% kwa kutumia hiyo telescope ?

Kwani telescope inauona mwezi kwa kuwa inauwezo huo wa kuona au telescope inauona mwezi kwa kuwa siku za mwezi kuonekana zimefika ?
 
Mkuu kwanza tambua kuwa ukiwa mwezi thelathini hata kama hukuuona mwezi basi kesho yake ni mwezi mosi ya mwezi uliopita.

Unatakiwa ujue kuwa kuingia mwezi mosi ni eidha uonekane mwezi au itimie mwezi thelathini.

Kiislamu hakuna mwezi 28 kama ulivyosema,sijui umeetoa wapi mwezi 28 kiislamu jamaa ?

Mwaka 93 kama sikosei mwezi ulionekana tarehe 29 ya waliotangulia huku bakwata ikiwa ni tarwhe 28,mufti akatangaza watu wasali iddi na wailipe siku ile.

Lau kama ingekuwa kuna siku 28 za mwezi kiislamu basi mufti asingetangaza watu walipe.

Kwa hiyo mkuu hata kama saudia wasingeuona mwezi hiyo juzi bado kesho yake lazima ingekuwa ramadhani kwa sababu ilishatimia tarehe 30 shaabani tayari kwa hiyo hapo unatoa madai ambayo kimsingi yanaonesha kwamba wewe unadhani kuwa kama hukuuona mwezi basi uende hata tarehe 32 huko jambo ambalo sio sawa.

Unaposema mwezi sahihi ni ule unaoonekana kwa macho ya kawaida unamaanisha kuwa wanaotumia telescope kuangalia mwezi wanatumia macho yasiyo ya kawaida sio ?

Sasa kama unakataa telescope kuutafuta mwezi kwa madai ya kuwa ati mwezi utafutwe kwa macho ya kawaida basi hata simu usipige kumpigia mtu wa zanzibar wewe ulieko dar kumuulizia mwezi kwa sababu..

Unapopiga simu kumpigia mtu wa zanzibar unatumia kifaa kumsikia mtu wa zanzibar akikupa taarifa za mwezi wakati ambao kwa macho ya kawaida huwezi kumsikia kabisa bila simu mtu aliyeko zanzibar.

Kwa hiyo hata simu tusitumie kuwapigia watu kuwauliza taarifa za mwezi kwa sababu kutumia simu sio njia locally ambayo inahusisha masikio peke yake kama ambavyo kutumia telescope sio njia locally inayohusisha macho peke yake.

Ukipinga telescope kuangalia mwezi pia unatakiwa upinge kutumia simu na tv kusikiliza habari zamwezi.

Ukiikubali simu itumike basi unataka kuingiza vifaa ambavyo havikutumika enzi hizo kuutafuta mwezi kabisa.

Alafu jee ukitumia telescope kuangalia mwezi siku ya 25 utauona japo kwa 0.1% kwa kutumia hiyo telescope ?

Kwani telescope inauona mwezi kwa kuwa inauwezo huo wa kuona au telescope inauona mwezi kwa kuwa siku za mwezi kuonekana zimefika ?
Kuhusu 28 nakiri nilikosea na nimesharekebisha.

Kaka haya maswali yako yote nakujibu kiurahisi kama ifuatavyo:
Kuangalia na kutafuta mwezi wa mwandamo katika eneo la magharibi wakati wa jioni wakati Jua linapozama, ndio msingi wa kuamua mwanzo na mwisho wa mwezi wowote wa Hijri katika Uislamu.

Ni kama amri nyingine yoyote katika Uislam, hii ndio njia iliyoelezewa na Mwenyezi Mungu katika Quran na kwa nabii Muhammad ﷺ katika Hadith. Ni Sharee'ah ambayo Mwenyezi Mungu alimtumia Nabii wetu Muhammad ﷺ (Rehma na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake). Ni ya ulimwengu na ya milele, mpaka Siku ya Kiyama. Ni halali kwa kila wakati na mahali, ikiwa sayansi za ulimwengu ni za hali ya juu au vinginevyo, ikiwa kuna darubini au la.

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Ila kiukweli ugumu wa kwenye kufunga kwa pamoja tunauleta sisi wenyewe waislam, ndani yake kuna mambo ya kisiasa. Kuanzia leo nikisikia mwezi umeonekana kokote kule nafunga, hayo ndio maagizo kutoka kwenye Quran na hata hadith, waislam tunatakiwa tushikamane na wala tusifarikiane. Akiuona mwezi muislam yoyote yule duniani inatakiwa iwe ni sawa na tumeuona waislam wote.

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Kuhusu 28 nakiri nilikosea na nimesharekebisha.

Kaka haya maswali yako yote nakujibu kiurahisi kama ifuatavyo:
Kuangalia na kutafuta mwezi wa mwandamo katika eneo la magharibi wakati wa jioni wakati Jua linapozama, ndio msingi wa kuamua mwanzo na mwisho wa mwezi wowote wa Hijri katika Uislamu.

Ni kama amri nyingine yoyote katika Uislam, hii ndio njia iliyoelezewa na Mwenyezi Mungu katika Quran na kwa nabii Muhammad ﷺ katika Hadith. Ni Sharee'ah ambayo Mwenyezi Mungu alimtumia Nabii wetu Muhammad ﷺ (Rehma na amani za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake). Ni ya ulimwengu na ya milele, mpaka Siku ya Kiyama. Ni halali kwa kila wakati na mahali, ikiwa sayansi za ulimwengu ni za hali ya juu au vinginevyo, ikiwa kuna darubini au la.

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"

Mkuu nimekuuliza maswali hujajibu kila swali kama nilivyouliza hapo juu.

Unasema msingi wa uislamu ni kuangalia mwezi magharibi pale unapoandama ili kupata tarehe hijri katika uislamu.

Kama ni hivyo Sasa saudia hizo telescope wanatumia adhuhuri kutizama mwezi au wanatumia muda wa magharibi ule ule kutizama mwezi ?

Alafu kama unakubali kuwa hakuna mwezi 28 katika uislamu jee umewahi kusikia saudia wanaangalia mwezi siku ya 28 au 27 au 26,alafu wakauona mwezi kwa hizo teleescope ?

Kama hawajawahi huoni kuwa wanatizama mwezi katika masiku ambayo kisheria ndo inatakiwa mwezi utizamwe ?

Na kama unakataa mwezi ambao unaonekana kwenye telescope mwezi ambao ni kweli mwezi na umeanza kuchomoza kwa hizo 2% na masiku ya kuangaliwa ni yale yale ya kishwria yaani 29 na 30 ila tu unaukataa kwa kuwa tu kinatumika kifaa cha kisayansi kusaidia kuuona

Kama ni hivyo mbona usizikatae simu ambazo zinatumika kutafuta taarifa za mwezi kutoka kwa mtu wa mbali.

Tena sauti unayoisikia hiwezi kuisikia katika hali ya kawaidia,yaani mtu wa kigoma na dar hawawezi kupeana taarifa za mwezi kwa kuongea bila simu kwa sababu ni maeneo mbali mbali,sasa ili iwe rahisi kwao kuwasiliana kikatumika hiki chombo cha kisayansi yaani simj kurahisisha mawasiliano ambayo locally hayawezi kufanyika na kuwezekana.

Kama pia ni hivi kwa nini unakataza saudia kutumia telescope ya kisayansi kutizama mwezi alafu wewe unatumia na kuhalalisha simu ambazo nazo ni za kisayansi zinatumika kufanya mawasiliano kuipata sauti ambayo huweI kuisikia localy ?

Sasa hapa nataka uninibu kila nukta niliyouliza mkuu ili na sisi tupate faida katika majawabu yako.

والله أعلم
 
Mkuu kwanza tambua kuwa ukiwa mwezi thelathini hata kama hukuuona mwezi basi kesho yake ni mwezi mosi ya mwezi uliopita.

Unatakiwa ujue kuwa kuingia mwezi mosi ni eidha uonekane mwezi au itimie mwezi thelathini.

Kiislamu hakuna mwezi 28 kama ulivyosema,sijui umeetoa wapi mwezi 28 kiislamu jamaa ?

Mwaka 93 kama sikosei mwezi ulionekana tarehe 29 ya waliotangulia huku bakwata ikiwa ni tarwhe 28,mufti akatangaza watu wasali iddi na wailipe siku ile.

Lau kama ingekuwa kuna siku 28 za mwezi kiislamu basi mufti asingetangaza watu walipe.

Kwa hiyo mkuu hata kama saudia wasingeuona mwezi hiyo juzi bado kesho yake lazima ingekuwa ramadhani kwa sababu ilishatimia tarehe 30 shaabani tayari kwa hiyo hapo unatoa madai ambayo kimsingi yanaonesha kwamba wewe unadhani kuwa kama hukuuona mwezi basi uende hata tarehe 32 huko jambo ambalo sio sawa.

Unaposema mwezi sahihi ni ule unaoonekana kwa macho ya kawaida unamaanisha kuwa wanaotumia telescope kuangalia mwezi wanatumia macho yasiyo ya kawaida sio ?

Sasa kama unakataa telescope kuutafuta mwezi kwa madai ya kuwa ati mwezi utafutwe kwa macho ya kawaida basi hata simu usipige kumpigia mtu wa zanzibar wewe ulieko dar kumuulizia mwezi kwa sababu..

Unapopiga simu kumpigia mtu wa zanzibar unatumia kifaa kumsikia mtu wa zanzibar akikupa taarifa za mwezi wakati ambao kwa macho ya kawaida huwezi kumsikia kabisa bila simu mtu aliyeko zanzibar.

Kwa hiyo hata simu tusitumie kuwapigia watu kuwauliza taarifa za mwezi kwa sababu kutumia simu sio njia locally ambayo inahusisha masikio peke yake kama ambavyo kutumia telescope sio njia locally inayohusisha macho peke yake.

Ukipinga telescope kuangalia mwezi pia unatakiwa upinge kutumia simu na tv kusikiliza habari zamwezi.

Ukiikubali simu itumike basi unataka kuingiza vifaa ambavyo havikutumika enzi hizo kuutafuta mwezi kabisa.

Alafu jee ukitumia telescope kuangalia mwezi siku ya 25 utauona japo kwa 0.1% kwa kutumia hiyo telescope ?

Kwani telescope inauona mwezi kwa kuwa inauwezo huo wa kuona au telescope inauona mwezi kwa kuwa siku za mwezi kuonekana zimefika ?
Allah akulipe shekh ,aiseee nimekupenda sana kwa ajili ya Allah.Nimejifunza kutoka kwako

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nimekuuliza maswali hujajibu kila swali kama nilivyouliza hapo juu.

Unasema msingi wa uislamu ni kuangalia mwezi magharibi pale unapoandama ili kupata tarehe hijri katika uislamu.

Kama ni hivyo Sasa saudia hizo telescope wanatumia adhuhuri kutizama mwezi au wanatumia muda wa magharibi ule ule kutizama mwezi ?

Alafu kama unakubali kuwa hakuna mwezi 28 katika uislamu jee umewahi kusikia saudia wanaangalia mwezi siku ya 28 au 27 au 26,alafu wakauona mwezi kwa hizo teleescope ?

Kama hawajawahi huoni kuwa wanatizama mwezi katika masiku ambayo kisheria ndo inatakiwa mwezi utizamwe ?

Na kama unakataa mwezi ambao unaonekana kwenye telescope mwezi ambao ni kweli mwezi na umeanza kuchomoza kwa hizo 2% na masiku ya kuangaliwa ni yale yale ya kishwria yaani 29 na 30 ila tu unaukataa kwa kuwa tu kinatumika kifaa cha kisayansi kusaidia kuuona

Kama ni hivyo mbona usizikatae simu ambazo zinatumika kutafuta taarifa za mwezi kutoka kwa mtu wa mbali.

Tena sauti unayoisikia hiwezi kuisikia katika hali ya kawaidia,yaani mtu wa kigoma na dar hawawezi kupeana taarifa za mwezi kwa kuongea bila simu kwa sababu ni maeneo mbali mbali,sasa ili iwe rahisi kwao kuwasiliana kikatumika hiki chombo cha kisayansi yaani simj kurahisisha mawasiliano ambayo locally hayawezi kufanyika na kuwezekana.

Kama pia ni hivi kwa nini unakataza saudia kutumia telescope ya kisayansi kutizama mwezi alafu wewe unatumia na kuhalalisha simu ambazo nazo ni za kisayansi zinatumika kufanya mawasiliano kuipata sauti ambayo huweI kuisikia localy ?

Sasa hapa nataka uninibu kila nukta niliyouliza mkuu ili na sisi tupate faida katika majawabu yako.

والله أعلم
Nataka kujibu hoja yako moja badala ya nyingine lakini kila nikiedit inapotea..

"Fᵒˡˡᵒʷ ᵉˣᶜᵉˡˡᵉⁿᶜᵉ ˢᵘᶜᶜᵉˢˢ ʷⁱˡˡ ᶜʰᵃˢᵉ ᵖᵃⁿᵗˢ ᵈᵒʷN"
 
Nawakumbusha pia ndugu zangu katika dini

katiika kufuturu tuache israfu tule kwa kiasi, kula chakula kwa saizi yako

Allah sw hawapendi wanaofanya israfu( hili lipo na ushahidi hata ndani ya quran na hadithi)

isije kuwa tunafunga funga zetu vizuri kisha tunakuja kuziharibu kwenye kufuturu
 
Mkuu kwanza tambua kuwa ukiwa mwezi thelathini hata kama hukuuona mwezi basi kesho yake ni mwezi mosi ya mwezi unaokuja

Unatakiwa ujue kuwa kuingia mwezi mosi ni eidha uonekane mwezi au itimie mwezi thelathini.

Kiislamu hakuna mwezi 28 kama ulivyosema,sijui umeetoa wapi mwezi 28 kiislamu jamaa ?

Mwaka 93 kama sikosei mwezi ulionekana tarehe 29 ya waliotangulia huku bakwata ikiwa ni tarwhe 28,mufti akatangaza watu wasali iddi na wailipe siku ile.

Lau kama ingekuwa kuna siku 28 za mwezi kiislamu basi mufti asingetangaza watu walipe.

Kwa hiyo mkuu hata kama saudia wasingeuona mwezi hiyo juzi bado kesho yake lazima ingekuwa ramadhani kwa sababu ilishatimia tarehe 30 shaabani tayari kwa hiyo hapo unatoa madai ambayo kimsingi yanaonesha kwamba wewe unadhani kuwa kama hukuuona mwezi basi uende hata tarehe 32 huko jambo ambalo sio sawa.

Unaposema mwezi sahihi ni ule unaoonekana kwa macho ya kawaida unamaanisha kuwa wanaotumia telescope kuangalia mwezi wanatumia macho yasiyo ya kawaida sio ?

Sasa kama unakataa telescope kuutafuta mwezi kwa madai ya kuwa ati mwezi utafutwe kwa macho ya kawaida basi hata simu usipige kumpigia mtu wa zanzibar wewe ulieko dar kumuulizia mwezi kwa sababu..

Unapopiga simu kumpigia mtu wa zanzibar unatumia kifaa kumsikia mtu wa zanzibar akikupa taarifa za mwezi wakati ambao kwa macho ya kawaida huwezi kumsikia kabisa bila simu mtu aliyeko zanzibar.

Kwa hiyo hata simu tusitumie kuwapigia watu kuwauliza taarifa za mwezi kwa sababu kutumia simu sio njia locally ambayo inahusisha masikio peke yake kama ambavyo kutumia telescope sio njia locally inayohusisha macho peke yake.

Ukipinga telescope kuangalia mwezi pia unatakiwa upinge kutumia simu na tv kusikiliza habari zamwezi.

Ukiikubali simu itumike basi unataka kuingiza vifaa ambavyo havikutumika enzi hizo kuutafuta mwezi kabisa.

Alafu jee ukitumia telescope kuangalia mwezi siku ya 25 utauona japo kwa 0.1% kwa kutumia hiyo telescope ?

Kwani telescope inauona mwezi kwa kuwa inauwezo huo wa kuona au telescope inauona mwezi kwa kuwa siku za mwezi kuonekana zimefika ?
Yawezekaka isiwe 30 kama walikosea mahesabu ya mwezi wa shaabani

Mimi binafsi sijawahi kuona mwezi 30 usionekane kwa macho ya kawaida

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom