mkuu vip kuhusu kutumia tofali za nch 5 kweny ukuta wa nyumba
vs. kutumia nch 6, kuna utofaut gan wakitaalam
Ukitumia tofali za nchi 6, kuta zako baada ya kupigwa plaster (ndani na nje) zitakuwa na upana wa almost nchi 7
Dirisha la grill huwa linatengenezwa kwa kutumia square pipe za nchi 1, na huwa linaflash na nyuso za kuta za ndani
Dirisha la Aluminium, profile zake huwa zinatofautiana upana, zipo za nchi 3, 4 na zipo zingine pana zaidi. Hizi nazo zinaflash na nyuso za kuta za nje.
Ukichukua hiyo nchi 7 ukatoa nchi 1 ya grill na nchi 3 ya aluminium profile utabakiwa na space ya nchi 3 (ambapo kwa hii case utaweza kutumia hata grill za 1¼ square pipe au ukatumia dirisha lenye profile za nchi 4 na bado nafasi kati grill na aluminium window ikabaki)
Kwa upande wa milango, upana wa fremu kawaida huwaga ni kuanzia nchi 4, kama utaweka geti la grill kwa kutumia square pipe za nchi 1 maana yake mpaka hapo una jumla ya inchi 5, nafasi kati ya geti na mlango itakuwa nchi 2
Kuna sehemu zingine unakuta wametengeneza kingo za plaster kwa nje kuzunguka madirisha ili dirisha za aluminium ziweze kukaa kwa sababu upana wa kuta ni mdogo, na profile ni pana
Kiufupi ukuta wako ukiwa mpana, utaweza kuweka milango ya mbao na mageti ya grill au dirisha za grill na aluminium zake za upana unaohitaji bila kuweka hizo kingo nilizosema hapo juu vinginevyo itabidi utumie material yatakayoendana na upana wa kuta zako
Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane