Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

Haya sasa mashikolo mageniii 🤣🤣🤣🤣 mambo ya tenaile forces sie tuliokimbia physics hapa bila bila
 
Sasa hizi open kitchen plan za misasa sii ndio majanga mwanawane
 
Umbali kati ya chemba na ukuta wa nyumba unatakiwa usipungue mita ngapi?
 
Mie nilijuaga ni urembo tuuu🤣🤣🤣🤣
 
Ewaaah! Hii ndio nilikuwa naisaka sana.
Ebwana wee nataka nijenge kisima cha kucolle t maji ya mvua toka kwenye gutter niyaelekeze humu.

Sasa eneo ambalo lina nafasi nzuri lipo mbele ya garage na hapo v8 ndio inapita kuingia garage. Na deaign vipi hizo cross beems ili ziweze kuhimili vi yangu kupita hapo juu? Nondo za mmm 16 au zaidi ndio zinahitajika? Zege ya ration gani?

Estimated ukubwa wa hicho kisima ni 3 x3 x 2.5m. na je nijenge cha duara au square au rectangular?
 
So mchanga amaluf ndio unamwaga zege la blainding?
 
Ili kuepuka gharama za kujenga mnara wa tank la maji, kibaraza cha mbele au cha nyuma juu weka zege badala ya bati ili upate nafasi ya kuweka tank juu

Ramani, Makadirio au Ushauri tuwasiliane
Kibalaza mwisho tank la litre ngapi i aweza beba? Au na ye yewe upige cross beams ili kubeba uzito zaidi?
 
Okay kumbe ni kama maofisini tuu huku, sometimes unaenda kula chakula cha mama ntilie na mlinzi pale alafu unamnunulia glass ya mtindi na ndizi asugumie ubwabwa.
 
Okay kumbe ni kama maofisini tuu huku, sometimes unaenda kula chakula cha mama ntilie na mlinzi pale alafu unamnunulia glass ya mtindi na ndizi asugumie ubwabwa.
Yah, siku moja moja unawapelekea hata matunda. Ukiwathamini, watafanya kazi yako kwa moyo wote lakini wakiona hauwathamini, wanaweza wakakuharibia kazi yako makusudi hata kama unawalipa

Kuna maboss wengine wakifikaga site, hata kuwasalimia tu mafundi wanaonaga shida (wanahisi kama wanajishusha, wanataka wao ndio wasalimiwe kila siku hata kama wao ndio wamewakuta mafundi). Sasa kama boss salam tu kwake ni shida, sidhani kama ataweza kuwafanyia hizo surprises mafundi
 
Ukishinda site kinachofata ni kukukomoa, mahali ambapo panahitajika mifuko mitatu ya cement, wenyewe watachanganya mifuko mitano. Lengo lao hasa ni kukutia hasara zaidi baada ya wewe kuamua kuwabana kupita kiasi
Kwa mahesabu uliyotupa na nondo hizi hakomolewi mtu hapa. Wanamwaga zege la columns tayari najua kabisa mifunko mingapi inahitajika, mchanga kiasi gani na kokoto kiasi gani
 
Kumbeee hapa ndio ninalpfeliiii.
Aisee mie nilikuwana natala nishime million 150 kabisa ndio niinue mjengo breki ya kwanza nipo ndani. Aisee hapa ngoja nikaanze na msingi
 
Umepigaje hapo kwenye round colum 4 imerokea wapi tena jamani hesabu hizi wenhine tulikimbia
 
Alooh! Lazima uchoke mwanawane. Pumua kwanza🤣🤣🤣🤣
 
Kuna hotel moja ipo kigoma aisee jamaa alivyo manuva ile slope na kutoa kitu hatari sana.
 
Umepigaje hapo kwenye round colum 4 imerokea wapi tena jamani hesabu hizi wenhine tulikimbia
Hiyo imetoka hapa
Area (A) = πR².....eqn (1), where R= d/2
A= π(d/2)²
A= πd²/4

d - diameter, r - radius
 
Hii ya kifusi then mawe then mchanga then zege ni kwa majengo yote au ghorofa tuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…