Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

Ramani, Makadirio, Elimu na Ushauri kuhusu Ujenzi

Wakati mwingine sio lazima sana kuchukua vifaa vyote vya ujenzi vikiwa ktk hali yake ya uzima mfano unapoenda kununua tiles, unanunua box za tiles ambazo ni nzima na ukifika site tiles zingine unazikata ili upate vipande vya kujazia na wakati huo huo pale hardware uliponunulia hizo tiles kuna box za tiles ambazo baadhi ya vipande vimekatika na muuzaji anauza kwa bei ya hasara hivyo kama ungechanganya box nzima na zile zilizokatika ungeokoa kiasi flani cha pesa

Hii pia unaweza ukaapply kwenye gympsum board ktk uwekaji wa dari, tofali n.k kwa lengo la lengo kupunguza gharama

Kabla ya kufanya uamuzi inabidi ufanye mahesabu ili upate makisio kwamba nyumba yako itahitaji vitu vizima vingapi, ili uweze kujua sehemu iliyobaki itahitaji kiasi gani cha material ambazo sio nzima (hapa simaanishi ubovu, namaanisha utimilifu)
Somo zuri sana la elimu ya fedha na matumizi.
 
Nami ningependa kujua haya mawe yanaongeza nini maana naona si kila project inatandika mawe kabla ya kumwaga zege. Labda mwenye uzoefu wa miradi ya serikali anaweza kutujuza. Mawe ni lazima au hapana?
Mawe yanatumika kwa ajili ya kuongeza uimara wa msingi/floor katika jengo. Wengi huwa wanakwepa kwa sababu ya gharama, lakini ukiweka inakuwa vizuri zaidi. Kama uchumi hauruhusu weka tu kifusi lakini ukishindilie vizuri kwa matabaka kuanzia chini mpaka kufikia level inayohitajika.

Kwa majengo kama mashule, mahospitali n.k mawe ni lazima na ni muhimu sana kwa sababu ni majengo ambayo yana muingiliano wa watu wengi na pia yanatumika kwa muda mrefu (yapo majengo yana miaka zaidi ya 50 na bado yanaendelea kutumika kwa sababu ya msingi imara)
 
Kama uchumi hauruhusu kuweka mkanda wa chini, basi ile kozi ya mwisho ya msingi na kwenye kona zote jengea tofali zenye vile vikokoto (huwa inaongezeka sh 100 ktk bei ya tofali za kawaida yaani cement & mchanga bila vikokoto)

Uimara wake hauwezi ukawa sawa na mtu aliyefunga mkanda lakini haiwezi ikawa sawa na mtu aliyejengea tofali za kawaida pote. Tofali zenye vikokoto zina compressive strength kubwa kulinganisha na tofali za kawaida hivyo itaongeza uimara zaidi
Vipi nimije ga kozi hiyo ya mwisho ya msingi na tofali hizo za mchnaga na kokoto...hapo sii msingi u akjwa ngangari kama nondo tuu
 
Safi sana kiongozi , nikiwa Moshi ufundi nilisoma Plumbing , nilifundishwa kuwa hata system ya choo na bafu havitakiwi kuwa na same path(destination) sababu , ya hao bacteria (anaerobes bacteria) ambao ndio huvunja vunja uchafu.
👍
 
Baada ya kupiga plaster msingi wako, paka black bitumen (changanya na solvent)
Kopo la 4Lts linauzwa kwenye 18,000 mpaka 20,000
Vipi nikijenga tiles?
Je hiyo bitumen i asaidia nini as opposed to kupaka rangi ya kawaida
 
Kwenye nguzo za vibaraza sio lazima uweke nguzo za zege, unaweza ukaweka nguzo ya shape ya "L" kwa kutumia tofali na bado nyumba yako ikavutia lakini pia ikakupunguzia gharama za nondo na ufundi
Tofali unalaza?
 
Bati lina upande dume na upande jike, katika upigiliaji upande jike unatakiwa uwe juu ya upande dume

Ramani, Makadirio na Ushauri tuwasiliane
Jike anakuwaje juu ya duume...this goes against nature bro
 
Leo tuangalie upande ambao SEBULE na VYOO vinapotakiwa vikae

Katika pande zote nne yaani Kaskazini, Kusini, Mashariki na Magharibi, upande wa Kaskazini ndio upande ambapo unapokea jua ama joto kwa kiasi kidogo na upande wa Kusini ndio upande ambao unapokea jua ama joto kwa kiasi kikubwa katika masaa yote ya siku (asubuhi mpaka jioni). Upande wa Mashariki hupokea joto jingi kuanzia asubuhi mpaka mida ya mchana, na upande wa Magharibi hupokea joto jingi kuanzia mchana mpaka jioni

Sebule inatakiwa ielekee Kaskazini kwa sababu ni sehemu ambayo muda mwingi watu watakuwa hapo (asubuhi mpaka jioni) hivyo haitakiwi iwe upande ambao utakuwa sio rafiki kukaa katika mazingira hayo

Tukija upande wa Kusini ambao unapokea joto jingi zaidi katika masaa yote ya siku, kitu ambacho unaweza kuweka upande huu (kusini) ni vyoo na mabafu. Hii ni kwa sababu chooni sio mahali ambapo watu hukaa muda mrefu, watu hukaa muda mfupi na pia ni kwa mara chache.

Ramani, Makadirio na Ushauri wa kitaalam tuwasiliane +255(0)624068809
Hili ebu fafanua vizhri na sie back bencher tuelewe vizuri.
Sasa kwa mfano kiwanja kipo kinafa e barabara kuu north wards na kimebanwa between other two plots. Slope yake ni towards the south na mie nataka kuweka mjengo hapo hiyo sebule nataka ipate madirisha on atleast two walls naiweka kwa wapi maana lazima ukuta mmoja utakuwa east au west. Nipe utaalam hapo mwanawane
 
Katika makubaliano ya gharama za kazi na fundi, jitahidi makubaliano yasiwe juu juu (ile kazi husika iwekee na vipengele vyake ili mwisho wa siku fundi asije akakuruka).

Mfano unaweza ukakubaliana na fundi kazi ya kukata miti katika eneo lako la ujenzi, sasa usishangae kuona mafundi wanakuja kukudai pesa yao baada ya kukata hiyo miti maana ukiwaambia mbona hamjaitoa watakuambia sisi tumekubaliana kazi ya kukata miti sio kuikata na kuitoa. Mpaka hapo itakulazimu uingie tena gharama zingine, maana itabidi mfanye tena makubaliano ya kazi ya kuhamisha miti

Sasa kwa mfano huu wa miti, itatakiwa uwaambie kwamba hiyo kazi itainclude kukata miti yote, kuihamisha eneo la ujenzi (na ikibidi waoneshe mahali ambapo unataka yakae hayo magogo, wasije wakayaweka tu pembeni baadae ukaingia tena gharama ya kutafuta watu wayasogeze pembeni zaidi), na malipo yote ni baada ya kazi kukamilika/kuisha. Ukijichanganya kuwalipa malipo kwa kazi waliyofanya, kesho wanaweza wasirudi hasa pale kazi inapokuwa ni ngumu, lakini kama hujawalipa kabisa au umewalipa kidogo hawawezi kukutoroka kesho wasije site.

Ramani, Makadirio na Ushauri kuhusu ujenzi tuwasiliane +255(0)624068809
🤣🤣🤣 Aise kumbe site kuna kuliana timing eeh 🤣🤣🤣🤣
 
Uzi mzuri sana kwa wanaohitaji kujenga mambo ya kujifunza hapa ni mengi sana.
 
UFUNDI UMEME


(1) Hata kama unampa ela ya vifaa fundi basi ni vizuri kuakikisha alichokiandika ni sahihi maana mafundi uwa tuna tamaa baada ya ela kuwa mikononi.unakuta fundi kakuandikia waya(kampuni ya euro)ila unashangaa analeta site waya usiojulikana.hii ni hatari sana kwa usalama wako na vifaa vyako.

(2) Kabla ya kufanya wiring ni vizuri wewe muhusika kumwambia fundi maitaji yako yote ya vitu ambavyo utakuja kutumia baadae ili isije ikatokea changamoto ya kufanya upanuzi wa maitaji mengine ya umeme.mfano kwenye stage ya kwanza(kuchimbia bomba) ni vizuri kuweka point nyingi ili hata ikitokea unaitaji kuongeza kibu basi kusiwe na changamoto.

(3) hakikisha umeme wowote unaopita chini ya ardhi basi ununue waya maalum kwa ajili ya chini ya ardhi.sio kila waya una uwezo wa kupita chini ya ardhi.hii baadae itakuja kukuletea shida wakati huo utashindwa kufanya kitu kwa sababu gharama ya marekebisho itakuwa kubwa.

(4)Hakikisha unanunua vifaa vya umeme ambayo kwa ndani vimetengenezwa kwa copper na sio chuma kilicholambishwa copper.kampuni yenye vifaa vilivyotengenezwa kwa pure copper kwa hapa nchini ni( Tronic,ABB,Africab,havels)


(5)Hakikisha fundi anatumia bomba kwenye kufanya wiring na pia anafunga na mifuniko kwenye sehemu zenye juction box ili kuzuia wadudu kufika kwenye switch au main switch.

(6) Hakikisha fundi anaorodhesha matumizi yako yote kwenye kuomba mita tanesco ili usije ukapewa mita ndogo ukashangaa umeme unaenda mwingi kumbe mita inazidiwa.hakikisha taarifa za matumizi alizoweka kwenye mchoro ni sahihi.





Kwa ushauri pamoja na kazi piga namba
0652868486
Ok...je nini tofauti ya single na 3 phase? Mbona sijawahi sikia 2 phase au 4 phase?
Kwa makadieio ya haraka haraka ya wiring ya nyumba ya vymba vitatu; ac kila chumba socket 2 kila chumba heater 3 vyooni yenye muundo wa corridor, chumba kulia chumba kushoto materials inaweza fika kiasi gani?
 
Hii bonge la elimu leo nimesoma page 10 tuu tayari munkari wakujenga nimepata.

Anyways great job sasa mie suggestion yangu tuu ni moja.
Unatupa nondo nzuri sana hapa mwanawane na katika kuborasha basi tutengeneze kipamflet ambacho kitakuwa na jshauri wote huu katika mpangilio mzuri i.e process yote kutoka kusaka plot mpaka finishing.

Kuwe na chapters mahusisi so mtu akifika stage flani anafungua tuu chapter flani.

So unakuwa na chapters kama hivi

Ununuzi wa kiwanja
Maandalizi ya site
Ujenzi wa msingi
Uje zi wa boma
Kupaua etc.

So hapo mtu anaenda direct kwa chapter husika.

Sasa najua wabongo tulivyo wangese nikisema hapa tuchangishe buku 2 kila mdau tupate hii ili tuwe tunatembea nayo au kuwa nayo nda i ya nyumba watapita kushoto.

But anyways unaweza tengeneza hicho kipamflet ukawa unauza mwanawane itasaidia wengi sana
 
Hili ebu fafanua vizhri na sie back bencher tuelewe vizuri.
Sasa kwa mfano kiwanja kipo kinafa e barabara kuu north wards na kimebanwa between other two plots. Slope yake ni towards the south na mie nataka kuweka mjengo hapo hiyo sebule nataka ipate madirisha on atleast two walls naiweka kwa wapi maana lazima ukuta mmoja utakuwa east au west. Nipe utaalam hapo mwanawane
Ili upate madirisha pande mbili katika sebule, inatakiwa sebule ikae ubavuni/pembeni mwa nyumba (ambapo mbele kutakuwa na dirisha na mlango wa kuingilia, na ubavuni pia kutakuwa na madirisha mengine mawili). Ramani nyingi ukiziangalia utaona sebule ipo kati na hivyo kufanya sebule iwe na dirisha upande wa mbele pekee huku ikitegemea mwanga na hewa zaidi kutoka madirisha ya Dinning room.
 
Ili upate madirisha pande mbili katika sebule, inatakiwa sebule ikae ubavuni/pembeni mwa nyumba (ambapo mbele kutakuwa na dirisha na mlango wa kuingilia, na ubavuni pia kutakuwa na madirisha mengine mawili). Ramani nyingi ukiziangalia utaona sebule ipo kati na hivyo kufanya sebule iwe na dirisha upande wa mbele pekee huku ikitegemea mwanga na hewa zaidi kutoka madirisha ya Dinning room.
Na hili unalosema mie naonaga sana kwenye ramani which i feel inanyima nyuma mzunguko mzuri wa hewa maana inatokea upande mmoja tuu.

Sasa kwa mantiki hiyo, dirisha na mlango vinatakiwa kutazama north alafu madirisha mawili mingine yatizame east au west? Which is better? East au west?
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] Aise kumbe site kuna kuliana timing eeh [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Yah, hizi scenario zipo nyingi sana..mfano mwingine unaweza ukakubaliana na mafundi kujenga msingi wote mpaka jamvi, sasa wakishamaliza kujenga kuta za msingi usishangae fundi akakuambia utafute watu wa kujaza kifusi ili baadae waje wamalizie kazi ya kumwaga jamvi (wakati huo wewe unajua pesa mliyokubaliana na fundi inajumuisha kila kitu)
 
Back
Top Bottom