Ramani ya fundi Maiko, inachorwa bila proportions lakini nyumba inasimama

Vibanda vyetu vingi tumejenga kwa namna hii ya michoro ya kina fundi maiko, au unamuita unampa maelekezo natakanyumba yangu iwe hivi, hivi na hivi imeisha hiyo, unaanza kujenga taratibu, unanunua tofali buku unapandisha mzigo, ukipata unapiga mpaka kozi ya 4,ukipata tena hivyo hivyo mpaka kibanda kinaisha [emoji2969]
 
Roho mbaya hiyo..ungekaa naye mkaifanyia marekebisho kulingana na mtazamo wako.

#MaendeleoHayanaChama
Nilimwambia hii plan haiko sawa,akaniuliza kwa dharau kama mimi ni engineer?
Dawa ya jeuri ni kiburi,nikaichana halafu nikatafuta fundi toka mjini gharama za kumleta kwangu
 
Nyumba nyingi sana zimepanda kwa style hiyo halafu fresh tu.
fresh wapi,unajenga nyumba haina layout nzuri baada ya muda unaona kikubwa nyumba tu ladha hakuna. Kama ni fundi kuweni tayari kujifunza. uzuri siku hizi mitandao imerahisisha house plan kibao gugo.
 
fresh wapi,unajenga nyumba haina layout nzuri baada ya muda unaona kikubwa nyumba tu ladha hakuna. Kama ni fundi kuweni tayari kujifunza. uzuri siku hizi mitandao imerahisisha house plan kibao gugo.
Nyumba niliyolelewa kajenga fundi maiko na ipo poa tu. Hata style ya kibaraza tuliona cha jirani tukamuuliza Fundi Maiko akafanya namna kimekaa vizuri tu
 
Nyumba niliyolelewa kajenga fundi maiko na ipo poa tu. Hata style ya kibaraza tuliona cha jirani tukamuuliza Fundi Maiko akafanya namna kimekaa vizuri tu
Na hapa si ajabu kuna walionuonya ramani ya fundi Maiko
 
Wakati mwingine kwenye linter fundi Maiko anakuletea nondo kwa bei yake, alikozitoa hujui lakini anakuambia ukipata hela utamlipa.
 
Wakati mwingine kwenye linter fundi Maiko anakuletea nondo kwa bei yake, alikozitoa hujui lakini anakuambia ukipata hela utamlipa.
Fundi maiko ashukuriwe saaana., ujenzi wa kujengewa na kampuni ama engineer sisi kajamba nani hatuwezi.
 
Fundi maiko ashukuriwe saaana., ujenzi wa kujengewa na kampuni ama engineer sisi kajamba nani hatuwezi.
Kuna vijana kule bush, wanapima kwa kamba lakini ukuta unanyooka. Mradi waielewe tu ramani na vifaa viwepo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…