RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

Yaani wamependekeza serikali 3
Ya shirikisho...
Ya Tanzania bara...
Ya Zanzibar...

Alafu wakajiamulia kutengeneza katiba ya serikali moja (shirikisho) peke yake!!! Sasa hizo mbili wamemuachia nani?!!! Ebo!

Mkuu hujaelewa, hii ni hatua ya kwanza ya kuunda kitu 'mama' then ikishapita ndo sasa katiba za serikali husika zitaundwa. Sasa hivi hicho unachotaka hakiwezi kuwepo kwa sababu this is just a proposal mkuu!
 
Mkuu naelewa. Ninachoona mimi ni kuwa huu mchakato wa katiba umefanywa ovyo kabisa ili 2015 ama tusiwe na uchaguzi, au tutumie ile ile katiba ya zamani.
Hebu jiulize; Mwaka 2014 hii katiba ya shirikisho ikikamilika, je 2015 Watanganyika tutapiga kura kuchagua viongozi wetu kwa kutumia sheria ipi? Tutatumia katiba ipi? Hiyo katiba itatengenezwa lini? Tume ya kutengeneza hiyo katiba itaundwa na nani? Endapo "Tanganyika" hatutafanya uchaguzi 2015, Je tutachagua raisi wa shirikisho na wa Zanzibar? Baada ya hapo Tanganyika itakuwa inaongozwa na nani (Kumbuka serikali ya shrikisho itahusika na mambo 7 tu)?

2015 tutafanya uchaguzi wa rais wa Tanganyika na Tanzania, ila katiba yetu itakuwa ipi sasa, zanzibar wenzetu wana katiba!
 
.
Madaraka ya rais ndiyo yaliyasababisha nchi kuwa masikini japo tuna rasilimali nyingi. Tukitaka katiba yenye ufanisi katika mageuzi ya kiuchumi ni lazima madaraka ya rais yapunguzwe.
Kuhusu wabunge kuwa wawili katika kila jimbo huu ni uvivu wa kufikiri. Tanzania hatuhitaji kutoa hisani kwa watu wasio walemavu kwa gharama kubwa namna hiyo. Wabunge wapambane wake kwa waume na mwisho wa siku apatikane mshindi mmoja kuwakilisha jimbo.
.
Nina wasiwasi kama ulielewa vizuri, hii ni katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Naiman itabd tuwe na katiba ya nchi yetu ya Tanganyika. Humo tutakuwa na wabunge ambao ni wawakilishi wa wananchi wa Tanganyika, wabunge hawa 75 ni wa Bunge la JMT. Bunge la Tanganyika pia litakuwepo kujadili mambo ya Tanganyika km vile ZNZ walivyo na Baraza la wawakilishi.
 
Kwa ujumla wamefanya kazi nzuri sana, niwapongeze sana kwa uchambuzi makini pamoja na vikwazo walivyopambana navyo ila wamefanya kazi njema, mapungufu hayakosekani ndio maana itajadiliwa tena na bunge la katiba ili kuiweka sawa.
Ni kweli!
ukiona mtu anapinga, ujue anawaza zaidi kuhusu hatima ya chama chake kuliko utaifa.Sijui atakapohama itakuwaje.
Naona kuna wengine wanasema hakuna jipya, hawajui kama haya mapendekezo yametokana na maoni ya wananchi na sio mtu mmoja.
 
mwenyekiti wa umoja wa vyama vya siasa peter kuga mzirai amewawakilisha na amechukua rasimu moja kwa niaba yao na atawagawia vyama vyote na pia ukumbuke kuwa hii ni katiba ya nchi sio ya vyama

Siungi mkono rasimu ya katiba.
Yani makamanda hawamo kwenye uzinduzi???
Mbowe,Slaa,Lema,Tundu hawamo?haiwezekani serikali ipendelee waziwazi,kama hawatatengua hayo sijui mauzinduzi yao na kuyatangaza upya ili makamanda nao wapewe shavu la kuhudhulia uzinduzi tutaandamana nchi nzima na tuko tayari kufa!

VIVA MAKAMANDA WENZANGU!
CC Ritz Ben Saanane
 
Last edited by a moderator:
wewe ni pimbi kweli? hujui kama zanzibar ina katiba yake? katiba ya tanzania bara itatengenezwa na watanzania bara wenyewe. sasa wewe unataka mambo ya bara yajadiliwe na wazanzibar? ebo

Sina mbavu kwa kucheka.
 
2015 tutafanya uchaguzi wa rais wa Tanganyika na Tanzania, ila katiba yetu itakuwa ipi sasa, zanzibar wenzetu wana katiba!
Tanzania bara hatuna katiba.
Wakati sie tunapiga domo huku, wenzetu Zanzibar walikuwa wanatengeneza katiba yao.
Ndiyo maana hata wimbo wa taifa wanatumia wao sio wa muungano.
sie tunaimba wimbo wa muungano.Hatuna wimbo wa taifa.
 
Hapa hizi mihimili mitatu bado zinaingiliana, haiwezekani Jaji mkuu ateuliwe na Rais, wakati ni kiongozi wa muhimili unaojitegemea.
 
inamaaana hao wabunge 75 watajadili mambo 7 ya muungano tu na kupitisha bajeti ya wizara 7 tu or ?
 
Wabunge wa sasa ni wajumbe pia katika bunge la katiba. Ninaamini kabisa wataipinga hoja ya kuwa na bunge lenye wabunge 75, kwani wengi wao bado hawajalipa mikopo ya hela walizotumia kwenye kampeni

Mkuu tunaweza fanya uchaguzi wa shirikisho then tukaendelea na utengenezaji wa katiba ya Tanganyika taratibu na ikikamilika uchaguzi wa Tanganyika unaitishwa mkuu.
 
Hapo nafikiri labda hujapaelewa vizuri, mimi nafikiri wana hoja ya maana kwamba, kama Mbunge akifariki basi hakuna haja ya Uchaguzi ili kuokoa gharama, basi mrithi wake atatoka Chama kile kile tu, hivyo ina maana Chama chake watateua tu, badala ya uchaguzi kufanyika, kwa maana nyingine tunapaswa tuchague Sera za Chama na SIO mtu!

Karne hii mambo ya kurithisha watawala yanatoka wapi, ni bora wangesema atakayerithi ni yule aliyeshika nafasi ya pili kwenye uchaguzi regardless ya chama anachotoka! Hii ya kurithi ni upuuzi acheni democrasia ikomae nchini, uchaguzi mmoja au miwili kwa mika mitano una hasara gani? CCM iache woga hayo hayawezi kuwa maoni ya watanzania wengi hata kama ni wengi si maoni ya kuzingatiwa na tume!
 
Kwa kweli mapendekezo mengi ya tume ni mazuri mno ila sina uhakika kama huko kwenye mabaraza ya katiba kama watayapitisha kama yalivyo mana huko kutatangulizwa maslahi ya ccm mbele.
Mkuu hata mie naona hii ya serikali tatu yawezekana imechomekwa tu ili kwenye mabaraza ikataliwe wapate sababu ya kuendelea na serikali mbili maana haitamkwi TANGANYIKA ki uwazi ila wamechomela Tanzania bara kwa nini???????
 
serikali yenye mamlaka na itakayofahamika kimataifa ni ile ya shirikisho.
duh kwa mantiki hiyo rais wa Tanganyika na wa Zanzibar watakuwa na mamlaka ya ndani ya nchi zao tu ila yule wa shirikisho ndiyo anakuwa overall kimataifa
 
Makamu wa raisi naye anapongeza ujinga... Watu wanapendekeza serikali tatu, alafu hawatoi muongozo kuwa serikali mbili kati ya hizo zianzeje?!!!

Tuko hapa naona inayochanganya ni hii ya katiba ya Tanzania bara,tume haijatoa mwelekeo wa kupatikana
kwake,ila ya Zanzibar tayari ipo,cha kujiuliza je hakuna contradiction katia ya katiba ya Zanzibar na hii ya Shirikisho'
 
Back
Top Bottom