RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

RASIMU ya Katiba Mpya Tanzania yazinduliwa

Dah!! Kama Kenya vile
Tukienda hivi basi Tanzania ni Mahali muhimu pa kuishi sasa na milele
 
Kiwango cha juu kabisa cha safari za raisi nje ya nchi kwa mwaka:yell:

Hahaahahahah!rais mwisho safari 3 kwa mwaka!nyingine anajilipia yeye mwenyewe

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
1. Kwanza kabisa Bado madaraka ya raisi ni makubwa mno hasa juu ya uteuzi na kinga ya kutoshitakiwa.
2. Kuhusu suala la mafao maana Rais mstaafu hulipwa asilimia 80 ya aliye madarakani tunataka iwe hivyo kwa watumishi wote kama ni mwalimu alipwe 80 na mwalimu wa wakati huo au hata ikipungua lakini iwe flat accross all positions.
3. Tatu na kubwa tunataka kupiga kura kwa aina yoyote kusiwe kwa kutumia sauti kama ilivyo bungeni unapima uzito wa sauti haifai hata kidogo hata kwa technologia unaweza kupiga kura kwa rahisi na kwa haraka watu wabonyeze kwa mfano bungeni mwisho screen ziwashwe watu wapige hata watazamaji tujiridhishe walokubali wameshinda au kushindwa.
4. Mikataba yote ya nchi ijadiliwe na kuridhiwa na bunge ili wananchi tushiriki nakujua uwazi wake
 
Kitendo cha kutomshtaki Rais akimaliza muda wake kimenikera sana,pamoja na swala la chief justice kuteuliwa na Rais,Hii rasimu bado sana
Kipengele hicho kitabadilishwa siku chache baadas ya CCM kuondoka madarakani.
 
Nanukuu:


MADARAKA YA RAIS

Ndugu Wananchi,
Tume inapendekeza kwamba, Rais abaki na madaraka ya uteuzi wa viongozi wa ngazi za juu. Hata hivyo inapendekezwa Rais ashirikiane na taasisi na vyombo vingine katika uteuzi. Kwa mfano:

Uteuzi wa Mawaziri na Manaibu Waziri, Rais atateua na Bunge litathibitisha.

Kuhusu Jaji Mkuu na Naibu Jaji Mkuu Rais atawateua kutokana na majina ya watu waliopendekezwa na Tume ya Uutumishi wa Mahakama na baada ya hapo Bunge litathibitisha.

Kuhusu Wakuu wa vyombo vya Ulinzi na Usalama inapendekezwa kianzishwe chombo kipya kitakachoitwa Baraza la Ulinzi na Usalama la Taifa, ambalo kati ya majukumu yake itakuwa ni kumshauri Rais kuhusu uteuzi wa Wakuu wa vyombo vya ulinzi na usalama.
Kuhusu Makatibu Wakuu na Naibu Makatibu Wakuu watateuliwa na Rais kutokana na mapendekezo ya Tume ya Utumishi wa Umma.

KINGA YA RAIS

Tume baada ya kupitia maoni ya Wananchi, inapendekeza Rais abaki na kinga kama ilivyo sasa na anaweza kushitakiwa na Bunge kama ilivyo Katiba ya sasa.

(Tume hapa inamaanisha rais ni Mungu asiyekosea,asiye na ndugu,asiyesoma mikataba kwa makosa,asiye mfanya biashara,ambaye hajatumia pesa zake na za washirika wake kuingia madarakani,
Kama sio,kwani awekewe kinga,hapa sio kuuza nchi na rasilimali zetu kwa kutumia kipengele hicho kinachomfanya mfalme na muungu mtakatifu?)

IDADI YA MAWAZIRI

Inapendekezwa Rais aunde Serikali ndogo iliyo na Mawaziri wasiozidi kumi na tano na mawaziri hao wasiwe wabunge. Mawaziri hawatahudhuria vikao vya Bunge isipokuwa kama watahitajika kutoa ufafanuzi kwenye kamati za Bunge.
(Hapa sielewi kabisa,hata cha kuandika sina)

BUNGE

Ndugu Wananchi,
Kuhusu Bunge kutakuwa na wabunge wa aina mbili. Kutakuwa na Wabunge wa kuchaguliwa na wabunge watano wa kuteuliwa na Rais kuwakilisha Watu wenye Ulemavu.

Kila Jimbo la Uchaguzi litakuwa na Wabunge Wawili mmoja mwanamke na mwingine mwanamume.

Tume inapendekeza kwamba, Mbunge akifukuzwa na Chama cha Siasa abaki kuwa Mbunge lakini akihama Chama atapoteza Ubunge wake.
(Je,inamaanisha wananchi tutakuwa tunachagua mtu au chama,kwanini ijichanganye na kutenda tofauti kwa mgombea huru,iwapo tunachagua mtu,kwanini chama kipewe nafasi ya kutupatia mtu ambaye sisi wananchi hatujamchagua,na kwakuwa kuna kipengele kinatoa nafasi wananchi wamtimue mbunge akichemka,je huu mwanya uliopo hapa hautatumiwa kumfukuza mbunge aliyechaguliwa na chama iwapo jimbo litakuwa wazi kwa sababu tajwa hapo juu?)

Inapendekezwa ukomo wa Ubunge uwe vipindi vitatu vya miaka mitano mitano. Hata hivyo, wananchi wanaweza kumwondoa mbunge wao kabla ya mwisho wa kipindi chake.

Inapendekezwa pia kusiwepo na uchaguzi mdogo isipokuwa kama nafasi inayokuwa wazi inatokana na Mbunge huru ndipo utafanyika uchaguzi mdogo kujaza nafasi hiyo, lakini kama nafasi ikiwa wazi kutokana na Mbunge wa Chama cha Siasa basi nafasi hiyo, ijazwe na mtu kutoka Chama hicho.

Inapendekezwa Spika na Naibu Spika wasitokane na Wabunge na wasiwe Viongozi wa vyama vya Siasa.


"Nachanganyikiwa kila ninaporudia kuisoma rasimu hii ya katiba ya Tanzania yetu"
mawazo yangu tu
~seen today~​
 
Wabunge watakaopingwa twawashauri wagombee uwakilishi kwenye bunge la Tanzania Bara....
Tanzania bara ndio kitu gani? kuiita nchi yenu Tanganyika nako ni shida?
Hebu angalia hapa.....

Tanganyika law society, hawa wana akili timamu.
 
Marekani Rais hawezi ongeza wizara au punguza bila kuomba ruhusa ya bunge
au kuvunja na kuunga wizara fulani

Tanzania right now as we speak kuna waziri asie na wizara maalum..
Idadai ya wizara ipo....kama sikosea mapendekezo kwenye rasimu ni 15(saurce TBC taifa waliokuwa wakitangaza live)
 
tunaitaka rasimu tuanze kuiangalia kuna mambo mengi ambayo wananchi bado hatujayajua,

kutakuwa na serikali tatu,

hii ni rasimu ya jamuhuri ya muungano nilivyoelewa ikisha kupitishwa, itatoa ruksa kwa kila upande wa bara(tanganyika) na visiwani (zanzibar)kuunda katiba zao,

yaani katiba ya tanzania bara (tanganyika)na katiba ya tanzania visiwani(zanzibar),

mimi niko interested na katiba ya tanzania bara(tanganyika) kuliko hata ya muungano

kuweni makini wadu msijadili kama vile bado tutakuwa na serikali mbili

labda niwape mfano rahisi tuujadil

1. kutakuwa na raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tz -dr. willbrad slaa
2. kutakuwa na raisi / waziri mkuu mtendaji wa Tanganyika ambaye atachaguliwa na wananchi wa bara ---zito zuberi kabwe
3. kutakuwa na raisi / waziri mkuu mtendaji wa wa zanzibar ambaye atachaguliwa na wananchi wa visiwani
 
where is the full document? hayo maeneo yote uliyoyagusia ni vague, the team did not do their work properly.
 
vitu vingi tunavyo jadili na kuvitaja kwenye hii thread vipo kwenye rasimu.......mzee warioba hajaacha kitu...baadhi ya mapendekezo wizara 15(mawaziri wasiwe wa chama) wabunge 75....spika awe independent sio wa chama...serekali tatu...mgombea binafsi...tume huru ya uchaguzi na mengine mengi saurce TBC_TAIFA iliyokua inatangaza live
 
Serikari mbili zenyewe ni kubwa sana! Mie nilitegemea serikari ingekuwa moja?sasa serikari tatu huo no mzigo kwa walipa kodi yaani badala ya kuwasomesha wazenji mpaka wajitambue na wakubali kuwa ndugumoja na wajue umoja ni nguvu huku kero zikitokomezwa.tunabuni serikari tatu !yaani tunatoka ktk unafuu na kujipeleka kwenye gharama kuendesha serikari Tatu!huku miungano nafuu inaogozwa na mawaziri wakuu kama kule UK inashangaza sana Nchi masikini kuwa na serikari tatu huku ikitegemea pesa za wafadhili kwenye bajeti yake .
 
Tume imependekeza wabunge 75, Tanganyika 50 Zanzibar 20, walemavu 5, wewe unataka kupunguza gharama kwa kuongeza wabunge kuwa 150.

Sijasoma rasimu yote lakini naweza kusema mambo kadhaa:
1. Inaonekana unatumia mfumo wa serikali mbili kujenga hoja zako
2. Hao wabunge 75 ni wale wa Shirikisho
3. Kutakuwa na wabunge wengine wa Bunge la Tanganyika na Bunge la Zanzibar
4. Idadi ya wabunge wote inaweza kuwa kubwa zaidi ukilinganisha na idadi ya sasa!!!

Nasimama kukosolewa maana sijaiona rasimu yote, najenga hoja kutoka kwenye Hotuba ya Warioba katika Uzinduzi wa Rasimu ya Katiba.
 
Kuwa na subira!

Sent from my BlackBerry 9780 using JamiiForums
 
Moja ya kazi ya Tume Huru ya Uchaguzi ni kudimamia kura ya maoni, nagtumai hii inahusisha na kura ya maoni ya Mswada huu wa Katiba. Ukiangalia jindi Tume yenyewe inavyoteuliwa utagunfua kuwa bado kuna tatizo la kuifanya kweli Tume huru na hasa ukizingatia mfumo tulionao sasa.
 
Salam wanaJF.

Kwa siku za hivi karibuni kumekuwa na taarifa kwamba kuna mipango inasukwa ili kumuongezea raisi Kikwete muda wa kukaa madarakani hadi mwaka 2017 ikiwa ni kuiwezesha nchi kuwa na katiba mpya kabla ya kwenda kwenye uchaguzi mkuu.

Kwa mujibu wa mapendekezo ya tume ya Jaji Warioba katika rasimu iliyotangazwa leo, ambayo inapendekeza muundo wa serikali tatu, ni dhahiri kuwa imemuwekea Kikwete mazingira ya kuendelea kuiongoza Tanganyika kwa takribani miaka miwili ili kuipa nafasi ya kutengeneza katiba yake.
Zanzibar wao tayari wana katiba yao kwahiyo mwaka 2015 wataingia katika uchaguzi wao bila shida na kujipatia viongozi wao.

Kwa maoni yangu Tanganyika tutahitaji serikali ya mpito wakati tukiandaa katiba yetu. Na serikali hiyo haiwezi kuwa hii ya sasa iliyotuchosha kwa kukosa uongozi thabiti na muono wa kueleweka. Namshauri Raisi Kikwete aanze kufikiria kupumzika mwaka 2015 na si vinginevyo.
 
Back
Top Bottom