Rasmi nimeamua kuachana na betting. Kubet ni kutafuta umasikini na ufukara

Rasmi nimeamua kuachana na betting. Kubet ni kutafuta umasikini na ufukara

Pole sana Mkuu, Ila hizi kauli mbiu ndio huwa zinamaliza Watu.., "Eti Bet Kistaarabu" Nani kasema kwenye Ulevi kuna Ustaraabu!!!
Yaani bora anaeweka 1000 kwenye odds 2000 maana huyo anafanya starehe, kuliko huu ujinga wa sure odds unaweza pigwa ukachakaa.
 
Kuna jamaa yangu alishinda 1.2m mwaka jana, akambetia jirani yangu nae akashinda 1.5m. Hiyo ni mwaka jana, mwaka huu anzia january jamaa ni vipigotu ukiangalia betslip yake lost lost lost, alafu mkeka haweki below 35k, yote ni vipigo mpaka mda huu. Ukimwambia swala la kubeti ananyong'onyea.
 
Kuna jamaa yangu alishinda 1.2m mwaka jana, akambetia jirani yangu nae akashinda 1.5m. Hiyo ni mwaka jana, mwaka huu anzia january jamaa ni vipigotu ukiangalia betslip yake lost lost lost, alafu mkeka haweki below 35k, yote ni vipigo mpaka mda huu. Ukimwambia swala la kubeti ananyong'onyea.
kama anaweza kuweka 35 kwenye mkeka huyo hana njaa.
 
Kuna jamaa yangu alishinda 1.2m mwaka jana, akambetia jirani yangu nae akashinda 1.5m. Hiyo ni mwaka jana, mwaka huu anzia january jamaa ni vipigotu ukiangalia betslip yake lost lost lost, alafu mkeka haweki below 35k, yote ni vipigo mpaka mda huu. Ukimwambia swala la kubeti ananyong'onyea.
Betting sio dili asee .
 
Kwanza niseme tu mimi nikati ya watu, waliokuwa wakiamini betting kwa asilimia 100, nilikuwa na imani betting ndio kitu itanitoa kimaisha, kuhusu betting ulikuwa huniambii kitu, kuna ile kauli watu huwa wanasema beti kama starehe, Lakini mimi nimekuwa nikiifanya kama kazi ya kujiingizia kipato.

Nilikuwa mstari wa mbele kutoa Matusi, kejeli husda na masimango kwa wale wote, waliokuwa wakionesha kupinga amakuleta hoja kinzani kuhusiana na gambling/betting
Katika kipindi kifupi takriban mwaka mmoja baada ya kumaliza masomo ndio nilianza kuifanya betting kama kazi.

Lakini kwa huo muda mfupi, imeniletea hasara kubwa kubwa kubwa ambayo sitokuja kuisahau ,yaani zile pesa ambazo nimepoteza ningesema badala ya kutuma kwenye betting company, niziweke kwenye kibubu now ningeweza kufungua biashara kubwa sana.

Baada ya vipigo kuzidi, huwa kuna msemo wanasema sikiliza wataalamu inaonekana strategies unazotumia sio salama,, Hao wanaojiita watalamu watakwambia usiweke timu nyingi weka timu chache ,"tafuta odds mbili halafu tia laki," Aloo huo msemo ndio umenifukia kabisa hadi sasa naandika hapa sina hata mia mbovu,
Jana kuna mkeka niliucopy kutoka kwa jamaa mtata sana humu jamii forum nikaweka pesa ya nauli ambayo leo nilikuwa naelekea dar es salaam, kwa mazingira ya kutatanisha sana pesa yote nimeliwa, mpaka muda huu nimejilaza hapa nasingizia naumwa.

Kwenye betting sio kwamba watu hawashindi wanashinda ila kunautofauti mkubwa sana kati kuliwa na kushinda so ukiifanya kwa muda mrefu ukaja piga mahesabu baada ya mwaka utajikuta na hasara kubwa Hadi utaogopa kama sio kulia.
Betting imefanya nashindwa hata kununua nguo mpya hadi zile nilizomaliza nazo masomo zimeanza kupauka sio kwamba hela sipati hapana zote zinaishia kwenye mikeka, yaani getto unaweza kuta nimenunua sukari robo, mchele kilo mbili halafu kwenye simu nimebet 50000 na yote inaliwa.

Mwaka jana nilikuwa nasimamia mashamba ya jamaa fulani sasa nilikuwa nikipokea hata pesa za kupalilia ,na mimi boss wa vibarua najitengea ekari yangu moja ya palizi maana nimepita jkt halafu 60000 naweka mfukoni,.kisha wale vibarua badala ya kuwa lipa 60000 nawalipa 40000 kwa ekari ,tutalima weee nikimaliza pesa yote naenda kuliwa kwenye betting.

Usiku wa leo nimekaa nikafanya projection nikiendelea hivi baada ya miaka 5 ijayo nitakuwa mmoja kati ya watu masikini zaidi Tanzania, At 20s vijana wengi hutumia kujenga future zao mimi natumia kubomoa, Betting imeniletea uvivu ,muda wote sina furaha ,nilikuwa napenda kusoma,kuongeza ujuzi,kutafuta kazi,kuwekeza,kuchangamana na watu, kufanya kazi, mdau wa michezo, mapenzi but now nimekuwa kama mtu aliepigwa bomu.

Bado sijachelewa, ninamuda wa kutosha kusahihisha makosa niliyoyafanya, sihitaji tena kuwa mtumwa, nimekubali kusahau yaliyopita na kufungua ukurasa mpya, sioni kama nitatizo kuanza moja, ninaamini tatizo ni kuendelea kukumbatia adui,na adui wangu ane hujumu uchumi wangu ni betting.
Tatizo ww unabeti kutoka kimaisha wengine tunabeti kama burudani
 
Kuna wafanyakazi wanakaribia kuingia rumande kisa kubet

Na wala hawajashtuka kama inawafilisi ndo kwanza wanalia waongezewe mshahara wanasahau nao pia hautatosha sababu ya bet

Shukuru umeshtuka hiyo kitu ni sawa na sembe.
Ni zaidi ya sembee maana inafanya mtu anakuwa na tamaa ya pesa nyingi. Badala yake unajikuta mfungwa wa vipigo kila kukicha
 
Kwani ukiweka 1000 ukapata 5000 kuna shida gani? Kwanini uweke pesa nyingi kwa tamaa ya utajiri kwenye shughuli za watu?
Hiyo ni starehe ila mimi nilikuwa nabet kutoka kimaisha,
Yaani siku nilikuwa nikibahatisha napata pesa nyingi na fungu kidogo natenga kwenda kula raha na mademu, sasa hiyo 3000 hata nikishinda nitafanyia nini hata pesa ya bundle haijarudi
 
Sawa. Sasa Chukua Beseni La Mihogo Uanze Kutembeza Barabarani, Betting Ina Wenyewe Ndio Kazi Pekee Inayotumia 70% Ya Akili Kene Ubungo Wako.
Siwezi tembeza mihogo ndugu. Ila pesa yangu kuliko kuipeleka kwa muhindi ni bora nifanyie vitu vya maana.

Kuhusu hiyo 70% unajidanganya labda uwe newbie kwenye gemu. Kwa kiswahili hiyo ni bahati nasibu
 
Jana kwa mfano unashindwaje kuweka tot win, barca win juve win na arsenal uweke 5000 upige 20,000. Mimi niliweka 1000 nikapiga 8000, naridhika na nafurahia mchezo sasa kama wew umefanya ni ajira shauri yako, acha tu.
 
Mkuu tatizo unabet kimaskini unaweka 500 ili ushinde million unaona inawezkana? Hio ni bht sana asee. Mimi niliweka 500k nikala 6m na usheee lakin ningeweka 500 hapo ningeshinda 6000 unaona utofauti hapo nmepata faida ya 5.5m. Ukibet ukaweke pesa ndogo lazma uweke tim nyingi ili dau liwe kubwa lakin ukiweka timu chache dau kubwa unakua na probability kubwa ya kushinda.
 
Back
Top Bottom