RASMI Serengeti Boys Yarejeshwa AFCON

RASMI Serengeti Boys Yarejeshwa AFCON

Hata kina Andrea Ayew walitokea kwenye timu ya vijana.Matumaini yangu wakifanya vizuri,utakuwa ndiyo mwanzo watanzania kukua kisoka.
 
Wamfanye Diamond Platinum kocha mkuu mbeba bendera, ana uzoefu na fainali na kuondoa ukweli wa kuqualify kimbelekombeleko
 
Mngejua kundi Alilopangwa serengeti ni bora angemwachia tu Congo akamalizane nao mwenyewe
[emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] [emoji2] Sasa mkuu bila kushndana nawalio Bora tutawezaje kuwa Bora ?
 
Wamfanye Diamond Platinum kocha mkuu mbeba bendera, ana uzoefu na fainali na kuondoa ukweli wa kuqualify kimbelekombeleko
[emoji3] [emoji3] [emoji1] [emoji3]
 
Fainali hizi za vijana sasa zitafanyika nchini Gabon.
 
HATIMAYE timu ya taifa ya vijana chini ya umri wa miaka 17 ya Tanzania, Serengeti Boys imerejeshwa kwenye michuano ya Mataifa ya Afrika kwa vijana wa umri huo.
Rais wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Jamal Malinzi akiwa mwenye furaha kubwa amesema jioni ya leo; "Timu ya Taifa ya vijana umri chini ya miaka 17 imefaulu kucheza fainali za Afrika. Hongera Serengeti Boys! Hongera Tanzania!,"amesema Malinzi bila kufafanua.​

Mwanzoni mwa mwezi uliopita, Shirikisho la Soka Afrika (CAF) liliwapa siku 10 Shirikisho la Soka Kongo (FECOFOOT) kumuwasilisha mchezaji Langa Lesse Bercy mjini Libreville, Gabon afanyiwe vipimo vya MRI ili kuthibitisha umri wake kama anaruhusiwa kucheza mashindano ya vijana chini ya umri wa miaka 17.

Katika kikao cha Kamati ya Utendaji ya CAF jana mjini Libreville, FECOFOOT walitakiwa kumpeleka mjini humo Langa Lesse Bercy akafanyiwe vipimo kufuatia malalamiko yaliyowasilishwa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), baada ya zoezi hilo kushindikana mara mbili.

Na hatua hiyo ilifuatia Rufaa ya TFF dhidi ya mchezaji huyo baada ya Kongo kuitoa U-17 ya Tanzania katika hatua ya mwisho ya mchujo wa kuwania tiketi ya fainali za mwaka huu zilizopangwa kufanyika Madagascar.

Awali, Kongo walitakiwa kumpeleka mchezaji huyo makao makuu ya CAF mjini Cairo, Misri kwa vipimo, lakini mara mbili wakashindwa kufanya hivyo.

source: binzubeir blog
Ngoja na sisi watukatie rufaa na vijeba vyetu!
waache kuweka mamluki, ni ujinga tu waafrika tunakuwa nao, ni heri timu itolewe mapema kwa kuwapa nafasi wachezaji wenye umri stahili, kuliko kuwa bingwa kwa kupanga mibabu iliyofoji umri!
lengo la mashindano ya vijana ni kusaidia nchi kuibua na kulea vipaji vya vijana ili wawe hazina hapo baadae ktk timu za taifa, huku kwetu mizee inadandia na ujinga wa mashirikisho ya soka, yanataka cosmetic sifa ilhali wakijua hawana kitu cha kujivunia kwa kuwa wali-cheat!
 
Mngejua kundi Alilopangwa serengeti ni bora angemwachia tu Congo akamalizane nao mwenyewe

Mkuu, haya ndio makundi yenyewe? Hapo Group A toa Madagascar weka Gabon. Na kwenye Congo weka Tanzania.

upload_2017-2-3_23-17-41.png
 
Ngoja na sisi watukatie rufaa na vijeba vyetu!
waache kuweka mamluki, ni ujinga tu waafrika tunakuwa nao, ni heri timu itolewe mapema kwa kuwapa nafasi wachezaji wenye umri stahili, kuliko kuwa bingwa kwa kupanga mibabu iliyofoji umri!
lengo la mashindano ya vijana ni kusaidia nchi kuibua na kulea vipaji vya vijana ili wawe hazina hapo baadae ktk timu za taifa, huku kwetu mizee inadandia na ujinga wa mashirikisho ya soka, yanataka cosmetic sifa ilhali wakijua hawana kitu cha kujivunia kwa kuwa wali-cheat!
Mkuu Tanzania tulishakutwa na hilo sakata la vijeba, timu yetu ilifuzu fainali za vijana U17 zilizopita ikaondolewa kwa kudanganya umri wa wachezaji. Naamini makosa hayajarudiwa.
 
Ngoja na sisi watukatie rufaa na vijeba vyetu!
waache kuweka mamluki, ni ujinga tu waafrika tunakuwa nao, ni heri timu itolewe mapema kwa kuwapa nafasi wachezaji wenye umri stahili, kuliko kuwa bingwa kwa kupanga mibabu iliyofoji umri!
lengo la mashindano ya vijana ni kusaidia nchi kuibua na kulea vipaji vya vijana ili wawe hazina hapo baadae ktk timu za taifa, huku kwetu mizee inadandia na ujinga wa mashirikisho ya soka, yanataka cosmetic sifa ilhali wakijua hawana kitu cha kujivunia kwa kuwa wali-cheat!
Mkuu mimi sijakuelewa
 
Mkuu Tanzania tulishakutwa na hilo sakata la vijeba, timu yetu ilifuzu fainali za vijana U17 zilizopita ikaondolewa kwa kudanganya umri wa wachezaji. Naamini makosa hayajarudiwa.
kwa maana hiyo unadhani vijeba hamna?
Ok, ni jambo jema!
sina nia mbaya na TFF na nchi yangu, Zaidi ya msisitizo juu ya mantiki mazima ya kombe husika, kuwa sio lengo kutwaa kombe, bali ni kuandaa timu bora za taifa. kufoji kuna wanyima nafasi chipukizi kujenga uwezo na kujiamini! unatoa nafasi kwa watu ambao in 5 - 10 years hawana tena mchango ktk timu ya taifa!
kama TFF wamepeleka watoto kweli tunawapa hongera na si lazima vijana warejee na kombe, wao waende kutuwakilisha na wakajifunze soka la kimataifa, @16-17 watakuwa na mengi ya kujifunza na safari ndio kwanza inaanza!
 
hj
Mkuu mimi sijakuelewa
hujanielewa kwamba nimeongea pumba au unahitaji ufafanuzi Zaidi:
kama unahitaji ufafanuzi:-
ni sawa tumefurahi kupata nafasi ya AFCON.
lkn isiwe nafasi hii na sisi tukaitumia vibaya kuweka wachezaji wazee wenye umri Zaidi ya miaka 17 (tukafoji ili tushinde)
lengo la mashindano ya under 17 na 21 ni kuzisaidia timu za taifa kuwekeza ktk vijana ambapo huku wakilelewa vema, huwa wanatengeneza timu bora kabisa za taifa!
kwa hiyo kwetu target kubwa isiwe kuchukua kombe kwa kuwapeleka kina mrisho ngasa (utani: kwa maana ya wachezaji wazuri lkn umri mkubwa) bali lengo letu liwe ni kupeleka vijana ili kuwajengea uwezo Zaidi hapo baadae!
 
Back
Top Bottom