Haya matatizo yangepungua sana kama wange ruhusu bange. nimesikiliza vijihotuba vya hao wanasiasa wenu sioni hata mmoja anaezungumzia mmea mtakatifu.....
Mkuu,ni watu wachache sana wanaojua ukweli kuhusu mmea huu,watu wengi wanaishi kama ng'ombe kwa kufuata kila wanachoambiwa bila kuhoji kama vile;
-Kuruhusu bangi katika baadhi ya maeneo na kukataza kwa maeneo mengine lakini wakati huohuo wanasema bangi ni haramu.
-Kuruhusu sigara/tumbaku na kukataza bangi lakini wakati huohuo wanatangaza kwamba matumizi sigara/tumbaku ni hatari kwa maisha.(taarifa za mpaka sasa zinaonesha bangi haijawahi kusababisha kifo hata kimoja,tumbaku husababisha vifo vingi sana kwa mwaka),lakini watu hawajui hili.
-Wanakataza watu wasilime bangi lakini wakati huohuo wanajua kwamba bangi ina uwezo wa kutibu cancer.
-Wanakataza bangi lakini wakati huohuo wanajua kwamba kenye heka moja ya bangi unapata zaidi ya lita 3500 za diesel ya kuendeshea mitambo ya viwandani,magari na mashine nyingine.
-Wanakataza bangi lakini wakati huohuo wanajua kwamba kwa kutumia bangi tunaweza kutengeneza karatasi zenye ubora mkubwa zaidi ya hizi za sasa.
Wanajua kwamba kuna matumizi zaidi ya 100 muhimu yanayotokana na bangi.Bangi ni hatari kwa biashara za wakubwa hasa mafuta na viwanda vya madawa.Watu wasiojua wanaishi kama mazuzu kwa kufuata sheria zilizowekwa na walafi wakubwa,watu hawana uwezo wa kuhoji wanakubali kila kitu kinachosemwa na wakubwa hawa.
Wakubwa hawa wanatunga sheria chafu na kuzipeleka/enforce UNO ili zitumike kwa mataifa mengine kama vile Tanzania nk.Na sisi tunapokea na kuzimeza kama kinda la ndege linavyokinga chakula kutoka kwa mdomo wa mama yake bila kujali kama anapewa sumu au la.
Kwa kweli inauma sana kuona karibu kila jambo muhimu kwenye dunia hii ni feki.Vita karibu zote ni feki,magonjwa mengi ni feki,kilimo kina mbegu feki,matumizi ya pesa nayo ni feki,vyakula ni feki,serikali ni feki,sheria ni feki,madawa ya hospitali ni feki,tafiti nyingi ni feki,Demokrasia ni feki,habari zinazotangazwa nazo ni feki,UNO ni feki,AU ni feki,UAE ni feki,uharamu wa bangi ni feki.Tuna kazi kubwa ya kubadilisha dunia hii.