RC Chalamila afafanua video inayo trend aliyosema "Kama hutaki kununua Gloves kajifungulie nyumbani"

RC Chalamila afafanua video inayo trend aliyosema "Kama hutaki kununua Gloves kajifungulie nyumbani"

  1. Kama huna nauli kwenda Kigamboni piga mbizi
  2. Watanzania watakula nyasi ili ndege ya Rais inunuliwe
  3. Kila mtu atauchukua mzigo wake
  4. Kama huna hela ya kuchangia huduma ya uzazi nenda kwa mumeo akuchane na mikasi
Hiyo ya kupiga mbizi ilikuwa ya anani?
 
  1. Kama huna nauli kwenda Kigamboni piga mbizi
  2. Watanzania watakula nyasi ili ndege ya Rais inunuliwe
  3. Kila mtu atauchukua mzigo wake
  4. Kama huna hela ya kuchangia huduma ya uzazi nenda kwa mumeo akuchane na mikasi
5. Kila mtu ale kulingana na urefu wa kamba yake.
 
Sasa kwanini upate pesa ya kuchezesha Ngoma ukose pesa ya kuchangia huduma ya kujifungua
We nae pumzika sasa! Eeh, usidhani watu wote wana nafuu ya maisha kama wewe mkuu..kuna watu masikini haswa, we shauri serikali itunge sheria iwe marufuku masikini kufanya mapenzi, mapenzi wafanye wenye uwezo kama wewe hata ukipewa mimba mumeo anajimudu
 
Nataka kumtetea chalamila lakini nashindwa, Samia msamee mchizi atakuwa Bado ana arosto ya gambe
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaaam, Albert Chalamila amewataka Watanzania kuacha kuingiza siasa katika masuala muhimu hasa katika afya kwani hazitasaidia badala yake zitawachelewesha na kusababisha kuwa na madhara makubwa zaidi kwa Wananchi.

Amesema hayo leo January 26,2025 wakati akitoa ufafanuzi baada ya taarifa iliyotolewa na chombo kimoja cha habari kuhusu kauli yake aliyomwambia Mwananchi mmoja wa Temeke kuwa kama hana vifaa vya kujifungulia kwamba aende akajifungulie nyumbani ambapo RC Chalamila amesema taarifa hiyo imenukuliwa kimakosa na lengo lake yeye ni kuhamasisha Wananchi kuwekeza kwenye afya huku ikisaidiana na Serikali nchini ambapo amesisitiza clip nzima ya yote aliyoyasema ipo ofisi ya RC na kutaka Watu wasisambaze clip ambayo imekatwakatwa ili kupotosha.

RC Chalamila amesisitiza umuhimu wa Watanzania wote kuachana na kauli chonganishi akisema hii inaweza kuleta athari kubwa kwa Tanzania kwa sasa akisema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi zaidi kwenye Sekta ya Afya ila pia muhimu kwa Wananchi kuwekeza kwenye masuala ya msingi na kuacha kuwekeza kwenye masuala yasiyofaa “Kuelekea uchaguzi upotoshaji ni mwingi”

My Take

Video hiyo hapo. Tuendelee kumsagia kunguni
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaaam, Albert Chalamila amewataka Watanzania kuacha kuingiza siasa katika masuala muhimu hasa katika afya kwani hazitasaidia badala yake zitawachelewesha na kusababisha kuwa na madhara makubwa zaidi kwa Wananchi.

Amesema hayo leo January 26,2025 wakati akitoa ufafanuzi baada ya taarifa iliyotolewa na chombo kimoja cha habari kuhusu kauli yake aliyomwambia Mwananchi mmoja wa Temeke kuwa kama hana vifaa vya kujifungulia kwamba aende akajifungulie nyumbani ambapo RC Chalamila amesema taarifa hiyo imenukuliwa kimakosa na lengo lake yeye ni kuhamasisha Wananchi kuwekeza kwenye afya huku ikisaidiana na Serikali nchini ambapo amesisitiza clip nzima ya yote aliyoyasema ipo ofisi ya RC na kutaka Watu wasisambaze clip ambayo imekatwakatwa ili kupotosha.

RC Chalamila amesisitiza umuhimu wa Watanzania wote kuachana na kauli chonganishi akisema hii inaweza kuleta athari kubwa kwa Tanzania kwa sasa akisema Serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imewekeza fedha nyingi zaidi kwenye Sekta ya Afya ila pia muhimu kwa Wananchi kuwekeza kwenye masuala ya msingi na kuacha kuwekeza kwenye masuala yasiyofaa “Kuelekea uchaguzi upotoshaji ni mwingi”
Anafanya siasa kwenye masuala serious? Anapwaya hapo
 
Back
Top Bottom