Pre GE2025 RC Chalamila ataka Tume Huru ya Uchaguzi iwe chini ya Rais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Heparin

JF-Expert Member
Joined
Sep 24, 2021
Posts
242
Reaction score
1,141
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila awashangaa wanaotaka Tume huru ya Uchaguzi isiwe chini ya Rais ama Rais asiwe na Mamlaka na Tume hiyo.

Hakuna tume itazaliwa Rais asiwe na mamlaka nayo, itakuwa siyo nchi. Mtu wa tume akikosea atawajibishwa na nani? Hakuna uhuru usio na mipaka, hata hapa Dar baadhi ya wazazi mmewapa watoro uhuru leo wamekuwa mashoga huru. Amesema RC Chalamila

Your browser is not able to display this video.
 
Rais akikosea anawajibishwa na nani??
 
mh! kwani hawawezi kuadabishwa na mwanasheria mkuu ama chombo cha sheria chochote..?
 
Muda wote imekuwa chini ya rais? Nini tumepata?
 
Watu kama Chalamila, maslahi yao ni kuongea kile kinachompendeza Mkuu wake kwa sababu tumbo lake ndiyo linategemea hapo na mdomo wake lazima uelekeze huko. Ni kama Mbwa, yaani "lap dog"
 
Uchawa unawafanya hata wasomi waonekane kama mbumbumbu wa mitaani
 
Hakuna jinsi. Watakao vimba wavimbe. Tume ni lazima iwe chini ya Raisi.

Susa Susa FC safari hii hawasusii tena Uchaguzi. Billioni 2.7 sio mchezo, lazima wa boogie tu.
 
Chalamila ni chizi haswa, hajui hata kama kuna mahakama
 
Safari bado ni ndefu sana kwakweli πŸ˜ƒ
 
Hajasema rais akiingilia tume na kuharibu uchaguzi nani atamuwajibisha. Kweli jamaa huyo amekuwa kama mtu asiye na ufahamu kabisa.
 
Chalamila naomba jibu nchi kama Kenya Tume ipo chini ya nani, usipojibu naomba rudi kwenu Iringa Dar imekushinda
 
Acha rais akienda nje aende na wasanii maana nchi ishakuwa ya kisanii tu

Ova
 
Na hiyo ndio demokrasia ya kweli tume ya uchaguzi haipaswi kuwa chini ya rais. La sivyo rais atakuwa hatoki madarakani kwa kura huru mpaka amalizr miaka 10.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…