Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
RC CHALAMILA ATIMIZA AHADI YA KUKUTANA NA WAFANYABIASHARA WA SIM 2000
-Awakutanisha DART, Manispaa ya Ubungo na Wafanyabishara wadogo.
-Aeleza dhamira ya Serikali kutekeleza mradi huo
-Asisitiza bado serikali itaendelea kujali na kuweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara wadogo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo julai 13,2024 amekutana na wafanyabishara wa Simu 2000 ikiwa ni ahadi aliyoitoa wiki iliyopita baada ya wafanyabiashara hao kufanya mgomo katika eneo hilo.
RC Chalamila akiwa katika eneo la kituo cha Simu 2000 amewakutanisha wafanyabiashara hao na wakala wa mabasi yaendayo kasi DART, na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ambapo mawasilisho ya utekelezaji wa mradi wa kujenga karakana kwa ajili ya mabasi ya mwendokasi na umuhimu wake kwa pande zote mbili Manispaa na DART yaliwasilishwa kwa uwazi mbele ya wafanyabiashara hao
Aidha RC Chalamila alitoa nafasi kwa wafanyabiashara hao kutoa maoni huku akiweka wazi dhamira ya serikali kutekeleza mradi huo ambao una masilahi mapana kwa umma na kuwahakikishia pamoja na kutekelezwa kwa mradi huo bado kuna sehemu ambayo wafanyabiashara hao watapatiwa ili kufanya biashara zao lakini pia katika kipindi chote cha kutekeleza mradi huo utaratibu utawekwa ili kutovuruga biashara zilizoko.
Vilevile RC Chalamila amesema hakuna serikali isiyojali wafanyabiashara bali inapotokea kuna mradi wenye masilahi mapana kwa umma lazima tupishe,pia sio vizuri kuwa na migomo ya mara kwa mara kama una maoni au ushauri wasilisha katika njia nzuri “wale wote waliotoa maoni leo yenye tija wakati wa kutekeleza mradi huo yatazingatiwa kwa umakini mkubwa”.Alisema Chalamila
Mwisho RC Chalamila ametoa rai kwa wakazi wa Mkoa huo kuilinda Dar es Salaam kwa nguvu zote Amani ikitoweka athari zake ni kubwa.
View: https://www.youtube.com/watch?v=ParVZCgSBAI
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema kuwa ni lazima wafanyabiashara wadogo (Wamachinga) waliopo Simu2000 waliodaiwa kugoma wakafahamu na kuelewa kuwa eneo walilopo ni la Serikali na ni lazima liendelezwe kwa manufaa ya Serikali na Wananchi.
"Wote lazima mfahamu kwamba hili eneo la Simu2000 ni eneo la serikali na ni lazima liendelezwe kwa manufaa ya serikali na wananchi, hii yote ni miradi ya serikali hata Kariakoo na Mwenge mnayoiona leo haikuwa hivo miaka ya nyuma lakini serikali imeendeleza maeneo hayo mpaka leo watu wanafurahia, mwanzo siku zote lazima utakuwa mgumu lakini serikali ina nia njema na wananchi wake" Albert Chalamila - Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam
Ameyasema hayo leo Jumamu Julai 13, 2024, siku ambayo aliwaahidi wafanyabiashara hao waliogoma siku ya Julai 8, 2024 na kufunga biashara zao na kuweka vizuizi vya kufunga barabara huku wakizuia magari kuingia na kutoka katika kituo cha daladala chanzo kikidaiwa ni kupinga uamuzi wa Manispaa ya Ubungo kukabidhi eneo wanalofanyia biashara kwa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kwa ajili ya kujenga karakana ya mabasi ya mwendokasi.
Itakumbukwa wafanyabiashara hao hawakuwa tayari kumsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo wakidai kuwa madai yao amshindwa kuyasikiliza kwa wakati, baada ya sintofahamu hiyo Chalamila alifika eneo hilo na kuwahasa wafungue biashara huku akiahidi kufanyia kazi madai hayo kwa kuketi na mamlaka nyingine na kuleta majawabu leo Julai 13, 2024,
"Wote lazima mfahamu kwamba hili eneo la Simu2000 ni eneo la serikali na ni lazima liendelezwe kwa manufaa ya serikali na wananchi, hii yote ni miradi ya serikali hata Kariakoo na Mwenge mnayoiona leo haikuwa hivo miaka ya nyuma lakini serikali imeendeleza maeneo hayo mpaka leo watu wanafurahia, mwanzo siku zote lazima utakuwa mgumu lakini serikali ina nia njema na wananchi wake" amesema Albert Chalamila
Hata hivyo Chalamila amewaonya wafanyabiashara hao kutorudia tena utaratibu wa kufunga barabara, ambapo amedai kwamba wakirudia kufanya hivyo hawatarudi kufanya biashara eneo hilo.
"Mkifanya tena mchezo kama mlioufanya juzi wa kufunga kituo cha mabasi cha Simu2000 nitawachukulia hatua wote kwasababu hiki kituo ni mali ya umma na sio yenu mngeweza kufunga maduka na biashara zenu mkaacha kituo kiendelee na shughuli zake lakini mkijaribu tena kufunga kituo mjue hamtorudi tena kwenye kituo cha simu 2000" amesema Albert Chalamila.
===============
CHALAMILA: ENEO LA SIMU2000 NI LA SERIKALI LAZIMA LIENDELEZWE
DAR ES SALAAM: Mkuu wa Mkoa, Albert Chalamila amesema lazima Wafanyabiashara Wadogo (Wamachinga) waliopo eneo la Simu2000 waliofanya mgoma na kuziba Barabara wafahamu kuwa eneo walilopo ni la Serikali na lazima liendelezwe kwa manufaa ya Nchi.
Akizungumzia mpango uliopo wa sehemu ya eneo hilo kukabidhiwa kwa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kwa ajili ya ujenzi wa karakana, jambo ambalo lilipingwa na baadhi ya Wamachinga waliofanya mgomo, Chalamila amesema “Hii yote ni miradi ya Serikali, hata Kariakoo na Mwenge mnayoiona leo haikuwa hivyo miaka ya nyuma.”
Amesema hayo leo Julai 13, 2024 baada ya baadhi ya Machinga kugoma na kufunga Stendi ya Daladala katika Kituo cha Simu2000, Julai 8, 2024.
CHALAMILA: HATUWEZI KUENDESHA MKOA UKIWA NA MIGOMO-MIKOMO
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewataka Wafanyabiashara kuheshimu mamlaka ya Serikali na ya Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza nao kuhusu mipango iliyopo kuhusu uendelezaji wa eneo la Simu2000, akiwakanya walioonesha kumpinga na kupinga mkakati huo.
Pia, ameonya tabia ya kufanya mgomo mara kwa mara kutoka kwa Wafanyabiashara akisisitiza sio njia sahihi ya kuendesha Mkoa, amesema hayo leo Julai 13, 2024 wakati akizungumza na Wafanyabiashara waliogoma na kufunga Stendi ya Daladala katika Kituo cha Simu2000, Julai 8, 2024.
CHALAMILA: CHEZEENI VIONGOZI WOTE ILA MSIGUSE HII KICHWA, NIPO LEVO NYINGINE YA MAAMUZI
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewaonya Wafanyabiashara waliofunga eneo la Stendi ya Daladala katika Kituo cha Simu2000, Julai 8, 2024, akisema bora wafunge biashara zao na sio kituo au Barabara.
Amesema “Kuna Watu mmepangana vilio, vimachozi, amekufinya mumeo unataka kuja kunililia mimi... chezeeni pote mnapoweza kuchezea, Viongozi wote chezeeni ila msiguse hii kichwa, nipo kwenye levo nyingine sana ya maamuzi.
Ameyasema hayo leo Jumamosi Julai 13, 2024 wakati wa kikao kati yake na Wafanyabiashara wa Simu2000.
-Awakutanisha DART, Manispaa ya Ubungo na Wafanyabishara wadogo.
-Aeleza dhamira ya Serikali kutekeleza mradi huo
-Asisitiza bado serikali itaendelea kujali na kuweka mazingira rafiki kwa wafanyabiashara wadogo
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe Albert Chalamila leo julai 13,2024 amekutana na wafanyabishara wa Simu 2000 ikiwa ni ahadi aliyoitoa wiki iliyopita baada ya wafanyabiashara hao kufanya mgomo katika eneo hilo.
RC Chalamila akiwa katika eneo la kituo cha Simu 2000 amewakutanisha wafanyabiashara hao na wakala wa mabasi yaendayo kasi DART, na Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo ambapo mawasilisho ya utekelezaji wa mradi wa kujenga karakana kwa ajili ya mabasi ya mwendokasi na umuhimu wake kwa pande zote mbili Manispaa na DART yaliwasilishwa kwa uwazi mbele ya wafanyabiashara hao
Aidha RC Chalamila alitoa nafasi kwa wafanyabiashara hao kutoa maoni huku akiweka wazi dhamira ya serikali kutekeleza mradi huo ambao una masilahi mapana kwa umma na kuwahakikishia pamoja na kutekelezwa kwa mradi huo bado kuna sehemu ambayo wafanyabiashara hao watapatiwa ili kufanya biashara zao lakini pia katika kipindi chote cha kutekeleza mradi huo utaratibu utawekwa ili kutovuruga biashara zilizoko.
Vilevile RC Chalamila amesema hakuna serikali isiyojali wafanyabiashara bali inapotokea kuna mradi wenye masilahi mapana kwa umma lazima tupishe,pia sio vizuri kuwa na migomo ya mara kwa mara kama una maoni au ushauri wasilisha katika njia nzuri “wale wote waliotoa maoni leo yenye tija wakati wa kutekeleza mradi huo yatazingatiwa kwa umakini mkubwa”.Alisema Chalamila
Mwisho RC Chalamila ametoa rai kwa wakazi wa Mkoa huo kuilinda Dar es Salaam kwa nguvu zote Amani ikitoweka athari zake ni kubwa.
View: https://www.youtube.com/watch?v=ParVZCgSBAI
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila amesema kuwa ni lazima wafanyabiashara wadogo (Wamachinga) waliopo Simu2000 waliodaiwa kugoma wakafahamu na kuelewa kuwa eneo walilopo ni la Serikali na ni lazima liendelezwe kwa manufaa ya Serikali na Wananchi.
Ameyasema hayo leo Jumamu Julai 13, 2024, siku ambayo aliwaahidi wafanyabiashara hao waliogoma siku ya Julai 8, 2024 na kufunga biashara zao na kuweka vizuizi vya kufunga barabara huku wakizuia magari kuingia na kutoka katika kituo cha daladala chanzo kikidaiwa ni kupinga uamuzi wa Manispaa ya Ubungo kukabidhi eneo wanalofanyia biashara kwa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kwa ajili ya kujenga karakana ya mabasi ya mwendokasi.
Itakumbukwa wafanyabiashara hao hawakuwa tayari kumsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Ubungo wakidai kuwa madai yao amshindwa kuyasikiliza kwa wakati, baada ya sintofahamu hiyo Chalamila alifika eneo hilo na kuwahasa wafungue biashara huku akiahidi kufanyia kazi madai hayo kwa kuketi na mamlaka nyingine na kuleta majawabu leo Julai 13, 2024,
"Wote lazima mfahamu kwamba hili eneo la Simu2000 ni eneo la serikali na ni lazima liendelezwe kwa manufaa ya serikali na wananchi, hii yote ni miradi ya serikali hata Kariakoo na Mwenge mnayoiona leo haikuwa hivo miaka ya nyuma lakini serikali imeendeleza maeneo hayo mpaka leo watu wanafurahia, mwanzo siku zote lazima utakuwa mgumu lakini serikali ina nia njema na wananchi wake" amesema Albert Chalamila
Hata hivyo Chalamila amewaonya wafanyabiashara hao kutorudia tena utaratibu wa kufunga barabara, ambapo amedai kwamba wakirudia kufanya hivyo hawatarudi kufanya biashara eneo hilo.
"Mkifanya tena mchezo kama mlioufanya juzi wa kufunga kituo cha mabasi cha Simu2000 nitawachukulia hatua wote kwasababu hiki kituo ni mali ya umma na sio yenu mngeweza kufunga maduka na biashara zenu mkaacha kituo kiendelee na shughuli zake lakini mkijaribu tena kufunga kituo mjue hamtorudi tena kwenye kituo cha simu 2000" amesema Albert Chalamila.
===============
CHALAMILA: ENEO LA SIMU2000 NI LA SERIKALI LAZIMA LIENDELEZWE
DAR ES SALAAM: Mkuu wa Mkoa, Albert Chalamila amesema lazima Wafanyabiashara Wadogo (Wamachinga) waliopo eneo la Simu2000 waliofanya mgoma na kuziba Barabara wafahamu kuwa eneo walilopo ni la Serikali na lazima liendelezwe kwa manufaa ya Nchi.
Akizungumzia mpango uliopo wa sehemu ya eneo hilo kukabidhiwa kwa Wakala wa Mabasi Yaendayo Haraka (DART) kwa ajili ya ujenzi wa karakana, jambo ambalo lilipingwa na baadhi ya Wamachinga waliofanya mgomo, Chalamila amesema “Hii yote ni miradi ya Serikali, hata Kariakoo na Mwenge mnayoiona leo haikuwa hivyo miaka ya nyuma.”
Amesema hayo leo Julai 13, 2024 baada ya baadhi ya Machinga kugoma na kufunga Stendi ya Daladala katika Kituo cha Simu2000, Julai 8, 2024.
CHALAMILA: HATUWEZI KUENDESHA MKOA UKIWA NA MIGOMO-MIKOMO
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewataka Wafanyabiashara kuheshimu mamlaka ya Serikali na ya Mkuu wa Mkoa wakati akizungumza nao kuhusu mipango iliyopo kuhusu uendelezaji wa eneo la Simu2000, akiwakanya walioonesha kumpinga na kupinga mkakati huo.
Pia, ameonya tabia ya kufanya mgomo mara kwa mara kutoka kwa Wafanyabiashara akisisitiza sio njia sahihi ya kuendesha Mkoa, amesema hayo leo Julai 13, 2024 wakati akizungumza na Wafanyabiashara waliogoma na kufunga Stendi ya Daladala katika Kituo cha Simu2000, Julai 8, 2024.
CHALAMILA: CHEZEENI VIONGOZI WOTE ILA MSIGUSE HII KICHWA, NIPO LEVO NYINGINE YA MAAMUZI
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila amewaonya Wafanyabiashara waliofunga eneo la Stendi ya Daladala katika Kituo cha Simu2000, Julai 8, 2024, akisema bora wafunge biashara zao na sio kituo au Barabara.
Amesema “Kuna Watu mmepangana vilio, vimachozi, amekufinya mumeo unataka kuja kunililia mimi... chezeeni pote mnapoweza kuchezea, Viongozi wote chezeeni ila msiguse hii kichwa, nipo kwenye levo nyingine sana ya maamuzi.
Ameyasema hayo leo Jumamosi Julai 13, 2024 wakati wa kikao kati yake na Wafanyabiashara wa Simu2000.