#COVID19 RC Dar: Kuvaa Barakoa kwenye Vyombo vya Usafiri na Vituo vya Mabasi ni lazima, sio hiari

#COVID19 RC Dar: Kuvaa Barakoa kwenye Vyombo vya Usafiri na Vituo vya Mabasi ni lazima, sio hiari

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema kuanzia sasa siyo hiari kuvaa barakoa bali ni lazima kwa watu wanaotumia usafiri wa umma au wanaokwenda au kuingia katika vituo vya mabasi.

Makalla ameeleza hayo, Jumatatu Agosti 2, 2021 wakati akizungumza na wanahabari kuhusu mwenendo wa uchukuaji wa tahadhari kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema wamefanya tathimini na kubaini kuna baadhi ya maeneo ikiwemo vyombo vya usafiri kuna ulegevu wa uchukuaji wa tahadhari.

Makalla ametoa msimamo huo, akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam, akisisitiza kuwa ugonjwa wa corona upo na wagonjwa wapo katika hospitali za Serikali na binafsi , lazima wananchi waendelee kuchukua tahadhari za kujikinga.

"Ukiingia kwenye gari, kivuko lazima uvae barakoa, hili ni moja ya sharti. Nimefanya survey ukienda Kivukoni Feri mtu anaingia na barakoa kwa sababu ya usimamizi akiwa ndani anaivua, akitaka kutoka anaiva tena," amesema Makalla.

"Tumepokea taarifa ya utekelezaji wa mwongozo wa Wizara ya Afya kuhusu kujikinga na corona kutoka kila wilaya tumebaini kuna ulegevu wa utekelezaji wa jambo hili. Sasa utekelezaji wa hiari haupo tena bali ni lazima ili kukabaliana na changamoto hii," amesema Makalla.

Makalla amesema wamiliki wa vyombo vya usafiri wa umma, vivuko lazima kuzingatia jambo hilo, akisema suala la kuchukua tahadhari ikiwemo kuvaa barakoa siyo hatua ya kuiridhisha mamalaka husika bali usalama wa mwananchi.
 
Haya matamko ya kila siku yasiishie kwenye daladala tu, huko masokoni, mashuleni, nyumba za ibada kote wavae barakoa kwa lazima.
 
Tatizo ugeugeu wa serikali ndio umesababisha watu kutokuwa makini na huu ugonjwa.

Kila achukulie covid vile anavyoona inafaa
 
huyu mkuu wa mkoa watu wanamdharau ama? kwa sababu hakuna anayevaa barako wala nini.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema kuanzia sasa siyo hiari kuvaa barakoa bali ni lazima kwa watu wanaotumia usafiri wa umma au wanaokwenda au kuingia katika vituo vya mabasi.

Makalla ameeleza hayo, Jumatatu Agosti 2, 2021 wakati akizungumza na wanahabari kuhusu mwenendo wa uchukuaji wa tahadhari kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema wamefanya tathimini na kubaini kuna baadhi ya maeneo ikiwemo vyombo vya usafiri kuna ulegevu wa uchukuaji wa tahadhari.

Makalla ametoa msimamo huo, akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam, akisisitiza kuwa ugonjwa wa corona upo na wagonjwa wapo katika hospitali za Serikali na binafsi , lazima wananchi waendelee kuchukua tahadhari za kujikinga.

"Ukiingia kwenye gari, kivuko lazima uvae barakoa, hili ni moja ya sharti. Nimefanya survey ukienda Kivukoni Feri mtu anaingia na barakoa kwa sababu ya usimamizi akiwa ndani anaivua, akitaka kutoka anaiva tena," amesema Makalla.

"Tumepokea taarifa ya utekelezaji wa mwongozo wa Wizara ya Afya kuhusu kujikinga na corona kutoka kila wilaya tumebaini kuna ulegevu wa utekelezaji wa jambo hili. Sasa utekelezaji wa hiari haupo tena bali ni lazima ili kukabaliana na changamoto hii," amesema Makalla.

Makalla amesema wamiliki wa vyombo vya usafiri wa umma, vivuko lazima kuzingatia jambo hilo, akisema suala la kuchukua tahadhari ikiwemo kuvaa barakoa siyo hatua ya kuiridhisha mamalaka husika bali usalama wa mwananchi.
Naanza kuona mkwamo.

RC anazungumza kuhusu uvaaji wa barakoa lakini hajawahi kutembelea vituo vya usafiri wa umma kuangalia adha wanazozipata abiria
 
Naanza kuona mkwamo.

RC anazungumza kuhusu uvaaji wa barakoa lakini hajawahi kutembelea vituo vya usafiri wa umma kuangalia adha wanazozipata abiria
Viongoz aina ya mafundi viatu
 
Haya matamko ya kila siku yasiishie kwenye daladala tu, huko masokoni, mashuleni, nyumba za ibada kote wavae barakoa kwa lazima.
Mkuu daladala bado zinajaza Kama kawaida na wanaovaa barakoa ni wachache sana.
Hapa napozungumza nina nusu saa gari zinapita zimejaa
 
Vinavyozumgumzwa na hali halisi ni tofauti kabisa....vituo vyote vya daladala, kwenye daladala zenyewe , mabasi etc wasiovaa barakoa Ni 98 asilimia..wananchi wavouchulia huu ugonjwa na matamko ya serikali haviendani kabisa..

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Huyu Makala amekuwa na matamko mengi ila utekelezwaji sifuri....alisema mabasi ya mkoani yaishie Mbezi na kupakia ila mbona bado yanapakia popote tu..........last week walitangaza level seats, ila ukiangalia mwendokasi zilivyofull .......atakuwa kama Makonda, matamko yasiyotekelezeka
 
Unavaa barakoa wakati konda anashika tiketi za wasafiri wote ndani ya basi anapofanya ukakuguzi kitu ambacho kinasabaza virusi kwa nji ya mikono.
Tujiangalie katika mambo sana vinginevyo kuvaa barakoa hakuna maana
 
Back
Top Bottom