#COVID19 RC Dar: Kuvaa Barakoa kwenye Vyombo vya Usafiri na Vituo vya Mabasi ni lazima, sio hiari

#COVID19 RC Dar: Kuvaa Barakoa kwenye Vyombo vya Usafiri na Vituo vya Mabasi ni lazima, sio hiari

Bila total lockdown huwezi kuidhibiti corona...

Bahati mbaya kwa Afrika huwezi fanya lockdown, raia watakufa njaa majumbani...
 
Huyu jiji limemshinda hana uwezo wa kuwaamuru watu jijini wasiendelee na mishentown zao
 
Yani makala amepuuzwa asipotumia askari na na watu wa vyombo vya umma kupigwa fine watu hawatafata utaratibu, Yani hapo wakipigwa fine konda hatakubali kuruhusu abiria asiye na barakoa na mask kupanda. Punda haendi bila mjeledi
Hili neno mjeledi linatumika sana mwambao wa pwani.
 
Wave ya kwanza watu ndio walikuwa serious na barakoa , "SANTAIZA" ,kunawa maji tiririka ila baada ya "MTU FURANI" aka JIKONO JANDAMA kuwaaminisha kwamba "KITU" kimeondoka na ni kama "MAFUA" tu basi wananchi wakaanza kuipotezea.

Kwenye madaladala hakuna cha barakoa wala level seat.
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema kuanzia sasa siyo hiari kuvaa barakoa bali ni lazima kwa watu wanaotumia usafiri wa umma au wanaokwenda au kuingia katika vituo vya mabasi.

Makalla ameeleza hayo, Jumatatu Agosti 2, 2021 wakati akizungumza na wanahabari kuhusu mwenendo wa uchukuaji wa tahadhari kwa wananchi wa mkoa wa Dar es Salaam.

Amesema wamefanya tathimini na kubaini kuna baadhi ya maeneo ikiwemo vyombo vya usafiri kuna ulegevu wa uchukuaji wa tahadhari.

Makalla ametoa msimamo huo, akiwa ameambatana na kamati ya ulinzi na usalama wa Mkoa wa Dar es Salaam, akisisitiza kuwa ugonjwa wa corona upo na wagonjwa wapo katika hospitali za Serikali na binafsi , lazima wananchi waendelee kuchukua tahadhari za kujikinga.

"Ukiingia kwenye gari, kivuko lazima uvae barakoa, hili ni moja ya sharti. Nimefanya survey ukienda Kivukoni Feri mtu anaingia na barakoa kwa sababu ya usimamizi akiwa ndani anaivua, akitaka kutoka anaiva tena," amesema Makalla.

"Tumepokea taarifa ya utekelezaji wa mwongozo wa Wizara ya Afya kuhusu kujikinga na corona kutoka kila wilaya tumebaini kuna ulegevu wa utekelezaji wa jambo hili. Sasa utekelezaji wa hiari haupo tena bali ni lazima ili kukabaliana na changamoto hii," amesema Makalla.

Makalla amesema wamiliki wa vyombo vya usafiri wa umma, vivuko lazima kuzingatia jambo hilo, akisema suala la kuchukua tahadhari ikiwemo kuvaa barakoa siyo hatua ya kuiridhisha mamalaka husika bali usalama wa mwananchi.
Matamko ni mengi kuliko data za kupima!!
Hii wizara ya afya na uongozi wake wote hawatufai! Misaada ya vifaa mmepokea lakini hatusikii vipimo vya kila wiki vinasemaje. Pia tume iliyoundwa kutathmini upokeaji wa chanjo haulioni hilo kuwa muhimu!
Hii ndio Tanzagiza kweli!!
 
Unaweza kumlazimisha punda kwenda mtoni,
Lakini huwezi kumlazimisha kunywa maji
 
Matamko ni mengi kuliko data za kupima!!
Hii wizara ya afya na uongozi wake wote hawatufai! Misaada ya vifaa mmepokea lakini hatusikii vipimo vya kila wiki vinasemaje. Pia tume iliyoundwa kutathmini upokeaji wa chanjo haulioni hilo kuwa muhimu!
Hii ndio Tanzagiza kweli!
Hizo data za Kila wiki zitakusaidia Nini? Kama unazihitaji Sana nenda hospital watakupa.
 
Huyu RC ni mzigo tu,anatoa maagizo halafu yuko ofisini kukuna makalio tu.
 
Nimeona madalada yamejaza na watu kusimama with no barakoas at all
Huyu Makala hajapanda hata Bajaj halafu anatudanganya kuwa kafanya utafiti, alipanda daladala la kwenda Mbagara skaona hayo anayoyasema?

Huyu jamaa ni pumba sana.
 
Dar kuna wagonjwa wangapi wa corona ambao wanaweza kuhalalisha huo ulazima ? Kama mnataka watu wapambane na corona inabidi washirikishwe kujua ukubwa wa tatizo !
 
Huyu Makala hajapanda hata Bajaj halafu anatudanganya kuwa kafanya utafiti, alipanda daladala la kwenda Mbagara skaona hayo anayoyasema?

Huyu jamaa ni pumba sana.
Makala ukuu wa mkoa wa Dar umemushinda full matamko ila utekelezaji sifuri ana kwama wapi aisee, na ana vyombo chini yake vingi yeye ni matamko tu hadi bashite mzee wa fa fa fa kamshinda mbali
 
Makala ukuu wa mkoa wa Dar umemushinda full matamko ila utekelezaji sifuri ana kwama wapi aisee, na ana vyombo chini yake vingi yeye ni matamko tu hadi bashite mzee wa fa fa fa kamshinda mbali
Yaani afadhali hata Bashite alikuwa active sana, ila huyu Makala hafai kuwa RC popote.

Madam atengue tu ukuu wa Makala
 
Back
Top Bottom