RC MAKALLA: UKAME NDIO CHANZO CHA UPUNGUFU WA MAJI.
- Asema mvua za Vuli zimechelewa ambazo huanza mwezi October Na upungufu wa maji ni lita 70 Milioni kwa siku.
- Apongeza operesheni ya wachepushaji maji imeongeza kiasi lakini upungufu Upo mpaka mvua zinyeshe.
- Awataka Wananchi kutumia maji vizuri na kutunza vyanzo vya maji.
- Kilichotolea Ni mabadiliko ya Tabia Nchi.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla amesema Mgao wa maji Jijini humo utaendelea kuwepo mpaka pale Mvua zitakapoanza kunyesha na kuongeza kina Cha maji kwenye vyanzo vya maji Ruvu Chini na Ruvu Juu ambavyo kwa Sasa vina upungufu wa maji.
RC Makalla amesema hayo wakati wa ziara ya kutembelea Vyanzo vya Maji vya Ruvu Juu na Ruvu Chini akiambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Watendaji wa DAWASA iliyolenga kujionea na kujiridhisha Hali ya Maji kwenye vyanzo hivyo.
Akizungumza katika ziara hiyo RC Makalla amesema baada ya Maelekezo yaliyotolewa na Rais Samia Suluhu Hassan na Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa yamesaidia uwepo wa Ongezeko la Lita Milioni 200 kutoka Lita Milioni 65 na kufanya upungufu wa Lita Milioni 70 kwa Ruvu Chini.
Aidha RC Makalla amesema upande wa Ruvu Juu Hali sio mbaya Sana Kutokana na uzalishaji wa maji kuendelea kuwa Lita Milioni 196 kwa siku.
Kutoka na Hilo RC Makalla ametoa wito kwa Wananchi kutumia Maji vizuri na kuendelea kutunza vyanzo vya maji huku akipongeza jitiada zinazofanywa na Wizara ya Maji na DAWASA.
Hata hivyo RC Makalla amesema mahitaji ya Maji kwa Mkoa wa Dar es salaam kwa siku ni Lita Milioni 540 na uzalishaji Lita Milioni 520 na asilimia kubwa ya Maji hayo yanategemea kunyesha kwa mvua lakini Kukosekana kwa mvua za Vuli kwa takribani miezi miwili Sasa imesababisha upungufu wa maji.
Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu DAWASA Mhandisi Cyprian Luhemeja amesema Mamlaka hiyo inaendelea kufanya kila jitiada kuhakikisha kila Mwananchi anapata Huda ya Maji licha ya kuwepo kwa Mgao.
Kwa mujibu wa DAWASA, Mtambo wa Maji Ruvu Juu unazalisha Lita Milioni 196 kwa siku na Mtambo wa Maji Ruvu Chini unazalisha Lita Milioni 270 kwa siku lakini Kutokana na upungufu wa maji kwa Sasa