RC Makalla: Ng'ombe wamesababisha uhaba wa maji

RC Makalla: Ng'ombe wamesababisha uhaba wa maji

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema mto Ruvu umacha kutiririsha maji kutokana na wananchi wa Mvuha, Dutumi na Kisaki Mkoani Morogoro kiwa na ng'ombe wengi.

Makalla na timu yake waliufuatilia mto Ruvu ili kujua sababu ya kutopitisha maji ambapo wamegundua shughuli za kibanadamu zinazofanywa katika vyanzo vya mto huo mkoani Morogoro, vimeathiri suala utiririshaji maji.

Ametoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo kuhama maeneo yaliyokatazwa. Amesema suala la ukosefu wa maji ni mabadiliko ya tabia nchi ambayo pia huchangiwa na shughuli za binadamu.
View attachment 2407677
Huo ni uongooo
 
Mkoa umemshinda, malori katikati ya mji, wamachinga kila kona, bajaji, bodaboda, changu doa, walevi, wezi wamefurika kariakoo, yeye anaenda kurukia morogoroooooo, angehimiza vijana wengi kulima na kuacha uchuuzi wa kuchora watu barabarani rangi za kucha, mimea ingestawi na mvua zingenyesha
 
So what are their coping strategies….sio kulalamika tu
Mkuu jitahidi kufuatilia mjadala kuliko kuonyesha umekurupuka ,mawazo mengi including water desalination (this need tanesco to up their game),man made water dams hasa kuzunguka miji mikubwa, tuyatumie vema maji ya hizi 3 big lakes tulizopewa na Muumba, DAWASA wakiweza to plug all water leaks, tutaokoa more than 30%ya maji, maji mengi yanapotea kwenye hizi distribution systems zao
 
Kuna kazi zingine zinahitaji wataalam sio akina na makalla. So nini kifanyike
 
Mkuu jitahidi kufuatilia mjadala kuliko kuonyesha umekurupuka ,mawazo mengi including water desalination (this need tanesco to up their game),man made water dams hasa kuzunguka miji mikubwa, tuyatumie vema maji ya hizi 3 big lakes tulizopewa na Muumba, DAWASA wakiweza to plug all water leaks, tutaokoa more than 30%ya maji, maji mengi yanapotea kwenye hizi distribution systems zao
Sasa kama mwanza hamna maji unategemea hawa wataalam wetu
 
Ng'ombe haziwezi kukausha maji. Maji hayawezi potea, ukiyanywa utayakajoa na yatarudi kule kule kwenye chanzo chake.

Kinachoathiri mzunguko wa maji ni ukataji wa miti uliopindukia na kusababisha mzunguko wa maji(water cycle) kupungua sana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyu Mzee mm nilimkataa tangu alipoteuliwa nikawa naomba turudishiwe Makonda...huyu kwakweli anafuga tu Tumbo ofsini kwake
 
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Amos Makalla amesema mto Ruvu umacha kutiririsha maji kutokana na wananchi wa Mvuha, Dutumi na Kisaki Mkoani Morogoro kiwa na ng'ombe wengi.

Makalla na timu yake waliufuatilia mto Ruvu ili kujua sababu ya kutopitisha maji ambapo wamegundua shughuli za kibanadamu zinazofanywa katika vyanzo vya mto huo mkoani Morogoro, vimeathiri suala utiririshaji maji.

Ametoa wito kwa wakazi wa maeneo hayo kuhama maeneo yaliyokatazwa. Amesema suala la ukosefu wa maji ni mabadiliko ya tabia nchi ambayo pia huchangiwa na shughuli za binadamu.
View attachment 2407677
Kuwa na N'gombe wengi ni tatizo kweli?....Makala anachekesha sana....uongozi sio lele mama aisee
Halafu kwa mambo kama haya tunaambiana anaupiga mwingi...very strange..huyu RC ni reflection ya utawala uliopo...inasikitisha sana.
 
Yaani Binadamu walivyo wabaguzi,au kwasababu ng'ombe hawasemi,Mungu aliuumba maji kwa ajili ya viumbe wote,binadamu alipendelewa Utashi..
Nilitegemea utashi wa mwanadamu angekunywa maji ya mabombani,halafu mifugo wanywe mtonibna mabwawa,kama mmeshindwa kutatua changamoto ya Maji kwa watu wa Dar es Salaam msilete visingizio kwa viumbe wengine wenye haki ya kutumia maji,
 
Back
Top Bottom