RC Makonda aagiza Wazee na Viongozi wa Dini kutopanga foleni kwenye ofisi za Umma

RC Makonda aagiza Wazee na Viongozi wa Dini kutopanga foleni kwenye ofisi za Umma

Hapana, hii haikubaliki kabisa,
Huku ni kuchochea vurugu katika utoaji wa huduma katika ofisi za umma, hii nchi sio watu wote wana dini au wanaziheshimu hizi dini.
Amesema viongozi wa dini na wazee kuanzia miaka 60,
Hao wasiokua na dini,watakua kwenye kundi la wazee.
 
Kiustaarabu kuna sehemu wazee na wajawazito hua wanapishwa. Viongozi wa dini hapana wana u special gani?
 
Wakuu kumekucha salama?

Huko Arusha Mkuu wa Mkoa huo Paul Makonda ameagiza kupewa kipaumbele kwa Viongozi wa dini na Wazee wote wa Mkoa wa Arusha pale watakapokuwa kwenye Ofisi zote za Umma Mkoani humo kwa ajili ya kutafuta huduma.

Mbele ya waumini wa Msikiti Mkuu wa Bondeni Jijini Arusha mwisho wa wiki, Ijumaa Oktoba 25, 2024, Makonda alisema: "Nawaomba viongozi wote wa Serikali hakuna kiongozi wa dini wala mzee wa Mkoa wa Arusha anayestahili kapanga foleni kwenye ofisi yoyote ya Umma anapotafuta huduma, Wazee wa miaka 60 wao wakifika wanaenda moja kwa moja kwenye ofisi, haya ni maagizo yangu"
Soma: RC Makonda aandaa hafla ya Wakuu wa Taasisi za Umma na Wafanyabiashara Arusha
Kuamini/kuwa na dini na kutokuwa na dini ni uamuzi wa mtu , lakini pia wajinga ahuzeeka, sasa mtu anaweza kujiulizaa, kijana anaamka saa kumi alfajiri kuwahi ardhi asajili Deedpoll ili aende nayo kwenye interview alafu anakuja kijana ambaye alikuwa mjinga sasa amezeeka , amelala kilabuni aje saa nne nimpishe na wakati mimi nawahi document ya kupeleka kwenye ajira?

Basi nafikiri sasa , wanasiasa na misafara yao ipishe wazee.
 
Back
Top Bottom