#COVID19 RC Mtaka: Hali si shwari Dodoma. Wananchi waendelee kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona

#COVID19 RC Mtaka: Hali si shwari Dodoma. Wananchi waendelee kuchukua tahadhari dhidi ya Virusi vya Corona

Miss Zomboko

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2014
Posts
4,599
Reaction score
9,532
Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Anthony Mtaka amewataka wakazi wa Dodoma kuchukua hatua za tahadhari dhidi ya ugonjwa wa corona kwa sababu hali si nzuri mkoani humo.

Ameyasema hayo leo Jumanne Agosti 3, 2021 wakati akizungumza na askari wa usalama wa barabarani na viongozi wa masoko wa mkoa wa Dodoma.

Amewataka askari hao, viongozi wa masoko na wafanyabiashara kuhakikisha wanachukua hatua za kujikinga katika maeneo yao kwa kuvaa barakoa na kunawa maji tiririka na sabuni au kutumia vitakasa mikono.

Pia amewataka askari wa usalama wa barabarani kuhakikisha watu wote wanakaa kwenye viti (level seat) kwenye daladala na bajaji na kwenye bodaboda kuhakikisha hawabebi abiria zaidi ya mmoja

Mwananchi
 
Mh.Mtakachiganga yuko sahihi....

COVID is really....

Kwa wasioguswa wanaona kama "movie" vile.....

Tuchukue tahadhari jama....

#TujitokezeTukachanjwe
#ChanjoNiBoraKulikoTiba
#NchiKwanza
 
Mtaka huyu huyu aliyekuwa kwenye uzinduzi wa duka na kina Baba levo ivi juzi?

Huu ni mwendelezo wa maigizo baada ya kuchukua mpunga wa mabeberu.

Mwanza kelele zilikuwa nyingi ila ni tofauti kabisa na kile tunachokiona/ uhalisia
 
Mtaka huyu huyu aliyekuwa kwenye uzinduzi wa duka na kina Baba levo ivi juzi?

Huu ni mwendelezo wa maigizo baada ya kuchukua mpunga wa mabeberu.

Mwanza kelele zilikuwa nyingi ila ni tofauti kabisa na kile tunachokiona/ uhalisia
Kwa hiyo wale wagonjwa waliojazana mahospitalini huku puani wana mipira ya gesi nao pia wanaigiza baada ya kuchukua huo "ubweche" wa mabeberu?!!

#TujitokezeniTukachanjwe
 
Jamani, tuliaminishwa kuwa Mungu yu pamoja nasi. sasa imekuaje? Katukimibia? Jiwe huko uliko hili ni swali la nyongeza kwenye hukumu yako.
 
wagonjwa wa,
1.KISUKARI
2.PRESHA
3.MOYO
4.SARATANI
5.UKIMWI
6.TB
wagonjwa wa maradhi hayo wanapaswa wachue tahadhari sana maana Corona inatumaliza sana.
Jana kuna jamaa yangu "saidia fundi "amenipigia simu akinieleza kuwa sasa ni siku ya 5 hasikii harufu yoyote ,hasikii ladha ya chakula na ana mafua makali....nikamueleze aende hospitali...akanijibu huku akicheka kuwa CORONA haiwapati "malofa" daah😲

Naye ni mfuasi kindakindaki wa askofu Gwajima.....

#TujitokezeniTukachanjwe
 
Duuh....

Hatari mno....

#TujitokezeniTukanjwe
Kwa kweli nimeogopa mkuu.
Serikali iseme tu ukweli nini kinaendelea ili watu waone umuhimu wa kuchukua hatua za kujilinda.
I've never seen this in my life.

Ilibidi nipaki mahali kuna kituo cha bodaboda niwaulize hii situation nnayoiona ilikuwepo kabla?Wakanijibu
"jomba hapana haikuwa hivi,huko mjini kuna tatizo na saa hizi wewe umepita hapa asubuhi hii,ungekaa na sisi ujionee hali inavyokuwa kuanzia saa kumi jioni gari zenye miili zinazopita hapa!huko mjini kuna tatizo kubwa jombaa!!".

Serikali semeni ukweli msifiche data,mnachangia watu kupuuzia.
 
Kwa kweli nimeogopa mkuu.
Serikali iseme tu ukweli nini kinaendelea ili watu waone umuhimu wa kuchukua hatua za kujilinda.
I've never seen this in my life.Ilibidi nipaki mahali kuna kituo cha bodaboda niwaulize hii situation nnayoiona ilikuwepo kabla?Wakanijibu "jomba hapana haikuwa hivi,huko mjini kuna tatizo na saa hizi wewe umepita hapa asubuhi hii,ungekaa na sisi ujionee hali inavyokuwa kuanzia saa kumi jioni gari zenye miili zinazopita hapa!huko mjini kuna tatizo kubwa jombaa!!".
Serikali semeni ukweli msifiche data,mnachangia watu kupuuzia.
It's havoc....

#TujitokezeniTukachanjwe
 
Bado tupo kwenye hizi mbio🤣👇
IMG_20210803_131435.png
 
Maigizo yanaendelea.

Tumeingia kwenye kumi na nane za mabeberu!

Chezea mpunga wewe!!
Kachanje chanjo we mzee.....

Mtapotosha mpaka lini ?!!

Hivi wewe huna jamaa ,ndugu ,jirani aliyeko katika "gesi hospitalini"?!!

Hujampoteza yeyote?!!
Unaishi kisiwani pekee?

#TujitokezeniKuchanjwaJ&J
 
Kwa kweli nimeogopa mkuu.
Serikali iseme tu ukweli nini kinaendelea ili watu waone umuhimu wa kuchukua hatua za kujilinda.
I've never seen this in my life.Ilibidi nipaki mahali kuna kituo cha bodaboda niwaulize hii situation nnayoiona ilikuwepo kabla?Wakanijibu "jomba hapana haikuwa hivi,huko mjini kuna tatizo na saa hizi wewe umepita hapa asubuhi hii,ungekaa na sisi ujionee hali inavyokuwa kuanzia saa kumi jioni gari zenye miili zinazopita hapa!huko mjini kuna tatizo kubwa jombaa!!".
Serikali semeni ukweli msifiche data,mnachangia watu kupuuzia.
Dalali la machanjo kazini. Acha propaganda za kitoto wewe!!

Kwahiyo ulipaki gari ukaanza kuangalia majeneza!??

Ulipoyahesabu ulibaini yako mangapi?
 
Back
Top Bottom