RC Robert Gabriel awachana wanawake wa Mwanza! Awataka wajifunze kuoga na kupulizia manukato

RC Robert Gabriel awachana wanawake wa Mwanza! Awataka wajifunze kuoga na kupulizia manukato

Hayo kayasema kama RC..., au kama Mdau / Stakeholder

Kwa nafasi yake kama mdau / mshauri hakuna neno ila sio kwa Kofia yake ya u-RC
 
Nchi tamu Sana hii,
By the way huyu jamaa ni mpendwa wa mwendazake ndio maana alipewa Geita na Chato kwa pamoja usishangae alikuwa akimaanisha maushungi nasio wasukuma
 
Huyo RC mjinga sana mambo ya wanawake aache wanawake wafunzane wenyewe

Siku hizi hata semina za wanawake nyingi makanisani hawaalikwi viongozi wa dini wanaume enzi za ohh kutakuwa na semina ya wanawake halafu Baba mchungaji mwanaume atafundisha hazipo tena sehemu nyingi

Mwanaume mzima na mambo ya mwanamke aweje wapi na wapi wapishe wanawake wafunzane wenyewe

Mkuu wa mkoa hayo ni mambo ya kitchen party aachie wanawake wanajielewa na wanayajua

Yeye kajuaje kama hawapaki perfume ? Nakala ya hili swali imfikie mkewe
 
Nchi tamu Sana hii,
By the way huyu jamaa ni mpendwa wa mwendazake ndio maana alipewa Geita na Chato kwa pamoja usishangae alikuwa akimaanisha maushungi nasio wasukuma
Nani alimteua yeye kuwa RC wa Mwanza?
 
Daah aisee mbona kama ana ugomvi nao
Labda mkewe hataki kupaka perfume waandishi mtafuteni mkewe mumhoji kama huwa anapala au la na je umeme huwa anamletea hizo perfume maana linaonyesha anazijua hadi bei perfume za wanawake
 
Duh!

Amejuaje hawapaki manukato?
Halafu hadi perfume za wanawake anazijua na bei zake kayajulia wapi hayo? Kuwa perfume nzuri ziko aina hii na hii na bei zake ziko hii na hii ya bei rahisi ni hii

Hiyo tuition alipata wapi?

Mke wa Mkuu wa mkoa wa Mwanza popote ulio njoo ujibu hili swali.Mwalimu wake wa mambo ya perfume za wanawake ni nani ? MBANE AKWAMBIE

Akigoma Mwambie Mama Suluhu Hassan amuulize
 
Rahisi sana [ingawa huwezi kusema ni wote]!

Kama mfumo wako wa unusaji haujaharibika, ukipishana na mtu ambaye anatoa harufu au ukikaa naye karibu, utaisikia tu harufu, iwe ni mbaya au nzuri.
Kwahiyo anapishana na Wanawake tu?

Hii ni dharau kwa wasukuma.
 
Back
Top Bottom