Uchaguzi 2020 RC wa Mwanza, John Mongela avunja Mwiko wa Kampeni Kwa Kuongea Ukweli Bayana!, "Tukimpa Mitano Tena, JPM Kuigeuza Tanzania Nchi ya Maziwa na Asali"

Uchaguzi 2020 RC wa Mwanza, John Mongela avunja Mwiko wa Kampeni Kwa Kuongea Ukweli Bayana!, "Tukimpa Mitano Tena, JPM Kuigeuza Tanzania Nchi ya Maziwa na Asali"

Pascal Mayalla

Platinum Member
Joined
Sep 22, 2008
Posts
53,857
Reaction score
121,995
Wanabodi,

Kwanza sikiliza hii



Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongela, ni moja wa Ma RC very bold katika kuusema ukweli bayana!, leo amevunja mwiko wa ukimya kwa viongozi wa serikali kutompigia kampeni zozote za kisiasa kwa mgombea yoyote, kwasababu hawa ni viongozi wa kiutendaji, lakini RC John Mongela, amevunja ukimya wa kumhusu JPM, kwa kuusema ukweli wa moyo wake kuwa bila Dr. John Pombe Joseph Magufuli, Tanzania, tusingefika hapa tulipo!, huo ndio ukweli wa mambo.

Mongela amesisitiza na hapa nina mnukuu, "Sisi ni Watanzania, lazima tuwe wazalendo, kwenye mambo ya msingi, hatuwezi kuwa na aibu kusema, tunasemea nchi yetu, tunasemea mustakabali wa kizazi chetu na vizazi vingine vijavyo, wazee waliotangulia walitimiza wajibu wao, na sasa tumepata kiongozi mzalendo mahiri, ambaye amejitoa sadaka kwa ajili ya nchi yetu, tuendelee kumuombea, lakini tarehe 28 October, mimi nikiwa kama kiongozi, niwaombeni tutoke, tukapige kura, ili Mhe Dr. John Pombe Joseph Magufuli, kama miaka mitano ilikuwa hivi, tukimpa tena miaka mitano mingine, itakuwaje?, na walioona kitabu cha ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, na mimi kwa nafasi yangu ndio mratibu na msimamizi mkuu wa utekelezaji wa ilani kwenye mikoa, tunakokwenda ni nchi ya maziwa na asali, tumuombee rais wetu, tumuunge mkono, tukapige kura, ili twende kwenye mafanikio makubwa ya kiuchumi na kijamii!.

Akiunga mkono hoja, mwandishi wa makala hii, alisisitiza, umuhimu wa waandishi wa habari na vyombo vya habari, kutoshabikia vyama wala wagombea, ila amesisitiza, kama tunataka maendeleo ya kweli, then, tunajua ni chama gani kinaweza kutuletea maendeleo ya kweli na sio ahadi, na ni mgombea gani anaweza kutuletea maendeleo ya kweli, hivyo tarehe 28, Watanzania, Tusifanye Makosa!.

Paskali
 
UPUUZI MTUPU!






Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongela, amevunja mwiko wa ukimya kwa viongozi wa serikali kutompigia kampeni zozote za kisiasa kwa mgombea yoyote, kwa kuvunja ukimya, kumhusu JPM, asema bila Dr. John Pombe Joseph Magufuli, Tanzania, Tusingefika hapa tulipo!, huo ndio ukweli wa mambo. "Sisi ni Watanzania, lazima tuwe wazalendo, kwenye mambo ya msingi, hatuwezi kuwa na aibu kusema, tunasemea nchi yetu, tunasemea mustakabali wa kizazi chetu na vizazi vingine vijavyo, wazee waliotangulia walitimiza wajibu wao, na sasa tumepata kiongozi mzalendo mahiri, ambaye amejitoa sadaka kwa ajili ya nchi yetu, tuendelee kumuombea, lakini tarehe 28 October, mimi nikiwa kama kiongozi, niwaombeni tutoke, tukapige kura, ili Mhe Dr. John Pombe Joseph Magufuli, kama miaka mitano ilikuwa hivi, tukimpa tena miaka mitano mingine, itakuwaje?, na walioona kitabu cha ilani ya uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, na mimi kwa nafasi yangu ndio mratibu na msimamizi mkuu wa utekelezaji wa ilani kwenye mikoa, tunakokwenda ni nchi ya maziwa na asali, tumuombee rais wetu, tumuunge mkono, tukapige kura, ili twende kwenye mafanikio makubwa ya kiuchumi na kijamii!.

Akiunga mkono hoja, mwandishi wa makala hii, alisisitiza, umuhimu wa waandishi wa habari na vyombo vya habari, kutoshabikia vyama wala wagombea, ila amesisitiza, kama tunataka maendeleo ya kweli, then, tunajua ni chama gani kinaweza kutuletea maendeleo, na ni mgombea gani anaweza kutuletea maendeleo ya kweli, hivyo tarehe 28, Watanzania, Tusifanye Makosa!.

Paskali
 
Emb potelea mbali huko mpuuzi wewe! Nilikuwa nakuona una akili kumbe ukabila umekujaa. Jinga zima wewe!
Ulitaka aambatane na yule bwana wa risasi kumi na sita kiunoni?

CHADEMA mnakwama wapi ? Mmekuwa wahubiri wazuri sana wa democracy, lakini mtu mmoja akitofautiana na ninyi kimsimamo mnamshambulia

Kwani huyu pascal huwa unamlisha hadi ifikie kipindi umpagie awe na mgombea yupi?

Pambaneni na dubwana lenu lisilouzika,baada ya uchaguzi hilo ubeligiji
 
Hawa wakuu wa Mikoa wanao teuliwa kisiasa na Mkuu wa Nchi unataka tuwaamini wanacho sema !?.Hawa hawa walioapa kutii Mamlaka za teuzi?

Hainiingii Akilini kabisa..
 
Umekuwa kada haswa, hakika nyakati hubadilika, this time wakikunyima hata u DAS watapata dhambi, huo uongo wa maziwa na asali nimeusikia zamani sana, nadhani CCM wana tatizo la kufikiri, wamechoka hawawezi hata kufikiria uongo mpya, wanarudia ule ule miaka yote.
 
Back
Top Bottom