RC wa Tabora, Paul Chacha awakabidhi wachezaji wa Tabora United Tsh. Milioni 50 kwa kusalia katika Ligi Kuu

RC wa Tabora, Paul Chacha awakabidhi wachezaji wa Tabora United Tsh. Milioni 50 kwa kusalia katika Ligi Kuu

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
WhatsApp Image 2024-06-20 at 14.49.30_d273161f.jpg
Baada ya kufanikiwa kusalia kwenye NBC Premier League, hatimaye Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amewakabidhi wachezaji wa Tabora United, kitita cha Shilingi milioni 50 aliyowaahidi endapo wangefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu Bara.

Tabora United imesalia NBC Premier League baada ya kuifunga Biashara United ya Mara, kwa jumla ya magoli 2-1 kwenye michezo yote miwili ya mtoano (play offs).
WhatsApp Image 2024-06-20 at 14.49.31_151d4adc.jpg
Msimamizi wa timu hiyo ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richald Abwao amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Tabora na mashabiki wao kuwa msimu ujao wanakwenda kufanya makubwa zaidi kulingana na changamoto walizopitia sasa wanakwenda kufanyia masahihisho na kuja kivingine nyuki wa Tabora.

Aidha, Abwao ameeleza "Msimu ujao hawaendi kushiriki bali wanaenda kuonesha upinzani kwa kila timu itakayo kuja mbele yao jukumu ni moja kushinda ndilo jukumu lililo mbele yetu."
 
Baada ya kufanikiwa kusalia kwenye NBC Premier League, hatimaye Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amewakabidhi wachezaji wa Tabora United, kitita cha Shilingi milioni 50 aliyowaahidi endapo wangefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu Bara.

Tabora United imesalia NBC Premier League baada ya kuifunga Biashara United ya Mara, kwa jumla ya magoli 2-1 kwenye michezo yote miwili ya mtoano (play offs).
Msimamizi wa timu hiyo ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richald Abwao amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Tabora na mashabiki wao kuwa msimu ujao wanakwenda kufanya makubwa zaidi kulingana na changamoto walizopitia sasa wanakwenda kufanyia masahihisho na kuja kivingine nyuki wa Tabora.

Aidha, Abwao ameeleza "Msimu ujao hawaendi kushiriki bali wanaenda kuonesha upinzani kwa kila timu itakayo kuja mbele yao jukumu ni moja kushinda ndilo jukumu lililo mbele yetu."
Matumizi mabaya ya hela
 
Hizi hela ni za kwake au za halmashauri?
RC anaweza kukusanya kusanya kwa wadau mfano wafanyabiashara kadhaa ndani ya mkoa. Kuna matajajiri wakiombwa hela na mkuu wa mkoa kwao ni sifa chapu wanatoa!
 
Bwana Afande hapo meza kuu anaangalia hayo maburungutu ya pesa Kwa hamuu mnoo,,jicho la matamanio haswaa
 
Baada ya kufanikiwa kusalia kwenye NBC Premier League, hatimaye Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amewakabidhi wachezaji wa Tabora United, kitita cha Shilingi milioni 50 aliyowaahidi endapo wangefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu Bara.

Tabora United imesalia NBC Premier League baada ya kuifunga Biashara United ya Mara, kwa jumla ya magoli 2-1 kwenye michezo yote miwili ya mtoano (play offs).
Msimamizi wa timu hiyo ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richald Abwao amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Tabora na mashabiki wao kuwa msimu ujao wanakwenda kufanya makubwa zaidi kulingana na changamoto walizopitia sasa wanakwenda kufanyia masahihisho na kuja kivingine nyuki wa Tabora.

Aidha, Abwao ameeleza "Msimu ujao hawaendi kushiriki bali wanaenda kuonesha upinzani kwa kila timu itakayo kuja mbele yao jukumu ni moja kushinda ndilo jukumu lililo mbele yetu."
Hongera sana kwa motisha, lkn Mhe RC ulisaliti vijana wa Nyumbani kwenu Mara wakapigwa mawe na marungu wakafungwa kwa mbwembwe na bado umetoa milioni 50 kwao. Nyumbani ni nyumbani tu ndugu zako wanakuchora siku ukienda kule kwenu andaa majihu.
 
Baada ya kufanikiwa kusalia kwenye NBC Premier League, hatimaye Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Paul Chacha amewakabidhi wachezaji wa Tabora United, kitita cha Shilingi milioni 50 aliyowaahidi endapo wangefanikiwa kusalia kwenye Ligi Kuu Bara.

Tabora United imesalia NBC Premier League baada ya kuifunga Biashara United ya Mara, kwa jumla ya magoli 2-1 kwenye michezo yote miwili ya mtoano (play offs).
Msimamizi wa timu hiyo ambaye ni Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Richald Abwao amewahakikishia wananchi wa Mkoa wa Tabora na mashabiki wao kuwa msimu ujao wanakwenda kufanya makubwa zaidi kulingana na changamoto walizopitia sasa wanakwenda kufanyia masahihisho na kuja kivingine nyuki wa Tabora.

Aidha, Abwao ameeleza "Msimu ujao hawaendi kushiriki bali wanaenda kuonesha upinzani kwa kila timu itakayo kuja mbele yao jukumu ni moja kushinda ndilo jukumu lililo mbele yetu."
Kweli fita ni fita mraaa......jamaa kawatuliza wa kwao
 
Back
Top Bottom