Real estate business Tanzania inaelekea kufa kabisa, kwa sasa inapumulia mashine

Real estate business Tanzania inaelekea kufa kabisa, kwa sasa inapumulia mashine

The Evil Genius

JF-Expert Member
Joined
Mar 21, 2014
Posts
6,017
Reaction score
19,506
Biashara ya kujenga na kupangisha Tanzania inaelekea kufa kabisa. Sasa hivi hii biashara inapumulia mashine ICU.

Kwa wakazi wa Dar es Salaam mtakuwa mashahidi, malls nyingi na majengo mengi ni matupu miaka sasa, Mkuki house sasa inaanza kujaa panya, Quality Centre and Plaza mnajua kinachoendelea pale.

Ukija jengo refu kuliko yote barabara ya Sam mujoma hapa karibu na Chuo /Mlima city iko wazi miaka sasa, hakuna wapangaji.

Ukienda zile flat za NHC zilizoko Morocco ziko tupu, China plaza Kariakoo inaelekea kuwa tupu, discount center wakitoka mle inakua gofu.

Ukienda mjini, Posta majengo mengi wameandika space to let, Rent here, space available.

Naona jengo jipya la Palm Village Millard Ayo amepewa kazi ya kupiga debe masaa 24, sina hakika kama wataweza kuhimili.

Je, hii inatokana na nini ama inaashiria nini kwenye uchumi huu wa kati?
 
Mkuu tulijaribu kufanya hivyo ila wanasema kuwa biashara iko very high na wateja wako wengi sana [emoji4] Ila mpaka leo Nikipita Hapo naona kuna vyumba viwili tu ndo vina watu
Duh hapo lazima uwe mpole.
 
Kuna siku niliwapigia simu wale jamaa wa Victoria Apartments kuhusu Ghorofa Lao [emoji3][emoji3][emoji2] Duuh eti single bedroom inagharimu 250 Millions [emoji1787][emoji1787][emoji1787]

Ni unanua? Kupangisha ni bei gani?
 
Chakustaajabisha ni pale jengo linakaa bure mmiliki hataki kushusha kodi na anaona ni bora likae tupu hata miaka kumi ilipaswa kwa wakati huu sisi wanyonge tukalie haya maghorofa
Kuna ukweli ukweli katika maelezo yako. Unajua Tanzania wenye nyumba wana utamaduni waliorithi tangu kipindi nyumba zikiwa adimu na wanauendeleza mpaka sasa. Utamaduni wa mwenye nyumba kuwa na jeuri ya hali ya juu. Utamaduni wa kupanga kodi anayotaka na kuongeza anavyotaka. Utamaduni wa kutaka kulipwa kodi ya muda mrefu. Hawajui kuwa siku hizi watu wengi wameweka vitega uchumi vya nyumba na soko lina ushindani. Ila ni vizuri kwani wateja watapata unafuu.
 
Back
Top Bottom