Refa amepiga filimbi ya kumaliza mpira baada ya kuona Simba SC wanataka kufungwa goli nyingine

Refa amepiga filimbi ya kumaliza mpira baada ya kuona Simba SC wanataka kufungwa goli nyingine

Jana Mdakuzi ulisema tumebebwa, hii ya leo ni nini?

Hili jambo linaleta afya kwa maendeleo ya mpira wetu?
Ndiyo maana nimesema kwa sasa ni ngumu kunielewa, maana tafsiri iliyoletwa hapa ni kwamba nimesema Yanga imebebwa, na ukweli sikusema hivyo.

Mimi nimezungumzia kwa kulaani vitendo vya rushwa kwenye soka, hasa kwa hatua niliyoina ni mpya, ya klabu kumweka benchi nyota wake wa kikosi cha ushindi.

Mimi sijaikemea klabu yoyote ile, ila nimekemea mazingira ya rushwa kwenye soka. Basi.

Ova
 
GSM anawadhamini Coasaea na Chama cha Marefarii. Hilo ndilo jibu rahisi la wasiofikiri.
 
Ndiyo maana nimesema kwa sasa ni ngumu kunielewa, maana tafsiri iliyoletwa hapa ni kwamba nimesema Yanga imebebwa, na ukweli sikusema hivyo.

Mimi nimezungumzia kwa kulaani vitendo vya rushwa kwenye soka, hasa kwa hatua niliyoina ni mpya, ya klabu kumweka benchi nyota wake wa kikosi cha ushindi.

Mimi sijaikemea klabu yoyote ile, ila nimekemea mazingira ya rushwa kwenye soka. Basi.

Ova
Sawa…

Basi naomba uongelee hili nililokuitia hapa, refarii kumaliza mchezo huku timu ikiwa kwenye move ya goli unaongelea vipi?
 
Namna refa alivyomaliza game hata mashabiki wa Koloz wameangua kicheko. Tumecheka wote bandani. Ligi imeanza kuwa comedy sasa
Inasikitisha, binafsi siangaliagi mechi za Simba toka zile mechi walizopewa penati za kutatanisha. Jana kwa kuwa sikuwa na kazi niliwasha TV na kukuta sakika ya 70 huko. Nikakutana na lile goli la 2 la Coastal.

Kiukweli, labda mtazamo wangu ni mbaya ila marefa wanaharibu na kuitia aibu ligi yetu. Nimesikitka sana namna mpora ukivyomalizwa wakati jamaa wakiwa kwenye move ya kutafuta goli la ushindi.

Inasikitisha sana.
 
Angeacha muvu iishe ndio amalize.
 
GSM anawadhamini Coasaea na Chama cha Marefarii. Hilo ndilo jibu rahisi la wasiofikiri.
Kama angekuwa anadhamini marefa kwa nini wameibeba simba hapa? Si refa angeacha wafungwe.
 
refa alimaliza mpira dakika ya 80 au na za nyongeza ziliisha?
 
Ni nini sababu ya kunitukana hivi? Ni huu mpira tu au kuna mengine ndugu yangu? Mbona maisha yangu humu huwa hayahusishi kumtukana yeyote?

Ni nini kilichokupa ujasiri wa kunitusi? Ni nini kimefanya uone unatosha kunivunjia heshima?

Nifah nadhani usiwe unaniita kwenye thread za hivi tena.

Ova
Nisamehe mimi mchumba, nimekosa mimi.
I’m sorry b…
 
Ni ajabu sana
Mpira ziliongezwa dakika 4
Rafa kamaliza mchezo dakika ya 4 na sekunde kadhaa.
Hapo kosa liko wapi.

Ulitaka amalize mpira wakati umetoka nje ?
Ulikuwa na uhakika gani kuwa Costal Union ingefunga goli ?
Kuna Sheria inasema kama timu ikishambulia refa asimalize mchezo?
Jinga kabisa
 
Ni nini sababu ya kunitukana hivi? Ni huu mpira tu au kuna mengine ndugu yangu? Mbona maisha yangu humu huwa hayahusishi kumtukana yeyote?

Ni nini kilichokupa ujasiri wa kunitusi? Ni nini kimefanya uone unatosha kunivunjia heshima?

Nifah nadhani usiwe unaniita kwenye thread za hivi tena.

Ova
Hakuna sehemu nimekutukana. Usinilishe maneno wala kunivunjia heshima, pia usijipe umuhimu mkubwa namna hiyo usio nao.
 
Hivi Aya mambo wanayo Fanya marefa wahusika, kamati ya waamuzi, Bodi ya Ligi hamjisikii vibaya!! Mbona ni mambo yanayo jirudia Tena kwa timu Moja hamuoni kama Yana shusha hadhi ya Ligi yetu.

Hii Ligi inaonekana mpaka nje ya mipaka yetu hivi tunaonekana vipi?
Badala ya ligi kupanda viwango marefa wanatuangusha sana
 
Back
Top Bottom