Refa wa Yanga afungiwa miezi sita

Refa wa Yanga afungiwa miezi sita

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
313428381_186706687218904_5974273179738793480_n.jpg

Florentina Zabron nje miezi 6

Mwamuzi Florentina Zabron ameondoshwa kwenye ratiba za michezo ya Ligi Kuu kwa kipindi cha miezi 6 ijayo kutokana na kuionea Klabu ya Geita Gold ilipocheza na Yanga SC pale CCM Kirumba Mwanza.

My Take
Kumekuwa na tetesi za Utopolo kuwawezesha marefa wanaofungiwa kwa ajili yao. PCCB fanyieni kazi.

=======

Mwamuzi Florentina Zabron amesimamishwa kwenye ratiba ya kuchezesha michezo ya Ligi kuu kwa kipindi cha miezi 6 ijayo na TFF kutokana na kushindwa kumudu mechi kati ya Geita Gold dhidi ya Yanga.

Mechi hiyo ambayo ilipigwa katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza huku Geita wakiwa ni wenyeji wa mchezo huo ambapo Florentina aliionea timu hiyo ya Geita kwa kuwapa penati klabu ya Yanga kwa kutafsiri kuwa mchezaji wa timu pinzani alishika mpira kwa mkono.

Lakini baada ya Bodi kukaa na kujidhihirisha na kuona kuwa mchezaji huyo wa Wachimba madini alikuwa nje ya boksi hivyo haikustahili kuwa penati, na baada ya hapo mwamuzi huyo atakuwa nje miezi sita.

Tukio hilo lilizua taharuki kwa mashabiki na wapenzi wa mpira kwa kuona kuwa Florentina hakuwa sahihi na maamuzi yake na penati hiyo ilipelekea Yanga kupata pointi 3 baada ya kushinda kwa bao 1-0.

Matukio haya yanajirudia sana hapa Tanzania hasa timu ndogo zinapocheza dhidi ya kubwa huwa waamuzi wanakosa umakini kitu ambacho mechi huisha kwa timu ndogo kuonewa kutokana na matokeo hayo

Tanzaniaweb.
 
View attachment 2410263
Florentina Zabron nje miezi 6

Mwamuzi Florentina Zabron ameondoshwa kwenye ratiba za michezo ya Ligi Kuu kwa kipindi cha miezi 6 ijayo kutokana na kuionea Klabu ya Geita Gold ilipocheza na Yanga SC pale CCM Kirumba Mwanza.

My Take
Kumekuwa na tetesi za Utopolo kuwawezesha marefa wanaofungiwa kwa ajili yao. PCCB fanyieni kazi.

=======

Mwamuzi Florentina Zabron amesimamishwa kwenye ratiba ya kuchezesha michezo ya Ligi kuu kwa kipindi cha miezi 6 a timu ndogo kuonewa kutokana na matokeo hayo

Tanzaniaweb.
Ameshakunja m10 za gsm hana waiwasi
 
Kwani Yule Refa aliye kataa goli Halali la Geita katika mechi iliyo wakutanisha Simba vs Geita pale Kwa Mkapa na mechi ikaisha Kwa ushindi wa Simba Kwa 2-1 alifungiwa miezi mingapi?[emoji1][emoji1]
 
Kuna yule mwamuzi Ahmada Simba! Aisee kila akichezesha mechi ya simba na timu yoyote ile, baada ya hiyo mechi lazima afungiwe kwa kuibeba simba kupitia maamuzi yake ya kutatanisha!
 
Kumbe na nyinyi wanawake mnakula rushwa namna hii.we Kalpama we embu tema mate chini,kha,,!
Hebu tag jina langu vizuri yakheee hahahaha mi nilijua mwanaume..huyo basi atakua mchumba wa Manara
 
Huyu mama hao utopwizo watakua damuni sio kwa ukavu ule aliouonyesha. Watu wakapeta eti un beaten lol ptuuuuh
 
Kufungiwa peke yake haitoshi, sheria ziangaliwe upya ili timu iliyopewa ushindi kimakosa inyang'anywe ipewe timu iliyofamyiwa dhuluma ili liwe fundisho kwa Mihigo fc waache kuhonga marefa
 
View attachment 2410263
Florentina Zabron nje miezi 6

Mwamuzi Florentina Zabron ameondoshwa kwenye ratiba za michezo ya Ligi Kuu kwa kipindi cha miezi 6 ijayo kutokana na kuionea Klabu ya Geita Gold ilipocheza na Yanga SC pale CCM Kirumba Mwanza.

My Take
Kumekuwa na tetesi za Utopolo kuwawezesha marefa wanaofungiwa kwa ajili yao. PCCB fanyieni kazi.

=======

Mwamuzi Florentina Zabron amesimamishwa kwenye ratiba ya kuchezesha michezo ya Ligi kuu kwa kipindi cha miezi 6 ijayo na TFF kutokana na kushindwa kumudu mechi kati ya Geita Gold dhidi ya Yanga.

Mechi hiyo ambayo ilipigwa katika uwanja wa CCM Kirumba Mwanza huku Geita wakiwa ni wenyeji wa mchezo huo ambapo Florentina aliionea timu hiyo ya Geita kwa kuwapa penati klabu ya Yanga kwa kutafsiri kuwa mchezaji wa timu pinzani alishika mpira kwa mkono.

Lakini baada ya Bodi kukaa na kujidhihirisha na kuona kuwa mchezaji huyo wa Wachimba madini alikuwa nje ya boksi hivyo haikustahili kuwa penati, na baada ya hapo mwamuzi huyo atakuwa nje miezi sita.

Tukio hilo lilizua taharuki kwa mashabiki na wapenzi wa mpira kwa kuona kuwa Florentina hakuwa sahihi na maamuzi yake na penati hiyo ilipelekea Yanga kupata pointi 3 baada ya kushinda kwa bao 1-0.

Matukio haya yanajirudia sana hapa Tanzania hasa timu ndogo zinapocheza dhidi ya kubwa huwa waamuzi wanakosa umakini kitu ambacho mechi huisha kwa timu ndogo kuonewa kutokana na matokeo hayo

Tanzaniaweb.
🤔🤔🤔🤔 african soccer
 
Back
Top Bottom