Rekodi ya Kibadeni kwenye derby ya Kariakoo ipo rehani

Rekodi ya Kibadeni kwenye derby ya Kariakoo ipo rehani

Kipimo sahihi kwangu Binafsi ni MICHEZO mi nne ijayo.

Kwa Baleke.

Yanga.
Azam.
Wydad.
Whydad.

Katika hii MICHEZO akifunga MAGOLI 3 hapo ndipo nitasema ni mshambuliaji mwenye uwezo.

Kwa sasa nisiseme nikamaliza
Raja ni kubwa kuliko hizo Yanga na Azam
 
Alishindwa Okwi itakuwa Baleke.
Simba akishinda 5 -0
Okwi mbili. 2
Kaseja.
Mafisango.
Sunzu.
Okwi alimuachia tu Kaseja apige Penalty aweke rekodi ya kuwa kipa pekee kufunga goli kwenye derby ya kariakoo la sivyo Emmanuel Emosting Okwi angevunja rekodi hiyo hata hivyo sio mbaya kwani Baleke ataimaliza hiyo kazi
 
Ni ukweli usiopingika kuwa kufunga magoli matatu yaani Hat trick kwa mchezaji mmoja katika mechi ya watani wa jadi yaani Simba na Yanga ni jambo gumu sana na ni rekodi ya aina yake.

Hata hivyo rekodi hiyo mpaka sasa inashikiliwa na mchezaji mmoja pekee,Abdala King Kibadeni aliyefany hivyo mnamo Julai 19, mwaka 1977 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, sasa Uwanja wa Uhuru, wakati Yanga ilipotandikwa 6-0 na Simba.

Siku hiyo, Kibadeni alitikisa nyavu za Yanga katika dakika za 10, 42 na 89, wakati mabao mengine ya Wekundu wa Msimbazi, yalitiwa kimiani na Jumanne Hassan 'Masimenti' dakika ya 60 na 73 na jingine Selemani Sanga wa Yanga alijifunga mwenyewe dakika ya 20 katika harakati za kuokoa krosi ya Ezekiel Greyson 'Jujuman'.

Rekodi hii ya Kibadeni iliyodumu kwa miaka mingi sasa huenda ikafikia ukomo hapo tar 16 April 2023 kwa mshambuliaji Hatari zaidi kwa sasa ndani ya Ligi kuu Tanzania Bara,Jean Bakeke atakapotikisa nyavu za Yanga mara 3 na kuandika rekodi mpya ya kuwa mwanadamu wa pili kufanya hivyo baada ya mwanasimba mwengine kufanya hivyo mwaka 1977.

Rekodi hii si rahisi kuivunja ukizingatia kwa kipindi chote hicho toka 1977 Simba na Yanga wamepita washambuliaji wengi hatari lakini hawakuweza kuivunja rekodi hiyo na sasa ni wazi Jean Baleke (Jini) anaenda kuonyesha utofauti wake na washambuliaji waliowahi kupita kwenye vilabu hivyo vikongwe kwa kuitamatisha rekod ya King Kibadeni Mputa na nina imani hata yeye atafurahi hili jambo likitokea wakati huu akiwa hai
Hapa washabiki wa yanga wanatetemeka[emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kipimo sahihi kwangu Binafsi ni MICHEZO mi nne ijayo.

Kwa Baleke.

Yanga.
Azam.
Wydad.
Whydad.

Katika hii MICHEZO akifunga MAGOLI 3 hapo ndipo nitasema ni mshambuliaji mwenye uwezo.

Kwa sasa nisiseme nikamaliza
Wewe nawe usiifanye akili yako kuwa ngumu. Ndio umeambiwa atawafunga itopolo goli 3. Kwaio ni kipomo tosha
 
Unaota wewe. Baleke, tarehe 16/4 , hatafunga goli lolote na ndiyo utakuwa mwisho wa hii HYPE mnayompa huyo Mzaire feki
Ama kweli "wajinga watu" hivi kwa moto huu alionao Baleke pale Yanga kuna kitu gani cha kumpunguza kasi mtu hatari kama yule asifunge hiyo tar 16
 
Hapa washabiki wa yanga wanatetemeka[emoji23][emoji23][emoji23]
Baleke ni kama Jinamizi kwenye njozi kila wakilala wana weweseka kiwa itakuwaje hiyo tar 16
 
Ni ukweli usiopingika kuwa kufunga magoli matatu yaani Hat trick kwa mchezaji mmoja katika mechi ya watani wa jadi yaani Simba na Yanga ni jambo gumu sana na ni rekodi ya aina yake.

Hata hivyo rekodi hiyo mpaka sasa inashikiliwa na mchezaji mmoja pekee,Abdala King Kibadeni aliyefany hivyo mnamo Julai 19, mwaka 1977 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, sasa Uwanja wa Uhuru, wakati Yanga ilipotandikwa 6-0 na Simba.

Siku hiyo, Kibadeni alitikisa nyavu za Yanga katika dakika za 10, 42 na 89, wakati mabao mengine ya Wekundu wa Msimbazi, yalitiwa kimiani na Jumanne Hassan 'Masimenti' dakika ya 60 na 73 na jingine Selemani Sanga wa Yanga alijifunga mwenyewe dakika ya 20 katika harakati za kuokoa krosi ya Ezekiel Greyson 'Jujuman'.

Rekodi hii ya Kibadeni iliyodumu kwa miaka mingi sasa huenda ikafikia ukomo hapo tar 16 April 2023 kwa mshambuliaji Hatari zaidi kwa sasa ndani ya Ligi kuu Tanzania Bara,Jean Bakeke atakapotikisa nyavu za Yanga mara 3 na kuandika rekodi mpya ya kuwa mwanadamu wa pili kufanya hivyo baada ya mwanasimba mwengine kufanya hivyo mwaka 1977.

Rekodi hii si rahisi kuivunja ukizingatia kwa kipindi chote hicho toka 1977 Simba na Yanga wamepita washambuliaji wengi hatari lakini hawakuweza kuivunja rekodi hiyo na sasa ni wazi Jean Baleke (Jini) anaenda kuonyesha utofauti wake na washambuliaji waliowahi kupita kwenye vilabu hivyo vikongwe kwa kuitamatisha rekod ya King Kibadeni Mputa na nina imani hata yeye atafurahi hili jambo likitokea wakati huu akiwa hai
mayele ndiye anayeweza kuvunja hiyo rekodi coz kashawahi kufunga hadi goli mbili safi kwenye hii derby
 
mayele ndiye anayeweza kuvunja hiyo rekodi coz kashawahi kufunga hadi goli mbili safi kwenye hii derby
Goli 2 sio Hat trick na kwenye kuitafuta Hat trick katika mechi moja hakuna uhusiano wowote na mechi zilizopita na ndio maana atatakiwa kuanza moja tena hadi 3 kama anaitaka Hat trick na sio kuanzia mbili alizofunga huko nyuma
Mayele sio Striker wa Hat trick ni mchezaji wa kigoli kimoja kimoja tu akijitahidi sana 2 Hat trick labda awakute Zalan ya Sudan Kusini
 
Goli 2 sio Hat trick na kwenye kuitafuta Hat trick katika mechi moja hakuna uhusiano wowote na mechi zilizopita na ndio maana atatakiwa kuanza moja tena hadi 3 kama anaitaka Hat trick na sio kuanzia mbili alizofunga huko nyuma
Mayele sio Striker wa Hat trick ni mchezaji wa kigoli kimoja kimoja tu akijitahidi sana 2 Hat trick labda awakute Zalan ya Sudan Kusini
Baeleze baelewe. Mayele yulee alishindwa, itakuwa huyu aliyejichokea na ambaye sasa uchoyo umemjaa attempts 10 atafunga moja tena la kulazimisha.
 
Goli 2 sio Hat trick na kwenye kuitafuta Hat trick katika mechi moja hakuna uhusiano wowote na mechi zilizopita na ndio maana atatakiwa kuanza moja tena hadi 3 kama anaitaka Hat trick na sio kuanzia mbili alizofunga huko nyuma
Mayele sio Striker wa Hat trick ni mchezaji wa kigoli kimoja kimoja tu akijitahidi sana 2 Hat trick labda awakute Zalan ya Sudan Kusini
sasa tukianzia hapo hapo ulipoandika mayele aliyewahi funga goli mbili dhidi ya simba na beleke ambaye hakuwahi kucheza kabisa hiyo mechi nani wa kumpa credit iyo...yani uhusiao wa beleke kufunga hatrik unatokea wapi kama yule aliyewahi kufunga goli mbili ktk iyo mechi hawezi kuhusiana na goli tatu
 
sasa tukianzia hapo hapo ulipoandika mayele aliyewahi funga goli mbili dhidi ya simba na beleke ambaye hakuwahi kucheza kabisa hiyo mechi nani wa kumpa credit iyo...yani uhusiao wa beleke kufunga hatrik unatokea wapi kama yule aliyewahi kufunga goli mbili ktk iyo mechi hawezi kuhusiana na goli tatu
Kinacho muhusisha Baleke hapo ni uwezo wake mkubwa wa kufunga Hat trick na kulifanya lionekane jambo rahisi tu na ndio maana kwenye mechi 06 za mwisho huyo mwamba ana Hat trick mbili
 
Back
Top Bottom