Review: Demographics, Population and Youth Leadership

Naomba upitie japo introduction ya hii article: Economic Empowerment of Women
women WORK but kazi yao haionekani sababu either ni kazi ambazo hazina direct economic value au ni informal (kupika, kuchota maji na mengine, au kuuza maandazi, kufuma mashuka etc). Men tend to grab most of the formal job and hence contribute to the economy of the household in a tangible manner. Mwanaume anae potea hata katika haya anaweza kuonekana from time to time akileta shillingi 50,000, au akilipa ada ya shule etc. it is quantifiable. Mwanamke anashinda kwa mtu akimpikia na kumfulia, akitoka huko anapewa kilo ya mchele na kopo la maha, it is less quantifiable.
But I get your point.
 

hapa umeungana na post yangu kwamba hizi community schools zilikuja with purpose ya kudelay fertility rate.
but asking hela za elimu zilikwenda wapi ni swali ambalo sikulitegema toka kwako as hata mtoto mdogo anajua kwamba hizi hela hazikufika zilikotakikana. shule niliyopo inawanafunzi 900+ OLEVEL -ALEVEL ila bajeti kwa mwaka ni 9 mil. tell me with such amount utafanya nini ili uboreshe elimu ndani ya shule??

kumbuka wazazi wengi nao ni wagumu ama sijui niseme hawakipi kipaumbele elimu kiasi cha kufanya mazingira ya shule kuwa magumu kuliko kawaida. to me swala la hela kwa serikali hii limekuwa ni gumzo.
 

I've never read the book, but I believe kila rule inatakiwa kua applied in context. To the question WHAT QUALITIES IN YOUR VIEW, ARE NEEDED TO BE A LEADER? Kuna mtu alisema (nukuu)
I guess the same is valid for the question what does a leader do?
 

This question is tricky. Zilikotakikana ni wapi hasa? Pale zinapohitajika zaidi, au pale waliposema watazifikisha? Maana ni vitu viwili tofauti. wanaweza kusema wanahitaji pesa zaidi kujilipa wenyewe au ku-organize meetings na safari wakati pesa zinahitajika zaidi kuwanunulia watoto chakula ili kupunguza dropout. Sasa audit ikionesha kua pesa zilifika waliposema zitafika hapo tutasema zilifika zilikotakikana au hazikufika? but this is a new topic...
 

na ndio maana nasema hizi sekta zisizo rasmi, zirasimishwe ili kuweza kuleta chachu ya maendeleo. wajua kazi kama za muuza vitumbua zirasimishwe na serikali itambue mchango wao na wawawekee platform ambayo itamwonyesha huyu mtu anaingiza kiasi gani na anatumia kiasi gani. hili litawafanya wanaume kuweza kujua kama wanashea equally ama la.

kwa mfano baba anayesema nitalipa ada tu ya mtoto may be kwa mwaka ni laki 3 max kwa shule za serikali ninaamini hatoi kiasi kikubwa cha mchango kama mama anayetoa sh 2000 kila siku kwaajili ya matumizi ya nyumban. baba anayesafiri na kurudi baada ya miez akiwa na sh 50000/= huyu kaleta lkn ajue kabisa mkewe ndani ya huo mwez katunia zaid na amezalisha zaid ya hizo.

napata kusononeka sana kwa jinsi ambavyo mwanamke anayeitwa mama nyumban asivyo kuwa counted kwenye kipatpo cha nyumban wakasahau kwamba kule kufua na kupika kwake kumepunguza gharama za maid hapo ndani. na kama ni hivyo basi alipwe kama h/maid halafu tuone kama hajaingiza kipato.
 
my dearest!!
nimekuwa mwl kwa miaka mingi sana ukisikia hela zimeongezwa elimu jua zimeongezwa kwaajili ya kuwapa watu safari and the like na sio kwaajili ya kuboresha shule.

nimeshuhidia kwa macho yangu sh 9mil zikiletwa shule na covering letter kuonyesha zitumikeje, utakuta pesa ziko alocated kwenye vitabu of which haitosh na nyingine kwenye maintanance thnk kwa mazingira ya shule maintanance ya less than 4 mil ni ya kufanya nini??

tena hata kuambiwa nendeni kwenye capacity building ni ishu mnapigwa panga mnapewa sh 10000/= kwa siku wakati bajeti imeletwa mlipwe per diem. the rest zinakwenda wapi eti mara zimekuwa re- alocated nashindwa kuelewa re-alocation ya fedha zilizokwisha andikiwa?? no body cares kama shule ina drop outs ama la ama kama kuna ubao ama la.

nilikaa shule hata choo cha waalim hakuna, yaani tundu ni moja halafu kimejaa kila siku nilikuwa na kazi ya kucheza na kemikali ili kisink manake harufu yake ilikuwa mbaya. ingawa nilijua nilikuwa naumiza mazingira kwa kutengeneza sumu huko chini but i had to do it ili tu kukwepa kufedheheka kwenye choo kinachonuka.

nakumbuka siku kikwete alikuwa anakuja shulen kwetu, tuliletewa hadi watu wa kusafisha njia nikajiuliza wanasafisha aje aikute shule safi for what?? kwann asije akakuta choo cha waalim kichafu?? laipaswa akute ili ajue hali halisi lkn ndo ivyo kilipakwa rangi na nikalazimishwa choo kizamishwe kisionekane na harufu isiwepo. there is a lot to tell huku bana thanks God kwakweli sasa sipo huko
 
Ila sasa miaka hii ya nyuma we have doubled the expediture in education, but we have also more than doubled the failure rate and doubled the dropout rate.....sijui hizi pesa tuli-invest in the education sector zinafanya nini kwa kweli...

Tumewekeza kwenye quantity badala ya quality. Hii ni sehemu ya hotuba ya Rais aliyoitoa Machi 14, 2013 mjini Morogoro wakati akizindua jengo la Kitivo cha Sayansi la Chuo Kikuu cha Kiislamu.


Suala ambalo watu wengi wamehoji ni whether hiyo strategy ni nzuri au ilitakiwa tu-balance both quantity and quality.
 
Would this help? (the haki elimu project, cash on delivery)

 

Rais anaweza kusema hivo kwenye hotuba but as we have all noted there is a discrepancy between what he says and what is actually done. Let's hope that for once what was done was better than what he said: a balance between quality and quantity... :thinking:
 
Reactions: EMT
Would this help? (the haki elimu project, cash on delivery)

View attachment 98020

do you think that this will add smthg??
as for me it wouldn't as they have so many written findings on how to improve our education and still no body is working on them. so far projects kama hizi hubaki kupamba mashelfu ya ofisi za viongozi tu but putting them in place is something else.

on the other hand its better to the study so as to reveal the true picture.
 

BUt the overall aproach unaionaje? you being from the sector would understand better. baada ya kuonesha kua (1) pesa za elimu hazifiki shuleni na (2) teachers are payed for their input instead of their performances, Wanapendekeza vitu 3:

  1. Transfer payment for input ( capitalisation grant) directly to school account
  2. Pay teachers a bonus for every children who can read and count (kumbuka it is for primary level)
  3. Combine payments for inputs and performances.
IF THIS WAS APPLIED, do you think itasolve baadhi ya matatizo ya elimu Tanzania?
 
ngoja nikwambie pesa za capitation huja directly toka hazina kwenye account ya shule ila huja na barua ya kuelekeza matumizi, so labda wangeniambia kwamba shule iachiwe iamue matumizi ila matumizi yafanyiwe retirement na kuwa audited hilo ni swala jingine.

lakini pia kwenye kulipa mwalimu kisa mwanafunzi kaweza kusoma na kuandika tu sio motivation sahihi manake kumbuka tunahitaj mtoto ajue zaid ya hapo. FYI watoto wadogo wana creaming capacity kubwa sana can cream even two full scapes pasi kujua alicho cream ni kitu gani. na tena akakariri hadi kinavyoandikwa. take it from me, Baba V njoo nisaidie hapa.

huko kucombine money for inputs na performance nako sikuelewi. unajua sikubaliani na swala kwamba mwl anahitaji extrinsic motivation ili afanye kazi yake kwa umakini la, najua wazi kabisa kwamba mwl anahitaji mazingira bora ya kufanyia kazi, mwanafunzi aliye na utayari pamoja na renumeration na incentives nzuri basi.

package ikiwa nzuri, nikapewa mwanafunzi mwenye utayari wa kujifunza hata kama ni slow learner na nikawa na miundo mbinu ya kunifanya niweze ku improvise na kumpa mwanafunzi rum ya kudiscover basi lazima ufaulu uwepo tu. hayo mengine yote ni mbwembwe tu.
 
Reactions: EMT

By balancing quality and quantity, I meant "Kuliko kujenga shule kumi zenye majengo mazuri na ya kupendeza na kuchagua wanafunzi wengi wa primary kwenda kwenye hizo shule bila vitendea kazi ni bora kujenga shule tano, halafu gharama za shule tano nyingine zilizobakia zitumike kuziboresha hizo shule in terms of kuwa na walimu wazuri na vitendea kazi. Kuwepo na uwiano kati ya quantity and quality."

Sasa hivi product ya shule za kata imeshaanza kutinga uraiani wakiwa watupu na wengi bado wataendelea kuja mpaka hapo tutakapofanikiwa ku-balance quantity na quality. Nadhani ni rahisi kujenga darasa lakini ghali and time-consuming ku-maintain hilo darasa na watu wake ndani.
 
EMT sikiliza nikwambie my swt bro,

shule kuongezeka interms of majengo ni swla zuri sana ata iwe katika kila kijiji sina tatizo nalo. ishu hapa ni kwamba modality gani inawapeleka hawa watoto shulen ndo ishu. to be honest bado naona ile system ya zamani ya kusomesha wanafunzi shule za bweni was perfect interms of behavioural change and knowledge acquired.

sasa hivi mtoto anazaliwa KIluvya madukani pr anasoma kiluvya shule ya msingi, sekondari anasoma kiluvya sec, akitoka anakwenda A-level MINAKI yaani kote huku haka km 15 alizokwenda mbali na nyumban, kiakili anadumaa. mwaka hadi mwaka anakaa mazingira hayo hayo hata uwezo wa kuelewa unakuwa static/stagnant.

to me mwanafunzi asome shule ya msingi mazingira ya nyumban ila selkondari aende mkoa mwingine huko atakutana na mazingira tofauti yenye watu toka maeneo tofauti, lazim ajifunze tu kuwa na akili na atajibidiisha kusoma. mazingira haya lazima yatamfanya kwanza apanuke kiakili by just seeing manedeleo ama geographical make up ya eneo jingine. hata kule kusafiri tu humfanya ajue kaskazini ni wapi kusini ni wapi.

sishangai kuona mwanafunzi wa form 4 hajui kaskazini mwa tz ni wapi manake hajapafika . ama ukimuuliza kigoma panakucha saa ngapi hawez kukwambia atasema saa 12 kama ilivyo hapa dar.


Maria montessori aliwah kusema mwanafunzi hujifunza vyema anapopata exposure na hivyo hizi shule zetu ziboreshwe ziwe za bweni wanafunzi wafanyiwe utaratibu wa kusoma bweni.


ni afadhali kuwa na shule 5 kwenye wilaya zote za bweni, kuliko kuwa na shule 10 halafu zote za kutwa
 
Last edited by a moderator:
gfsonwin umeongelea kitu ambacho sikuwahi kukitilia maanani sana but very important. Maana nakumbuka enzi zetu O Level tulikuwa tunakutana na wanafunzi kutoka sehemu mbalimbali za nchi na pia kutoka dini tofauti.

Hata ukisoma kwenye wilaya yako bado ilikuwa unakutana na watu kutoka sehemu mbalimbali za nchi. Lakini kwa hizi shule za kata sidhani kama hiyo kitu ipo tena. Hakuna tena kuwachanganya wanafunzi mashuleni.

Badala ya kutoa "elimu kombo" tunatoa "elimu kimbizi." Katika sehemu ya hotuba yake aliyoitoa mwaka 1985 mjini Dodoma wakati akifunga Mkutano wa Chama Cha Elimu ya Watu Wazima (CHAWATA), Mwali Nyerere alisema:


Chanzo: Nyerere:-Wasomi wameiharibu Elimu; Wafungua shule kwa pupa; Watoa

 
Threads kama hii sie vilaza wa ungwini tulozoea kuintagret na kudiferenshiet with respect to X bila kujali limits tunalazimika kukaa kimya na kugonga ma Likes tu. Hahahaha anayebisha naweza kumpruvia kwa mathematical induction.

Baada ya kusema hayo napenda kuwahakikishieni Roulette, gfsonwin na EMT kuwa nimeprint haya ma yuziful posts mliyoyamwaga hapa kwa ajili ya kizazi changu kijacho. (Kabinti kangu Matesha naona kama kanaelekea kingwiningwini flani hivi, nalazimika kumpa haya matirio ya kukamata digrii ya mabachela tena with honour)

Naendelea kuwasoma na kuprinti matirioz, haya develop, develop......:A S 576:
 
Last edited by a moderator:
yap Nyerere had a point hapa na ukiisoma hii article yake utagundua kwamba aliona jinsi ambavyo elimu tuipatayo inavyotuandaa kuwa tegemezi.

let me tell you, the days naanza shule education for self relience was key issue. na hata madarasani we had shambaz, and bustaniz plus other vocational skills and on top of that the home economics classes.
ilikuwa wakati wa msimu kama ni shamba tunapanda tena tukiwa supervised na waalim wetu, kisha tunapalilia paliz zote mbili halafu tunakuja kuvuna na kuhifadhi. yote haya tuliyafanya na yalitufunza kuwa independent kiasi kwamba ukirud home wewe ndo mwl wa shamba.

madarasa ya home economics tulifundishwa kuanzia personal hygiene, usafi wa mazingira na hata mapishi na utunzaji wa vitu. nakumbuka mimi kufua nimefundishwa darasani nikiwa class 3, hata jins ya kuosha viatu, kupika kadhalika. ukitoka hapo ukirudi nyumban wewe kazi yako ni kupractice tu ulichojifunza yani hadi mzazi hapati shida manake anajua utajifunza tu.

mashuleni tulikuwa na vocational skils kufuma mikeka, vitambaa, kutengeneza mafagio, kuchonga mwiko, panga, visu vigoda et al tulifunzwa kuanzia darasa la tano.

sasa turudi kwenye elimu ya kileo, mwanafunzi toka anaingia shule hadi anatoka anafundishwa kusoma na kuandika tu, hana ujuzi mbadala anaoupata ili hata kama atafeli basi aweze kuwa na cha kufanya hakuna. tunatengeneza mambumbumbu zaid kuliko wasomi. hakuna anayejali mwanafunzi akitoka form 4 katoka nanini cha ziada zaidi ya scores zake kwenye masomo. na hapo ndipo utakuta mtu akipata div 4 inakuwa ni tatizo.


let me tell you, ingekuwa kwamba shulen wanafunzi wetu wanafunzwa kuyatumia mazingira yao kikamilifu, kiasi kwamba wanatoka wakiwa na elimu ya maisha na elimu ya darasani basi ni wazi kwamba hata kama wangefeli ungekuta wamejiendeleza zaid kifani kuliko kuhangaika mtaani miaka 3-4 kuresit na wasifaulu.

kwanza kabisa sioni hata maniki ya kuresit hii mitihani wanayofeli manake kama alifeli kwa mara ya kwanza basi angetakiwa system yenyewe imchagulie alternative solution lkn sio kumfanya mwanafunzi asote kitaa na re sitting mwaka hadi mwaka pasi la msingi na hela zinazidi kuisha. niliwah kujenga logic kwamba hii resitting ni njia ya baraza la elimu kula hela za watu nikashambuliwa kama mpira wa kona but huo ndio msimamo wangu manake tuambiwe leo hii imekuwa na tija kwa watu wepi?? zaid ya kuzidi kuwa frustrae tu hawa wanafunzi?? na je maisha ni mapaka ufaulu tu form 4 ama 6?? why not looking for an alternative means??

Hope you will agree with me kwamba elimu ya self reliance ingebaki hadi leo hii, basi tungeona vikundi vingi sana vya vijana vya kimaendeleo kuliko hali ilivyosasa?? na tungeona almost kiwango cha uzalishaji kimeongezeka kuliko ilivyo hivi sasa. watu kukaa na kuonyesha projection ya number of youths pasi kutafuta the real and valid solutions ni bure kabisa.
vijana wangeweza kuwa mobilized wakawa na vikundi ambavyo watafanya kazi na kupewa training ili kuboresha ujuzi wao na maisha yakasonga mbele. kuliko kumkopesha kijana mmoja mmoja, basi kwenye kikundi ni rahisi aid na wakafanya vitu ambavo hata serikali inge wasapoti kwa kuwa tafutia masoko usingewakuta wengi wako jobless kitaa. kwa Kiongozi mwenye akili njema wingi wa vijana kwake ni hazina kwani anajua hii ndio nguvu kazi na injini ya utendaji kwenye taifa lake. Lakini kwa taifa kama Tanzania vijana ni mzigo na hata wengine wakadiriki kusema ni bomu linalosubiri kulipuka jambo ambalo ni kashfa sana.
 
hahahaha, I am sure ukitaka kuchangia utachangia tu. kwani sisi tumesema mapya gani hapa yasio julikana? tunajaribu tu ku-underline implications za demography ya Tanzania. Nchi inapo kua na more under 18, what happens? what should the government do? Presentation imesema mengi. Umeipitia?
 

Very interesting... I never saw it this way.
But unacho sema sio tofauti sana na wanacho pendekeza haki elimu: kwa hiyo, hii ya bonus on performance (yaani expected output ni mtoto akijua kusoma na kuhesaabu) na hiyo payment for input (the traditional salary, for teaching his lessons) inatosha kwa mwalimu. Upande wa wanafunzi nao maybe mazingira bora (building, desks, vitabu) and that would solve MOST OF the problems. But you have added a new element that was not in the proposal: Mwanafunzi awe tayari kujifunza... and this I believe is the parent and student part... :A S 39:
 

Zaidi ya hayo uliosema hapo nadhani this will help consolidate that patriotic feeling ya wakati ule. Of course I believe the content of the course will also be adapted so as to nurture this.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…