Rich Mavoko aishtaki WCB kwa ‘mkataba wa kinyonyaji’

Rich Mavoko aishtaki WCB kwa ‘mkataba wa kinyonyaji’

Rich Mavoko ameleta mkataba wake na WCB na tutaupeleka kwenye kamati ya iliyoundwa na Waziri Mwakyembe ya kuangalia mikataba ambayo ni yakinyonyaji kwa wasanii" Katibu Mtendaji BASATA
 
Yaani badala ya kwenda mahakamani yeye anaishitakia serikali, chombo chenye mamlaka ya kutoa uamzi ktk mambo ya kisheria ni mahakama tu.

Halafu kwani kipindi anausaini huo mkataba hakuuona kama ni wa kinyonyaji anakuja kuuona leo au akili zake hazikua timamu kipindi anausaini(mwezi mchanga) au umri wa kuingia mikataba ulikua bado kwa hyo mtu alimsainia badala yake leo kakua ndio kagundua mkataba ulikua wa kilaghai.

Nyie wasanii mkome kabisa maana mnawaona wanasheria kama walipoteza muda wao kwenda shule, hapa ungekua na mwanasheria angekushauri kuhusu huo mkataba kabla hujausoma, wanasheria wanatumia technical terms ktk mikataba ambayo mara nyingine layman ni ngumu kugundua unakuja kugundua kumekucha.

Ninauhakika sasahivi umeahauriwa na lawyer na ishakuwa too late boy, pambana tu na hali yako unless you have to prove the opposite.
wakati ana sign alikuwa amelewa
 
Apambane kwenye game tu, huko kwingine atajimaliza tu angeendelea kimyakimya wengi wangemsifu
 
Kama mavoko amechoka kweli basi angeomba kumalizana vizuri tuu na WCB maana ameshajifunga minyororo na mkataba, hawezi kwenda popote, hiyo tume sijui kitu gani haiwezi ikabatilisha mkataba halali ulioingiwa kwa mujibu sheria zetu wenyewe.

Mavoko asipoangalia atalazimika kupambana na WCB mahakamani ataishia kupoteza pesa na muda wake mahakamani kufuatilia kesi, japo kuna wachache watamsifia na kumjaza ujinga ila ajue anaenda kjipoteza, angetafuta njia ya busara zaidi kuondoka WCB , njia ya ugomvi inaweza kutoa sadaka career yake yote.
 
Kwani alilazimishwa kutia sahihi huo mkataba? Au anatafuta kiki za kumuweka kwenye chat?

Yeye ni mwanaume kama alivyo aliyeanzisha wcb. Apambane nayeye aanzishe label yake


Alilogwa na Babu Tale hakuona baadhi ya maandishi
 
Kama mavoko amechoka kweli basi angeomba kumalizana vizuri tuu na WCB maana ameshajifunga minyororo na mkataba, hawezi kwenda popote, hiyo tume sijui kitu gani haiwezi ikabatilisha mkataba halali ulioingiwa kwa mujibu sheria zetu wenyewe.

Mavoko asipoangalia atalazimika kupambana na WCB mahakamani ataishia kupoteza pesa na muda wake mahakamani kufuatilia kesi, japo kuna wachache watamsifia na kumjaza ujinga ila ajue anaenda kjipoteza, angetafuta njia ya busara zaidi kuondoka WCB , njia ya ugomvi inaweza kutoa sadaka career yake yote.
Assume clouds media iko myuma ya mavoko,hapo vp?
 
ALISAINI?
NANI KAVUNJA YEYE AU WCB?



AWALIPE!
ndo watajua maana ya kuwa na washauri wa kisheria.
 
BADO ATAKAYEUMIA NI YEYE AS AN INDIVIDUAL!
ana HELA YA KUWALIPA WCB kwa kuvunja mkataba?
Hivi mkuu mchezaji wa Simba akivunja mkataba wake na kuhamia yangu,nani ambae hua analipia hio pesa ya kuvunja mkataba?Ni Yanga iliyomnunua au huyo mchezaji?
 
Hivi mkuu mchezaji wa Simba akivunja mkataba wake na kuhamia yangu,nani ambae hua analipia hio pesa ya kuvunja mkataba?Ni Yanga iliyomnunua au huyo mchezaji?
MUULIZE MRISHO NGASSA!
 
Na ni kweli ndiyo maana walikuwa wanaplay nyimbo zake redioni kumbe wanamkakati. Sasa watampeleka wapi?
Mkuu tujiulize kwanini wkt Rich yuko huko WCB clouds ilikua kama haimuoni vile,ghafla paap nyimbo zake zinapigwa fresh baada ya kutoka WCB?

Nadhani next project ya Ruge ni kumrudisha bwn mdogo kwny chat,uzuri akitulia kipaji Rich anacho.
 
Hivi mkuu mchezaji wa Simba akivunja mkataba wake na kuhamia yangu,nani ambae hua analipia hio pesa ya kuvunja mkataba?Ni Yanga iliyomnunua au huyo mchezaji?
NA HAPO UNAZUNGUMZIA TIMU ZA MPIRA!

CLOUDS NI LEBO YA MUZIKI?
 
NA RICHI SASA HIVI ANA MZIKI GANI KIASI HASA CLOUDS WAINGIE HIYO GHARAMA YA KUMLIPIA KUVUNJA MKATABA ALIOSAINI MWENYWE KWA UZUZU WAKE?
 
Back
Top Bottom