Rich Mavoko aishtaki WCB kwa ‘mkataba wa kinyonyaji’

Kama mambo yaliyoandikwa kweny mkataba hayatekelezw kwanini msanii uendelee kubaki hapo
 
Ngoja namm nipitie mkataba niliosaini na demu wangu
 
Mkuu tujiulize kwanini wkt Rich yuko huko WCB clouds ilikua kama haimuoni vile,ghafla paap nyimbo zake zinapigwa fresh baada ya kutoka WCB?

Nadhani next project ya Ruge ni kumrudisha bwn mdogo kwny chat,uzuri akitulia kipaji Rich anacho.
mkuu lini wamepiga nyimbo za rich mavoko?
 
AH MAVOKO WANGU WEEEE.ACHA IBAKI STORI MIMI NAWEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEEE
 
Mavoko na wanaompa kichwa wasipocheza hii muvi kwa akili itakula kwao,,bora WCB wangekuwa wanavunja wao mkataba,ila sasahivi yeye mwenyewe anauvunja na aliusaini akiwa na akili timamu tena mbele ya basata wenyewe,,namwonea huruma sana mavoko,,kuvunja mkataba ulio halali kisheria na mlikubaliana nikazi ngumu na yenye gharama za kutosha tu na itamgharimu sana ,atapata stress pia akicheza hovyo,Kama mnakumbuka Diamond alivyovunja mkatabata na Aljaazilla Entertainment chini ya meneja Papa misifa alivyopata tabu sana enzi hizo(2011 au 2010)alidaiwa mil 500 ila kafanyiwa fair tu akalipa Mil 100 japo kwa awamu,sasa najaribu kumfikiria ndugu yangu hapa mavoko anavyotaka kuvunja mkataba wa miaka 10 kizembezembe tu,,think big mavoko,wanaokupa kichwa watakucost sana,wewe si umekimbilia BASATA?wenzio wataenda mahakamani kwenye sheria na wataku sue kesi inavyoendelea hautakuwa ukifanya kazi za mziki tena zaidi ya kurekodi tena kwa siri maana wewe bado unamkataba hai so haitaruhusiwa kupanda jukwaa lolote la burudani unless kesi iwe imeisha..Utapata tabu saana dogo..Fikiria upya maamuzi yako,kheri ukaenda mkayamaliza kishikaji tu,kibinadamu maana wote mnatafuta mkate wa kila siku ili wakuachie salama na kwa amani..
 
well said
 
[
Rich Mavoko ameleta mkataba wake na WCB na tutaupeleka kwenye kamati ya iliyoundwa na Waziri Mwakyembe ya kuangalia mikataba ambayo ni yakinyonyaji kwa wasanii" Katibu Mtendaji BASATA
Inabidi wakati wanapeleka hiyo mikataba ya kinyonyaji atoe tafsiri kwa wanamuziki maana ya MKATABA na awaulize kama walishikwa nguvu kusaini mkataba
 
KUNA MTU ANASEMA ATALIPIWA NA CLOUDS KWA KUWA CMG wana LEBO YA MUSIC INAITWA THT!
ATI MBONA WACHEZAJI TEAM ZA MPIRA WANAVUNJA MKATABA!
ahahahahahahahhahaha AMUULIZE NGASSA ndo atajua maana ya MKATABA NA KUUVUNJA!
TEN YRS CONTRACT UKAAMUE TU UMEAMKA ASBH NA CAROLITE ZAKO OH SITAKI!
ehehhehhee!
 
Inabidi Diamond akamatwe kwa utapeli. Ndio maana Mavoko amekonda sana kwasababu anakosa hata hela ya kula hela zote Diamond anajirusha na wakina Mobetu
Akamatwe kwa kosa lipi,wakati mkataba unajieleza wazi na afu isitoshe akulazimishwa kusign mkataba na kimantinki diamond platinumz anakosa lolote like,yeye rich mavoko apambane na hali yake na ndo kashapotea hivyo na atapata tabu Sana mwaka huu
 
Hivi mkuu mchezaji wa Simba akivunja mkataba wake na kuhamia yangu,nani ambae hua analipia hio pesa ya kuvunja mkataba?Ni Yanga iliyomnunua au huyo mchezaji?
Ujue hapa ni pande mbili tofauti,Kama angekuwa na meneja basi ndo Ange incur cost za kuvunja mkataba but kwasababu Ni mavoko as individual yeye mwenyewe ndo itambidi atoboke kinoma kama 1 billion ok mng'ato
 
Mkataba wa miaka mingi ni ule unaokufaidisha we we, na kwa terms zako
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…