Richard Temu, mlanguzi wa kakao Kyela anayepambana kuua Ushirika ili apate bei ya chini toka kwa wakulima moja kwa moja

Richard Temu, mlanguzi wa kakao Kyela anayepambana kuua Ushirika ili apate bei ya chini toka kwa wakulima moja kwa moja

Kuna vyama vya msingi. Ambavyo vinaweza kuundwa na wakulima kuanzia watano na kuendelea. Kisha kinakuwepo Chama cha Ushirika Cha wilaya. Mfano Kyela kuna vyama vya msingi takribani 39.
Sasa swali linakuja: inakuwaje hawa watu waliojiunga kwenye vyama vyao vya msingi wasiweze kujitetea mbele za hawa walanguzi?
Binafsi ningetegemea kwamba kujiunga kwao kwenye vyama hivyo ni pamoja na kuwapa sauti ya kujilinda dhidi ya hawa wanaofanya mambo ya kuhujumu juhudi zao zisifanikiwe.
 
Sasa swali linakuja: inakuwaje hawa watu waliojiunga kwenye vyama vyao vya msingi wasiweze kujitetea mbele za hawa walanguzi?
Binafsi ningetegemea kwamba kujiunga kwao kwenye vyama hivyo ni pamoja na kuwapa sauti ya kujilinda dhidi ya hawa wanaofanya mambo ya kuhujumu juhudi zao zisifanikiwe.
Changamoto hawa walanguzi hutoa hongo kwa baadhi ya viongozi wanaoshirikiana nao
 
Kuna vyama vya msingi. Ambavyo vinaweza kuundwa na wakulima kuanzia watano na kuendelea. Kisha kinakuwepo Chama cha Ushirika Cha wilaya. Mfano Kyela kuna vyama vya msingi takribani 39.
Sasa hao wenye vyama vya msingi wanaweza jitafutia wateja? Lazima chama cha msingi kiwe member wa chama cha wilaya? Ushirika wa kupangiwa na serikali ni wizi kama mwingine tu.
 
Mfumo wa ushirika unasaidia sana hata ukusanyaji wa mapato ya Serikali. Lakini zaidi unalenga kuboresha maisha ya wakulima na kuhakikisha wanapata bei bora ya mazao. Serikali huweka bei elekezi kulingana na bei ya soko la dunia.
Sasa mara nyingi wakulima wa vijijini hawajui bei ya soko la dunia. Hivyo ni rahisi kuwanyonya na wakati mwingine wanajidai wamegoma kununua hadi mnawapa kwa bei wanayotaka. Na wengi wanaofanya haya ni watanzania wasio na uzalendo wanaotumiwa na wahindi.

Sasa Serikali ikiweka utaratibu maana yake ni kuwa katika wilaya husika basi mzigo wote lazima upitie katika huo mfumo.

Lakini pia kupitia vyama vya msingi AMCOS kama wakipata mteja moja kwa moja mwenye bei nzuri basi wanaruhusiwa pia kuuza moja kwa moja bila kupitia stakabadhi ghalani. Bado lengo ni kuuza katika umoja ili kuwa na nguvu ya bargaining.

Mfano kila mtu akiruhusiwa kuuza atakavyo ni rahisi kuwachezea na kuwagawa na hatimaye kuwanyonya.
Lengo la ushirika ni serkali kuchukua chao kwa urahisi. Tena kuchukua kingi.
 
Richard Temu, ni mfanyabiashara mlanguzi wa kakao katika Wilaya ya Kyela, ambaye hulangua kwa bei ya chini toka kwa Wakulima na kuziuza kwa mfumo uliowekwa na Serikali wa Stakabadhi ghalani. Akishazipeleka pia hutumiwa na kampuni za wahindi kupeleka bid yao katika mnada ili waweze kununua na kuzipeleka nje ya nchi.

Yeye na wahindi wanaomtumia wanaona Chama Cha Ushirika cha KYECU na mfumo uliowekwa na Bodi ya Maghala ya Serikali (WRRB) ni kikwazo kwa sababu bei elekezi ya Serikali ya kakao kwa kilo moja ni Tshs. 4200.

Na kabla ya mfumo huo kuwepo walikuwa wakiwalangua wakulima kwa bei chini ya 1000 kwa kilo. Na iwapo mfumo huu watafanikiwa kuua na wakulima wakakosa soko la uhakika wao watawapangia bei ya kununua zao hilo sababu Mkulima hatakuwa na namna nyingine.

Na hiyo bei elekezi ya 4200 ni minimum kuanzia mnada, na kuna wakati kakao inanunuliwa hadi kwa zaidi ya 5000 kwa kilo moja. Hivyo kuwafanya walanguzi hawa kukosa kupiga margins kubwa zaidi huku wakiwanyonga na kuwanyonga Wakulima.

Richard Temu na wafanyabiashara wanaomtumia wanapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu ili kuzuia hujuma wanazofanya ili kuua Ushirika jambo litalopelekea Serikali kukosa kodi ya uhakika na wakulima kukosa bei nzuri na soko la uhakika.

Kwenu Taasisi za Umma.
Piga busha uyo unachelewesha nn
 
Lengo la ushirika ni serkali kuchukua chao kwa urahisi. Tena kuchukua kingi.
Sio kweli eti wanachukua kingi. Ushuru unajulikana. Katika ushirika serikali inakusanya kodi kwa urahisi maana kampuni inayonunua ndio inalipa moja kwa moja. Nje ya ushirika wanakusanya ushuru kwa idadi ya magunia. Sasa mkusanya ushuru anapewa chake. Anasema kuna gunia 10 kumbe ziko 100. Mapato yanapotea na serikali inashindwa kufanya kazi muhimu ya kuwasaidia wakulima japo hata kupata mbegu bora.
 
Sasa hao wenye vyama vya msingi wanaweza jitafutia wateja? Lazima chama cha msingi kiwe member wa chama cha wilaya? Ushirika wa kupangiwa na serikali ni wizi kama mwingine tu.
Chama cha msingi kinaweza kujitafutia mteja kwa mujibu wa muongozo wa ushirika. Hivyo vina uhuru. Muhimu wasiuze chini ya bei elekezi ya Serikali.
 
Hapo sasa!
Hilo ndilo tatizo linalotakiwa kupigwa vita bila ya huruma yoyote.
Muulize kwamba kwanini pamoja na hoja yake kwamba KYECU inanunua kwa bei nzuri lakini wakulima wanaamua kuuza kwa bei ya chini kwa walanguzi ?

Mimi pia natoka Kyela , naijua KYECU
 
Muulize kwamba kwanini pamoja na hoja yake kwamba KYECU inanunua kwa bei nzuri lakini wakulima wanaamua kuuza kwa bei ya chini kwa walanguzi ?

Mimi pia natoka Kyela , naijua KYECU
Nafikiri hujaelewa. Wakulima wanapeleka KYECU. Sasa huyu jamaa kupitia wanaomtumia wanapambana KYECU ife ili wajipangie bei sababu mkulima hatakuwa na chombo cha kuregulate bei nzuri.
 
Richard Temu, ni mfanyabiashara mlanguzi wa kakao katika Wilaya ya Kyela, ambaye hulangua kwa bei ya chini toka kwa Wakulima na kuziuza kwa mfumo uliowekwa na Serikali wa Stakabadhi ghalani. Akishazipeleka pia hutumiwa na kampuni za wahindi kupeleka bid yao katika mnada ili waweze kununua na kuzipeleka nje ya nchi.

Yeye na wahindi wanaomtumia wanaona Chama Cha Ushirika cha KYECU na mfumo uliowekwa na Bodi ya Maghala ya Serikali (WRRB) ni kikwazo kwa sababu bei elekezi ya Serikali ya kakao kwa kilo moja ni Tshs. 4200.

Na kabla ya mfumo huo kuwepo walikuwa wakiwalangua wakulima kwa bei chini ya 1000 kwa kilo. Na iwapo mfumo huu watafanikiwa kuua na wakulima wakakosa soko la uhakika wao watawapangia bei ya kununua zao hilo sababu Mkulima hatakuwa na namna nyingine.

Na hiyo bei elekezi ya 4200 ni minimum kuanzia mnada, na kuna wakati kakao inanunuliwa hadi kwa zaidi ya 5000 kwa kilo moja. Hivyo kuwafanya walanguzi hawa kukosa kupiga margins kubwa zaidi huku wakiwanyonga na kuwanyonga Wakulima.

Richard Temu na wafanyabiashara wanaomtumia wanapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu ili kuzuia hujuma wanazofanya ili kuua Ushirika jambo litalopelekea Serikali kukosa kodi ya uhakika na wakulima kukosa bei nzuri na soko la uhakika.

Kwenu Taasisi za Umma.
Kwanini msigome kuuza

Gomeni msiishie kulalamika

Chukueni hatua

Kwani mkigoma kuuza mtalazimishwa kuuza

Ova
 
Muulize kwamba kwanini pamoja na hoja yake kwamba KYECU inanunua kwa bei nzuri lakini wakulima wanaamua kuuza kwa bei ya chini kwa walanguzi ?

Mimi pia natoka Kyela , naijua KYECU
Haya mambo ndiyo huwa yananipa taabu sana kuyaeleza watu wayaelewe vizuri, na nina wasiwasi (suspect) hata wewe huenda tusielewane juu ya hili, kutokana na maneno machache uliyotumia hapa.

Niulize: Je KYECU ni kweli wananunua kwa bei ya juu kuliko bei wanayolipa wafanya biashara, halafu bado wananchi wanaamua kuuza mazao yao kwa wafanya biashara? Hili linaingia akilini kweli?

Na kama bado hunielewi ni hivi: KYCU, bila shaka ina matatizo yake makubwa ndiyo maana wananchi hawaendi huko.
Na mimi nasema:

kwani ni lazima KYECU iwe na matatizo hayo?

Inakubalika kwamba ni jambo la kawaida KYCU kuwa na hayo matatizo?

Inategemewa na kukubalika na watu, na viongozi, kwamba KYECU inabidi iwe na matatizo hayo?

KYCU haitazamiwi kufanya kazi zake kwa ufanisi?

Hawa wafanya biashara binafsi hawana mchango wowote katika matatizo ya KYCU?

Kwa nini?

Ninaomba tu unielewe mkuu wangu Erythro, kwa haya ninayoyasema hapa, kwa sababu najua hii ni sehemu ambayo tunapishana (kidogo), lakini tunapishana kwa kuheshimiana. Na naomba ibaki hivyo hivyo.
 
Nafikiri hujaelewa. Wakulima wanapeleka KYECU. Sasa huyu jamaa kupitia wanaomtumia wanapambana KYECU ife ili wajipangie bei sababu mkulima hatakuwa na chombo cha kuregulate bei nzuri.
Haya mambo yapo kila sehemu ndani ya nchi hii, na haya ndiyo yanayotukwamisha, wakati tukiwachekea nyani wanaomaliza mahindi yetu!
 
Nafikiri hujaelewa. Wakulima wanapeleka KYECU. Sasa huyu jamaa kupitia wanaomtumia wanapambana KYECU ife ili wajipangie bei sababu mkulima hatakuwa na chombo cha kuregulate bei nzuri.
Kama wakulima wakikataa kushirikiana naye itakuwaje ?
 
Back
Top Bottom