Na wala yeye hawalazimishi bali wao ndio wanamfuata ili wapate pesa ya ubwalwa(pombe), Wanyakyusa wa Kyela ni pasua kichwa ni wajuaji mno wakati hakuna kitu.Kama wakulima wakikataa kushirikiana naye itakuwaje ?
Dah ridh1Nyuma yake kuna mtu anaitwa MO na bila Shaka unajua nyuma ya MO kuna akina nani, kila la heri katika mapambano yenu!!!
Kyecu ijichunguzeNa wala yeye hawalazimishi bali wao ndio wanamfuata ili wapate pesa ya ubwalwa(pombe), Wanyakyusa wa Kyela ni pasua kichwa ni wajuaji mno wakati hakuna kitu.
Hoja yako ni nzuri , wala hatupishani sana , ni hivi kabla ya Kyecu kulikuwa na KYERUCU , mleta uzi anajua hili , na pia anajua kwanini hivi vyama vilikufa , lakini pia anajua kwanini utaratibu wa Stakabadhi ghalani uliletwa na Magufuli na kupigiwa upatu na Mwakyembe , Ubunge wa Mwakyembe ulipeperushwa kwa kiasi kikubwa na jambo hili , wananchi hawataki vyama vya ushirika kwa sababu vinachelewesha malipo yao .Haya mambo ndiyo huwa yananipa taabu sana kuyaeleza watu wayaelewe vizuri, na nina wasiwasi (suspect) hata wewe huenda tusielewane juu ya hili, kutokana na maneno machache uliyotumia hapa.
Niulize: Je KYECU ni kweli wananunua kwa bei ya juu kuliko bei wanayolipa wafanya biashara, halafu bado wananchi wanaamua kuuza mazao yao kwa wafanya biashara? Hili linaingia akilini kweli?
Na kama bado hunielewi ni hivi: KYCU, bila shaka ina matatizo yake makubwa ndiyo maana wananchi hawaendi huko.
Na mimi nasema:
kwani ni lazima KYECU iwe na matatizo hayo?
Inakubalika kwamba ni jambo la kawaida KYCU kuwa na hayo matatizo?
Inategemewa na kukubalika na watu, na viongozi, kwamba KYECU inabidi iwe na matatizo hayo?
KYCU haitazamiwi kufanya kazi zake kwa ufanisi?
Hawa wafanya biashara binafsi hawana mchango wowote katika matatizo ya KYCU?
Kwa nini?
Ninaomba tu unielewe mkuu wangu Erythro, kwa haya ninayoyasema hapa, kwa sababu najua hii ni sehemu ambayo tunapishana (kidogo), lakini tunapishana kwa kuheshimiana. Na naomba ibaki hivyo hivyo.
poleni na matatizo. Hebu tujuze bei za mnada?Richard Temu, ni mfanyabiashara mlanguzi wa kakao katika Wilaya ya Kyela, ambaye hulangua kwa bei ya chini toka kwa Wakulima na kuziuza kwa mfumo uliowekwa na Serikali wa Stakabadhi ghalani. Akishazipeleka pia hutumiwa na kampuni za wahindi kupeleka bid yao katika mnada ili waweze kununua na kuzipeleka nje ya nchi.
Yeye na wahindi wanaomtumia wanaona Chama Cha Ushirika cha KYECU na mfumo uliowekwa na Bodi ya Maghala ya Serikali (WRRB) ni kikwazo kwa sababu bei elekezi ya Serikali ya kakao kwa kilo moja ni Tshs. 4200.
Na kabla ya mfumo huo kuwepo walikuwa wakiwalangua wakulima kwa bei chini ya 1000 kwa kilo. Na iwapo mfumo huu watafanikiwa kuua na wakulima wakakosa soko la uhakika wao watawapangia bei ya kununua zao hilo sababu Mkulima hatakuwa na namna nyingine.
Na hiyo bei elekezi ya 4200 ni minimum kuanzia mnada, na kuna wakati kakao inanunuliwa hadi kwa zaidi ya 5000 kwa kilo moja. Hivyo kuwafanya walanguzi hawa kukosa kupiga margins kubwa zaidi huku wakiwanyonga na kuwanyonga Wakulima.
Richard Temu na wafanyabiashara wanaomtumia wanapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu ili kuzuia hujuma wanazofanya ili kuua Ushirika jambo litalopelekea Serikali kukosa kodi ya uhakika na wakulima kukosa bei nzuri na soko la uhakika.
Kwenu Taasisi za Umma.
Hapo sasa,ndipo tatizo linapoanzia,Wakulima kwanini waende kwake kuuza kwa 1000 wakati wanajua serikali wananunua kea 4200?
Hili ndilo tatizo ambalo naamini halihitaji digrii kubwa kubwa kulimaliza, lakini ni tatizo linalopaliliwa lizidi kushamiri, kwa sababu kuna watu wanaofaidika kutokana na tatizo hilo kuwepo.wananchi hawataki vyama vya ushirika kwa sababu vinachelewesha malipo yao .
ukweli ni kwamba serikali haina hela za kununua mazao ya wakulima , inawakopa halafu itawalipa baada na yenyewe kuyauza , hapa ndipo penye ucheleweshaji , yaani serikali hailipi mpaka ipate cha juu kwanza .Hili ndilo tatizo ambalo naamini halihitaji digrii kubwa kubwa kulimaliza, lakini ni tatizo linalopaliliwa lizidi kushamiri, kwa sababu kuna watu wanaofaidika kutokana na tatizo hilo kuwepo.
Nchi nzima tatizo ni hili hili, lakini serikali nayo haina uwezo wa kulishughulikia! Maajabu si ni hayo?
Hiki ndicho kinachonizungusha akili nionekane kama hayawani wakati mwingine.ukweli ni kwamba serikali haina hela za kununua mazao ya wakulima , inawakopa halafu itawalipa baada na yenyewe kuyauza , hapa ndipo penye ucheleweshaji , yaani serikali hailipi mpaka ipate cha juu kwanza .
kwa bahati mbaya sana Vyama vya ushirika vinawajibika kwa serikali badala ya kuwajibika kwa wakulima ambao ndio wanachama , sijui kwanini , Viko kama TUCTAHiki ndicho kinachonizungusha akili nionekane kama hayawani wakati mwingine.
Chama cha Ushirika, kama KYECU ni ya serikali, au ninakusoma vibaya?
Hata hivyo, kiwe au isiwe ya serikali kwa kweli hakuna kinachobadilika, kwa sababu wote tunajua utendaji wao ni mbovu; na ndiyo maana, tokea huko nyuma hadi hapa tulipofikia, wimbo wetu maarufu ni kwamba :Serikali haiwezi kufanya biashara!
Lakini mbona serikali inafanya biashara na wafanya biashara wenyewe kila siku, na hakuna anayeuliza juu ya hilo?
Mkuu, Erythro, tuyaache haya, yapo nje ya uwezo wetu. Hata tuimbe vipi, hakuna kitakachobadilika. Wakulima wataendelea kunyongwa hivyo hivyo, na wafanya biashara wataendelea kuneemeka juu ya migongo ya hawa watu, kwa sababu serikali inayotakiwa kuwa kati kusimamia maslahi ya kila upande haina uwezo wa kufanya hivyo kwa utashi wake yenyewe.
Na hao wakulima wenyewe, hata hawaoni ushiriki wa serikali yao katika kuendeleza uduni wa maisha yao, kila mwaka!
Wafanya biashara, wanakwenda kukopa, ili wakanunue mazao ya wakulima kwa bei itakayowafaa wao; serikali inakwenda kukopa pia, lakini malengo yake ni mbali kabisa na kuwanufaisha wakulima.
Hata mababu pia hupeleka kakao katika mfumo wa stakabadhi gharani.Mkuu kokoa nipande mimi,nihangaike nazo mimi halafu kutoka kusiko julikana eti serikali au mtu waje wanipangie bei au mtu wa kununua, nadhani wana Kyela hapa tuwe wabunifu inatakiwa tutafuta wenyewe masoko, na tungekuwa na akili tungeweza hata kuanzisha usharika wa kiwanda kidogo cha kuongezea thamani bidhaa ya kakau, si mmeona kakao yetu inapendwa sana nje na kuna makampuni yananunua moja kwa moja hii kakau, hebu angalieni mfano wa Mababu Cocoa farms wanavyofanya.
Umeuliza swali Kuntu.Wakulima kwanini waende kwake kuuza kwa 1000 wakati wanajua serikali wananunua kea 4200?
Kwanza hakuna bodi ya kokoa.Tafuta taarifa ndio uongee haya. Ushirika wa mahala husika unaundwa na Wakulima wa zao husika. Na bodi ya huo Ushirika inaundwa na wakulima waliochaguliwa na wakulima wenyewe. Na bodi hiyo ndio ina mamlaka na maamuzi ya mambo yote katika ushirika. Na siku ya mnada wakulima ndio wanaamua bei ya kuuza zao kutokana na kampuni iliyoweka bei kubwa. Wasiporidhika mnada unaahirishwa kwa siku mbili.
Tafuta pesa acha majunguRichard Temu, ni mfanyabiashara mlanguzi wa kakao katika Wilaya ya Kyela, ambaye hulangua kwa bei ya chini toka kwa Wakulima na kuziuza kwa mfumo uliowekwa na Serikali wa Stakabadhi ghalani. Akishazipeleka pia hutumiwa na kampuni za wahindi kupeleka bid yao katika mnada ili waweze kununua na kuzipeleka nje ya nchi.
Yeye na wahindi wanaomtumia wanaona Chama Cha Ushirika cha KYECU na mfumo uliowekwa na Bodi ya Maghala ya Serikali (WRRB) ni kikwazo kwa sababu bei elekezi ya Serikali ya kakao kwa kilo moja ni Tshs. 4200.
Na kabla ya mfumo huo kuwepo walikuwa wakiwalangua wakulima kwa bei chini ya 1000 kwa kilo. Na iwapo mfumo huu watafanikiwa kuua na wakulima wakakosa soko la uhakika wao watawapangia bei ya kununua zao hilo sababu Mkulima hatakuwa na namna nyingine.
Na hiyo bei elekezi ya 4200 ni minimum kuanzia mnada, na kuna wakati kakao inanunuliwa hadi kwa zaidi ya 5000 kwa kilo moja. Hivyo kuwafanya walanguzi hawa kukosa kupiga margins kubwa zaidi huku wakiwanyonga na kuwanyonga Wakulima.
Richard Temu na wafanyabiashara wanaomtumia wanapaswa kufuatiliwa kwa ukaribu ili kuzuia hujuma wanazofanya ili kuua Ushirika jambo litalopelekea Serikali kukosa kodi ya uhakika na wakulima kukosa bei nzuri na soko la uhakika.
Kwenu Taasisi za Umma.
wakuu huu mfumo wa stakabadhi ghalani unafanyaje kazi?wengine ambao mikoa yetu haina mifumo hiyo tuko gizani.wanaouelewa vzr plz just a hint ili na sisi tupate elimu.Zao hili ni mti. Ukipanda unaanza kuvuna baada ya miaka mitatu. Na utavuna kwa hadi miaka 50. Na zao hili halina msimu, kwa maana kuwa unavuna kila wiki. Tofauti tu kuna muda uzalishaji uko juu na wakati mwingine uko chini. Lakini ukilima una uhakika wa kupata pesa kila wiki kama wachezaji wa mpira wa Ulaya. Kiufupi ni kilimo kizuri. Hata Mvomero tayari hivi sasa wanavuna na kuuza kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani.