Ridhiwani Kikwete: Mfumo wa usaili wa ajira sasa kufanyika online. Hakuna tena kwenda Dodoma kwa usaili

Pfizer

JF-Expert Member
Joined
Mar 25, 2021
Posts
590
Reaction score
807
Your browser is not able to display this video.

Naibu Waziri, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema mfumo wa usaili kwa njia ya kidigitali utapunguza gharama kwa kiasi kikubwa kwa wasailiwa wa ajira tofauti na hapo awali ambapo watu walilazimika kusafiri hadi Jijini Dodoma kwa ajili wa usaili wa ajira.

Kikwete ameyasema hayo leo katika uzinduzi wa usaili kidigitali baada ya kutembelea kituo cha usaili kidigitali Jijini Dar es Salaam na kufafanua kuwa serikali itaendelea kuboresha mfumo huo ikiwemo kuongeza vituo vya usaili nchini ili kila mtu mwenye sifa aweze kupata ajira

Nao baadhi ya wasailiwa waliojitokeza katika kituo hicho wameishukuru serikali kwa kuanzisha mfumo huo na kuongeza kuwa sasa wamepunguziwa gharama ikiwemo chakula, nauli na malazi pindi wanapotakiwa kwenda kwenye usaili wa ajira Jijini Dodoma.

#KaziInaendelea


Pia soma: Usaili kada za Serikali kufanyika Dodoma ni kipengele. Mfumo ubadilishwe
 
Moja ya mambo mengi mazuri ambayo Serikali ya awamu ya 6 imefanya ni kuwapunguzia Vijana wanatafuta kazi gharama Kwa kuanzia mfumo wa usaili kimtandao yaani online interview.

Hakika hili ni jambo la kupongezwa sana na nitoe kongole nyingi Kwa Rais Samia Kwa ubunifu huu wenye Tija.


My Take: Sasa nyie jobless mshindwe Wenyewe hakuna kisingizio tena.

View: https://www.instagram.com/reel/C5bfLBrPCqv/?igsh=OWljY2Jobnh2NWh2
 
Kazi nzuri ya Samia hii
 
Hii ni nzuri sana...


Lakini msisisahau jinsi Nape anavyobana internet, sijui kama mtatoboa maana 4G coverage yenyewe bado ni tatizo..

Pia mabando yako juu sana..
Acha kuwa lomolomo bila sababu za msingi. Maximum time ya kufanya hiyo test ni 90 minute hutumii hata GB 2 ambazo ni kama 5000 tu.

Sasa twende kwenye uhalisia wa kwenda Dodoma Kwa mtu anayetokea Dar es salaam tu. Nauli atatumia zaidi 50000 kwenda na kurudi, atatumia zaidi ya 30000 kwa ajili ya kula siku zote mpaka kusubiri matokeo ya written, atatumia zaidi 50000 Kwa ajili malazi na Kwa makadirio ya chini mtu anayetoka Dar kwenda Dodoma Kwa ajili ya usaili anatakiwa kuwa na 150000 mfukoni hapo sijamgusia kabisa anayotoka kigoma au mara huko.

Sasa umerahisishiwa kutoka 150000 mpaka 5000 ya bando Bado unalalamika gharama ya bando, kweli watanzania ni walalamishi sana
 
Samia hana mpinzani

View: https://www.instagram.com/reel/C5bfLBrPCqv/?igsh=OWljY2Jobnh2NWh2
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…