Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

This is Curse kwetu sisi waafrika, Mh Waziri mkuu, Waziri wa nishati na madini na wote waliosomwa katika ripoti ya Mh. Mwakyembe walipaswa kuwa tayari kujiuzulu kwa kulinda heshima ya taifa letu na demokrasia ya nchi changa kama Tanzania, haina haja ya Mh. RAIS kufamya mabadiliko ya baraza la mawazili, ni vizuri viongozi wetu wakajua thamani na umuhimu uwajibikaji na kulinda heshima ya nchi badala ya masilahi yao binafsi. ni aibu kungojea maamuzi tofauti, na wanampa wakati mgumu mh. Raisi na kuiweka serikali ya CCM katika wakati mgumu kwa viburi vyao!!!!
 
Je Mwakyembe ana beef na EL? Je hawpatani? Je ndani aya CCM kuna mgawanyiko?

Au simply watu wamechoshwa na skandali za kila siku wakaona waseme ukweli?

Je Mwakyembe ni mwadilifu nae? Rekodi yake ikoje?

kwa nini kila mtu anapotimiza wajibu wake kunaibuka hisia kuwa watu hawaaminiani?

Mwakyembe katimiza wajibu wake na ni wajibu wa kila kiongozi kusema ukweli sio kuficha maovu kama haya .

Wanaelewana sana ila yeye mwakyembe ni mkweli.
 
Je Mwakyembe ana beef na EL? Je hawpatani? Je ndani aya CCM kuna mgawanyiko?

Au simply watu wamechoshwa na skandali za kila siku wakaona waseme ukweli?

Je Mwakyembe ni mwadilifu nae? Rekodi yake ikoje?

Mzalendohalisi,

Kwa leo ni hii ya hawa mafisadi akina Lowasa, Msabaha, Karamangi na wengine wote waliohusika na hii Richard Monduli.

Ya Mwakyembe kama yapo ipo siku tutamjadili tu. Kwa leo anastahili pongezi kwa haya ambayo yeye na kamati yake wamefanya, kazi ya kumfunga paka kengele, it is official sasa kwamba Lowassa ni FISADI.
 
Je Mwakyembe ni mwadilifu nae? Rekodi yake ikoje?

JF wakati mwingine bwana, ukimchunguza sana sana bata nyama yake unaweza usiile...mwacheni baba wa taifa linaoangamia Mh H.Mwakyembe rekodi yake ni nzuri, si umeona kazi yake ? nini zaidi heko mwakyembe
 
ukweli tutafurahi kikao cha CCM kikitoka na kile ambacho watanzania wengi tunakisibiri.


watanzania tuko tayari kukupa 100% JK ukitufanyia kile tunachokitaka.


na si chengine ila wahujumu wa nchi yetu uwafukuze serikalini na uwafunge mtoni kwa kuiba mtoto wa jumbe
 
Mpaka Kieleweke,
Usikonde nasubiri ripoti ya BOT,nadhani humo bwana Mkapa atakuwepo.Mimi sina muda wa kumuangalia mtu usoni.Hawa watu wametufanya sisi Watanzania mazumbukuku na sisi tumekubali kwa kuimbishwa ka wimbo ka AMANI.
 
kwa nini kila mtu anapotimiza wajibu wake kunaibuka hisia kuwa watu hawaaminiani?

Mwakyembe katimiza wajibu wake na ni wajibu wa kila kiongozi kusema ukweli sio kuficha maovu kama haya .

Wanaelewana sana ila yeye mwakyembe ni mkweli.

mpaka kieleweke,

Unajua duniani kuna mengi- pia kuna kulipiza visasi, kukumoana, au to represent reality!

Kwa hiyo hii reporti yawezekana kuna mengine yamefichika- sisi hatujui! Unajua ni mara ya kwanza kupata ripoti kama hii tena toka Mwkiti wa kamati akiwa mwana CCM!

Pia yawezekana Mwakyembe amesema ukweli kama inavyopasa! I just want to look into the matter in a larger picture!
 
Kinachosubiriwa sasa hivi ni utekelezaji wa haya yote... walking the talk..... Kuna kawaida ya viongozi kuja na maneno makali na matamu..... maisha bora kwa kila mtanzania na kadhalika.....

subiri uone usanii unaofuatia hapa...

tik tak tik tak tik tak...............

Mimi nasema sisi ndo wenye nchi huyu JK,najua atajaribu kupindisha mambo ili akina LOwasssa wasimpige dongo naye kwenye BOT kwa sababu huko inaonekana naye yumo.Sasa hatuna haja ya kumwacha Rais anayeweka maslahi yake mbele zaidi ya nchi.Asipochukua hatua zinazostahili;Watanzania tuingie barabarani.Asitubabaishe,hii nchi bila yeye itaenda tu.
 
Jamani mwakyembe kaacha nyumba inaungua moto. Nani atauzima moto huu? Au ndipo umeanza?
 
Mwakyembe , Dr. Harrison G.
GENERAL
ID No.:
MEMBER'S PICTURE
Salutation:
First Name:
Middle Name:
Last Name:
Member Type:
Constituent:
Political Party:
Office Location:
Office Phone:
Office Fax:
Office E-mail:
Member Status:
Start Date:
End Date:
Date of Birth
EDUCATION
School Name/Location Course/Degree/Award Start Date End Date Level
University of Torin - Italy PostGraduate Certificate in Intellectual Property 2001 2001 POSTGRADUATE
University of Hamburg (FRG) Doctor of Laws 1992 1995 PHD
University of Hamburg (FRG) Master of Laws (LL.M) 1990 1991 MASTERS DEGREE
University of Dar es Salaam Master of Laws (LL.M) 1984 1986 MASTERS DEGREE
University of Dar es Salaam Bachelor of Laws (LL.B) Hons 1980 1983 GRADUATE
Tanzania School of Journalism DIploma in Journalism 1975 1977 DIPLOMA
Milambo Secondary School A-Level Education 1973 1974 HIGH SCHOOL
Tabora Secondary School O-Level Education 1969 1972 SECONDARY
Kituli Primary School - Shinyange Primary Education 1962 1969 PRIMARY
Tukuyu Primary School - Rungwe Primary Education 1961 1962 PRIMARY
CERTIFICATIONS
Certification Name or Type Certification No. Issued Expires
No items on list
EMPLOYMENT HISTORY
Company Name Position From Date To Date
Zanzibar Goverment Commissioner 2001 2005
East African Community Member of Parliament 2001 2005
University of Dar es Salaam Head, Department of Constitutional Admin. Law 1999 2002
University of Dar es Salaam Senior Lecturer in Law 1998 2005
University of Dar es Salaam Head, Department of International Law 1997 1999
University of Dar es Salaam Lecturer in Law 1991 1997
University of Dar es Salaam Assistant Lecturer in Law 1986 1990
University of Dar es Salaam Tutorial Assistant in Law 1984 1986
Tanzania News Agency (SHIHATA) Journalist 1978 1980
Information Services Division Jounalist 1977 1977
POLITICAL EXPERIENCE
Ministry/Political Party/Location Position From To
Chama Cha Mapinduzi - CCM Youth Commander - Dar es Salaam 2004 2005
Chama Cha Mapinduzi - CCM Law Advisor 2001 2005
Chama Cha Mapinduzi - CCM Managing Director - UPL 1996 2005



PUBLICATIONS

Description
Published Date
No items on list
SPECIAL SKILLS
Skill Name or Description Years Experience Acquired Through Skill Level
No items on list

WHO IS WHO
Honourable Faki , Bakari S. [CUF]
Hon. Faki , Bakari S. [CUF]
Ole Constituency
Questions(9)
Supplementary Questions(3)
Contributions(9)
More Members>>

GLOSSARY

Bills
A Bill is a proposal for a new law, or a proposal to change an existing law that is presented for debate before Parliament. Bills are introduced in the House for examination, discussion.

Hansards
The official record of everything that is said in the House of Parliament, published on a daily basis.

Committee System
Tanzania Parliament possesses an organised system of committees which comprises Committees of parties or caucus, committees of the whole House, standing committees and Select Committees
FEEDBACK

If you need assistance concerning the technical aspects of the site please Click here
PRE-BUDGET DEBATE
Read Proceedings
 
Sasa na sisi tuwe makini basi.... maana imekuwa Mwakyembe... Mwakyembe.... Jamani kumbukeni alikuwa mwenyekiti tu... kuna wajumbe wenzake behind... him...

Kwa hiyo pongezi ziende kwenye kamati Nzima....
 
CCM mambo mazito

Waandishi Wetu, Dar na Dodoma Februari 6, 2008
Raia Mwema

HALI si shwari ndani ya Chama cha Mapinduzi (CCM) na Serikali yake na mji wa Dodoma sasa unatisha kutokana na dalili za wazi za kuwapo mgawanyiko mkubwa miongoni mwa viongozi na watendaji wa chama hicho tawala.

Mgawanyiko huo unatokana na wabunge wa CCM sasa kubaini kwamba chama chao kinakwenda mrama kutokana na kunyamazia uoza mwingi na masuala ya msingi yaliyoibua hoja kama za kampuni ya umeme ya Richmond na ubadhirifu ndani ya Benki Kuu (BoT).

RAIA MWEMA imefahamishwa kwamba pamoja na kuwapo vikao rasmi mjini Dodoma, vikao kadhaa visivyo rasmi vinafanyika usiku na mchana kujadili mipango na mikakati ya kuokoa jahazi.

Hali hiyo inatokea wakati wabunge wakitarajia kukabidhiwa leo ripoti ya Kamati Teule ya Bunge iliyochunguza kampuni ya Richmond na baadaye usiku baada ya kuahirishwa kwa kikao, wabunge wa CCM watakutana.

Pamoja na Rais Jakaya Kikwete kuwasili mjini Dodoma, juzi usiku kulifanyika kikao maalumu kilichowashirikisha mawaziri na manaibu mawaziri katika kile kilichoelezwa kuwekana sawa kuitetea Serikali ndani ya Bunge.

Mambo yanayoisumbua CCM na Serikali yake na ambayo yanatarajiwa kuibua mjadala na maamuzi mazito mjini Dodoma, ni uchunguzi wa kampuni ya Richmond na lile sakata la Benki Kuu ya Tanzania (BoT), linaloendelea kufukuta.

Aidha, kauli ya Rais Kikwete kwamba mawaziri na wabunge wanapaswa kuchagua kati ya biashara na siasa na uamuzi tata wa Spika wa Bunge, Samuel Sitta, kuahirisha safari yake ya kwenda Marekani ni ishara tosha kwamba hali ya kisiasa ndani ya CCM ni tete.

Wachunguzi wa mambo ya kisiasa mjini Dodoma wanasema hali ilivyo sasa haijapata kutokea katika historia ya CCM katika siku za karibuni na hiyo inazidishwa na misimamo ya kushitukiza ya Kikwete na hivyo kuonekana kama kiongozi asiyetabirika.

Wakati Spika Sitta anatangaza kwenda nchini Marekani kikazi, aliwaambia wabunge kwamba mambo yote mazito yatasubiri arejee, ikiwamo ripoti ya Richmond na ile ya ukaguzi wa BoT, sasa uamuzi wake wa ghafla kuahirisha safari hiyo na kurejea Dodoma unatoa mwangwi wa mtikisiko ndani ya CCM.

Taarufa zinasema Kamati Teule ya Bunge iliyoundwa kuchunguza mkataba wa kuzalisha umeme wa dharura uliokabidhiwa kampuni ya Marekani ya Richmond imekuwa katika shinikizo kubwa la kuiweka hadharani ripoti yake na hata baadhi ya viongozi wa juu wa Serikali hawajaiona ripoti hiyo iliyokabidhiwa kwa Spika Sitta.

Mwenyekiti wa Kamati hiyo teule, Mbunge wa Kyela (CCM) Dk. Harrison Mwakyembe na Makamu wake, Stela Manyanya, wamekua kimya tokea waikabidhi ripoti hiyo kwa Spika, lakini joto la ripoti hiyo limepanda na kuwafanya wabunge kuonyesha wazi kuwa “wakali.”

Mwishoni mwa wiki iliyopita, wabunge wote wakiwamo wa CCM walionyesha makali katika semina ya Wizara ya Nishati na Madini ambako walikataa kuchangia wala kusikiliza majumuisho kutoka kwa Waziri wa wizara hiyo, Nazir Karamagi na Naibu wake, William Ngeleja, wakisisitiza kupata kwanza ripoti ya Richmond.

Kitendo cha wabunge hao kilikua ni ishara tosha kuonyesha uwezekano wa wabunge wa CCM kushikamana kuwachukulia hatua mawaziri wake, katika mfululizo wa maamuzi mazito ndani ya chama hicho.

Awali Kamati Kuu ya CCM ilifanya maamuzi magumu ikiwa ni pamoja na uamuzi wa kutaka viongozi wasijihusishe na biashara lakini pia kutaka kuundwa kwa sheria ya kudhibiti matumizi ya fedha za kampeni, uamuzi ambao ulinukuliwa na Rais Kikwete katika hotuba yake ya mwisho wa mwezi Januari, 2008.

Katika kuonyesha mambo si shwari, Waziri Mkuu Edward Lowassa, anaelezwa kuitisha “kikao cha kikazi” cha mawaziri na manaibu wao mjini Dodoma juzi usiku, akiwataka kusaidia “kuwaelimisha” wabunge kuhusu nia njema ya Serikali katika kuileta kampuni ya Richmond.

Taarifa za ndani ya kikao hicho zinasema katika kikao hicho, lugha kali zilitolewa ikiwa ni pamoja na maonyo kwa mashabiki wa masuala ya Richmond badala ya kuitetea Serikali.

Hata hivyo mawaziri hao wanaelezwa kusita kuitetea Serikali kwa kitu ambacho hawajakiona na wengi walisema watafanya uamuzi wa kuitetea Serikali baada ya kuiona ripoti ya Richmond kwa maana inaweza kuwa na mapendekezo ama maoni ya kuisaidia Serikali badala ya hofu iliyopo kwamba huenda kamati itaikandamiza Serikali.

Mawaziri hao walielezwa pia kwamba ripoti hiyo ya kamati haitawasilishwa kwenye kamati ya wabunge wa CCM pekee na badala yake itawasilishwa kwa wabunge wote ili kuepuka kuonekana kwamba kuna nia ya kulindana uamuzi ambao uliungwa mkono na mawaziri wote.

Hata hivyo, uamuzi wa Spika kutangaza kwamba ni lazima mambo hayo yajadiliwe akiwamo ni kutokana na yeye kuwa ndiye pekee aliyekaa na ripoti hiyo kwa muda mrefu na kuisoma na hivyo kuwa rahisi kwake kusimamia mjadala wake tofauti na Naibu wake, Anne Makinda.

Kitendo cha yeye kurejea Dodoma kwa haraka akitokea Dar es Salaam alipofika tayari kwa safari, kunaelezwa kutokana na shinikizo kutoka kwa watu walio karibu naye, akiwamo Rais Jakaya Kikwete, ambaye waliongozana kwa safari ya Dodoma waliko sasa.

Wabunge karibu wote wa CCM sasa wameungana na wenzao wa upinzani katika kuhakikisha wanawawajibisha mawaziri wanaoonekana kuwa mzigo kwa wananchi na chama chao, kwa kile kinachoelezwa kwamba ni “moyo waliopewa na Rais Kikwete.”

Habari zaidi zinaeleza kwamba Naibu Waziri mmoja amekuwa akitangaza hadharani kwamba waziri mmoja anayatejwa kuhusika na sakata la Richmond, “anataka kuondoka na mtu” kwa hiyo wabunge wasimsikilize na badala yake waitetee Serikali.

“Sasa anapotuambia tuitetee Serikali halafu anamtaja waziri mmoja na kumuacha mwingine ana maana gani?” anasema Mbunge mmoja wa CCM aliyetembelewa na Naibu Waziri huyo jana.

Wakati Richmond ikisumbua vichwa vya viongozi wa Serikali, uchunguzi unaoendelea kuhusiana na kashfa ya Akaunti ya Fedha za Madeni (EPA) ndani ya BoT, nao unaendelea huku wanasiasa wanaotajwa kuhusika wakiendelea kuhaha kuhakikisha kwamba hawahusishwi.

Katika juhudi hizo benki moja nchini imehusishwa na kuficha nyaraka muhimu zinazomhusu mwanasiasa mmoja anayetajwa kuhusika na sakata hilo bila kujua kwamba nyaraka hizo zimekwisha kuchukuliwa na vyombo vya dola hata kabla ya kuundwa kwa timu ya wachunguzi.

Kwa mujibu wa habari hizo, benki hiyo inatuhumiwa kuwa katika hatua za mwisho za kuharibu ushahidi wa kadi ya kufungulia akaunti ambayo RAIA MWEMA limethibitisha kuwa na picha na saini ya mwanasiasa mmoja maarufu ambaye anatumia nguvu kubwa kuhakikisha hafahamiki.

Kamati inayoongozwa na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, imekuwa ikifanya kazi usiku na mchana ikiwa na vijana wenye utaalamu na mahesabu na nyaraka kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) na Polisi.

Vijana hao wanaelezwa kukabidhiwa vifaa na magari pamoja na mamlaka yenye nguvu za kufanya upekuzi na uchunguzi kwa mtu yeyote wakiwamo maofisa wa Serikali na wafanyabiashara wenye nguvu kubwa.

Kwa mujibu wa habari hizo, tayari mmoja wa watuhumiwa ambaye hajawahi kutajwa popote amekwisha kuhojiwa kwa saa kadhaa na ameonyesha kuchanganyikiwa kutokana na ushahidi uliopatikana kumhusu.

Kiongozi mmoja mwandamizi ameiambia RAIA MWEMA wiki hii kwamba, pamoja na misuguano yote inayotokana na matukio ya Richmond na BoT, Rais Kikwete ndiye anayeweza kuhitimisha kwa kufanya maamuzi mazito ili kuweza kuwaonyesha Watanzania kuwa ana nia ya dhati ya kuisafisha serikali yake na pengine chama.




 
Sasa tunataka wabunge kama wameyaona haya shinikiza kamati ya BOT iundwe tuone madudu ya huko nina uhakika tutapata Miziki ya kuruka majoka kama M. Jackson kama siyo Sarakasi za Kichina
 
Hawa majambazi wote Watanzania tunahitaji kuwatosa bila huruma. Tuko nao nadani ya boti moja lakini wenzetu wanaitoboa ili izame wakati wao wamevaa lifejackets.Sisi walalahoi tusio na lifejackets na tusiojua kuogelea ndo tutakaoangamia pale mtumbwi utakapozama. Tusiwaonee haya tuwatose kabla ya kuutoboa mtumbwi wetu.
 
njia ya kwenda ktk mafanikio ni ngumu sana siku zote, lakini njia ya Tanzania ni ngumu zaidi.Hawa jamaa wanadhani kasheshe za Nrb zimeota kama uyoga.Vijana na wapenda maendeleo wote tuamke sasa,kama mlinzi ndiye mwizi kuna haja gani ya kumpa kazi???
 
Hawa ndo Mafisadi wahusika wakuu wa sakata lote la Ricmond, ambao bila huruma wanawafanya watanzania waishi katika maisha mabovu mpaka sasa kwa kuangalia maslahi yao wenyewe. Wako wemgi sana kwenye listi, ila hawa ndo vinara wenyewe wanaojifanya Tanzania ni mali yao, wanaamua kwa jinsi wanavyofikili tu. Jamani watanzania, mnaonaje, hawa si wanatakiwa kuachia ngazi na Mkondo wa sheria kutembea juu yao? Maana hatuna imani nao hata kidogo na hawatufai kabisa. Ndugu JK watanzania 80% walikuamini na kukupa kura zao, sasa leo tunasubiri ufanye watanzania walichokuagiza na si vinginevyo. Mungu akubariki ufanye maamuzi yenye Busara ili kulinusu Taifa letu. Amen
View attachment 1078

Asante babaH kwa picha za mafisadi....

tik tak tik tak....
 
"Bw. Mohammed A. Gire alikiri mbele ya Ujumbe wa Kamati Teule uliotembelea Houston, Texas, Marekani kuwa moja ya sababu zilizoifanya kampuni yake kusitisha shughuli zake ni kutokana na kuandamwa kwa kuandikwa kila siku na vyombo vya habari vya Tanzania. Ikamlazimu kuajiri kampuni ya G&S Media Consultancy ili kupunguza makali ya maumivu aliyokuwa anayapata, haikusaidia"

Ningekuwa na uwezo wa kumnunulia kila mwana jambo Brandy au whisky ningefanya hivyo, hiyo para hapo juu bila shaka alikuwa anaisema JF maana JF walimkoma nyani kisawa sawa.
Tumeona tena kuwa TAKUKURU si chochote ni upuuzi tu, wanakamata mahakimu wa mahakama za mwanzo. Bila aibu mtu mzima akasema Richmond hakuna mazingira ya Rushwa, labda yeye kwake rushwa ni mlungula tu, poor Hosea!!
 
mpaka kieleweke,

Unajua duniani kuna mengi- pia kuna kulipiza visasi, kukumoana, au to represent reality!

Kwa hiyo hii reporti yawezekana kuna mengine yamefichika- sisi hatujui! Unajua ni mara ya kwanza kupata ripoti kama hii tena toka Mwkiti wa kamati akiwa mwana CCM!

Pia yawezekana Mwakyembe amesema ukweli kama inavyopasa! I just want to look into the matter in a larger picture!

Jamani nimekumbuka kuna tume iliundwa na Raisi, mwenyekiti akiwa jaji Kisanga (sina uhakika) iliwakilisha ripoti enzi za BWM, akaikataa, sinto shangaa hata hii wabunge wa CCM na mwenyekiti wao wakaibuka kuwa hii ya Mwakyembe imejaa wivu na visasi vya kisiasa wakaiweka kapuni kama ile ya jaji Warioba...
 
Haondoki mtu hapa! Lowassa for president 2015!!

Mkuu AV

Hii itakuwa Bomba maana Edward alipofikishwa Wapinzani hawaitaji kupiga hata kampeni.

Huyu ni kupiga miluzi tu ya FISADI.

Ulishawahi kusukuma Mlevi? Nina uhakika itakuwa kama hivyo labda atumie u-Kibaki ambao nina uhakika hawezi.
 
Waziri Karamagi alalamika kamati ya Richmond haikumtendea haki
Na Tausi Mbowe, Dodoma

Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi wamesema kamati hiyo haikuwatendea haki kwa kuwa haikuwapa nafasi ya kutoa maoni yao kama Watanzania wengine.


Akizungumza na Mwananchi jana mara baada ya ripoti hiyo kusomwa Bungeni, Waziri Karamagi alisema anasikitishwa na Kamati hiyo kwani haikumtendea haki kwa kuwa haikumpa nafasi ya kumuita na kumuhoji juu ya ufisadi huo hivyo Kamati hiyo ilitoa matokeo yake kwa hisia tu.


?Wote waliotajwa watakuwa wameitwa na kuulizwa na Kamati hiyo, mimi sikuulizwa ni suala la mantiki tu, walitakiwa kuniuliza ili adhabu hii ikitolewa na aadhibiwe mtu anayestahili na si kubambikizwa kwa mtu asiyestahili,?alisema Karamagi.


Hata hivyo, Waziri Karamagi alisema kuwa kuna mambo mengine yaliyosemwa katika ripoti hiyo yana mantiki, lakini pia kuna mengine hayana mantiki na kwamba maamuzi yake yametolewa kwa hisia tu.


Huku Karamagi akisema hivi, baadhi ya wabunge waliozungumza na Mwananchi walipongeza ripoti hiyo na kusema kuwa imeonyesha mwanga na kutika kufichua uozo uliopo na vitendo vya kifisadi vinavyoendelea.


Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Ziito Kabwe aliipongeza ripoti hiyo kwa kufanyakzi kwa uwazi na kuitaka serikali kuendea kufichua uozo uliopo katika sekta mbalimbali nchini.


Naye Mbunge wa Same Mashariki (CCM), Anna Kilango alisema sasa ameona Bunge linanguvu kwakuwa limeweza kutetea maslahi ya wananchi wake ambao kwa muda mrefu wamekuwa wakiumizwa na watu wachache wenye uchu wa maslahi yao.


Kilango alisema sasa wananchi watakuwa wameona wenyewe aliyoipeleka Shirika la Umeme Nchini (Tanesco) katika chumba cha Wagonjwa Mahututi (ICU) na kwamba ni lazima watu hao wajiuzulu.


Mbunge wa Karatu, Dk Willibrod Slaa amempongeza Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk Harrison Mwakyembe na wajumbe wengine kwa kufanya kazi nzuri yenye kutetea maslahi ya Taifa na kumtaka Rais Jakaya Kikwete kuwawajibisha wote waliohusika katika ufisadi huo.


?Kamati hii haikufuata itikadi, imezingatia maslahi ya nchi na Taifa kwa ujumla,

maeneo yote tuliyokuwa na wasiwasi yamewekwa hadharani, mapendekezo yapo wazi,?alisema Dk Slaa na kuongeza kuwa wote waliohusika moja kwa moja hawana budi kujiuzulu.


Alisema ingekuwa nchi ya Demokrasia jana wote waliotuhumiwa wangejiuzulu , lakini hapa chini watu wanashindwa kufanya hivyo, hivyo basi ni lazima Rais achukue hatua za haraka ili kuinusuruu hali hii,?alisema Dk Slaa.


Kiongozi wa Upinzani Bungeni, Hamad Rashid Hamad alisema Kamati hiyo imefanya kazi nzuri na kumtaka Rais Kikwete afuate taratibu za kiutawala kushughulikia wote waliotajwa kuhusika katika ufisadi huo.


Kiongozi huyo pia aliwataka wabunge kuweka pembeni tofauti zao za kiitikadi na badala yake kuweka mbele maslahi ya wananchi na Taifa ili Watanzania wapate mapendekezo yasiyoangalia utashi wa siasa pindi watakapopata fursa ya kuchangia ripoti hiyo.


Hata Hivyo, Waziri wa Miundombinu, Andrew Chenge alisema kuwa Kamati hiyo imechukua vitu kwa ujumla katika masuala ya sheria na kwamba imeshindwa kusema ni kifungu gani kinamakosa na wangefanya nini ili kunusuru hali hiyo.


?Kamati imefanya majumuhisho tu uwezo wa vijana waliopo katika ofisi ya Mwanasheria Mkuu katika masuala ya sheria ni mkubwa, watu watashangaa kusikia Kamati hiyo imekisema kuwa Mwanasheria Mkuu alishindwa kutoa ushauri mzuri,"alisisitiza Chenge.


Naye Mwenyekiti wa Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, aliukosoa ushauri wa Kamati Teule ya Bunge aliouita wa ?kumbembeleza? Lowassa wa kumtaka atumie utu uzima kufikiria juu ya yote yaliyoelekezwa kwake na ripoti ya kamati.


Alisema wanachotakiwa kukifanya wabunge, ni kutumia sasa mamlaka yao kufuta ajira ya Lowassa waliyoithibitisha baada ya rais kuwasilisha jina lake bungeni.


Vilevile alishauri wote waliohusika na kashfa ya Richmond wafikishwe mahakamani haraka iwezekanavyo ili kudhibiti wasitoroke nchini, ikiwa ni pamoja na kutaifisha mali zao.


mwanachi
 
Back
Top Bottom