Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

Ripoti ya Richmond Bungeni (FULL TEXT) na yatokanayo

You mean he was smart to them CCM......not to the rest of us....I dont think that he is still smart
 
He is a king maker; waweza kukuta ameshaandaa majaji, ameshapanga mambo yote halafu anakuja kututishia nyau

Mimi nashangaa sana nchi yetu, mtu anakuja anakuibia, anakutukana halafu anasema nataka akupe hadi mtu wa kumchunguza na kutoa hukumu... na ukikataa anasema eti ataacha mbinu zote na mirija yote anayoitumia kukuibia na kukugawia chenji, who the hell is this guy?

Sh!T

mkuu naomba niongeze pia iwe:

who the https://jamii.app/JFUserGuide is this guy?

inauma na inasikitisha sana jinsi tunavyobakwa kwa nchi yetu wenyewe ..

sorry mods ..
 
RA anatakiwa arudishwe kwao alikozaliwa shida ni usalama wa Taifa wanamwacha afanye analotaka wananchi waendelee kuteseka.

Hajahudhuria vikao vya bunge, alionekana tu pale JK alipotinga Bungeni kwenye suala la EPA. Yeye anaonekana kwenye CC na NEC huko ndo anapakusemea kwani kuna wenzie Makamba, Chenge, EL n.k Sasa ebu tusubiri NEC ijayo tupime nguvu zake, ameiteka nchi.

K4jolly!
Nina uhakika hufahamu nguvu aliyonayo Rostam Aziz yeye ndiye aliMWAMRISHA Kikwete amteue Lowasa kuwa Waziri Mkuu. Kwa bahati nzuri Teddy Lowasa aliachiwa laana na Julius Kambarage Nyerere that is how kwa muujiza ameweza kuachia ngazi. Bosi wa Usalama wa Taifa amaeteuliwa na RA ikiwa ni pamoja na yule changudoa Sophia Simba.Wateule wa R.Aziz ni wengi nikianza kuwataja hapa kurasa hazitoshi.
The Bastard is well connected na analindwa na hao Polisi/usalama wa Taifa na special Branch. Actually Jakaya Mrisho Kikwete aliingizwa Ikulu na Rostam Aziz na pesa zetu wenyewe za EPA kama mwabisha kwa nini Kagoda imefilisiwa and some fools believe it can come back to life. Hapa panatakiwa mtu kama marehemu Sokoine atumia sheria ya uhujumu uchumi awakate vichwa wahusika wote and I mean it wate hata presida kama aligusa ile senti kwani kisheria it is a closed subject ndio maana huyu jambazi anataka kuunda tume ya majaji ambao wate kawateua yeye including the Chief Justice .

NOTHING IS GOING TO HAPPEN TO MAFISADI WOTE and Narudia as long AS jakaya Mrisho kIKWETE yuko pale ikulu. Kwa lugha ya kijiweni imekula kwetu.
Watu wamelia wee lakini hadi dakika hii Salva Rweyemamu mteule wa RA bado yuko kule ikulu. Mpaka atakapoamua RA Vinginevyo hakuna cha tume ya Harrison malafyale au Alhaji Hassan Mwinyi. Let me tell you the presidency of JMKikwete is the worst na definately is nursing the burial of CCM
 
vipi tena jamani mambo ya nyangumi?
Umefurahi kwa kuwa rostam kaiweka nchi mfukoni?
Si unaona anavyo weza kumburuza jk kuhusu nini kifanyike juu yake?
Kamati teule ile makini ya bunge mbona imetoa ripoti beyond uchunguzi wa kipolisi na imefanya uchunguzi ambao takukuru walishindwa na hawawezi.
Basi kwa kuwa jk.eostamu,lowasa na vikaragosi wengine wanaiamini zaidi takukuru basi tuiombe irudie tena uchunguzi wake.......................
Nilichoaandika hapo,ni kwamba hakuna aliyemsafi.
Wewe kwa akili yako unaamini John Samwel Malecele ni msafi?Tangu kuwa mkuu wa wilaya ya Rungwe miaka ya 70 mpaka kuwa waziri mkuu amefisadi vingapi?.Kilichomshitua leo na kupiga kelekele nini?

Unaamini Samwel Sitta ni mtu Safi?Tangu serikali ya mwinyi mpaka leo amefisadi vingapi?.Leo ameshituka nini?

Cha maana hapa ni sisi wananchi kusema sasa basi,ondokeni.Lakini ukiamini porojo za mwimbaji wa hip hop ndugu mwakyembe,unaona ni upuuzi.njaa tu hapo
 
Rostam Aziz anaichezea Serikali na kutukejeli Watanzania. Kwa hulka yake bila shaka ameishadhani anaweza kuwaweka mfukoni baadhi ya majaji ili wafanye anavyotaka. Na jinsi nchi hii inavyokwenda, haitashangaza kama watakuwepo majaji walio upande wa mafisadi papa. Rostam asingalithubutu kukurupuka na kutamka hivyo kama angelikuwa hana uhakika wa kuwapata majaji ambao wanaweza kuwa upande wake.

Aidha, bila shaka kwa kipindi chote hiki tangu uanzwe uchunguzi kuhusu Richmond au hata kabla, Rostam alikuwa akifanya kazi ya kuharibu na kufuta tracks ambazo zingaliweze kuthibitisha without reasonable doubt kwamba anahusika moja kwa moja na Richmond. Ni kweli na ni wazi kwamba Serikali haina ubavu wa kumchukulia hatua yoyote ya maana kwa sababu hadi leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa dhidi yake.

Shughuli hiyo ya kujaribu kufuta tracks ni mchezo mchafu unaofanywa na mafisadi papa. Hata Chenge anaucheza mchezo huo kwa sababu tunaanza kudokezewa taratibu kwamba vijisenti vya New Jersey havina uhusiano na manunuzi ya Rada! Na hao mafisadi papa wakianza kubebwa na Waziri anayehusika na Utawala Bora, basi tujue kwamba uwanja umeishatayarishwa na 'hakuna kesi ya kujibu'.

Nduguzanguni, kuna madudu na madhambi lukuki ambayo waheshimiwa wa nchi hii wameyatenda na wataendelea kuyatenda kwa kutumia madaraka tuliyowapa sisi wananchi kwa mategemeo kwamba watatuhudumia badala ya kujihudumia wao kwa kutumia mali za nchi ambazo zingaliweza kutumika katika kuleta maendeleo yetu kama taifa. Watu wa aina ya Rostam ambao kwa namna moja ama nyingine wametenda 'dhambi' ya kuwadhulumu wananchi wasio na hatia tusiwaachie wakaendelea kutukejeli; tuzidi kuwapigia kelele. Naamini kwamba hata kama itakuwa vigumu haki kutendeka lakini wanastahili kupata mateso kwa kusoma na kuzisikia kelele zetu dhidi yao kila kukicha. Nina hakika tangu sakata hili la Richmond na mengine yanayofanana nalo yaanze, Rostam na wahusika wengine hawapati/hawalali usingizi wa raha. Mwenyezi Mungu azidi kuwaadhibu hapa hapa duniani kwa dhuluma waliyoifanya kwa wananchi na Taifa letu kwa ujumla!
 
mkuu achana nae mimi naujua uadilifu wako Personally tangu ukiwa Stakishari, inatosha kuubeba mzigo wako , na wazee wakabeba wao, wewe ni mtu mzima, jiamini simama mwenyewe kama ambavyo siku zote umekua ukisimama, huna haja yakujiingiza kwenye mijadala ya kitoto.
.

Nguvumali.
Kuna watu wazima wajinga na ndiyo kama huyu.
Tatizo ni kujiweka hapa kama msafi wakati ni fisadi tu.

Mmetuibia vya kutosha sasa ondokeen! nasema ondokeen.
 
CCM wanadai Rostam ni Mtanzania, huwa najiuliza alizaliwa wapi? alisoma shule gani? alikulia wapi? maana hakuna hata mmoja anayesema alikuwa pamoja na Rostam, shule ya msingi, secondary ama hata university...jamaa aliibukia tu kwenye ufisadi na kuwa King Marker wa CCM na sasa anaogopewa kuliko hata raisi wa nchi. Rostam is everything in my beloved country.....!
 
Inadaiwa alitinga Tanzania mara ya kwanza 1979 toka Shirazi akija kwa wajomba zake waliokuwa wawindaji huko Igunga.Ni marehemu Azan Al-Jaabry ndio aliemtia CCM kwa mgongo wa marehemu Charles Kabeho.Sijawahi kusikia scoolmate,playmate,collegemate wake hata mmoja.Mbaya hakupita JKT ndio maana malafi hivyo......
 
Bob Marley aliimbana nukuu "You can fool some people sometime but you can't fool all the people all the time" Kama Rostam ansoma JF asome na kama wapambe wapo wamtaarifu kila kitu kina mwisho aache umafia wake it is too much.
 
Nilichoaandika hapo,ni kwamba hakuna aliyemsafi.
Wewe kwa akili yako unaamini John Samwel Malecele ni msafi?Tangu kuwa mkuu wa wilaya ya Rungwe miaka ya 70 mpaka kuwa waziri mkuu amefisadi vingapi?.Kilichomshitua leo na kupiga kelekele nini?

Unaamini Samwel Sitta ni mtu Safi?Tangu serikali ya mwinyi mpaka leo amefisadi vingapi?.Leo ameshituka nini?

Cha maana hapa ni sisi wananchi kusema sasa basi,ondokeni.Lakini ukiamini porojo za mwimbaji wa hip hop ndugu mwakyembe,unaona ni upuuzi.njaa tu hapo

Ni vizuri kama unaelezea hapa ukatoa ushahidi wa hao unaowataja! Mambo ya unajua........... leleleee............. hapa haitusaidii!

Huyu RA ripoti ipo inaeleza, soma Mwanahalisi ya leo jinsi Serelii alivyomchambua RA, kila mtu anajua na kila mtu anaelewa. Angalia usijeonekana kama mama SS unaposema sijui wote ni mafisadi kusudi kupoteza ushahidi! JITAMBUE CHUKUA HATUA!!!
 
Ni vizuri kama unaelezea hapa ukatoa ushahidi wa hao unaowataja! Mambo ya unajua........... leleleee............. hapa haitusaidii!

Huyu RA ripoti ipo inaeleza, soma Mwanahalisi ya leo jinsi Serelii alivyomchambua RA, kila mtu anajua na kila mtu anaelewa. Angalia usijeonekana kama mama SS unaposema sijui wote ni mafisadi kusudi kupoteza ushahidi! JITAMBUE CHUKUA HATUA!!!
ni kama vile Rostam anavyojiteteaga kuwa Mengi anamadeni mengi , ni yeye alifilisi NBC ...NA UPUMBAVU MWINGINE kama huo,
Kilichopo hapa ni namna gani RA amefilisi nnchi, anachofisadi HUYU MWARABU NI ZAIDI YA posho za kina Mwakyembe, huyu yuko kati ya hazina na BOT, AMETEGA BOMBA ZAKE HAPO, ANAINYONYA NNCHI kwelikweli, huyu ameshiriki kila kitukibaya katika nnchi hii,
Hakuna muda wakushughulikia vibaka wa kuku wakati kuna majangili, kama RA na wenzake wa kariba yake kama JEETU, manji , mzee wa Monduli na mzee wa vijisenti
 
Inadaiwa alitinga Tanzania mara ya kwanza 1979 toka Shirazi akija kwa wajomba zake waliokuwa wawindaji huko Igunga.Ni marehemu Azan Al-Jaabry ndio aliemtia CCM kwa mgongo wa marehemu Charles Kabeho.Sijawahi kusikia scoolmate,playmate,collegemate wake hata mmoja.Mbaya hakupita JKT ndio maana malafi hivyo......

Asante sana! Ni kweli hana school mate wala play mate hapa Tanzania. Ila CCM ukiwa fisadi wanakukaribisha mara moja....nchi yetu tujifunze kuwa na vetting sytem mtu hana hata uraia sasa hivi ni untouchable anaweza fanya lolote kwenye jamhuri ya Muungano hakuna wa kumyoshea kidole. Siwezi shangaa upupu alousema ndo ukatekelezwa kwa gharama nyingine kubwa. Tume ya majaji kumsafisha Rostam
 
kachelewa mpira upo bungeni, huko ndo lazima mshindi apatikane, hata kama raisi atakubali bado kiporo cha maazimo 23 lazima kiishe na mbaya zaidi wanavyozidi piga chenga ndo muda unayoyoma, bao hawarudishi, alas! uchaguzi huo 2010, image haisafishiki, sijui mhe. atanadiwa na nani, wapambe wamegombana...........
 
Sidhani kama tunafikiria sawa, ila RA ana huakika wa kutokutwa na tatizo maana aliwatumia wabongo wenzenu kufanya hayo.

He is smart!

Mbele za Mwenyezi Mungu hayuko smart midhali amefanya dhambi ya dhuluma kwa wananchi na Taifa. Tusubiri, time will tell, adhabu ataipata tu kwa namna moja ama nyingine.

Ni kweli ngozi nyeusi tunadanganyika na tunatumiwa sana kwa manufaa ya wengine. Angalia magazeti hivi sasa yanatia aibu maana haingii akilini kwamba Watanzania wenye uelewa kama Waandishi wa Habari wanaweza kushabikia mafisadi wakielewa wazi kwamba ufisadi ulitendeka/unatendeka. Badala ya kuandika ukweli kwa manufaa ya Taifa, wao hupindisha kwa sababu ya kupewa/kuahidiwa chochote ama huwakingia kifua maswahiba bila kujali kwamba kwa kufanya hivyo Taifa linaangamia. Kwa mfano gazeti la Tanzania Daima, Ssku hizi linatia kichefuchefu hata kusoma baada ya kuona frontpage headlines! Aibu, inasikitisha sana.
 
this is shame, hii nchi kwani hatuna sheria?? hatuna uongozi?? tunaongozwa na nini?? hili suala la richmond litaendelea mpaka lini? je JK haoni athari yake sasa, limevuruga serikali sasa linavuruga chama,bunge....sasa wanataka na mahakama ingilie..tutauwa nchi...
1. hawa wahusika wa richmond ni wababe sana, hakuna wakuthubutu kuwashika, ni miunguwatu
2. uongozi uliokuwepo umenufaika sana na ufisadi wa wahusika
3. uongozi unahusika moja kwa moja katika hii kashfa....

kama JK hatakuwa makini, nchi itamshinda, tumeongea sana kuhusu hili suala mpaka sasa inatia uvivu....
NANI WA KUMLILIA, KULA WAMEKULA WAO NA WAMETAJILIKA WAO...KISHA WANATAKA KUTUANGAMIZA KWA UBABE WAO...
JE JK ANAJUA WAJIBU WAKE KAMA MWENYEKITI WA CHAMA?
JE JK ANAJUA WAJIBU WAKE KAMA RAISI WA NCHI? MBONA KAMA HASHTUKI AU YEYE HAYUPO NCHI HII AMBAYO WANANCHI WAKE WAMEMPA UAMINIFU WA KUTUONGOZA...F**%%$&k
 
Asante sana! Ni kweli hana school mate wala play mate hapa Tanzania. Ila CCM ukiwa fisadi wanakukaribisha mara moja....nchi yetu tujifunze kuwa na vetting sytem mtu hana hata uraia sasa hivi ni untouchable anaweza fanya lolote kwenye jamhuri ya Muungano hakuna wa kumyoshea kidole. Siwezi shangaa upupu alousema ndo ukatekelezwa kwa gharama nyingine kubwa. Tume ya majaji kumsafisha Rostam

Nduguyangu Masanilo,
Ustaarabu na uadilifu wa vetting system ulikwenda kaburini hata kabla hajafariki Mwalimu Nyerere aliyekuwa anathamini na kutumia system hiyo kikamilifu katika utawala wake wa Awamu ya Kwanza. Kama umri ungelikuwa ukirudishwa nyuma wangelirudishwa akina Dr. Augustin Mahiga ambao walikuwa wakielewa nini maana ya uadilifu katika Idara nyeti kama ya Usalama wa Taifa.

Naam, tunahitaji sana kumpata Sokoine mwingine atakayeweza kurekebisha uozo unaoendelea nchini mwetu la sivyo Tanzania inasambaratika kwa kukosa nguvu ya kukemea maovu bila kusita.
 
Rostam asipokamatwa kwa Crimes against TZ, nchi itapasuka...my prediction
 
Ni hatari sana mchezo anaotaka kuucheza RA. Anataka na mhimili wa tatu uingie kwenye malumbano. Tunaona tayari mihimili miwili ya dola yaani serikali na Bunge inalumbana na kutishia uhai wa dola; sasa RA anataka mhimili wa tatu, yaani mahakama, nao uingizwe. Hii itakuwa vurugu tupu. Yaani serikali inasema lake, bunge linasema lake, na mahakama inasema lake.
Naunga mkono wazo la mafisadi kufanywa kama China - kupigwa risasi hadharani; lakini nani afanye hivyo? wakati chombo chenye uwezo wa kufanya hivyo ni serikali ambayo tayari RA ameiweka mfukoni?
Tunatakiwa tumpate mtu jasiri kama Kinjeketile Ng'wale - atutie ujasiri kuwa huyu RA na wenzake ni nyau tu, hata FFU wakija na mabomu yao tuamini kuwa ni majimaji tu, na tusonge mbele.
Wapi jasiri kama Mkwawa? wapi jasiri kama Mirambo wa Tabora? Maskini Sitta, umeshindwa kufikia angalau 5% ya ujasiri wa Mirambo!
Ebu ona ujasiri wa wafanyakazi wa TRL - 100%, nawahakikishieni wahindi wale wataondoka!!
Ebu ajitokeze Kinjeketile Ngw'ale wa karne hii - hakika tutamfuata wengi
 
Ni vizuri kama unaelezea hapa ukatoa ushahidi wa hao unaowataja! Mambo ya unajua........... leleleee............. hapa haitusaidii!

Huyu RA ripoti ipo inaeleza, soma Mwanahalisi ya leo jinsi Serelii alivyomchambua RA, kila mtu anajua na kila mtu anaelewa. Angalia usijeonekana kama mama SS unaposema sijui wote ni mafisadi kusudi kupoteza ushahidi! JITAMBUE CHUKUA HATUA!!!
.
Hilo ndilo tatizo kubwa la sisi wana jf.utafikiri watu hawajaenda shule.

Nikisema soma gazei la mtanzania alivyosema Sophia simba juu ya Anna Kilango, ndiyo ya ukweli?.Nikisema soma Nipashe aliyovyasema Mwakyembe juu ya Lowasa ni kweli?..

Mh Zito juzi alifafanua hapa kuwa kila mmoja ana mhariri wake.mara wakitoka uko kwenye vikao wanawapigia simu.

Sasa ,Mh Sererii kumchambua RA ndiyo hukumu ya mahakama?Walianza lini kumchambua RA?.Mbona mengi alichambuliwa na mpaka vielelezo kupelekwa pccb?haya ya ukweli?.Usiwe kasuku ndugu yangu.

Ifikike mahali sasa tusema basi.Wao wamezidiana kete humo ndani na kutuletea kelele za kuigiza hapa.
 
jamani....hii sasa ni kali ..........yaani imefikia mpaka jamaa anatupangia ni nani wamchunguze!...........damn!
 
Back
Top Bottom