Nelson Jacob Kagame
JF-Expert Member
- Dec 26, 2022
- 9,576
- 13,545
Ilikua usiku wa manane simu ikaita, na mara nyingi namba za nje ya nchi inamuwiaga vigumu kupokea..Akapokea na moja kwa moja sauti akaitambua ni ya nani""Safari hii mpigaji anazungumza vizuri kiswahili kuliko awali"".
Mpigaji alikuja na ofa na akaiweka wazi kwa mlengwa namaanisha mpigiwaji simu.Kuna valid item inatakiwa ichukuliwe kutoka kwa muhusika kabla makachero wengine hawajaiwahi na kuharibu mpango endelevu.
Na mpaka simu hii inapigwa muhusika yupo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Senou pale Bamako na haijulikani anaunganisha ndege ya kwenda wapi,ila cha muhimu kinachotakiwa ni mzigo alioubeba kwenye begi zake ndogo mbili.
Baada ya maelezo hayo mafupi mpigaji akawa kimya kisha akauliza""Upo tayari komredi kuchukua hii ofa"""au tuwape wale wayahudi?. Una dakika kumi na moja za kunipa jibu.
Kijana akapata ukakasi kujibu,kwanza simu imekuja ghafla,pili hataki ugomvi tena na vyombo vya dola vya nchi yoyote ile na tatu hataki kuiweka roho yake rehani kisa pesa, maana hajui hii oparesheni kiundani asije kua mbuzi wa kafara kuwanufaisha wanasiasa.
Kilichomuumiza kichwa ni kua ukikataa ofa ni kama umevunja kiapo na malipo yake ni kuonekana msaliti au mhaini unayestahili kifo ndani ya taasisi.
Bila kusita akasema nimekubali nipe details mkuu,nijue naanzia wapi.Na pia mkuu hakikisha target yetu pale Bamako Senou international airport, hapandi ndege za kwenda Athens au Kigali au Bangui au Brazzaville,ila arudi N"Djamena itakua kazi rahisi.
Na yeye kijana tumwite""Nyakamba"akasema baada ya 44hrs atakua Kabalaye akimsubiria amalize kazi ya kumpokonya mizigo hitajika..Nanukuu""Fanya chochote unachoweza mkuu jamaa arudi Chad"""mwisho wa kunukuu.
Mpiga simu akauliza nikuwekee kiasi gani cha pesa cha kuanzia operasheni,na akajibiwa dola elfu tisini za kuanzia zipatikane akifika Nairobi atazichukua cash na hati ya kusafiria ya Uganda pamoja na hati ya kusafiria ya Tanzania.
Baada ya hapo akifika Nairobi akute tiketi za ndege kwenda Bangui zipo tayari mezani.Mpiga simu akasema tutakutana kesho jioni Nairobi na akakata simu.
Nyakamba hakupata usingizi tena akaanza kuwaza mambo mengi sana na akakumbuka misheni ya mwisho ilivyofeli vibaya na akaishia kua mtu anaetafutwa na vyomba vya ulinzi na usalama nchini Congo Brazzaville.
Lakini akajipa moyo hii ndio kazi aliyoichagua cha msingi ni awe tu mwangalifu,akaamka na kuanza kujiandaa na safari ya kesho kwenda Nairobi kukutana na mkuu.
ITAENDELEA...
Kufika asubuhi na mapema hii ilikua july 16 1996 kijana Nyakamba anasikia honi nje ya geti la nyumba aliyokua amepanga kule kurasini kota""Pooh pooh""na upigaji wa honi hii ulikua sio mgeni kwake sababu ni code za mawasiliano za washirika wa taasisi.Fasta fasta akajua kumeiva akatokea mlango wa nyuma wa ua ya ile nyumba mpaka barabarani akaisogelea ile gari kwa nyuma.Mazungumzo yakawa hivi na yule mtu aliekaa kwenye usukani wakaanza kuzungumza kwa lugha ya kinyarwanda na kifaransa kwa sauti ya chini kabisa.
NYAKAMBA: Kaka sio kawaida yako kunipigia honi kwa code hiyo vipi kuna tatizo na usijisahau kaka tupo nchi ya watu huwezi kujua watu wanaotuzunguka.
DEREVA: Ndugu ebu tulia kwanza nisikilize kwa umakini""Jana ulipokea simu""namaanisha ulipokea simu kutoka kwa mkuu???
NYAKAMBA:Ndio kaka nilipokea maagizo ambayo ni amri siwezi kuyapinga na leo mchana naondoka kwenda nairobi kupokea maagizo zaidi na vitendea kazi.
DEREVA:Ndugu hivi mkuu amekupa details kamili kuhusu hiyo oparesheni????
NYAKAMBA:Hapana ndugu
DEREVA:Nyakamba wewe ni ndugu yangu sitokuficha kitu na unakumbuka yaliyotukuta kule Congo Brazzaville na sitaki yajirudie na pili tutafanyia kazi hawa wanasíasa mpaka liní???.Hii fursa tuitumie kaka na sisi tujitajirishe au wewe hutaki kupigiwa saluti na kutandikiwa zuria jekundu???
NYAKAMBA:Ndugu tukutane nairobi kesho tuzungumze hili suala maana hapa tulipo sio salama sana kulijadili hili suala na ukumbuke Kisangani hakukaliki waganda wamevamia na wenzetu wote wamekimbilia Burundi ili warudi Ubelgiji hakuna maisha tena Zaire.
DEREVA:Sawa kaka kesho nitakuepo nairobi ila kumbuka lengo ni sisi kujitanua ili tufikie malengo na hii ndio fursa hata mkuu ikibidi tumzunguke tu kwa manufaa yetu katika hii operasheni.
NYAKAMBA:Ndugu tutazungumza nairobi,na ukiwa dar es salaam usipende sana kutumia magari yenye namba za usajili za ubalozi.Be careful subiri nije unifikishe kariakoo.
Nyakamba akarudi ndani akachukua begi lake akafunga mlango wa ile nyumba na kumwita mlinzi afu akampa maelekezo mafupi kisha akatoka nje akapanda ile gari kuelekea kkoo.
Hawakujua kua nyuma yao walikua wanafuatiliwa na makachero wa serikali ya Zaire waliokua wanamuziki pia wa Bendi maarufu hapa mjini Dar es salaam,lakini bahati ilikua upande wao maana wale makachero walipata hitlafu ya gari lao hivyo wakaacha kuwafuatilia.Lakini Nyakamba alihisi kitu ndio maana walipofika kariakoo akamwambia dereva ""nipeleke uwanja wa ndege niende nairobi mda huu sababu kuna mtu ana tiketi yangu ya kwenda nairobi ananisubiri,ila chochote tulichoongea ibakie siri yetu""na tuzingatie kiapo.
ITAENDELEA..............
July 17 inamkuta Nyakamba ndani ya mitaa ya Kayole Nairobi amekwisha onana na mkuu na kupewa vitendea kazi kwa oparesheni ile alioitiwa.Lakini kuna kitu aliona hakijakaa sawa alipokua anaongea na mkuu.Na akajiapiza kama mkuu ana mpango wa kumsaliti basi ataanza yeye kuwasaliti na kutokomea sababu Zaire hakuna maisha tena kwa upande wake.Pale nairobi hakutaka kuzurura kabisa alikaa ndani pale kwa mkuu kusubiria tu aletewe hati zake za kusafiria akatimize wajibu.Lakini kichwani alikua na mawazo mengi maana aliona hakuna haja ya kupokea amri kutoka kwa serikali inayoelekea kupinduliwa,lakini viapo alivyoapa vilimfanya atulie kwanza.
SIMU TATA:Mara akaona simu yake ya mkononi inayotumia satellite inaita"Kumbuka huo mwaka 1996"simu za mkononi zilikua chache hasa kwa maeneo mengi ya afrika.Yeye alikua na simu ya satellite sababu alikua mfanyakazi wa ubalozi wa Zaire nchini Tanzania kama kazi yake kivuli.
SIMU TATA:Mpigaji alikua yule dereva waliekutana kule dar es salaam nchini tanzania mitaa ya kurasini alipokua amepanga karibia na kota za wafanyakazi wa bandari.Na mazungumzo yao yalikua kwa lugha ya kinyarwanda na kibangubangu hawakuongea kuswahili tena.
SIMU TATA:Kaka unajua waasi wanakaribia kinshasa na hakuna wa kuwazuia.
NYAKAMBA:Kwani Kongolo yupo wapi mpaka mda huu???
SIMU TATA:Kongolo anaharibu mambo kutokana na umri wake na watu wanaogopa kumwambia ukweli kwa heshima ya mzee.
NYAKAMBA:Nenda moja kwa moja kwenye pointi ndugu.
SIMU TATA:Inaweza kutuchukua miaka kumi mpaka ishirini kurudi tena Kinshasa kaka.Sasa ukumbuke mpango wetu ukifika N"Djamena.Maana hata siku ile nilipokuja kwako pale dar es salaam tulikua tunafuatiliwa,kabla hawajatusaliti lazima tuwaonyeshe sisi ni akina nani.
NYAKAMBA:Tukutane N"Djamena usipige simu tena sio salama kwa sasa sababu hakuna wa kumwamini.
SIMU TATA:Sawa kaka tukutane N"Djamena umeeleweka vyema.
Nyakamba alikua anawaza mengi sana kichwani,kama kinshasa itaangukia mkononi mwa wale wanyarwanda basi hana kitu tena.Lakini akajiapiza kua lazima apambane na lolote litakalokuja mbele hakuna jinsi na mambo mengine atayamaliza baada ya kujua hatima ya hii oparesheni.
Jioni ile palepale kayole kwenye ile nyumba ya mkuu,kila kitu kikawekwa sawa kwa ajili ya kazi baina yake na mkuu na malipo ya pesa cash za kianzio akapewa.Kilichobaki kilikua ni kupata zile hati za kusafiria ili apande ndege kuelekea Bangui kama mfanyakazi wa WFP tawi la Kenya,na akifika Bangui atatafuta usafiri wa kuingia Chad either kwa kupitia Cameroon au ndege za umoja wa mataifa.
Kuhusu target (Mlengwa) taarifa zikaja kua yupo tayari ndani ya ndege na atatua uwanja wa kimataifa wa Chad pale N"Djamena international airport (IATA) baada ya masaa matatu ila ni kwa upande ule wa ndege za kijeshi sio upande wa ndege za kiraia na amebeba item zote anazotakiwa kunyanganywa.Hiyo ilikua tarehe 17 July 1996 saa mbili na dk 45 usiku kwa saa za afrika mashariki na saa moja na dk 45 usiku kwa saa za afrika ya kati.
Hati za kusafiria zililetwa na Nyakamba akafanikiwa kupata ndege ya umója wa mataifa akafika Bangui usiku ule kutokea nairobï.Na kutokea Bangui akapata ndege ya mizigo ya WFP mpaka N"Djamena hiyo ilikua tarehe 19 July 1996.Akafikia mitaa ya Kabalaye moja ya vitongoji vilivyochangamka jijini N"Djamena Chad.
Mpigaji alikuja na ofa na akaiweka wazi kwa mlengwa namaanisha mpigiwaji simu.Kuna valid item inatakiwa ichukuliwe kutoka kwa muhusika kabla makachero wengine hawajaiwahi na kuharibu mpango endelevu.
Na mpaka simu hii inapigwa muhusika yupo uwanja wa ndege wa kimataifa wa Senou pale Bamako na haijulikani anaunganisha ndege ya kwenda wapi,ila cha muhimu kinachotakiwa ni mzigo alioubeba kwenye begi zake ndogo mbili.
Baada ya maelezo hayo mafupi mpigaji akawa kimya kisha akauliza""Upo tayari komredi kuchukua hii ofa"""au tuwape wale wayahudi?. Una dakika kumi na moja za kunipa jibu.
Kijana akapata ukakasi kujibu,kwanza simu imekuja ghafla,pili hataki ugomvi tena na vyombo vya dola vya nchi yoyote ile na tatu hataki kuiweka roho yake rehani kisa pesa, maana hajui hii oparesheni kiundani asije kua mbuzi wa kafara kuwanufaisha wanasiasa.
Kilichomuumiza kichwa ni kua ukikataa ofa ni kama umevunja kiapo na malipo yake ni kuonekana msaliti au mhaini unayestahili kifo ndani ya taasisi.
Bila kusita akasema nimekubali nipe details mkuu,nijue naanzia wapi.Na pia mkuu hakikisha target yetu pale Bamako Senou international airport, hapandi ndege za kwenda Athens au Kigali au Bangui au Brazzaville,ila arudi N"Djamena itakua kazi rahisi.
Na yeye kijana tumwite""Nyakamba"akasema baada ya 44hrs atakua Kabalaye akimsubiria amalize kazi ya kumpokonya mizigo hitajika..Nanukuu""Fanya chochote unachoweza mkuu jamaa arudi Chad"""mwisho wa kunukuu.
Mpiga simu akauliza nikuwekee kiasi gani cha pesa cha kuanzia operasheni,na akajibiwa dola elfu tisini za kuanzia zipatikane akifika Nairobi atazichukua cash na hati ya kusafiria ya Uganda pamoja na hati ya kusafiria ya Tanzania.
Baada ya hapo akifika Nairobi akute tiketi za ndege kwenda Bangui zipo tayari mezani.Mpiga simu akasema tutakutana kesho jioni Nairobi na akakata simu.
Nyakamba hakupata usingizi tena akaanza kuwaza mambo mengi sana na akakumbuka misheni ya mwisho ilivyofeli vibaya na akaishia kua mtu anaetafutwa na vyomba vya ulinzi na usalama nchini Congo Brazzaville.
Lakini akajipa moyo hii ndio kazi aliyoichagua cha msingi ni awe tu mwangalifu,akaamka na kuanza kujiandaa na safari ya kesho kwenda Nairobi kukutana na mkuu.
ITAENDELEA...
Kufika asubuhi na mapema hii ilikua july 16 1996 kijana Nyakamba anasikia honi nje ya geti la nyumba aliyokua amepanga kule kurasini kota""Pooh pooh""na upigaji wa honi hii ulikua sio mgeni kwake sababu ni code za mawasiliano za washirika wa taasisi.Fasta fasta akajua kumeiva akatokea mlango wa nyuma wa ua ya ile nyumba mpaka barabarani akaisogelea ile gari kwa nyuma.Mazungumzo yakawa hivi na yule mtu aliekaa kwenye usukani wakaanza kuzungumza kwa lugha ya kinyarwanda na kifaransa kwa sauti ya chini kabisa.
NYAKAMBA: Kaka sio kawaida yako kunipigia honi kwa code hiyo vipi kuna tatizo na usijisahau kaka tupo nchi ya watu huwezi kujua watu wanaotuzunguka.
DEREVA: Ndugu ebu tulia kwanza nisikilize kwa umakini""Jana ulipokea simu""namaanisha ulipokea simu kutoka kwa mkuu???
NYAKAMBA:Ndio kaka nilipokea maagizo ambayo ni amri siwezi kuyapinga na leo mchana naondoka kwenda nairobi kupokea maagizo zaidi na vitendea kazi.
DEREVA:Ndugu hivi mkuu amekupa details kamili kuhusu hiyo oparesheni????
NYAKAMBA:Hapana ndugu
DEREVA:Nyakamba wewe ni ndugu yangu sitokuficha kitu na unakumbuka yaliyotukuta kule Congo Brazzaville na sitaki yajirudie na pili tutafanyia kazi hawa wanasíasa mpaka liní???.Hii fursa tuitumie kaka na sisi tujitajirishe au wewe hutaki kupigiwa saluti na kutandikiwa zuria jekundu???
NYAKAMBA:Ndugu tukutane nairobi kesho tuzungumze hili suala maana hapa tulipo sio salama sana kulijadili hili suala na ukumbuke Kisangani hakukaliki waganda wamevamia na wenzetu wote wamekimbilia Burundi ili warudi Ubelgiji hakuna maisha tena Zaire.
DEREVA:Sawa kaka kesho nitakuepo nairobi ila kumbuka lengo ni sisi kujitanua ili tufikie malengo na hii ndio fursa hata mkuu ikibidi tumzunguke tu kwa manufaa yetu katika hii operasheni.
NYAKAMBA:Ndugu tutazungumza nairobi,na ukiwa dar es salaam usipende sana kutumia magari yenye namba za usajili za ubalozi.Be careful subiri nije unifikishe kariakoo.
Nyakamba akarudi ndani akachukua begi lake akafunga mlango wa ile nyumba na kumwita mlinzi afu akampa maelekezo mafupi kisha akatoka nje akapanda ile gari kuelekea kkoo.
Hawakujua kua nyuma yao walikua wanafuatiliwa na makachero wa serikali ya Zaire waliokua wanamuziki pia wa Bendi maarufu hapa mjini Dar es salaam,lakini bahati ilikua upande wao maana wale makachero walipata hitlafu ya gari lao hivyo wakaacha kuwafuatilia.Lakini Nyakamba alihisi kitu ndio maana walipofika kariakoo akamwambia dereva ""nipeleke uwanja wa ndege niende nairobi mda huu sababu kuna mtu ana tiketi yangu ya kwenda nairobi ananisubiri,ila chochote tulichoongea ibakie siri yetu""na tuzingatie kiapo.
ITAENDELEA..............
July 17 inamkuta Nyakamba ndani ya mitaa ya Kayole Nairobi amekwisha onana na mkuu na kupewa vitendea kazi kwa oparesheni ile alioitiwa.Lakini kuna kitu aliona hakijakaa sawa alipokua anaongea na mkuu.Na akajiapiza kama mkuu ana mpango wa kumsaliti basi ataanza yeye kuwasaliti na kutokomea sababu Zaire hakuna maisha tena kwa upande wake.Pale nairobi hakutaka kuzurura kabisa alikaa ndani pale kwa mkuu kusubiria tu aletewe hati zake za kusafiria akatimize wajibu.Lakini kichwani alikua na mawazo mengi maana aliona hakuna haja ya kupokea amri kutoka kwa serikali inayoelekea kupinduliwa,lakini viapo alivyoapa vilimfanya atulie kwanza.
SIMU TATA:Mara akaona simu yake ya mkononi inayotumia satellite inaita"Kumbuka huo mwaka 1996"simu za mkononi zilikua chache hasa kwa maeneo mengi ya afrika.Yeye alikua na simu ya satellite sababu alikua mfanyakazi wa ubalozi wa Zaire nchini Tanzania kama kazi yake kivuli.
SIMU TATA:Mpigaji alikua yule dereva waliekutana kule dar es salaam nchini tanzania mitaa ya kurasini alipokua amepanga karibia na kota za wafanyakazi wa bandari.Na mazungumzo yao yalikua kwa lugha ya kinyarwanda na kibangubangu hawakuongea kuswahili tena.
SIMU TATA:Kaka unajua waasi wanakaribia kinshasa na hakuna wa kuwazuia.
NYAKAMBA:Kwani Kongolo yupo wapi mpaka mda huu???
SIMU TATA:Kongolo anaharibu mambo kutokana na umri wake na watu wanaogopa kumwambia ukweli kwa heshima ya mzee.
NYAKAMBA:Nenda moja kwa moja kwenye pointi ndugu.
SIMU TATA:Inaweza kutuchukua miaka kumi mpaka ishirini kurudi tena Kinshasa kaka.Sasa ukumbuke mpango wetu ukifika N"Djamena.Maana hata siku ile nilipokuja kwako pale dar es salaam tulikua tunafuatiliwa,kabla hawajatusaliti lazima tuwaonyeshe sisi ni akina nani.
NYAKAMBA:Tukutane N"Djamena usipige simu tena sio salama kwa sasa sababu hakuna wa kumwamini.
SIMU TATA:Sawa kaka tukutane N"Djamena umeeleweka vyema.
Nyakamba alikua anawaza mengi sana kichwani,kama kinshasa itaangukia mkononi mwa wale wanyarwanda basi hana kitu tena.Lakini akajiapiza kua lazima apambane na lolote litakalokuja mbele hakuna jinsi na mambo mengine atayamaliza baada ya kujua hatima ya hii oparesheni.
Jioni ile palepale kayole kwenye ile nyumba ya mkuu,kila kitu kikawekwa sawa kwa ajili ya kazi baina yake na mkuu na malipo ya pesa cash za kianzio akapewa.Kilichobaki kilikua ni kupata zile hati za kusafiria ili apande ndege kuelekea Bangui kama mfanyakazi wa WFP tawi la Kenya,na akifika Bangui atatafuta usafiri wa kuingia Chad either kwa kupitia Cameroon au ndege za umoja wa mataifa.
Kuhusu target (Mlengwa) taarifa zikaja kua yupo tayari ndani ya ndege na atatua uwanja wa kimataifa wa Chad pale N"Djamena international airport (IATA) baada ya masaa matatu ila ni kwa upande ule wa ndege za kijeshi sio upande wa ndege za kiraia na amebeba item zote anazotakiwa kunyanganywa.Hiyo ilikua tarehe 17 July 1996 saa mbili na dk 45 usiku kwa saa za afrika mashariki na saa moja na dk 45 usiku kwa saa za afrika ya kati.
Hati za kusafiria zililetwa na Nyakamba akafanikiwa kupata ndege ya umója wa mataifa akafika Bangui usiku ule kutokea nairobï.Na kutokea Bangui akapata ndege ya mizigo ya WFP mpaka N"Djamena hiyo ilikua tarehe 19 July 1996.Akafikia mitaa ya Kabalaye moja ya vitongoji vilivyochangamka jijini N"Djamena Chad.