Rishi Sunak anaweza kutangazwa kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza leo Oktoba 24, 2022

Rishi Sunak anaweza kutangazwa kuwa Waziri Mkuu wa Uingereza leo Oktoba 24, 2022

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
1666592746957.png

Boris Johnson ajiondoa kwenye kinyang'anyiro cha kumtafuta Waziri Mkuu mpya

Waziri Mkuu wa zamani wa Uingereza Boris Johnson Jumapili alijiondoa katika kinyang'anyiro cha kumrithi Liz Truss kama kiongozi wa nchi hiyo inayoendelea kukabiliwa na misukosuko ya kisisasa.

Johnson alisema wabunge wachache walikuwa wanamuunga mkono, ikilinganishwa na wale wanaomuunga mkono Waziri wa Fedha wa zamani Rishi Sunak, katika juhudi za kuwania wadhifa huo.

Hata hivyo, Johnson alisema kwama awali, alikuwa katika nafasi nzuri ya kufaulu katika uchaguzi na wanachama wa Chama cha Conservative, kabla ya Sunak kuonekana kuwa na ufuasi mkubwa zaidi.

Mwanasiasa huyo, ambaye hakuwahi kutangaza rasmi azma yake ya kurejea Downing Street, alitumia wikendi nzima kujaribu kuwashawishi wabunge wa Conservative kumuunga mkono na akasema Jumapili kwamba alikuwa na uungwaji mkono wa 102 kati yao.

Alihitaji kuungwa mkono na wabunge 100 kufikia Jumatatu ili kuendelea hadi hatua inayofuata, ambayo ingempelekea kupambana na Sunak.

Sunak, ambaye kujiuzulu kwake kama waziri wa fedha mwezi Julai kulichangia kuondoka kwa Johnson, alikuwa ameondoa kizingiti cha wabunge 100 waliohitajika kuendelea hadi hatua inayofuata.

Iwapo Sunak atakuwa Waziri Mkuu, atamridhi Truss aliyejiuzulu wiki jana baada ya kukabiliwa na mzozo mkubwa wa kisiasa.
===


Rishi Sunak could be named as the new Prime Minister later today after Boris Johnson bowed out of the Tory leadership race - as Penny Mordaunt insists she will 'fight on' despite appearing to be significantly short of the 100 supporters she needs to remain in contention ahead of the 2pm deadline.

The former Chancellor, who officially launched his campaign yesterday morning, has received the public backing of more than 150 Tory MPs - with more joining team Sunak following Mr Johnson's departure from the race.

As of last night, 155 MPs had said they are backing Mr Sunak, while just 25 had spoken out in support of Ms Mordaunt. But a further 54 who were hoping Mr Johnson would return to the premiership are yet to publicly reveal to whom they have switched allegiance.


Source: DailyMail
 
Rishi Sunak Anaenda kushinda

Damu ya kitanzania hiyo.

Mama yake Mtanzania

Kama mtanzania namtakia lila la heri
 
Wakenya wasivo na aibu wanakwambia huyu kanjibay ana asili ya kwaoView attachment 2396182
... ila si ndio ukweli wenyewe Mkuu? Kwamba Sunak ana sili ya Kenya that's obvious. Nakumbuka kuna mhandisi mmoja mwenye asili ya Tanzania alionekana kwenye karakana ya Boeing, wengi humu JF walipongeza; sembuse kuwa PM wa UK au President wa US!
 
Baba yake Rishi Sunak ni Mkenya na mama yake ni Mtanzania

Tukienda kwa uzao wa mama Rishi Sunak nl mtanzania. Baba huwa hazai wodini
Baba mkenya, mama mtanzania.... Wote wenye asili ya India.

Basi sawa
 
Baba mkenya, mama mtanzania.... Wote wenye asili ya India.

Basi sawa
Baadhi ya Watanzania wana ujinga fulani vichwani

Mbona huwa hawasemi mchaga mwenye asili ya kilimanjaro

Au mhaya mwenye asili ya Kagera
Au kusema mwarabu mwenye asili ya uarabuni

Kwa nini wanapenda sana kutumia hili neno la mhindi mwenye asili ya India.Mbona kwa waarabu huwa hatutumii hilo neno au kwa wazungu ?
 
Watanzania kuna ujinga fulani

Mbona huwa hatusemi mchaga mwenye asili ya kilimanjaro

Au mhaya mwenye asili ya Kagera
Au kusema mwarabu mwenye asili ya uarabuni

Kwa nini tunapenda sana kutumia hili neno la mhindi mwenye asili ya India.Mbona kwa waarabu huwa hatutumii hilo neno au kwa wazungu ?
Basi yaishe....

Tufanye ni mhindi mwenye asili ya Tandahimba.
 
Baba mkenya, mama mtanzania.... Wote wenye asili ya India.

Basi sawa
Wanaume wa Kenya Mbegu Bora

Baba yake Obama Raisi wa Marekani alikuwa Mkenya mjaluo

Sasa baba mwingine Mkenya baba yake Rishi Sunak kafyatua mtu ambaye anaenda kuwa Waziri mkuu wa Uingereza

Wanaume wa Tanzania vipi kulikoni? Wengi naona mnazalisha Panya road tu wanaomsumbua mkuu wa Polisib IGP Wambura na polisi wenzie

Wanawake watanzania kaoleweni Kenya mkazae watoto wa kueleweka
 
Back
Top Bottom