mpasta
JF-Expert Member
- Jan 17, 2011
- 919
- 2,004
- Thread starter
-
- #41
HUJUMA NZITO-PART 15
Asubuhi hiyo alikuwa ameitwa kuja kusaidia upatikanaji wa risiti za safari feki ya nchini Uingereza, dili ambalo alitegemea litampatia zaidi ya milioni moja taslimu, halafu hapo hapo inaunganika na dili lingine lililoungwa juu kwa juu toka ofisi yake ya kupigia pesa ya "JUAKALI GENERAL SUPPLIES".
Moja kwa moja alipotua maeneo yale akaelekea kwenye ofisi aliyoitwa kwa ajili ya tenda hiyo chafu. Huko akakaa kama saa moja na dakika kadhaa, ndipo akawa amemalizana nao wapigaji wenzake. Alipotoka tu akaanza kuipiga namba ya simu ya Yasmine aliyotumiwa.
"Hellow...sistery, upo wapi mbona sikuoni?...usiulaze usiku mapema mapema, wakati ni ukuta..hapa sasa hivi nimepigiwa simu Ikulu kuna issue natakiwa nikarekebishe huko....Oooh OK. Sawa nisubiri hapo hapo nje !!" akakata simu yake.
Alikuwa anafanya mawasiliano na Kachero Yasmine huku akimtia ndimu kuwa ameitwa Ikulu wakati ni uzushi mtupu, lengo ni kujionyesha yeye ni mtu wa thamani sana anasakwa kila kona kama lulu vile, ili akikutajia dau lake usichomoe.
Yasmine hakutaka wakutane ndani ya jengo la Wizara, alitaka wamalizane nae nje ya jengo. Hivyo akamfahamisha yupo nje ya jengo kwenye kiduka cha Mangi anapoza koo kwa kujiburudisha kwa soda.
"Habari Aisee, Salaamu aleikum Bibie hongera kwa kupendeza.....!!" ilikuwa ndio salamu yake kwa Yasmine mara tu baada ya kuonana uso kwa uso. Tayari sura ya mrembo Yasmine ilishamchanganya, kumvuruga na kumkoroga vilivyo. "Vitu vya rangi ya Mtume ndio ugonjwa wangu huu....!!" alijiwazia kichwani mwake "Muddy Comp" huku wakipeana mikono ya salamu na Yasmine.
"Mie habari yangu ni nzuri, yaani nimefurahi sana kukutia machoni mjuba wewe. Maana ulivyo adimu kama mguu wa sisimizi uliodumbukizwa kwenye mchuzi wa rosti" alijishebedua Yasmine mbele yake na kumfanya Muddy ajione ni mtu wa thamani sana, kumbe anampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
"Acha tu mrembo, kwanza hapa nikitaka nipige chini dili lako maana Ikulu nasumbuliwa sana, kuna Afisa mmoja ananisumbua sana, namdanganya foleni kali. Alikuwa tayari atume gari zao zile na eskoti juu ya polisi ili mradi tu niwahi kufika, lakini wale JUAKALI naheshimiana nao sana nikaona sio vizuri kumuangusha yule Mkurugenzi" alizidi kujifagilia na kujikweza matawi ya juu.
"Jamani ahsante kwa kujali, Mungu atawalipa kwa upendo wenu, sasa tunaweza kwenda kuzungumzia ndani ya gari?" alibadilisha mada Yasmine sasa akimvuta taratibu kwenye lengo lake mahususi analolikusudia.
Nalo ni kumchukua "Muddy Comp" mpaka nyumbani kwake Mbweni. Alitaka ampeleke akamsulubishe, na kumpa mfueni vilivyo mpaka aropoke kila kitu pesa alizokuwa anapokea toka "Nyasa Empire Supporters" (NES) zilikuwa na madhumuni gani haswa. Kama zilikuwa ni mahari ya binti yake, au mchango wa matibabu atapike kila kitu anachokijua juu ya pesa zile kodi ya walalahoi, wavuja jasho wa Tanzania.
"Hamna shida tena itakuwa bora maana jua limeanza kunoga huko angani Malaika msimamizi wake hatuonei huruma, yeye analichochea tu makali yake" alijibu Muddy huku anamfuata sako kwa bako Kachero Yasmine kuelekea kwenye gari lake.
"Kaka yangu, mimi nafanya kazi Benki Kuu sasa kuna dili fulani inabidi ifojiwe saini ya Rais wa Benki Maendeleo ya Africa "ADB" ndio liweze kukamilika, naomba sana msaada wako kuna chambichambi ya kutosha usiwe na hofu na mgao wako..!" alizungumza kwa sauti ya kubembeleza huku amemlegezea macho "Muddy Comp", kwa mtindo wa kurembua.
Akajitia kushusha pumzi ndefu, kuonyesha amepewa mtihani mzito kuukabili. Kisha akaa kimya kitambo kifupi anajifanya anatafakari, halafu akafungua mdomo wake.
"Mie kweli ni mpigaji madili kama ulivyoelekezwa pale "JUAKALI GENERAL SUPPLIES" lakini dili sampuli hiyo unayonieleza ya kufoji saini za watu nimeachana nazo kitambo kirefu sana. Nilishawahi kupata matatizo na vyombo vya dola siku za nyuma ilibakia chupuchupu nikanyee mtondoo gerezani" alijitia kubadilika na kuipanjua dili hilo hadharani mchana kweupe.
Kachero Yasmine alipomuangalia "Muddy Comp" wakati anajieleza aligundua fika kwa kumuangalia uso wake, kuwa anaongopa mchana kweupe, ni ndumilakuwili tena mnafiki mkubwa hasa kutokana na elimu yake ya saikolojia ya wahalifu wanayofundishwa katika Vyuo vya Ukachero.
"Jamani weweeh...kaka yangu Muddy nisaidie kwa leo tu mara moja mwenzako..chonde chonde tafadhali" alizidi kubembeleza Yasmine huku sasa akiwa amekifumbata kiganja cha mkono wake wa kushoto kwenye mkono wa "Muddy Comp". Kitendo cha kushikwa kiganja cha mkono tu, akaanza kulainika kama siagi kwenye uji wa moto, huku anajichekesha chekesha tu kama mwehu.
Jinsi Kachero Yasmine alivyo mjanja akawa anamchezea vidole vyake huku anambembeleza kwa maneno matamu yenye kumtoa nyoka pangoni. Mawazo mwake Muddy alishakubali waondoke alitamani sana wapite nae maskani Magomeni walau awaongopee rafiki zake kuwa leo kaopoa kifaa kipya.
"Daah..majaribu haya unaniletea binti, jela inaniita hivi hivi nitakuwa peke yangu ujue, huku wewe unakula mbwanda na familia yako uraiani" aliongea kwa sauti ya chini, akiwa ameshagandishwa ulimi kuonyesha yupo tayari kuifanya hiyo kazi.
Baada ya mazungumzo mafupi wakakubaliana na kufikia muafaka yupo tayari kufanya kazi hivyo waelekee huko Mbweni akakabidhiwe mchongo mzima. Kachero Yasmine alikuwa anaendesha gari lake kwa mtindo wa halambe halumbe.
Mara amekosa kugongana na gari hili, mara kamkosa kumgonga mtu ili mradi tafrani njia nzima. Alishavurugwa tayari alikuwa anataka mambo yaende haraka haraka. Walishakuwa wapo nyuma ya muda kuwatia mbaroni wahalifu wa "Nyasa Empire Supporter" (NES).
Muddy alikuwa muda wote ana furaha ghaya, akiona kabisa anaenda kupiga pesa ndefu na huenda akikomaa akang'oa kabisa mtoto wa Kizenji, Yasmine. Kumbe hakujua anaenda kupata suluba na kalinyekalinye za kufa mtu mpaka atajuta kuzaliwa.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Ratiba ya Kachero Manu na rafiki yake Dr.Edson Nkube ilibidi ipinduliwe kichwa chini miguu juu. Mishemishe zao badala ya kuanzia kwenye ofisi ya "DNA Diagnostics Centre" (DDC) walipopeleka sampuli ya mwili unaodhaniwa wa marehemu Dr.Pius Chilembwa, kwa ajili ya uchunguzi wa vinasaba vya marehemu, wakabadilisha kibao wakaamua waanzie kwanza mizunguko yao mtaa wa "Adolf Goertz Street", kule dukani kwa Mhindi "Bhatti Shop".
Sababu ya mabadiliko hayo ya ratiba yalitokana na taarifa walizopokea toka kwenye vyanzo vyao vya Kiintelijinsia. Penyenye ziliwafikia kuwa kuna ghasia na machafuko yanayotarajiwa kuanzia kurindima nchi nzima ya Afrika ya Kusini.
Wazawa walikuwa wanataka kuandaa maandamano kushinikiza serikali yao kuwafukuza Wafanyabiashara wa kigeni ambao ndio wamekamatia asilimia 80% ya Uchumi wa Afrika ya Kusini. Wakileta madai ya kuwa wageni hao wamekimbia nchi zao zenye hali ngumu za kimaisha wamekimbilia nchini Afrika ya Kusini, nchi yenye neema ya asali na maziwa.
Iliwachukua kama nusu saa tu wakiwa na usafiri binafsi, kuwasili dukani kwa Mr.Bhatti. "Good Morning Mr.Bhatti, How are you?" alianza kusalimia Kachero Manu kwa uso wa bashasha, akafuatia Dr.Nkube nae kusalimiana naye huku wanapeana nae mikono ya salamu.
"Habari yangu nzuri sana iko karibuni sana" alijibu salamu kwa lugha ya kiswahili jambo ambalo liliwafanya Dr.Nkube na Kachero Manu waangaliane usoni na kutabasamu wakiwa hawamini kama Mhindi yule anaweza kuongea Kiswahili fasaha kiasi chake.
"Nashangaa nini, mimi meishi Tanzania miaka zaidi ya 20, wazazi iko kule wekeza zamani kiwanda cha kusindika nyanya, Dumila-Morogoro. Hivyo najua swahili na mlipoingia dukani nilikusikieni naongea swahili nikafurahi sana, nikajua nyie ni dugu zangu toka nchi ya Nyerere" alijieleza Bwana Bhatti wapi alipojulia lugha ya kiswahili.
Baada ya mazungumzo ya hapa na pale, wakajitambulisha kuwa wao ni waandishi wa habari wa kimataifa wa kujitegemea. Wapo nchini Afrika ya Kusini kutafuta habari za kichaa aliyepotea kwenye mazingira ya kutatanisha anayetafutwa kwa udi na uvumba na ndugu zake. Mr.Bhatti kwanza alionekana kuhuzunishwa sana na taarifa kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha kwa majinuni huyo. Pia alionyesha kufurahishwa na ujio wa Wanahabari wale ili huenda Kichaa huyo akaonekana.
"Van-Dubbe kama alivyokuwa anajiita mwenyewe alizoea sana hapa mtaa wa Adolf Goertz Street. Tazunguka huku na kule lakini lazima rejee hapa. Menyewe penda jiita Rais wa Mtaa". Alifungua utangulizi wa mahojiano baina yao Mr.Bhatti kwa kuelezea namna alivyokuwa anamjua Majinuni aliyetoweka Van-Dubbe. Kachero Manu akafungua rasmi mahojiano baina yao.
Kachero Manu: "Kwanini alikuzoea wewe na sio wana mtaa wengine?, maana hata taarifa ya SABC-News ilionyesha polisi wamekuja kukuhoji wewe! "
Mr.Bhatti: "Swali zuri, watu wa huku roho baya sana, sasa mie iko mpa yeye chakula, maji na hata mavazi ndio maana Van-Dubbe iko hakauki hapa dukani kwangu! "
Kachero Manu: "Je siku chache kabla hajapotea, kuna mienendo yoyote ya hatari dhidi yake ulinusa hasa kutokana na ukaribu wenu?"
Mr.Bhatti: "Eeeh...iko watu wageni jitokeza ghafla jifanya nampenda sana kuja hapa nunulia mikate, soda naondoka nae kisha namrudisha, karibia wiki zima hivi..!!". Jibu la Mr.Bhatti likawafanya Dr.Nkube na Kachero Manu waangaliane usoni na kupeana ishara kuashiria kuwa hao watu huenda ndio wahusika wakuu.
Kachero Manu: "Unaweza kutuonyesha video zilizorekodiwa na CCTV-Camera ya hapa dukani kwako za wiki za mwisho mwisho kabla hajapotea?"
Mr.Bhatti:"Hamna shida mie CCTV yangu natunza matukio mpaka miezi tatu kisha nafuta, twende mkaone" alisema yule Mhindi huku wakisimama kuelekea nyuma ya duka lile, pembe za chaki kabisa, wakimuacha mtumishi wake mmoja Mr.Bhatti kuendelea kutoa huduma kwa wateja wake wachache waliokuwa wanaingia na kutoka hapo dukani.
ITAENDELEA
Sent from my TECNO CC6 using JamiiForums mobile app
Asubuhi hiyo alikuwa ameitwa kuja kusaidia upatikanaji wa risiti za safari feki ya nchini Uingereza, dili ambalo alitegemea litampatia zaidi ya milioni moja taslimu, halafu hapo hapo inaunganika na dili lingine lililoungwa juu kwa juu toka ofisi yake ya kupigia pesa ya "JUAKALI GENERAL SUPPLIES".
Moja kwa moja alipotua maeneo yale akaelekea kwenye ofisi aliyoitwa kwa ajili ya tenda hiyo chafu. Huko akakaa kama saa moja na dakika kadhaa, ndipo akawa amemalizana nao wapigaji wenzake. Alipotoka tu akaanza kuipiga namba ya simu ya Yasmine aliyotumiwa.
"Hellow...sistery, upo wapi mbona sikuoni?...usiulaze usiku mapema mapema, wakati ni ukuta..hapa sasa hivi nimepigiwa simu Ikulu kuna issue natakiwa nikarekebishe huko....Oooh OK. Sawa nisubiri hapo hapo nje !!" akakata simu yake.
Alikuwa anafanya mawasiliano na Kachero Yasmine huku akimtia ndimu kuwa ameitwa Ikulu wakati ni uzushi mtupu, lengo ni kujionyesha yeye ni mtu wa thamani sana anasakwa kila kona kama lulu vile, ili akikutajia dau lake usichomoe.
Yasmine hakutaka wakutane ndani ya jengo la Wizara, alitaka wamalizane nae nje ya jengo. Hivyo akamfahamisha yupo nje ya jengo kwenye kiduka cha Mangi anapoza koo kwa kujiburudisha kwa soda.
"Habari Aisee, Salaamu aleikum Bibie hongera kwa kupendeza.....!!" ilikuwa ndio salamu yake kwa Yasmine mara tu baada ya kuonana uso kwa uso. Tayari sura ya mrembo Yasmine ilishamchanganya, kumvuruga na kumkoroga vilivyo. "Vitu vya rangi ya Mtume ndio ugonjwa wangu huu....!!" alijiwazia kichwani mwake "Muddy Comp" huku wakipeana mikono ya salamu na Yasmine.
"Mie habari yangu ni nzuri, yaani nimefurahi sana kukutia machoni mjuba wewe. Maana ulivyo adimu kama mguu wa sisimizi uliodumbukizwa kwenye mchuzi wa rosti" alijishebedua Yasmine mbele yake na kumfanya Muddy ajione ni mtu wa thamani sana, kumbe anampaka mafuta kwa mgongo wa chupa.
"Acha tu mrembo, kwanza hapa nikitaka nipige chini dili lako maana Ikulu nasumbuliwa sana, kuna Afisa mmoja ananisumbua sana, namdanganya foleni kali. Alikuwa tayari atume gari zao zile na eskoti juu ya polisi ili mradi tu niwahi kufika, lakini wale JUAKALI naheshimiana nao sana nikaona sio vizuri kumuangusha yule Mkurugenzi" alizidi kujifagilia na kujikweza matawi ya juu.
"Jamani ahsante kwa kujali, Mungu atawalipa kwa upendo wenu, sasa tunaweza kwenda kuzungumzia ndani ya gari?" alibadilisha mada Yasmine sasa akimvuta taratibu kwenye lengo lake mahususi analolikusudia.
Nalo ni kumchukua "Muddy Comp" mpaka nyumbani kwake Mbweni. Alitaka ampeleke akamsulubishe, na kumpa mfueni vilivyo mpaka aropoke kila kitu pesa alizokuwa anapokea toka "Nyasa Empire Supporters" (NES) zilikuwa na madhumuni gani haswa. Kama zilikuwa ni mahari ya binti yake, au mchango wa matibabu atapike kila kitu anachokijua juu ya pesa zile kodi ya walalahoi, wavuja jasho wa Tanzania.
"Hamna shida tena itakuwa bora maana jua limeanza kunoga huko angani Malaika msimamizi wake hatuonei huruma, yeye analichochea tu makali yake" alijibu Muddy huku anamfuata sako kwa bako Kachero Yasmine kuelekea kwenye gari lake.
"Kaka yangu, mimi nafanya kazi Benki Kuu sasa kuna dili fulani inabidi ifojiwe saini ya Rais wa Benki Maendeleo ya Africa "ADB" ndio liweze kukamilika, naomba sana msaada wako kuna chambichambi ya kutosha usiwe na hofu na mgao wako..!" alizungumza kwa sauti ya kubembeleza huku amemlegezea macho "Muddy Comp", kwa mtindo wa kurembua.
Akajitia kushusha pumzi ndefu, kuonyesha amepewa mtihani mzito kuukabili. Kisha akaa kimya kitambo kifupi anajifanya anatafakari, halafu akafungua mdomo wake.
"Mie kweli ni mpigaji madili kama ulivyoelekezwa pale "JUAKALI GENERAL SUPPLIES" lakini dili sampuli hiyo unayonieleza ya kufoji saini za watu nimeachana nazo kitambo kirefu sana. Nilishawahi kupata matatizo na vyombo vya dola siku za nyuma ilibakia chupuchupu nikanyee mtondoo gerezani" alijitia kubadilika na kuipanjua dili hilo hadharani mchana kweupe.
Kachero Yasmine alipomuangalia "Muddy Comp" wakati anajieleza aligundua fika kwa kumuangalia uso wake, kuwa anaongopa mchana kweupe, ni ndumilakuwili tena mnafiki mkubwa hasa kutokana na elimu yake ya saikolojia ya wahalifu wanayofundishwa katika Vyuo vya Ukachero.
"Jamani weweeh...kaka yangu Muddy nisaidie kwa leo tu mara moja mwenzako..chonde chonde tafadhali" alizidi kubembeleza Yasmine huku sasa akiwa amekifumbata kiganja cha mkono wake wa kushoto kwenye mkono wa "Muddy Comp". Kitendo cha kushikwa kiganja cha mkono tu, akaanza kulainika kama siagi kwenye uji wa moto, huku anajichekesha chekesha tu kama mwehu.
Jinsi Kachero Yasmine alivyo mjanja akawa anamchezea vidole vyake huku anambembeleza kwa maneno matamu yenye kumtoa nyoka pangoni. Mawazo mwake Muddy alishakubali waondoke alitamani sana wapite nae maskani Magomeni walau awaongopee rafiki zake kuwa leo kaopoa kifaa kipya.
"Daah..majaribu haya unaniletea binti, jela inaniita hivi hivi nitakuwa peke yangu ujue, huku wewe unakula mbwanda na familia yako uraiani" aliongea kwa sauti ya chini, akiwa ameshagandishwa ulimi kuonyesha yupo tayari kuifanya hiyo kazi.
Baada ya mazungumzo mafupi wakakubaliana na kufikia muafaka yupo tayari kufanya kazi hivyo waelekee huko Mbweni akakabidhiwe mchongo mzima. Kachero Yasmine alikuwa anaendesha gari lake kwa mtindo wa halambe halumbe.
Mara amekosa kugongana na gari hili, mara kamkosa kumgonga mtu ili mradi tafrani njia nzima. Alishavurugwa tayari alikuwa anataka mambo yaende haraka haraka. Walishakuwa wapo nyuma ya muda kuwatia mbaroni wahalifu wa "Nyasa Empire Supporter" (NES).
Muddy alikuwa muda wote ana furaha ghaya, akiona kabisa anaenda kupiga pesa ndefu na huenda akikomaa akang'oa kabisa mtoto wa Kizenji, Yasmine. Kumbe hakujua anaenda kupata suluba na kalinyekalinye za kufa mtu mpaka atajuta kuzaliwa.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]
Ratiba ya Kachero Manu na rafiki yake Dr.Edson Nkube ilibidi ipinduliwe kichwa chini miguu juu. Mishemishe zao badala ya kuanzia kwenye ofisi ya "DNA Diagnostics Centre" (DDC) walipopeleka sampuli ya mwili unaodhaniwa wa marehemu Dr.Pius Chilembwa, kwa ajili ya uchunguzi wa vinasaba vya marehemu, wakabadilisha kibao wakaamua waanzie kwanza mizunguko yao mtaa wa "Adolf Goertz Street", kule dukani kwa Mhindi "Bhatti Shop".
Sababu ya mabadiliko hayo ya ratiba yalitokana na taarifa walizopokea toka kwenye vyanzo vyao vya Kiintelijinsia. Penyenye ziliwafikia kuwa kuna ghasia na machafuko yanayotarajiwa kuanzia kurindima nchi nzima ya Afrika ya Kusini.
Wazawa walikuwa wanataka kuandaa maandamano kushinikiza serikali yao kuwafukuza Wafanyabiashara wa kigeni ambao ndio wamekamatia asilimia 80% ya Uchumi wa Afrika ya Kusini. Wakileta madai ya kuwa wageni hao wamekimbia nchi zao zenye hali ngumu za kimaisha wamekimbilia nchini Afrika ya Kusini, nchi yenye neema ya asali na maziwa.
Iliwachukua kama nusu saa tu wakiwa na usafiri binafsi, kuwasili dukani kwa Mr.Bhatti. "Good Morning Mr.Bhatti, How are you?" alianza kusalimia Kachero Manu kwa uso wa bashasha, akafuatia Dr.Nkube nae kusalimiana naye huku wanapeana nae mikono ya salamu.
"Habari yangu nzuri sana iko karibuni sana" alijibu salamu kwa lugha ya kiswahili jambo ambalo liliwafanya Dr.Nkube na Kachero Manu waangaliane usoni na kutabasamu wakiwa hawamini kama Mhindi yule anaweza kuongea Kiswahili fasaha kiasi chake.
"Nashangaa nini, mimi meishi Tanzania miaka zaidi ya 20, wazazi iko kule wekeza zamani kiwanda cha kusindika nyanya, Dumila-Morogoro. Hivyo najua swahili na mlipoingia dukani nilikusikieni naongea swahili nikafurahi sana, nikajua nyie ni dugu zangu toka nchi ya Nyerere" alijieleza Bwana Bhatti wapi alipojulia lugha ya kiswahili.
Baada ya mazungumzo ya hapa na pale, wakajitambulisha kuwa wao ni waandishi wa habari wa kimataifa wa kujitegemea. Wapo nchini Afrika ya Kusini kutafuta habari za kichaa aliyepotea kwenye mazingira ya kutatanisha anayetafutwa kwa udi na uvumba na ndugu zake. Mr.Bhatti kwanza alionekana kuhuzunishwa sana na taarifa kupotea kwenye mazingira ya kutatanisha kwa majinuni huyo. Pia alionyesha kufurahishwa na ujio wa Wanahabari wale ili huenda Kichaa huyo akaonekana.
"Van-Dubbe kama alivyokuwa anajiita mwenyewe alizoea sana hapa mtaa wa Adolf Goertz Street. Tazunguka huku na kule lakini lazima rejee hapa. Menyewe penda jiita Rais wa Mtaa". Alifungua utangulizi wa mahojiano baina yao Mr.Bhatti kwa kuelezea namna alivyokuwa anamjua Majinuni aliyetoweka Van-Dubbe. Kachero Manu akafungua rasmi mahojiano baina yao.
Kachero Manu: "Kwanini alikuzoea wewe na sio wana mtaa wengine?, maana hata taarifa ya SABC-News ilionyesha polisi wamekuja kukuhoji wewe! "
Mr.Bhatti: "Swali zuri, watu wa huku roho baya sana, sasa mie iko mpa yeye chakula, maji na hata mavazi ndio maana Van-Dubbe iko hakauki hapa dukani kwangu! "
Kachero Manu: "Je siku chache kabla hajapotea, kuna mienendo yoyote ya hatari dhidi yake ulinusa hasa kutokana na ukaribu wenu?"
Mr.Bhatti: "Eeeh...iko watu wageni jitokeza ghafla jifanya nampenda sana kuja hapa nunulia mikate, soda naondoka nae kisha namrudisha, karibia wiki zima hivi..!!". Jibu la Mr.Bhatti likawafanya Dr.Nkube na Kachero Manu waangaliane usoni na kupeana ishara kuashiria kuwa hao watu huenda ndio wahusika wakuu.
Kachero Manu: "Unaweza kutuonyesha video zilizorekodiwa na CCTV-Camera ya hapa dukani kwako za wiki za mwisho mwisho kabla hajapotea?"
Mr.Bhatti:"Hamna shida mie CCTV yangu natunza matukio mpaka miezi tatu kisha nafuta, twende mkaone" alisema yule Mhindi huku wakisimama kuelekea nyuma ya duka lile, pembe za chaki kabisa, wakimuacha mtumishi wake mmoja Mr.Bhatti kuendelea kutoa huduma kwa wateja wake wachache waliokuwa wanaingia na kutoka hapo dukani.
ITAENDELEA
Sent from my TECNO CC6 using JamiiForums mobile app