Riwaya: "Hujuma Nzito"

Siyo mara yake ya kwanza kuwepo katika jukwaa hili na uzuri huwa akianzisha story inafika mwisho isipokuwa msako wa mwehu. Hivyo bado ninaimani ataifikisha mwisho
Khaaa msako wa mwehu ukishafika mwisho, MODERATOR alichanganywa tukainza upya kwa ID ya mtu mwingine ngoja niitafute nikutagg

Sent from my TECNO CC6 using JamiiForums mobile app
 
RIWAYA-HUJUMA NZITO-PART 33


Alipowasha taa tu ya chumbani mwake alipigwa na mshtuko wa ghafla nusra aanguke chini kwa presha. Alichokiona kitandani pake kilimstaajabisha sana. Mwanamke mrembo akiwa amejifunga kilemba kichwani mwake, juu kavalia fulana iliyochongoa chuchu chake ndogo alikuwa amejilaza kitandani mwake.
Mwanzoni aliogopa kumsogelea akijua huenda ni Jini mahaba amejigeuza mwanamke kuja kumtega. Lakini alipomuangalia vizuri akaona ana bastola mapajani mwake. Akapata nguvu kujua huyu ni adui yake.

Akachomoa bastola yake kiunoni, akavaa ujasiri na kuanza kumsogelea kwa tahadhari kubwa akiogopea isije ukawa ni mtego kwake.
Alipomkaribia kabisa na kumgeuza sura yake, ndipo akamgundua kuwa ni Yasmine. Alipomuona ni yeye tena akiwa amebeba silaha akajua asilimia 100% kabisa kuwa ni adui yake. Alikuwa anataka kumuamsha usingizini ili apambane ana kwa ana, lakini akili na mwili vilikuwa vinakosa ushirikiano.

Mwili ulikuwa haujiwezi tayari umeshashikwa na matamanio, hasa alivyokuwa anakiangalia kifua cha Yasmine, chuchu zilimtoa udenda. Alikuwa haamini kama umri wake ni juu ya miaka 27, alikuwa na kifua cha binti wa darasa la 5B aliyevunja ungo karibuni tu. Akajikuta anaingiwa na tamaa za kutaka kumbaka usingizini kisha akimaliza haja zake ndio apambane nae.

Akajikuta tayari ameshasaula suruali yake, Nathanieli amebakia na chupi yake tu huku mkononi amekamatia bastola yake.
Akaitanua miguu ya Kachero Yasmine akajibana katikati ya miguu na kuanza kumpapasa Yasmine kifuani. Mpaka akajikuta bastola inamporonyoka pembeni hakujali tena.

"Pliiiz...Manu, acha banaaa, sitaki kuvunja heshima yangu, namheshimu mpenzi wangu Dr.Rishedy Shareefy...!" alijikuta anajilazimisha kuzungumza wakati anamtoa kifuani mwake Manu wa ndotoni ambaye kiuhalisia yupo nchini Afrika ya Kusini.


Aliposhtuka usingizini na kufumbua macho yake taratibu, alishikwa na mzumbao. Alimuona adui yake Nathanieli anafanya utalii haramu kifuani mwake kadri anavyojisikia yeye, akiwa ameshazidiwa na mihemko ya ngono hajitambui.
Akakusanya nguvu zake za miguuni na kumpa kifuti kimoja matata sana cha sehemu za siri.

"Mamaaaaaah...nakuf....a... aaah...!!" aligugumia kwa sauti kubwa huku akiwa ameshaanguka sakafuni juu za zulia anagaragara kwa maumivu.
Hakutaka kumchelewesha akamrukia pale pale chini kama chui mwenye njaa kali na kuanza kumsukumizia makonde yasiyo na idadi hasa akichukizwa na kitendo cha kumpasulia sidiria yake na kumpapasa kimahaba bila ridhaa yake. Ndani ya dakika mbili na nusu Nathanieli alikuwa hoi hatamaniki usoni.


Sura yote imevimba manundu huku macho yamebonyea ndani na kuwa madogo kama Mchina vile. Alipomuongelesha akawa akijaribu kuongea anabubujikwa na damu mdomoni hawezi kuongea kitu. Usicheze na ngumi za komandoo wewe, watu ambao wakiwa mazoezini ndoo ya ugali ya lita 10 ikijaa pomoni anaikata mtu mmoja tu.
Makomandoo ambao wakiwa mafunzoni wanapanda milima huku wamebeba matairi ya trekta kichwani. Wakitaka kuoga, wanatumia maji ya baridi kutoka kwenye friza, acha Bwana usicheze na hao watu, wana roho za ujasiri na miili ya chuma.


Kachero Yasmine alishajua jamaa hana maisha marefu na akimuacha hai atakuja kumsumbua kazini na kwa washirika wake. Akanyakua bastola yake yenye kiwambo cha kuzuia sauti akamtwanga risasi tatu za kichwa ikawa habari ya Nathanieli duniani hapa imekwisha.


Ugavana wa kinjozinjozi aliokuwa anauota kila siku kuwa ataukwaa pindi Dola ya Nyasa ikitangazwa ukawa umeota mbawa. Siku zote chambilecho tamaa mbele mauti nyuma, alisahau kabisa usemi huo.
Nathanieli akawa anatapatapa sakafuni kwa kutupa miguu huku na kule, yamini wa yasari uchungu wa sakarati mauti. Kachero Yasmine hakuchelewa akapiga simu kwa watu wa kitengo maalumu waje kuhamisha ushahidi muhimu uliopo kwenye maktaba ya Nathanieli kuanzia kompyuta na vikorokoro vingine vitakavyosaidia mahakamani kuwatia hatiani mabaradhuli hawa wa Nyasa Empire Supporters(NES).


Wakati anawasubiri wenzake waje, alipokuwa anamungalia Nathanieli kwa umakini kifuani akaona kajichora tatoo ya mwenge wa uhuru umeshikiliwa na mikono miwili iliyochomoza juu ya ziwa Nyasa huku chini yake kuna namba 8019. Akaanza kuitafakari hiyo namba 8019 ina maana gani haswa lakini hakuwa na jibu na anayepaswa kumpa maana ya hiyo namba tayari kashatangulizwa jongomeo.


Ile tatoo aliyojichora mjuba Nathanieli kwa uwelewa wake wa haraka haraka alielewa kuwa mwenge unawakilisha uhuru, na huo uhuru wa kweli utapatikana baada ya kusimamishwa Dola ya Nyasa, na vuguvugu la uhuru huo limeasisiwa na watu wenye asili ya ziwa Nyasa.


Walipokuja wenzake tu na kuwakabidhi lindo, kisha kwa njia za Kininja kama alivyokuja ndivyo alivyotoweka eneo lile. Aliwapa uhuru wenzake wa kutimiza wajibu wao. Akawa anakatisha mitaani giza totoroo majira ya saa 6 usiku.
Akaomba msamaha kwa Mola kwa kuwasababishia giza la makusudi wakazi wa eneo lile lakini ni kwa lengo zuri tu wapate kuishi kwa amani na usalama katika nchi yao ya Tanzania.


Akalifikia gari lake akaliwasha na kutimka eneo lile kurejea Mbweni nyumbani kwake kujipumzisha huku akisubiria asubuhi inayofuata kupewa taarifa za msiba wa Bosi wake Nathanieli. Pia alishapanga kutafuta makazi mapya Safe House” ya kuhamia kwa sababu hapo tayari maadui zake wameshapajua hivyo hamna usalama tena.
[emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586][emoji3586]

SURA YA KUMI NA NNE

Kulipokucha tu, Profesa akatuma ujumbe kwa Kachero Manu kuwa leo watakutana mara mbili. Wakutane kwanza asubuhi hiyo na kisha watakuwa na kikao cha mwisho usiku na sio usiku pekee kama walivyokubaliana jana yake.

Kachero Manu akajua lazima kuna jambo la dharura limetokea. Kachero Manu alikuwa ameshapata taarifa zote za kifo cha Nathanieli na ujio wa Dr.Pius Chilembwa nyumbani kwa Profesa. Taarifa hizi alitumiwa na Kachero Yasmine kwa mfumo wa mawasiliano wa kijasusi unaitwa 'Morse Code'.

Mfumo ambao ulikuwa unatumia nukta na alama za dashi katika kutengeneza herufi wanazojua wao tu Makachero. Wakati mwingine walikuwa wanawasiliana kwa mfumo wa herufi maalumu zinazochapwa kwa kutumia mashine inaitwa 'Enigma', mashine maalumu iliyokuwa inatumika sana na mashushushu wa Kijerumani wakati wa vita kuu vya pili vya dunia.

Walijua kwa vyovyote ulinzi nyumbani kwa Profesa kwa upande wa mambo ya kuthibiti mawasiliano utakuwa mkubwa, hivyo lazima wachukue tahadhari zote. Pia alishafanikiwa kuinasa sura ya Profesa Asante-Rabbi kimafia.
Alichofanya ni kuichukua ile sauti aliyoirekodi jana yake na kuingiza sauti hiyo kwenye 'App' maalumu ya utambuzi wa sura za watu maarufu duniani kwa kutumia sauti zao. Ilikuwa ni 'App' ambayo ukiingiza sura ya mtu yoyote maarufu katika kila nchi duniani ina uwezo wa kukupa pia sauti yake.


Kwa mara ya kwanza baada ya kumaliza kupata staftahi akakutanishwa ndani ya chumba kimoja na Profesa. Lakini alikuwa bado amejifunika uso wake kwa barakoa maalumu.

"Leo nina huzuni kuliko kawaida, mwili wangu ni dhaifu na roho yangu imekuwa nyepesi sana. Nimempoteza kijana wangu mpambanaji Nathanieli ambaye alikuwa anafanya kazi kwa ukaribu zaidi na Bosi wako Newton Temba" alifungua mazungumzo Profesa akiwa anamhadithia Kachero Manu bila kufahamu huyo anajua kila kitu na ndio mhusika wa kifo cha Nathanieli kupitia pacha wake Yasmine.

Kisha Profesa akaendelea, machungu ninayoyapata ni kama siku kijana wangu Hamza Bendelladji wa Algeria alipokamatwa". Alipofikia hapo kwenye maelezo yake ya kumtaja Hamza, Kachero Manu alipigwa na butwaa na kuachwa mdomo wazi kwa sekunde kadhaa akiwa haamini kumbe Hamza, mhalifu nguli alipikwa kiuhalifu na Profesa.

Huyu Hamza Bendelladji ni mhalifu aliyefanikiwa kuiba pesa nyingi zaidi za mabenki kwa njia ya mtandao. Alikuwa ni kijana mdogo sana (25) raia wa Algeria, ambapo miaka kadhaa iliyopita alihukumiwa kifungo cha miaka 15 gerezani kwa uhalifu wa kuiba zaidi ya Bilioni 500 (Tsh) kutoka kwenye benki 217 za Ulaya na Marekani.

Mashirika yote ya habari duniani kuanzia televisheni mpaka redio yaliripoti taarifa zake kijana huyo.
Kachero Manu akaanza kuomba kimoyomoyo Mwenyezi Mungu aweke baraka zake wamtie mbaroni Profesa ili dunia nzima iweze kujua kuwa Tanzania ina mashushushu bobezi kama wale waliopo katika mashirika makubwa kama CIA, FBI, MOSSAD, KGB na mengineyo yenye heshima ya kutukuka duniani.
ITAENDELEA
Profesa anamwaga mchele kwenye kuku wengi bila kujijua
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji91][emoji91][emoji1732][emoji1732][emoji1732]

Sent from my TECNO CC6 using JamiiForums mobile app
 
Dah Nathanael ameshatnagulia Jongomeo.Please Kamanda Manu sorry mpasta please tupia vipande kama viwili hivi siku ya leo.Kufidia week end!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…