Riwaya: I died to save my President

Riwaya: I died to save my President

Dah bwana Elvis anataka pita na blueprint ya Godson kiundavaundava
 
To every action there is equal and opposite reaction,.
Unapata kitu unakosa kitu, hatar saana
 
IDIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 15

kwamba wewe
ndiye mwanamke wa pekee
ninayekupenda na ninayekutaka
maishani mwangu.Patricia najua
uliumizwa na mambo yale
yaliyokupata wakati ule lakini
naomba ufahamu kwamba mambo
yote yaliyotokea si kigezo cha
kunizuia mimi kukupenda wewe”
“ Elvis ni ukweliulio wazi
kwamba lengo la watu wawili
kuingia katika mahusiano ni ili
siku moja waishi pamoja na
waanzishe familia.Mimi sina uwezo
wa kupata mtoto katika maisha
yangu yote yaliyobaki hapa
duniani kwa hiyo sina thamani
kwa mwanaume yeyote Yule katika
dunia hii.Siku zote matarajio ya
mwanaume kwa mke wake ni
kumzalia watoto na kutengeneza
familia iliyo bora,uwezo huo mimi
sina tena na ndiyo maana suala la
mahusiano nimekwisha lifuta katika akili yangu” akasema
Patricia
“ Patricia nakupenda wewe na
kila ulicho nacho.Suala la kupata
mtoto si suala ambalo linaweza
kunifanya nishindwe kuwa nawe”
akasema Elvis
“ Elvis hili si suala dogo kama
unavyodhani.Hili ni suala zito
sana na linaloniumiza mno kila
nikilifikiria.Sitaki mtu kama wewe
uumizwe na makosa niliyoyafanya
mimi.Elvis wewe ni mtu mwenye
upendo wa ajabu sana ,you
deserve someone better than me.Si
haki hata kidogo ukaishi maisha
yako bila kuwa na familia”
“ Patricia maneno yako yanazidi
kuniumza zaidi” akasema Elvis
“ Samahani Elvis lakini huo
ndio ukweli .I made a mistake
once and I have to pay for my
mistake for the rest of my life.I’m
not that woman who can be loved
by anyone.I’m valueless.Samahani kwa maneno haya lakini hivyo
ndivyo ninajisikia mimi moyoni
mwangu” akasema Patricia
“ Patricia ninafahamu
umeumizwa kwa kiasi kikubwa
sana na ninayahisi pia maumivu
yako.Tafadhali nipe nafasi ya
kukuonyesha upendo wangu
kwako,nipe nafasi ya kukufanya
malkia wa ulimwengu wangu na
kukufanya uwe mwanamke
mwenye furaha kupita wote
duniani.Nipe nafasi katika moyo
wako.Nomba uufungue moyo wako
na uuruhusu kupenda tena”
Maneno yale yakaonekana
kumuingia Patricia na kumfanya
atoe machozi.Akamtazama Elvis
na kusema
“ Elvis ni bahati ilioje kupendwa
na mwanaume kama wewe lakini
nasikitika kwamba moyo wangu
hauna hata chembe ya mapenzi
ndani yake na itanichukua muda
mrefu kupenda tena .I’m sorryElvis” akasema Patricia.Elvis
akamtazama usoni na kusema
“ Patricia haujawahi hata mara
moja kuwa na hisia zozote juu
yangu?
Patrcia akainama akafikiri
halafu akajibu
“ No ! sijawahi kufikiria
chochote kuhusu wewe kuhusiana
na suala la mapenzi.Kwangu wewe
ni rafiki yangu mkubwa sana
kupita wote” akasema Patricia
halafu akainama chini
“ Patricia naomba unitazame
usoni” akasema Elvis na Patricia
akainua uso wake na kumtazama
Elvis
“ Nitazame machoni na
uniambie kwamba hujawahi kuwa
na hisia zozote juu yangu.Tell me
the truth and I swear I’ll believe
you”
“ Ouh Elvis ……!! Patricia
akashindwa kujizuia akainama na
kuanza kulia.Elvis akambembeleza Elvis you don’t know how
much I love you and I’ve been
dreaming how happy I could be if
you were my man.Nilipokutana
nawe Dodoma kwa mara ya
kwanza moyoni mwangu nilihisi
kuna kitu kipo kati yetu lakini
niliporudi Dar nikakutana na
Godson nikajikuta nikimpenda na
kuamini kwamba ndiye
mwanaume wa maisha
yangu.Baada ya kutengana naye
taratibu ulianza kuniinga moyoni
mwangu nikaanza kuvutiwa nawe
na kukupenda lakini tayari
nilikwisha chelewa.Tayari
nilikwisha yaharibu maisha
yangu.Nimekuwa nikipigana na
moyo wangu ili usiendelee
kukuwaza lakini kadiri siku
zinavyozidi kwenda nimejikuta
nikishindwa na hilo limekuwa
linanitesa mno.Nakupenda
Elvis.Nakupenda sana kiasi ambacho siwezi kukuelezea lakini
….”
“ Lakini nini Patrica…?!
Akauliza Elvis.Patricia akashindwa
kuongea kitu akabaki
anamtazama Elvis
“ Patricia ahsante kwa kuwa
muwazi kwangu.Ahsante kwa
kunipenda.kwa mara ya kwanza
katika maisha yangu ninajiona ni
mtu wenye bahati sana kupendwa
na mtu kama wewe” akasema
Elvis na kumkumbatia Patricia.
“ Patricia kwa kuwa sote
tunapendana hakuna kitu
kinachoweza kutuzuia mimi na we
tusiwe wapenzi.Naomba tuwe
wapenzi na hatimaye siku moja
tuweze kufanikiwa kufunga ndoa
kwani ndoto yangu kubwa ni kuwa
nawe katika maisha yangu yote
hadi kifo kitutenganishe.Nataka
uwe malkia wa moyo
wangu.Nataka nikufanye
mwanamke mwenye furaha kubwa duniani” akasema Elvis.Patricia
ambaye machozi yalikuwa
yanamtoka akamtazama Elvis
usoni na kusema
“ Elvs najua unanipenda na sina
shaka hata kidogo na upendo
wako kwangu,lakini pamoja na
kunipenda nadhani unafahamu
fika kwamba mimi ni mwanamke
ambaye siko kamili tena ,ina
maana sina tena uwezo wa kuzaa
jambo ambalo najua hata kama
tukiwa wapenz litakuumiza
sana.Ninapata mashaka ya
kuingia tena katika mahusiano
nikiwa katika hali hii kwa kuogopa
kumuumiza mwenzangu na mimi
mwenyewe kuumia pia. “ akasema
Patricia
“ Patricia I love you with all my
heart .Nakupenda
ulivyo.Ninayafahamu matatizo
yako na niko tayari kuyabeba
pamoja nawe.Hilo si suala ambalo
linaweza kutufanya mimi nawe tusiwe pamoja na wala si suala
linaloweza kutufanya tukakosa
furaha.Tafadhali nikubali niwe
wako Patricia.Niruhusu
nikuonyeshe namna gani
ninakupenda ewe malaika wangu”
akasema Elvis.Patricia
akashindwa kuwa na kigugumizi
tena kwani alimpenda Elvis na
ndoto yake ilikuwa ni siku moja
yeye na Elvis wawe wapenzi lakini
alikuwa akisita kila alipofikiria
kwamba hakuwa tena na uwezo
wa kuzaa jambo lililomfanya
kukata tamaa kabisa ya siku moja
kuwa na maisha ya furaha akiwa
na mwanaume ampendaye.
Ukurasa mpya ukafunguliwa
kati ya Elvis na Patricia.Waliingia
rasmi katika ulimwengu wa
wapendanao
MIAKA 13 BAADAE Miaka 13 imekwisha pita sasa
toka Elvis na Patricia
walipoufungua ukurasa wa
mapenzi kati yao na kuwa
wapenzi. mapenzi yao yalikuwa
mazito na ya kutiliwa
mfano.Walipendana kwa dhati ya
mioyo yao
Patricia alihitimu shahada yake
ya kwanza ya udakatari katika
chuo kikuu cha sayansi na tiba
cha Muhimbili na baadae akaenda
tena nchini Marekani kuendelea
na masomo zaidi katika fani yake
hii .Kwa sasa anafanya kazi katika
hospitali kuu ya magonjwa ya
fahamu.
Elvis kwa upande wake alijiunga
na jeshi la wananchi wa Tanzania
kwa mafunzo ya kijeshi ya miaka
mitatu na baadae akapelekwa na
serikali kwa mafunzo ya ujasusi
katika chuo cha ujasusi cha CIA
university nchini Marekani ambako alihitimu kwa kiwango
cha juu na cha kushangaza
sana.Baada ya kuhitimu mafuzo
yake akarejea nchini na kujiunga
rasmi na idara ya ujasusi ya taifa
akiwa ni jasusi wa kiwango cha
juu kabisa nchini.Alifurahi sana
kuifanya kazi hii ambayo
amekuwa akiota kuifanya toka
akiwa mdogo
Tayari Elvis na Patricia
wamehitimisha ile ndoto yao
kubwa na ya siku nyingi ya kuishi
pamoja baada ya kufunga
ndoa.Maisha yao yalijaa furaha na
amani na waliendelea na kazi zao
kama kawaida.Patricia akiwa ni
daktari katika hospitali kuu ya
magonjwa ya akili na vile vile
alikuwa ni daktari aliyekuwa
akimtibu mke wa rais aliyekuwa
akisumbuliwa na tatizo la kupooza
mwili upande mmoja na kwa
msaada mkubwa wa Patricia hali
yake imekuwa ikiendelea vizuri naviungo vyake vilivyokuwa
vimepooza vimeanza kufanya kazi
tena.Kila siku kabla ya kuelekea
kazini kwake Patricia hupita
kwanza ikulu kumjulia hali
mgonjwa wake na kukagua
maendelo yake kitendo
kilichojenga ukaribu mkubwa
sana kati yake na familia ya rais
Siku ya kumbu kumbu ya
miaka kumi na tisa toka
alipofariki kanali Braison Tarimo
baba mzazi wa Elvis
iliwadia.Ndugu wengi ,marafiki na
jamaa wa karibu walikutana
katika ibada maalum inayofanyika
kila mwaka kwa ajili ya
kumuombea heri kanali Tarimo ili
mwenyezi Mungu aweze
kumrehemu.Baada ya kumalizika
kwa ibada ya misa takatifu,ndugu
wote wakaelekea katika makaburi
alikozikwa kanali Tarimo ambako
waliwasha mishumaa katikakaburi lake ishara ya kuendelea
kumkumbuka
Toka makaburini watu wote
waliohudhuria kumbu kumbu hii
wakiongozwa na mjane wa
marehemu Bi Carmelita tarimo
mama mzazi wa Elvis wakaelekea
nyumbani kwa marehemu Mbezi
kwa ajili ya kumalizia shughuli
zilizobaki.Bi Carmelita kwa sasa
amekwisha staafu kazi yake ya
uuguzi aliyokuwa akiifanya jjini
Arusha na kwa sasa anaishi jijini
Dar es salaam katika nyumba yao
iliyoko mbezi akiendela
kuisimamia miradi mbali mbali
iliyoachwa na marehemu mume
wake.
Nyumbani kwa marehemu
kuliandaliwa chakula na vinywaji.
Watu walikula na kunywa
wakifurahia maisha aliyoyaishi
kanali Tarimo hapa
duniani.Wakati watu wakiendelea
kula na kunywa huku wakikumbushana mambo
mbalimbali ambayo kanali Tarimo
amewahi kuyafanya katika enzi za
uhai wake,Bi Carmelita akamuita
mwanae Elvis wakaelekea
bustanini
“ Elvis nashukuru sana kwa
kupata nafasi hii ya kukaa nawe
leo.Ni muda mrefu hatujapata
nafasi ya kukaa pamoja na
kuongea kwa uhuru na nafasi
kuhusiana na mambo
yanayotuhusu” akasema Bi
Carmelita
“ Kweli mama ni muda mrefu
hatujapata nafasi ya kukaa
pamoja kama hivi na kuongea.Kazi
yangu inanibana sana na ndiyo
maana tunashindwa kuonana”
“ Nalifahamu hilo Elvis lakini
nashukuru kwa kuwa haujawahi
kupitisha hata siku moja bila ya
kunipigia simu kunijulia
hali.Nashukuru sana kwa hilo” akasema Bi Carmelita na
kumfanya Elvis atabasamu
“ Mama usijali kuhusu
kutokuniona.Kila nitakapokuwa
nikipata muda nitakuwa nikija
kukusalimu”
“ Ahsante sana Elvis.Vipi
maisha yako na mkeo
yanaendeleaje?
“ Tunashukuru Mungu
tunaendelea vizuri sana
mama.Hatuna tatizo lolote”
“Nafurahi kusikia hivyo Elvis
lakini kuna jambo mimi binafsi
linaniumiza sana moyo wangu”
“ Jambo gani mama? Akauliza
Elvis
“ Elvis mimi na baba yako
tulikupata kwa taabu
sana.Tulikwisha kata tamaa
kabisa ya kupata mtoto maishani
mwetu na ndipo tulipofanikiwa
kukupata na baada yako
hatukufanikiwa tena kupata mtoto
mwingine na ndiyo maana unaona uko peke yako.Kama tungefanikwa
kupata watoto zaidi hivi sasa
mngekuwa hata zaidi ya kumi
kwani baba yako alipenda sana
kuwa na watoto wengi.” Akasema
Bi Carmelita na kumfanya Elvis
acheke kidogo.
“ Baba yako alipofariki
alituachia mali nyingi na mrithi
pekee ni wewe .Kitu
kinachoniumiza mimi ni kwamba
muda mrefu sasa umepita toka
umefunga ndoa na Patricia lakini
hakuna dalili zozote za kuniletea
mjukuu.Unawaza nini kuhusu
suala hili? Akauliza Bi Carmelita.
Swali lile likaonekana kumstua
sana Elvis kwani hakuwa
amelitegemea.
“ Mambo yameanza..Wamenza
kudai toto wao ..!! akawaza Elvis
“ Elvis ! akasema Bi Carelita na
kumstua Elvis aliyeanza kuzama
mawazoni Ndoto yangu kubwa ni
kukuona ukiwa na familia kubwa
na hatinaye tupate warithi wa
kuziendeleza mali hizi.Sitaki
kuingilia masuala yako ya ndani
ya ndoa kwani sijui
kinachoendelea kati yako na mkeo
lakini ninachotaka ni kupata
maoni yako kuhusu nini unafikiria
kuhusiana na suala hili la mtoto?
Elvis akainama akatafakari na
kusema
“ Mama naomba tafadhali
usiumize kichwa kwa suala
hili.Nafahamu kiu yako ya kupata
mjukuu lakini naomba usiwe na
hofu.Muda utakapowadia
utampata mjukuu” akasema Elvis
huku akijitahidi kutabasamu.
“ Mwanangu ni miaka zaidi ya
mitatu sasa imepita toka
mmefunga ndoa kitu gani
mnachokisubiri? Mnasubiri hadi
ipite miaka mingapi? Bado tunajipanga mama kabla
ya kuamua kupata mtoto”
“ Kitu gani unachokisubiri
Elvis? Nyote wawili mna kazi za
maana.Mna kila kitu
mnachokihitaji.Mnataka kujipanga
nini? Mnataka hadi muwe na
ndege yenu binafsi?
“ Mama kuna mambo mengi
ambayo tunatakiwa kufanya
kabla ya kumleta kiumbe duniani”
akasema Elvis
“ Elvis ni maandalizi gani hayo
mnayoyafanya?Kama ni fedha
niambieni kiasi gani
mnachokitaka ili niwapatie”
“ Tatizo si pesa mama.Yapo
mambo mengi tu ya kujipanga”
Akasema Elvis.Mama yake
akamtazama usoni na kusema
“ Elvis niambie ukweli kuna
tatizo lolote katika ndoa yenu?
Kuna mmoja wenu ana matatizo
katika masuala ya uzazi? Kama
kuna tatizo lolote kati yenu naomba niweke wazi ili kwa
pamoja tutafute namna ya
kufanya.” Akasema Bi
Carmelita.Elvis akatabasamu na
kusema
“ Huko unakofika mama ni
mbali sana.Hakuna mtu mwenye
tatizo kati yetu.Sisi sote tu wazima
kabisa.Naomba unipe muda
kidogo tuweke mambo sawa na
utafurahi mwenyewe” akasema
Elvis na mara Jackline binamu
yake Elvis
akaingia.Akakumbatiana na Elvis
kwani ni muda mrefu
hawajaonana
“ Elvis habari za siku?
Nimefurahi sana kukuona”
“ Habari nzuri Jack.Ninaendelea
vizuri tu.Vipi maendeleo yako?
“ Ninaendelea vizuri hata mimi
ila nasikitika sana hukuweza
kuhudhuria katika harusi yangu” Utaisamehe Jack.Nilikuwa nje
ya nchi lakini mke wangu alifika
kuniwakilisha”
“ Usihofu Elvis.Namshukuru
Mungu mambo yalikwisha salama
na mambo ni mazuri” akasema
Jack huku akitabasamu na
kulishika tumbo lake kubwa.Elvis
akatabasamu
“ Wow ! hongera sana
Jack.Nahisi muda si mrefu mambo
yatakuwa mambo” akasema Elvis
“ Kweli kabisa Elvis.Mambo
yatakuwa mazuri hivi karibuni”
“ Hongera sana Jack.” Akasema
Elvis
“ Ahsante sana Elvis.What
about you?What are you waiting
for? Akauliza Jack
“ Hilo ndilo jambo ambalo hata
mimi nilikuwa namwambia hapa
sasa hivi.Umekuwa ni muda mrefu
sasa na hatuoni chochote.Nadhani
ni wakati muafaka sasa kwa Elvis
kutuletea mtoto.Ninahitaji kumuona mjukuu wangu kabla
sijafa” akasema Bi Carmelita
“ Ni kweli Elvis hayo
ninayoyasema shangazi.Ni wakati
muafaka sasa wa kutafuta mtoto”
akasema Jack Elvis akatabasamu
na kusema
“ Nimekwisha ongea na mama
na kumuahidi kwamba nitalifanyia
kazi suala hilo.Hata mimi na mke
wangu tuna mipango yetu ya
ndani na suala hili tunalifahamu
na liko katika mipango yetu kwa
hiyo nawaomba muwe na subira
na muda muafaka utakapowadia
tutafanya mnavyotaka” akasema
Elvis
“ Sawa Elvis ,hatutaki kuingilia
masuala yenu ya ndani lakini ni
muhimu kama ukalifanyia kazi
suala hili.” Akasema Bi Carmelita
“ Usijali mama .Nitalifanyia kazi
kama nilivyokuahidi” akasema
Elvis halafu akaondoka pale
bustanini na kuwaacha mama yake na Jack,akaenda kuungana
na ndugu zake.Kichwa chake
kilijaa mawazo mengi sana
kutokana na maongezi yake na
mama yake.
“ Mpaka mama amefikia hatua
ya kunieleza wazi wazi kuhusiana
na suala la mtoto basi lazima
litakuwa ni suala ambalo
limemsumbua na kumuumiza
sana kichwa chake.Nilitegemea
mambo kama haya kujitokeza na
sasa yameanza,natakiwa
nikabiliane nayo” akawaza Elvis
“ Lazima nikabiliane na suala
hili na shinikizo lolote toka kwa
ndugu.Lazima nihakikishe
kwamba Patricia haumizwi na
suala hili.Nilikubali kumuoa
Patricia hali nikifahamu kabisa
kwamba hana uwezo wa kupata
mtoto na nilifanya hivyo kwa
sababu ninampenda kwa moyo
wangu wote na suala la
kutokupata mtoto kwangu mimi si kigezo cha kushindwa kumpenda
Patricia.Nitasimama imara na
sintakubali mtu yeyote Yule awe ni
mama au ndugu yeyote aingilie
masuala yangu ya ndani ya ndoa.”
Akawaza Elvis
Saa mbili za usiku Elvis na
mkewe Patricia wakaondoka na
kurejea nyumbani kwao.
********************
Ni siku ya jumatatu ,baada ya
kutoka ikulu kuangalia maendeleo
ya mke wa rais ,Patricia akaelekea
kazini kwake.Mara tu alipowasili
akapata taarifa kwamba kuna
mgeni wake aliyekuwa akimsubiri
toka saa mbili asubuhi.Moja kwa
moja akaelekea kwanza ofisini
kwake akavaa koti lake la
kitabibu halafu akaelekeakatika
kantini ya hospitali ambako
aliekezwa kwamba ndiko aliko
mgeni wake. Alipofika kantini,Patricia
akapigwa na butwaa baada ya
kukutana na mama mkwe wake
yaani Bi Carmelita mama yake
Elvis.Nywele zikamsisimka na kwa
kiasi Fulani akaogopa.Haikuwahi
kutokea hata mara moja kwa Bi
Carmelita kumfuata pale
hospitali.Mara nyinig awapo na
tatizo lolote au akihitaji msaada
wa aina yoyote huwasiliana kwa
simu lakini kitedo cha kumfuata
pale hospitali kilimstua na
kumshangaza sana Patricia.
“ Mama shikamoo..” akasema
Patricia akimsalimia mama mkwe
wake kwa adabu
“ Marahaba
Patricia.Unaendeleaje?Samahani
kwa kuja ghafla bila taarifa
.Nilikuwa na shughuli hapo jirani
na hospitali yenu hivyo nikaona ni
vyema endapo nitapita hapa na
kukusalimu .Nilipofika hapa
nikaambiwa kwamba kila siku lazima upite kwanza ikulu
kumuangalia mke wa rais “
“ Ndiyo mama kila siku asubuhi
lazima nipite ikulu kumjulia hali
mke wa rais na kuangalia
maendeleo yake.Alipatwa na tatizo
la kupooza mwili upande mmoja ”
akasema patricia
“ Vipi maendeleo yake?
“ Anaendelea vizuri kwa sasa na
viungo vyake vinaweza kufanya
kazi tena.”
“ Nafutahi kusikia hivyo.Lakini
naomba unisamehe mwanangu
kwa kuja namna hii bila
kukutaarifu”
“ Usihofu mama.Hakuna tatizo
lolote .Karibu sana.Utapenda
kutumia kahawa?
“ Ouh ahsante sana Patricia
lakini tayari nimekwisha
hudumiwa kila
nilichokihitaji.Wahudumu
walipoambiwa kwamba mimi ni
mgeni wako wamenichangamkia na kunipatia kila
nilichohitaji.Ahsante sana
Patricia” akasema Bi
Carmellita.Patricia akamuita
muhudumu na kumuomba
amletee kahawa.
“ Patricia mwanangu
utanisamehe pia kwa kutumia
muda wako wa kazi lakini kuna
jambo moja ambalo limenileta
hapa kwako asubuhi hii” akasema
bi Carmelita
“ Usijali kuhusu muda mama
.Kuna tatizo gani? Akauliza
Patricia
“ Si tatizo bali ni suala dogo tu
ambalo nataka niongee nawe
kama mama na mwanae”
“ Nakusikia mama endelea..”
“ Patricia kama unavyoniona
haliyangu mimi mama yako
nimekwisha kuwa mzee.Nguvu
zinaniisha taratibu.Nafurahi kwa
Elvis kumpata mke ambaye hata
kama nikifa leo basi sina wasi wasi hata kidogo ninajua
mwanagu amebaki katika mikono
salama” akasema bi
Carmelita.Patricia akatabasamu
“ Patrcia moyo wangu una
furaha kubwa kwa wewe kukubali
kuolewa na mwanangu.Kwa dunia
ya sasa kupata mwanamke kama
wewe ni jambo la bahati sana.Toka
ndani ya moyo wangu
ninakuhakikishia kwamba
ninakupenda sana”
“ Ouh ahsante sana mama.Hata
mimi ninakupenda pia na
ninashukuru kumpata mume
kama Elvis na mama mkwe
mwenye upendo kama
wewe.Ninafurahi sana mama “
akasema Patricia .Bi Carmelita
akatabasamu na kusema
“ Ahsante sana Patricia.Nafurahi
kusikia hivyo.Pamoja na hayo
kuna jambo moja dogo tu ambalo
napenda tuliongee” Jambo gani mama? Akauliza
Patricia
“Ni kuhusu mtoto “
Patricia aliposikia neno mtoto
likitajwa,alisikia kitu kama
nyundo nzito ikiupiga utosi
wake.Moyo wake ukabadili mapigo
na kuanza kwenda kwa kasi ya
ajabu .Kijasho chembamba
kikamtoka.Mstuko alioupata
ulikuwa wa dhahiri kiasi kwamba
hata mama mkwe wake aligundua.
“ Samahani Patricia kama
nimekustua lakini nimeona
nikutane nawe ili tuongee nijue
kama kuna tatizo lolote kuhusiana
na suala hili.Kama unavyojua ni
zaidi ya miaka mitatu sasa imepita
toka mmeoana na hatujaona dalili
zozote za kutuletea mjukuu.Kuna
tatizo gani mwamangu?Au bado
mnajipanga? Akauliza Bi
Carmelita.Patricia akainama
akashusha pumzi ,akafikiri na
kusema Mama umewahi kuzungumza
na Elvis kuhusiana na suala hili?
“ Ndiyo nimewahi kuzungumza
naye lakini jibu alilonipa
halikunifurahisha na ndiyo maana
nimekuja kwako ili tuongee na
uniambie mna mipango gani au
kama kuna tatizo basi nifahamu ili
tuweze kulitafutia ufumbuzi.”
Akasema Bi Carmelita.Patricia
akavuta pumzi ndefu akafikiri
kidogo na kusema
“ Mama kwa kweli hakuna tatizo
lolote.Tumechelewa kwa sababu
ya kujipanga na kuweka mazingira
mazuri” akasema Patricia
“ Patricia mwanangu
nilipoongea na Elvis naye alinipa
jibu kama hilo kwamba muda
haujafika na kwamba bado
mnajipanga.Mnasubiri miaka
mingapi ndiyo muwe tayari?
Mnajipanga kitu gani? Akauliza bi
Carmelita.Patricia jasho
likaendelea kumtoka mama kuna masuala mengi ya
kujipanga kabla ya kumleta mtoto
duniani.Tunashughulikia suala
hili na muda utakapofika
utafurahi mwenyewe.Naomba
utupe muda mama” akasema
Patricia
“ Patricia kuna jambo ambalo
limeanza kunipa wasi wasi
.Inaonekana kuna jambo ambalo
hamtaki kuliweka wazi.Kuna tatizo
gani? Kuna mmoja wenu ana
tatizo lolote? Kama kuna mmoja
ana tatizo kuweni wazi ili
tuangalie ni namna gani ya
kumsaidia kwani masuala haya ni
ya kawaida sana hivi sasa” kauli
ile ya bi Carmelita ikaendelea
kumtoa jasho Patricia na
kukitonesha kidonda ambacho
kimekwisha pona tayari..Akajikaza
na kusema
“ Mama tatizo linalotufanya
tusiwe tayari kwa sasa ni
majukumu ya kikazi na zaidi ya yote nimechaguliwa kwenda
kuendelea na masomo nje ya nchi
kwa muda wa miaka mitatu.Elvis
naye kuna kazi anatarajiwa
kuifanya nje ya nchi na hatujui
itamchukua muda gani kwa hiyo
hilo ndilo suala linalotupa ugumu
kwa sasa.Tunataka tutakapokuwa
tayari kupata mtoto sote tuwe na
muda wa kutosha kwa kumlea
mtoto huyo” akasema Patricia
“ Kama mkiweka mbele
majukumu ya kazi zenu ni lini
basi nafasi hiyo itapatikana?
akauliza bi Carmelita
“ Sote tunajaribu kutafuta
uwezekano wa kuomba kusitishwa
au kuahirishwa kwa safari
hizo.Tayari nimekwisha wasiliana
na viongozi wangu na nimekwisha
wasilisha kwao maombi yangu na
wanayafanyia kazi .Elvis naye
amekwisha fanya hivyo lakini bado
hajapatiwa majibu” akasema
Patricia
 
I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 16

Ahsante nimekuelewa
Patricia.Ninawaombea Mungu
maombi yenu yakubaliwe ili
muweze kupata nafasi nzuri ya
kutafuta mtoto.Kitu kingine
ambacho nataka kukuomba ni
kwamba muda wowote kama kuna
tatizo lolote usisite kunifahamisha
na tukatafuta ufumbuzi wa
haraka” akasema bi Carmelita
huku akiinuka
“ Nitafanya hivyo mama usijali”
akasema Patricia huku naye
akiinuka wakaagana na bi
Carmellita na kisha akaeleka
ofisini kwake.
Miguu ilikuwa mizito hata
kupiga hatua .Alihisi kama
amebeba kitu kizito
kichwani.Mambo aliyoongea na
mama mkwe wake yalimstua
mno.Baada ya kuingia ofisini
kwake Akakaa kitini na kuvuta
pumzi ndefu Ouh Mungu wangu ! Mambo
yameanza.Nilitegemea tu lazima
mambo kama haya yatatokea siku
moja na sasa yametimia.Ndugu
wameanza kudai mtoto
wao.Mpaka ifikie hatua ya mama
mkwe kunieleza wazi wazi basi
lazima suala hili liwe limekwisha
jadiliwa sana katika ngazi ya ukoo
na wameamua kunieleza wazi
wazi. Ouh Mungu wangu nitafanya
nini mimi? Nitamtoa wapi mtoto
wanayemtaka? Akawaza Patrica
.Alihisi kama kichwa chake
kinataka kupasuka kwa mawazo
.Alichanganyikiwa na hakujua
afanye nini.
“ Sina uwezo wa kuzaa tena na
hakuna muujiza wa kuniwezesha
kupata mtoto.Kama ndugu
wameanza shinikizo la kudai
mtoto basi furaha yote ya ndoa
yangu iko hatarini
kutoweka.Nampenda sana Elvis na
sitaki mtu yeyote anitenganishe naye.Yeye ndiye kila kitu
kwangu.Nimetoka naye mbali sana
,ananifahamu vizuri,anayajua
matatizo yangu na amekubali
kuishi nami kwa sababu
ananipenda na hata siku moja
hajawahi kunitamkia au kuniuliza
chochote kuhusiana na suala la
mtoto.Amenifanya ni mwenye
furaha na nijisikie ni moja kati ya
wanawake wenye bahati duniani
lakini nimeanza kuingiwa na
shaka kama ataendelea
kuivumilia hali hii ya kukosa
mtoto hadi kifo kitutenganishe
kutokana na shinikizo la ndugu
zake.Nina wasi wasi anaweza
akaamua kutafuta mwanamke
mwingine ili kuwaridhisha ndugu
zake na hapo ninahisi penzi lake
kwangu litakuwa limefika
ukomo.Hatakuwa tayari
kunipenda tena mtu ambaye sina
faida yoyote kwake.Ouh gosh I’m
so scared” akawaza Patricia kichwa chake kikajaa mawazo
kiasi kwamba alishindwa hata
kufanya kazi.Akavua koti lake la
kidaktari na kutoka mle ofisini
bila kuongea na mtu yeyote
akapanda gari lake na kuelekea
moja kwa moja kanisani.Milango
ya kanisa ilikuwa wazi akaingia
akapiga magoti na kuanza kusali
huku machozi mengi yakimtoka
“ Ee Mungu wangu nimekuja
mbele zako ,najua nimekukosea
sana.Najua wewe ni mwema sana
na ninafahamu umekwisha
nisamehe kosa langu kubwa
nililolifanya la kutoa mimba,lakini
bado naendelea kukulilia ee
Mungu wangu endelea kuwa nami
katika matatizo yangu.mambo
yameanza kuniharibikia na furaha
ya maisha yangu iko mbioni
kutoweka.Ndugu za mume wangu
wanaanza kudai mtoto na mimi
sina uwezo wa kuzaa mtoto.Ee
Mungu naomba uinusuru ndoa yangu isivunjike.Elvis ndiye kila
kitu kwangu na sijui maisha
yangu yatakuwaje bila ya kuwa
naye.Nipe nguvu na ujasiri wa
kulibeba jambo hili mpaka mwisho
wake” akaomba Patricia huku
akilia.Alitoa machozi mengi hadi
kifua chake kikaloa machozi
halafu akapanda gari lake na
kurejea nyumbani akajifungua
chumbani
********************
Saa moja za jioni ,Elvis akarejea
nyumbani na kushangazwa na
kitendo cha kumkuta mke wake
akiwa chumbani amelala.Siku zote
Patricia hakuwa mtu wa kupenda
kulala lala.
“ Hallo darling..Unaumwa? Si
kawaida yako kuwa kitandani
mida kama hii” akasema Elvis huku akimbusu mkewe katika paji
la uso.
“ Siumwi Elvis ,ila najisikia
uchovu sana siku yaleo” akajibu
Patrica huku akinuka na kukaa
“ Matilda ameniamia kwamba
leo umerejea mchana.Kulikoni?
Una matatizo gani? Akauliza Elvis
“ Ni kweli nimewahi sana kurudi
leo,sikuwa nikijisikia vizuri.Pole na
kazi”
“ Ahsante sana mke wangu.Pole
nawe.Unajisikiaje sasa hivi?
“ Hivi sasa ninajisikia
vizuri.Nimekunywa dawa najisikia
afadhali.” Akasema Patricia kisha
akamsaidia mume wake kuvua
nguo halafu wote wakaingia bafuni
kuoga.Kisha oga wakaenda kupata
chakula cha usiku kilichoandaliwa
na Matilda mfanyakazi wa
ndani.Kisha kula wakaenda
chumbani kwa mapsumziko. Mama alikuja leo kazini”
akasema Patricia akiwa amekaa
na mumnewe kitandani.
“ Mama alikuja kazini kwako?!
Elvis akashangaa
“ Ndiyo.Nilipofika tu hospitali
baada ya kutoka ikulu nilimkuta
pale akinisubri”
“ Asubuhi namna hiyo? Alikuwa
anataka nini? Anaumwa? Akauliza
Elvis
“ Hapana haumwi
chochote.Alipita tu kunisalimu na
kuniletea ujumbe”
“ Ujumbe ? Ujumbe gani?
Akauliza Elvis kwa
mshangao.Patricia akatabasamu
na kusema
“ Mama anataka mtoto”
Kauli ile ikayafanya mapigo ya
moyo wa Elvis yabadilike ghafla na
kuanza kwenda kwa kasi isiyo ya
kawaida Kwa nini wanataka kuanza
kuingilia maisha yangu? Akasema
Elvis kwa hasira
“ Calm down my love.Calm
down” Patricia akasema akijaribu
kumtuliza mumewe
“ Pole sana Patricia najua
uliumia mno na ndiyo maana
ukawahi kurudi nyumbani
leo.Wewe ulimjibu nini?
“ I lied to her.Nilimdanganya
kwamba sote tumechaguliwa
kwenda kimasomo na kikazi nje ya
nchi kwa hiyo suala la mtoto
litasubiri hadi hapo tutakapokuwa
na nafasi yakutosha.I’m so sorry
that I lied to your mother.”
Akasema Patricia huku machozi
yakimtoka
“ Usihofu Patricia.You did the
right thing na ninakuomba
tafadhali usiumie wala usihofu
kuhusu suala hili.Hauna mtu
yeyote mwenye ruhusa ya
kukuuliza jambo lolote kuhusanana suala la mtoto.Mimi ndiye
niliyekuoa na ninafahamu tatizo
lako na siko tayari ukose furaha
kwa sababu tu ya suala hili la
mtoto.Nitasimama dhidi ya yeyote
Yule ambaye atakunyooshea
kidole” akasema Elvis na
kumkumbatia mke wake.Patricia
akafuta machozi na kusema
“ Elvis najua unanipenda na
sina shaka hata kidogo na upendo
wako kwangu .Najua uko tayari
kwa lolote kwa ajili yangu.Elvis
hata mimi nakupenda sana zaidi
ya ninavyoweza kukueleza.Pamoja
na upendo huu mkubwa tulio nao
ambao nina hakika hauwezi
kutetereka lakini ninafahamu toka
ndani kabisa mwa moyo wako
utakuwa unaumia sana kwa
kukosa mtoto na kutokuwa na
tumaini kabisa la kupata mtoto
katika maisha yako.” “ Patricia !!..Elvis akamkatisha
Patricia ili asiendelee kusema
alichotaka kukisema
“ Elvis tafadhali naomba
unisubiri nimaize kusema kile
ninachotaka kukwambia.Hata
mimi mwenyewe suala hili
linaniumiza sana Elvis.Natamani
kukuona ukiwa na furaha ,ukiwa
na mtoto nawe ukiitwa
baba.Natamani kuona nyumba
yetu ikiwa imechangamka ikiwa
na furaha lakini ninaumia sana
kwa kuwa niliyepaswa kuyafanya
yote haya yakamilike na mimi na
sina uwezo huo tena.,Siwezi
kukuzalia mtoto na siwezi
kuikamilisha furaha yako .Kwa
kuwa ninakupenda zaidi ya kitu
chochote kile sitaki kukuona
ukikosa furaha kwa hiyo kuna
jambo nimelifikiria”
“ Patricia what are you trying to
say? Mawazo gani hayo
unayoyawaza? Akauliza Elvis Elvis,let me be honest,you’ll
never be happy in your lfe without
a kid”
“ Stop it Patricia…please don’t
ever say that again.Sitaki kusikia
mambo kama hayo tena.Please my
love this conversation is over”
akasema Elvis
“ Elvis naomba unisikilize
ninachotaka
kukwambia.Ninachokisema ni
ukweli mtupu,najua wewe
unaweza kuvumilia kwa sababu
unanipenda lakini sina hakika
kama ndugu zako wanaweza
wakavumilia hali hii na lazima
litatokea shinikizo toka kwako la
kukutaka utafute mtoto.Najua
itafika wakati ambao utashindwa
kuvumilia.Sitaki kusubiri hadi
wakati huo ufike.Nataka tutafute
suluhisho la jambo hili sasa kabla
suala hili halijachukua sura mpya
kwani tayari moshi umeanza
kufuka.” “ Hakuna suluhisho lolote la
suala hili Patricia.Mjadala huu
tumekwisha ufunga muda mrefu
sana.Niliyekuoa ni mimi na si
ndugu yangu yeyote kwa hiyo
masuala ya ndani ya ndoa yangu
hakuna yeyote anayepaswa
kuyaingilia.”
“ Nalifahamu hilo Elvis mpenzi
,lakini sitaki ukose amani mume
wangu kwa sababu ya shinikizo la
ndugu .Nataka kukuona ukiwa na
furaha na amani siku zote katika
maisha yako kwa maana hiyo
nimefikiria sana na kufikia
maamuzi kwamba utafute
mwaname ambaye utazaa nae
mtoto ili usikose mrithi wa mali
zako .Naomba usistushe na jambo
hili.Haya ni maamuzi yangu na
sintakuwa na tatizo lolote
lile.Moyo wangu mweupe
kabisa.Mtoto huyo utakayempata
nitampenda na kumlea kama
mwanangu” akasema Patrcia .Elvis akamtazama na kucheka kidogo
kisaha akasema
“ patricia unawaza nini leo?
Mawazo hayo umeyatoa wapi? Kitu
gani kinakufanya uwaze mambo
kama hayo? Akauliza Elvis akiwa
amemkumbatia mkewe
“ Elvis usinielewe vibaya mume
wangu lakini hili ndilo suluhisho
pekee la kunusuru ndoa
yetu.Ninakupenda sana Elvis
.Nakupenda zaidi ya ninavyoweza
kukueleza na sitaki hata siku
moja nikukose katika maisha
yangu.Wewe ndiye kila kitu
kwangu.Wewe ndiye maisha
yangu.Please my love do that for
me”
“ Patricia..!!..akasema Elvis
“ Please my love naomba
ukubali kufanya hivyo.Tafuta
mwanamke ambaye utazaa naye
mtoto.Sintakuwa na tatizo lolote
hata kidogo na mwanamke huyo
na siku zote nitamuheshimu.Bila mtoto I swear we’ll never be happy
na ndoa hii itavunjwa na ndugu
zako.” Akasema Patricia.Elvis
akacheka
“ Mbona unacheka mpenzi?
Jambo gani limekufurahisha?
Akauliza Patricia.Elvis akambusu
na kusema
“ Ninacheka kwa sababu
sijawahi kusikia au kutegemea
kama siku moja ungeongea jambo
la ajabu namna hii” akasema Elvis
“ Elvis,hili si jambo la utani hata
kidogo.Ninaamaanisha
ninachokiongea “
“Patricia mke wangu hata kama
unamaanisha unachokisema
lakini naomba nikuhakikishie
kwamba jambo hilo unalolitaka
katu haliwezekani.Siwezi kufanya
jambo la namna hiyo na ninaomba
tusiendelee kuliongelea suala
hilo.Let’s talk about your coming
birthday this week” “ Elvis hatuwezi kuliacha jambo
hili hivi hivi.Naomba unielewe
mume wangu,nimeamua hivi kwa
sababu nakupenda na
ninakujali.Tafadhali naomba
unikubalie ombi langu hili.Endapo
tutapata mtoto haijalishi ni kwa
namna gani lakini itanusuru ndoa
yetu”
Elvis akamtazama mke wake
machoni kwa makini na kugundua
kitu Fulani.Akaacha mzaha na
kusema
“ Naomba unisikilize
Patricia.Mimi ndiye niliyekupenda
na kukuoa.Toka awali nililifahamu
tatizo lako na kwa moyo wangu
mmoja nikakubali kulibeba tatizo
hilo kwa sababu ya upendo wangu
kwako usio na kipimo.Nilikupenda
kabla hata ya kupatwa na
matatizo yale na sikufahamu
wakati ule kama una uwezo wa
kuzaa au huna.Nilikuwa nawe
wakati wa matatizo yale nilisimama pamoja nawe kwa
sababu ninakupenda.Nakuomba
usiendelee kujilaumu kwa
kilichotokea.Hupaswi kuadhibiwa
kwa makosa ya wakati ule kwa
sababu hukuwa na namna
nyingine ya kufanya zaidi ya vile
ulivyofanya .Patricia nakupenda
mno na nina furaha kubwa kuwa
nawe.Maisha yetu yana furaha
kubwa kwa hiyo nakusihi
usiwape watu nafasi ya kuingilia
maisha yetu ya furaha.Haya ndiyo
maisha yetu na hatuna kitu
kingine cha ufanya zaidi ya
kukubaliana na hali halisi
kwamba hatuwezi kuwa na mtoto
katika maisha yetu” akasema
Elvis.Patricia akatabasamu lile
tabasamu lake adimu sana ambalo
siku zote huwa lina mpagawisha
Elvis
“ Siku zote maneno yako
matamu yamekuwa
yakiupagawisha moyo wangu.Nashukuru kwa maneno
hayo mazito uliyonambia nami
nakuahidi kwamba sintaacha
kukupenda hata kwa sekude
moja.Pamoja na hayo yote lakini
bado moyo wangu unakosa
amani.Nina hakika lazima
kutakuwa na shinikizo kubwa
toka kwa ndugu zako pale
watakaogundua kwamba sina
uwezo wa kuzaa mtoto kwani
hutaweza kuificha siri hii milele.”
“ Patricia ,tulikula kiapo
kanisani kwamba tutapendana
katika shida na raha hadi kifo
kitutenganishe.Nitasimama katika
kiapo hicho hata siku moja
sintakwenda kinyume na kiapo
nilichoapa cha kukupenda wewe
peke yako na kukuvumilia hadi
kifo kitutenganishe.Naomba
tafadhali ufute kabisa wazo kama
hilo.Siwezi kufanya jambo kama
hilo unalotaka
nilifanye.Nakupenda sana Patriciana katu siwezi kukufanyia jambo
la ajabu namna hiyo.Naomba
mjadala wa suala hili uishie hapa ”
Akasema Elvis na kumbusu
Patricia halafu wakaendelea na
maongezi mengine kuhusiana na
sherehe ya siku ya kuzaliwa kwa
Patricia.
*************************
Saa saba za mchana siku
iliyofuata ,Patricia akataarifiwa
kwamba kuna mgeni
wake.Alikuwa na miadi ya
kukutana na rafikiye
Doreen..Akavua koti lake na
kutoka ofisini kwenda kuonana na
Doreen kisha wakaelekea Papino
Restaurant kwa ajili ya kupata
chakula cha mchana.Maongezi
yalikuwa mengi huku wakiendelea
kupata chakula halafu Patricia
akabadili maongezi. “ Doreen nimekuita kuna jambo
ambalo ninahitaji sana msaada
wako ndugu yangu”
Jambo gani Dr Patrica? Wewe
ni rafiki yangu mkubwa na niko
tayari kukusaidia katika tatizo
lolote” akasema Doreen msichana
mwenye uzuri wa kipekee.Binti
huyu ambaye mama yake ni
mzungu toka ufaransa na baba
mtanzania alikuwa ni rafiki
mkubwa wa Patricia ambaye
walikutana masomoni nchini
Marekani.Doreen kwa sasa ni
mfanyakazi wa kampuni moja ya
simu hapa nchini
“ Doreen nina matatizo
makubwa ndugu yangu”
“ Matatizo gani Patricia?
Naomba unieleze tafadhali”
“ Kwa kuwa wewe ni rafiki
yangu wa karibu nitakueleza ni
jambo zito na la ndani sana
kuhusiana na maisha yangu kwa
hiyo naomba tutakachoongea hapakibaki kuwa ni siri yetu” akasema
Patricia .Doreen akanywa funda
moja kinywaji na kusema
“ Patricia mimi nawe ni zaidi ya
marafiki.Mambo mengi ya siri
tumekuwa tunaambiana.Naomba
uniamini na uniambie jambo lolote
lile linalokusumbua”
Patricia akavuta pumzi ndefu na
kuanza kumsimulia Doreen
historia ya maisha yake hadi
alipopata ujauzito akiwa shuleni
hadi alivyotoa mimba ile na
kuhatarisha maisha yake jambo
lililomsababishia atolewe kizazi na
kupoteza uwezo wa kuzaa.
Doreen jasho likamtoka.Pamoja
na kumfahamu Patricia kwa muda
refu lakini hakuwahi hata siku
moja kulifahamu tatizo lile
alilokuwa nalo.Alitoa kitambaa na
kujifuta kijasho kilichoanza
kumchuruzika usoni.
“ Pole sana Patricia.Kwa kweli
suala hili ni gumu sana na sikuwahi kujua kama unaweza
kuwa na tatizo kama hili” akasema
Doreen
“ Ahsante sana Doreen.Ndiyo
maisha yalivyo” akasema Patricia
“ Matatizo kama haya ni ya
kawaida na yanaweza kumtokea
mtu yeyote.Nijambo lenye kuumiza
sana hasa ukifahamu kwamba
hutaweza tena kupata mtoto
katika maisha yako.Namshukuru
sana Elvis kwani analifahamu fika
tatizo langu lakini amekubali
kulibeba kwa moyo wake
wote.Pamoja na hayo kuna tatizo
limejitokeza” akasema Patricia
“ Tatizo gani Patricia? Akauliza
Doreen
“ Ndugu za Elvis tayari
wameanza kudai mtoto”
“ Gosh ! Tayari imeshafika
hapo?
“ Mambo tayari yameanza
Doreen.Tayari ndugu wameanza
kuhisi kuna tatizo na wameanza kudai mtoto.Jana mama mkwe
alinifuata kazini na kunihoji kwa
nini mpaka leo hatujapata mtoto”
“ Ouh my gosh ! Umemjibu nini?
“ Nilikosa cha kumjibu
ikanilazimu nimdanganye”
“ Ina maana mama mkwe hajui
chochote kuhusiana na tatizo hili?
Doreen akashangaa
“ Hakuna anayefahamu
chochote kuhusiana na tatizo
hili.Hata marehemu mama yangu
ambaye sikuwa nikimficha
chochote hakuwahi kuifahamu siri
hii.Ni siri yangu mimi na Elvis
kwani wakati mambo haya
yanatokea yeye ndiye aliyekuwa
pamoja nami na kwa sababu
ananipenda aliamua kunioa hivyo
hivyo.Wewe ndiye mtu pekee
ambaye nimekuamini kukwambia
siri hii na nina imani utanisaidia”
“ Niko tayari kukusaidia Patricia
kwani nafahamu ni namna gani
suala hili linavyotesa.Kuna rafiki yangu mmoja ninafanya naye kazi
anateseka sana kwa kukosa
mtoto.Ananyanyaswa mno na
ndugu za mume.Kwa hiyo
umepanga kufanya nini Patricia?
Akauliza Doreen.Patricia akanywa
maji kidogo akamtazama Doreen
na kusema
“ Doreen kuna jambo nimefikiria
kulifanya kunusuru ndoa yangu
ambayo sina hakika kama
itadumu endapo hakutakuwa na
mtoto”
“ Umefikiria kufanya nini
Patricia? Nimechanganyikiwa
mwenzako na sijui nifanye nini”
akasema Doreen
“ Kuna kitu nataka nikifanye
Doreen japokuwa ni kugumu
lakini sina budi kukifanya”
“ Niambie Patricia ni kitu gani
hicho unachofikiri kukifanya?
“ Doreen wewe ni zaidi ya rafiki
na ndiyo maana ninakuomba
msaada wako” Niambie Patricia niko tayari
kukusaidia kwa jambo lolote lile”
“ Nashukuru kusikia
hivyo.Ninakuomba uzae na Elvis”
akasema Patricia
Doreen akastuka na kuinuka
akashika kiuno na kumshangaa
Patrica
“ Patrica.!!! akasema Doreen
kwa mshangao.Patricia akainuka
akamshika mkono na kumetisha
kitini
Doreen akatoa kitambaa
akafuta jasho
“ Calm down Doreen.Najua
nimekustua na kukushangaza
sana.Naomba usistuke ndugu
yangu”
“ Patricia ni kweli umenistua
sana”
“ Usistuke Doreen.Usistuke
ndugu yangu” akasema
Patricia.Doreen akavuta pumzi
ndefu “akasema Tafadhali Patricia naomba
ukirudie tena kile
ulichokisema.Pengine sikusikia
vizuri”
Patricia akamtazama Doreen
kwa makini na kusema
“ Doreen matatizo yangu ni
kama nilivyokueleza.Nina tatizo
kubwa sana ndugu yangu.Ndoa
yangu iko mashakani baada ya
ndugu za Elvis kuanza kudai
mtoto.Sina uwezo wa kuzaa mtoto
kwa hiyo kuna hatari ndugu
wakamshinikiza Elvis atafute
mwanamke mwingine ili azae naye
mtoto.Na pindi ikitokea hivyo basi
ndoa yangu itakuwa matatani na
ndiyo maana ninakuomba wewe
unisaidie kwa hilo.Naomba uzae
na Elvis ili ndugu watulie baada
ya kusikia Elvis ana mtoto”
akasema Patricia.Doreen akacheka
kidogo na kusema
“ Patricia that’s
impossible.Hicho ni kitu ambacho hakiwezekani kabisa na sijui
mawazo haya umeyatoa wapi”
“ Doreen inawezekana .Naomba
unisaidie ndugu yako niko katika
matatizo makubwa.Najua si jambo
rahisi kutokea lakini mpaka
nimefikia hatua ya kukueleza
jambo kama hili ujue kwamba
mambo yamenifika
shingoni.Naomba unisaidie
Doreen.Bila msaada wako
nitamkosa Elvis”
Doreen akainama akafikiri na
kusema
“ Patricia nimekosa neno la
kusema.Naumia moyoni kwa
mateso unayoyapata na
ninatamani kukusaidia lakini
nasikitika kwamba katika suala
hili sintaweza kukusaidia.Siwezi
kuzaa na mumeo.Hilo ni jambo
lisilowezekana
kabisa.Utanisamehe Patricia.Mimi
kama rafiki yako sikushauri
ufanye hivyo unavyotaka kufanya Mpango huo ni hatari zaidi kwa
ndoa yako kwani huwezi kujua
nini kitatokea baada ya
mwanamke mwingine kumzalia
mtoto Elvis.Lakini kama unataka
kuendelea na mpango wako basi
nakushauri tafuta mwanamke
ambaye unamuamini kwamba
ataendelea kukuheshimu hata
baada ya kumzalia mtoto mumeo
na hatakuwa na tamaa ya kutaka
kuchukua nafasi yako kama mke
wa pili” akasema Doreen.Patricia
akatabasamu na kusema
“Ahsante kwa ushauri wako
lakini naomba ufahamu kwamba
haya ni maamuzi magumu
niliyoyaamua kuyafanya katika
maisha yangu na niko tayari kwa
chochote kitakachotokea.Najua ni
suala lenye changamoto nyingi na
ndani yake lazima kutakuwa na
maumivu mengi na makubwa
lakini niko tayari kuyakabili yote
hayo kwa lengo moja tu la Elvis apate mtoto.Ninampenda sana
Elvis na yeye ndiye kila kitu
kwangu na japokuwa hawezi
kunieleza wazi wazi ninaamini
ndani ya moyo wake anaumia kwa
kukosa mtoto” akasema Patricia
“ Patricia sikukatazi kufanya
hivyo unavyotaka kufanya lakini
nina mashaka kidogo kama
maisha yako na Elvis yataendelea
kuwa sawa baada ya kitendo hiki
kufanyika.Are you sure things will
continue to be the same?
Patricia akainama akafikiri na
kusema
“ Elvis loves me so much and
will never do anything to hurt
me.As much as we love each other
I hope we’ll continue to be the
same” akasema Patricia kwa
kujiamini
“ Ahsante sana kwa kujiamini
kiasi hicho lakini pamoja na hayo
nakusihi tafuta mtu ambaye
unamuamini na ambaye atakuwa na moyo wa kukusaidia kwa tatizo
lako na si bora mtu.Hili si jambo
rahisi sana kwa mtu kukubali
kulifanya”
“ Ndiyo maana nimekuamini na
kukuchagua wewe Doreen”
akasema Patricia
“ Patricia let me be honest with
you darling,I cant do such a thing
to you.Kuniambia nizae na mumeo
ni sawa na kuniambia nizae na
ndugu yangu jambo ambalo
haliwezekani .Patricia wewe ni
zaidi ya rafiki kwa hiyo siwezi
kufanya jambo kama hili kwa mtu
kama wewe ambaye
ninakuchukulia kama dada yangu
so I cant do that”
“ Yes you can do it Doreen”
akasisitiza Patricia
“ No Patricia I cant”
“ Yes you can” akasema tena
Patricia
“ If you love me and you value
our friendship you are gong to help me in this.I trust you so much
that’s why I’ve chosen
you.Naomba unisaidie Doreen
ninateseka mwenzio” akasema
Patricia huku macho yake
yakilengwa na machozi.Doreen
akamtazama rafiki yake
akamuonea hurma sana.Alitamani
kumsaidia lakini suala lile lilikuwa
gumu sana kwake.Alihisi kama
kuchanganyikiwa
“ Doreen endapo hutanisaidia
kuna hatari kubwa maisha yangu
yakaharibika endapo Elvis
atashindwa kuvumilia shinikizo la
ndgu zake na kuamua kutafuta
mwanamke mwingine wa kuzaa
naye.Ikiwa hivyo sintakuwa tena
na thamani kwa ndugu zake na
hawatataka kuniona tena.Sitaki
jambo hilo linitokee na ndiyo
maana ninakuomba unisaidie
wewe mtu ambaye ninakufahamu
na ambaye nina uhakika mkubwa
hata baada ya kuzaa na mume wangu bado hakuna
kitakachobadilika kati yetu”
akasema Patricia
Doreen akamtazama Patricia
usoni na kusema
“Why do you trust me that
much?
“ I don’t know Doreen but I do
trust you,my heart trust you “
akajibu Patricia
Kimya kifupi kikapita kila
mmoja akiwaza lake
“ Are you going to help me?
Akauliza Patricia
“ Patricia unaniweka katika
wakati mgumu sana.Nashindwa
nifanye nini.Ninaumia
unavyoteseka na ninatamani
kukusaidia lakini……”
“ Lakini nini Doreen? Kitu gani
ambacho kinakupa ugumu?
“ Suala hili si rahisi kama
unavyolichukulia Patricia.Hili ni
suala zito sana na gumu.Siku zote
nilipanga kwamba nitazaa mtoto na mwanaume ambae nitafunga
naye ndoa,kwa hiyo endapo
nitakubali kuzaa na mumeo basi
ndoto yangu hii haiwezi
kukamilika.Nitakuwa nimeharibu
mfumo mzima wa maisha yangu”
“Nalifahamu hilo
Doreen.Nafahamu changamoto
zake na ndiyo maana ninakuomba
toka moyoni mwako ukubali
kunisiaidia.Sina mtu mwingine
ambaye ninaweza kumkimbilia
kwa wakati huu”
Doreen akainama akafikiri na
kusema
“ Patricia kila ninapojaribu
kuufanya moyo wangu ukubaliane
nawe lakini unakataa kabisa”
“ Doreen uko tayari kuiona ndoa
yangu ikivunjika? Elvis ndiye kitu
pekee kinachonipa furaha na
sababu ya kuishi .He’s all I’ve got
now.I don’t have a father or
mother but I have Elvis.Sina
uwezo wa kupata mtoto kwa hiyo mtoto wangu ni Elvis
pekee.Endapo nikimkosa yeye basi
sintakuwa na sababu nyingine ya
kuendelea kuishi tena.Tafadhali
naomba unisaidie Doreen”
“ Patricia siko tayari kuiona
ndoa yako ikisambaratika..”
“ Kama hauko tayari basi
naomba nisaidie”
Doreen akainama akafikiri na
kusema
“ Mumeo anajua chochote
kuhusiana na mpango huu?
“ Nilimwambia…..” akasema
Patricia na kusita kidogo
“ Akasemaje? Alikubali ?
“ Hapana hakukubaliana
nami.Hayuko tayari kufanya kitu
kama hicho”
“ Kama hakubaliana nawe
utautekelezaje basi mpango huo?
Huoni kwamba unaweza ukazusha
tena suala lingine gumu?
“ I Have a plan how I’m going to
do it” akasema Patricia Bila ya mumeo kufahamu?
“ Ndiyo.Elvis hataelewa chochote
na atakapokuja kugundua
hatakuwa na la kufanya tena
kwani tayari kitendo kitakuwa
kimeshafanyika”
“ Patricia huoni kama unafanya
jambo la hatari sana? kulifanya
jambo hili kwa siri bila ya mumeo
kujua ni hatari.Hata kama
nikiamua kukusaidia siwezi
kufanya hivyo bila ya mume wako
kujua kwani endapo atagundua
jambo ulilomfanyia atakuwa na
hasira sana na jambo hili linaweza
kuzua matatizo makubwa”
“ Doreen namfahamu vizuri
Elvis katu hatakubali kufanya
jambo hili kwa ridhaa yake na
ndiyo maana kuna mpango
nimeubuni”
“ Mpango gani huo Patricia?
Patrcia akanywa maji halafu
akakohoa kidogo na kusema “ Siwezi kukwambia kwa sasa
mpaka nitakapokuwa na uhakika
kwamba uko tayari
kunisaidia.Naomba ukubali
Doreen I’ll take care of you.I’ll do
everything for you.Nitakupa hata
kiasi chochote cha pesa
utakachohitaji”
“ Patricia kama nikiamua
kukusaidia si kwa sababu ya pesa
lakini ni kwa sababu ya moyo
wangu umekubali kufanya
hivyo.Patricia wewe ni mtu
ambaye niko tayari kufanya
chochte kwa ajili yako lakini kwa
jambo hili najaribu kuwaza bila
kupata majibu”
“ Jambo gani linakusumbua?
Doreen akavuta pumzi ndefu na
kusema
“ Ninawaza endapo nitakubali
kuzaa na Elvis nini kitafuata
baada ya hapo? What if Elvis falls
for me? Siombi jambo hili litokee
lakini linawezekana kabisa kutokea na linaweza kuleta
mgogoro mkubwa kati yetu.Pili
jamii itanielewaje? Familia yangu
itanichukuliaje? Vipi kuhusu
maisha yangu? Mambo mengi
nitakuwa nimeyapoteza.Sina
maana kwamba nahitaji fidia
lakini tayari nitakuwa
nimepunguza vigezo vya kumpata
mwanaume wa ndot zangu kwani
wanaume siku hizi hawapendi
kuoa mwanamke ambaye
amekwisha zaa mtoto na
mwanaume mwingine.Kitu kingine
vipi kuhusu marafiki zetu na
wanaotufahamu wakigundua
kwamba nimezaa na mumeo?
Itakuwa ni aibu kubwa mno kwetu
.Tutazificha wapi nyuso zetu?
Patricia jambo hili ni gumu sana
na ndio maana inaniwia ugumu
hata kukubali kukusaidia”
akasema Doreen.Patricia akafikiri
kidogo na kusema “ Doreen naomba nikutoe hofu
kwamba Elvis hawezi akahamisha
mapenzi kwako.Ninamfahamu
vizuri na nina uhakika hawezi
kufanya jambo hilo kwa hiyo
usiwe na shaka na hata kama
ikitokea hivyo nina uhakika
kwamba huwezi kukubali
litokee.Naomba nikuhakikishie vile
vile kwamba kwa pamoja tutamlea
mtoto huyo na atakapofika umri
wa kuanza shule tutamchukua na
kuishi naye nawe utapata nafasi
ya kuendelea na maisha yako ya
kawaida na ninakuomba nikutoe
hofu kuhusu kuolewa.Siku hizi
wanaume wanapenda kuoa
mwaname ambaye ana uwezo wa
kuzaa.Mwanamke kama mimi
ambaye sina uwezo huo katu
siwezi kupata mume wa kunioa
ndiyo maana ninamuona Elvis
kama malaika wangu kwa sababu
pamoja na kufahamu hali yangu
lakini bado amekubali kunioa nakunifanya nami nionekane
mwanamke katika jamii.Kuhusu
familia ndugu na marafiki
wanaotujua ni lazima watakuwa
na mengi ya kusema lakini siku
moja watanyamaza, hakuna haja
ya kuwajali sana.Kwa hiyo
umeamuaje Doreen,utanisaidia?
“ Patricia nashindwa kukupa
jibu la m0ja kwa moja
kwasasa.Naomba unipe mda wa
kulitafakari suala hili halafu
nitakupa jibu baada ya tafakari ya
kina.Hili si suala la kulitolea
maamuzi ya haraka.Naomba unipe
siku mbili nikalifikirie” akasema
Doreen kisha wakaendelea na
maongezi mengine halafu
wakaondoka.
*******************
Jumamosi tulivu mwisho wa
wiki ,wengi wa wafanyakazi wakiwa katika mapumziko
,nyumbani kwa akina Elvis
kulikuwa na pilika pilika nyingi.Ni
siku ya kumbu kumbu ya
kuzaliwa kwa Patricia.Toka
asubuhi Patricia alionekaa ni mtu
mwenye furaha kubwa.Sherehe
iliandaliwa katika eneo kubwa la
bustani yao.
Pamoja na furaha aliyokuwa
nayo hakuna aliyefahamu
kilichokuwamo ndani ya moyo
wake.Alikuwa na furaha
iliyochanganyika na wasiw asi.
Kilichokuwa kikimfanya awe na
wasi wasi ni kwamba siku hii ni
siku ambayo alitazamia
kuutekelza mpango wake
alioupanga.Pamojana wasi wasi
huo alikuwa nao katika
kuutekelza mpango wake alikuwa
na furaha pia kwa rafikiye Doreen
kukubali ombi lake la kuzaa na
mumewe Elvis.Patricia na Doreen
ni marafiki wakubwa sana na
 
Yaani Patricia kaharibu kabisaaa
Hakuna mapenzi tena hapo
Na akili zake bwana hata kuwaza kuadopt mtt hajawaza
 
I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 17


ambao wamekuwa wakisaidiana
katika mambo mengi na ndiyo
maana baada ya kutafakari sana
Doreen aliamua kukubali
kumsaidia rafiki yake ambaye
alikuwa katika wakati mgumu
sana.
“ I’m so scared but I have to do
it today.Elvis will get angry at me
but I have to make it looks like an
accident.Endapo zoezi hili likienda
vizuri na Doreen akifanikiwa
kupata ujauzito amani itakuwepo
katika ndoa yangu” akawaza Elvis
wakati akiwa saluni akitengeza
nywele kwa ajili ya sherehe
itakayoanza jioni.Mara picha ya
mama yake ikamjia
“ Laiti mama yangu angekuwepo
angekuwa ni mfariji wangu
mkubwa katika wakati huu
mgumu nilionao.Mama yangu
alifariki bila kufahamu chochote
kuhusiana na siri yangu ya
kutokuwa na uwezo wa kupata mtoto.Aliniusia endapo nitapata
mtoto nimuite jina lake,hakujua
kama sina uwezo huo” machozi
yakamlenga
Baada ya kumaliza kupambwa
akapanda gari lake na kurejea
nyumbani ambako wageni tayari
walianza kuwasili.Miongoni mwa
wageni waliokuwa wamewasili
alikuwemo pia Doreen ambaye
kwa siku hii ya leo alikwa
amependeza sana akiwa ndani ya
ganun refu jekundu .Kwa uzuri
Doreen alijaaliwa uzuri wa kipekee
kiasi kwamba amekuwa akiwatoa
udenda wanaume wengi
kupagawishwa na uzuri wake
Patricia akawasalimu wageni
waliokwisha wasili halafu
akamshika mkono Doreen
wakaelekea pembeni
“ Nashukuru sana umekuja
Doreen.Nilikuwa na wasiwasi sana
pengine ungeweza kuogopa na
kuahirisha” akasema Patricia Doreen akacheka kidogo na
kusema
“ Siwezi kuahirisha shoga
yangu.Siwezi kukuangusha
ingawa nina wasi wasi sana”
“ Usiogoipe Doreen.Ni kweli si
jambo rahisi and I don’t know if
I’m doing the right thing but we
have to do it today” akasema
Patricia
‘Patrica how are we going to do
it? Bado hujaniambia ni namna
gani tutakavyofanya .Are we gong
to talk to him? Akauliza
Doreen.Patricia akatabasamu na
kusema
“ relax Doreen.Sherehe zikianza
nitakuambia.Tulia ,pata kinywaji
na uendelee kusubiri” akasema
Patricia halafu akaelekea
chumbani kwake kujiadaa.
“ Uphhhh…!!!!!!” Doreen akavuta
pumzi ndefu akachukua glasi yake
iliyojaa mvinyo akanywa funda
moja Patricia ana tatizo kubwa na
nimekubali kumsaidia.Ouh gosh !
suala hili ni zito sana.Nimeingia
katika mgogoro mkubwa lakini
kwa ajili ya kumsaidia rafiki
yangu.I don’t now what’s going to
happen but then I have to do
it.Patricia is my friend and I must
help her” akawaza Doreen.
“ Wow ! my angel you are so
amazing today” akasema Elvis
aliyeingia ghafla chumbani na
kumkuta Patricia
akijiremba.Akamsogelea na
kumbusu
“ You are so pretty my queen.I
love you” akasema Elvis
“ Thank you my love.I love you
too” akasema Patricia huku
akitabasamu
Saa moja za jioni ,wageni wote
walioalikwa tayari walikwisha
wasili na aliyekuwa akisubiriwa ni
Patricia pekee ajitokeze ili sherehe
zianze “ It’s time .let’s go” akasema
Elvis aliyekuwa chumbani na
Patricia akamshika mkono
wakaanza kutoka chumbani
“ Are you nervous? Akauliza
Elvis
“ Not much” akasema Patricia
kisha wakatoka nje na kuanza
kutembea katika zuria jekundu
lililotandikwa kuanzia
mlangoni.Muziki laini ulikuwa
unapigwa wakati Patricia akiwa
ameshikwa mkono na mumewe
wakielekea bustanini.Watu wote
walisimama huku wakiwapigia
makofi
Haikuwa sherehe kubwa sana
lakini ilifana vilivyo.Kila
aliyehudhuria sherehe ile
alisuuzika moyo wake.Kila kitu
kilikwenda kwa mujibu wa ratiba
na hatimaye zoezi la mwisho
likawa ni muziki.Patricia na
mumewe Elvis wakafungua muziki Walikumbatiana na kucheza kwa
mahaba mazito
“ Patricia,you’ll forever be my
one and only true
angel.Nakupenda zaidi ya
ninavyoweza kukueleza” akasema
Elvis wakati wakicheza halafu
akambusu
“ Ahsante sana Elvis kwa
maneno hayo mazito.Hata mimi
nakupenda na nitakupenda hadi
pumzi yangu ya mwisho” akasema
Patricia kisha wakakumbatiana
kwa nguvu zaidi
Wageni waalika nao wakajiunga
na akina Elvis kulisakata rhumba
huku wakiendelea kunywa
vinywaji .Kulikuwa na vinywaji vya
kila aina.Wakati muziki
ukiendelea,Patricia akamvuta
pembeni Doreen
“ Sikiliza Doreen.Elvis si
mnywaji sana wa pombe.Glasi
mbili tu za mvinyo huwa amelewa
na kawaida yake alewapo basi hulala usingizi mzito .Toka akiwa
chumbani nimeanza kumnywesha
pombe kali na mpaka sasa hivi
bado anaendelea kunywa kwa
maana hiyo muda si mrefu toka
sasa atazimika.Unamuona
anavyocheka? Akasema Patrica na
wote wawili wakaelekeza macho
yao mahala alikokuwa amekaa
Elvis na wenzake wakipata
kinywaji.
“ Basi ile ni dalili tosha kwamba
tayari amekwisha lewa.Nitakuwa
ninamtupia macho kwa karibu na
nikisha ona tayari amezidiwa
nitamchukua na kumpeleka
chumbani halafu nitazima taa na
kumuacha amelala.Wewe utaingia
chumbani na utalala
naye.Utafanya kila uwezalo ili
ufanya naye mapenzi.kwa kuwa
hizi ni siku zako za hatari kama
ulivyoniambia basi nina hakika
kabisa kwamba ukifanikisha
kufanya naye mapenzi utashika mimba na mpango wetu utakuwa
umefanikiwa.Najua atakapostuka
asubuhi na kukuta umelala naye
atapandwa na hasira lakini
utajitetea kwamba ulikuwa
umelewa na hukuwa ukielewa
chochote na ndiyo maana
ukajikuta mle chumbani .”
akasema Patricia
“ Patricia I’m so scared”
akasema Doreen kwa wasi
wasi.Patricia akavuta pumzi ndefu
na kusema
“Nafahamu hilo Doreen hata
mimi ninaogopa vile vile lakini
hakuna namna nyingine lazima
tufanye hivyo.” Akasema Patricia
halafu wakarejea tena katika
sherehe na moja kwa moja Patricia
akaenda katika meza ya vinywaji
akachukua chupa ya pombe kali
na kwenda nayo katika meza
aliyokuwa amekaa Elvis na rafiki
zake.Gentlemen hii ni zawadi yangu
kwenu” akasema Patricia na
kuiweka mezani ile chupa ya
pombe kali.
“ Wow ! Whazard !..akasema
moja wa marafiki wa Elvis kwa
furaha.Patricia akatabasamu na
kuifungua pombe ile na kuanza
kuimimina katika glasi.
“ I’m not going to take that.Its
too strong for me” akasema
Elvis.Patricia akamfuata
akambusu na kumnong’oneza
sikioni.
“ My love this is my gift to you
so you have to drink it .I want all
of us to drink it “ akasema Patricia
huku akiendelea kumimina pombe
ile katika glasi halafu kila mmoja
akashika glasi yake mkononi
halafu wakagonganisha na
kumtakia Patricia maisha marefu
yenye furaha.Baada ya kama
dakika kumi hivi Elvis akainamia
meza.Hakuwa akijiwezatena.Tayari alikwisha lewa
kupindukia
“ Ngoja nimpeleke Elvis
chumbani akapumzike” akasema
Patricia huku akimuinua Elvis na
kumsaidia kutembea kuelekea
chumbani.Elvis alikuwa amelewa
sana na walipofika tu chumbani
akajitupa kitandani kama furushi
.Patricia akamvua nguo na viatu
akamlaza vizuri na haikuchukua
muda mrefu Elvis akaanza
kukoroma Patricia akatabasamu
akazima taa na kutoka
“ Now its time” akasema Patricia
na kumfuata Doreen.
“Tayari nimekwisha mpeleka
chumbani na hafai kwa
usingizi.Tusubiri muda kidogo
halafu utaenda chumbani .Mimi
nitajifanya nimelewa sana na
nitalalala sebuleni” akasema
Patricia halafu wakaendelea na
vinywaji na ilipotimu saa saba za
usiku Patricia akamfanyia ishara Doreen aelekee chumbani .Doreen
aliondoka pale shereheni huku
akionekana kuyumba kwa
kuzidiwa na kilevi.Kila aliyemuona
aliamini kwamba alikuwa amelewa
sana.Doreen akaingia ndani na
kutazama kila upande kuhakiki
kwamba hakuna mtu yeyote mle
ndani halafu akaelekea moja kwa
moja katika mlango w a chumba
cha akina Elvis.Taratibu
akakinyonga kitasa cha mlango na
kuingia ndani.Taa ya chumbani
ilikuwa imezimwa lakini chumba
kilikuwa na mwanga hafifu wa
kumuwezesha kuona uliotoka
katika taa iliyokuwa nje.Kwa
hatua za taratibu Doreen
akatembea hadi kitandani na
kumshuhudia Elvis akiwa amelala
fofofo.Mapigo ya moyo yalikuwa
yakimuenda kwa kasi ya
ajabu.Mwili ulikuwa
unamtetemeka. Ouh gosh ! This is too hard for
me but then I have to do it”
akawaza Doreen huku
akimtazama Elvis pale kitandani
“ If you love me and you value
our friendship you are going to help
me.I trust you so much that’s why
I’ve chosen you.Naomba unisaidie
Doreen.Ninateseka sana mwenzio.”
Maneno haya ya Patricia yakamjia
tena kichwani
“ I have to help her.Nilikubali
kumsaidia na lazima nifanye
hivyo” akawaza Doreen akavua
viatu na kupanda kitandani
akajifunika shuka na
kumkumbatia Elvis
“ I must do it” akawaza Doreen
halafu akaanza utundu wa
kuyaamsha mashetani ya Elvis.
Wakati Doreen akiwa
chumbani na Elvis,wageni
wachache waliobaki nao wakaaga
na kuondoka wakabaki Patricia na
mtumish wao wa ndani .Patricia akaenda sebuleni na kujitupa
sofani.Akaijkunja mikono yake na
kuiweka kifuani.Alikuwa na wasi
wasi mwingi kuhusiana na
inachoendela chumbani kati ya
mume wake na rafikiye Doreen.
“ I’m so scared whats
happening in there.Ninafanya
jambo la hatari sana kumuacha
mume wangu alale na mwanamke
ambaye ni rafiki yangu
kipenzi.Ninamuamini vipi Doreen
kama yuko salama na hana
maambuki ya hili gonjwa letu la
siku hizi au hata magonjwa
mengine? Ni vipi kama atampa
Elvis penzi la kiwango cha juu na
kumfanya anogewe na kutaka tena
na tena? Ni vipi kama Doreen naye
atanogewa na kutaka kuendelea
kwa siri na Elvis s ….ouh No !
hawezi kufanya hivyo.Ninamuamini sana
Doreen.Ingawa wanadamu
hawaaminiki lakini sina namna
nyingine ya kufanya .Nataka Elvis
apate mtoto.Nataka awe na furaha
kwa kupata mtoto hata kama ni
kwa mwanamke mwingine kwa
sababu sina uwezo wa kumzalia
mtoto.Lakini hata kama akizaa na
mwanamke mwingine lazima awe
ni mwanamke ninayemjua na
kumuamini ili isije ikatokea
akanipora mume wangu
ninayempenda sana na ndiyo
maana nikamchagua Doreen.Ni
rafiki yangu wa muda
mrefu,tunapendana na
kuaminiana sana.Nina hakika
Doreen amekubali kunisaidia kwa
moyo mmoja” akawaza Patricia n a
kujilaza sofani Doreen alijifunika shuka
huku akiwa na uoga mwingi.Mwili
ulimsisimka alipogusana na Elvis.
“ Ninaogopa sana kwa jambo
hili ninalotaka kulifanya.Lakini
nimekwisha amua kulifanya na
tayari niko kitandani na mume wa
rafiki yangu.Sina ujanja tena,I
have to do it” akawaza Doreen
halafu akaunyoosha mkono wake
na kuanza kumpapasa Elvis
kifuani.Akapatwa na msisimko wa
aina yake,akafumba macho na
kuhisi raha ya ajabu sana
“ Nimemtamani Elvis kwa
muda mrefu sana.Ni mmoja kati
ya wanaume wanaonivutia na
kunisisimua sana kila
nikimuona.Kwa kiasi Fulani huwa
ninamuonea sana wivu Patricia
kwa kumpata mwanaume kama
huyu ambaye kila mwanamke ana ndoto za kuwa naye.Siamini kama
leo niko naye kitandani japo si
kwa ridhaa yake lakini ninahisi
raha ya ajabu.” Akawaza Doreen
huku akiendelea kumpapasa Elvis
.mwili wote ulimsisimka na tayari
mzuka ulikwisha mpanda na
alitamani sana kufanya mapenzi
na Elvis.Taratibu akaupeleka
mkono wake hadi katika bukta
aliyovaa Elvis,akaishika na
kuishusha chini hadimagotini
halafu akaitoa nguo ya ndani ya
Elvis na kuingia ikulu.Alisisimkwa
sana pale mzee alipokasirika na
kusimama kwa hasira.Mara Elvis
akageuza kichwa,Doreen naye
akastuka na kuacha alichokuwa
anakifanya.Kwa sauti ya uchovu
na ulevi,Elvis akasema
“ Patricia my angel,I’mso tired
today,tutafanya kesho,.Niache nipumzike.” Akasema Elvis kwa
suati ya kilevi na kugeukia
upande wa pili .Baada ya Elvis
kuanza kupitiwa na usingizi
Doreen akaanza tena utundu wake
lakini pamoja na jitihada zake
zote bado Elvis hakuwa tayari
kufanya mapenzi usiku ule.
“ Juhudi zangu zote
zimeshindikana.What am I going
to do? Ina maana kutapambazuka
bila ya kufanya kile kilichonileta
hapa? Akajiuliza Doreen
“ hapana lazima nifanye kila
linalowezekana kabla
hakujapambazuka.Nina hamu
sana na Elvis kwani tayari
mashetani yangu yamekwisha
panda.Ni muda mrefu sijakutana
na mwanaume.kwa sasa ngoja
kwanza nimuache alale na baadae
ulevi ukianza kumtoka lazimanihakikishe nimetimiza malengo
yangu.Hakutapambazuka leo bila
kufanya mapenzi na Elvis.Gosh
mwanaume huyu ni mzuri sana
jamani I wish angekuwa ni
mwanaume wangu.Kwa bahati
mbaya sana watu kama hawa
huwa hawatupati watu kama
sisi.Kitu gani alimpendea Patricia
mwanamke ambaye hana hata
uwezo wa kumzalia watoto? Lakini
anyway ngoja niache kuwaza hayo
mambo,Patricia ni rafiki yangu na
amenitaka nimsaidie.Ngoja
nimsaidie ” Akawaza Doreen na
kugeuka akaupeleka mkono wake
kifuani kwa Elvis na
kumkumbatiaakafumba
macho.Alijiona kama yuko katika
sayari nyingine *******************
Kengele ya saa ndogo iliyoko
katika meza ndogo iliyo pembeni
mwa kitanda,ikalia na kumstua
Elvis toka usingizini.Ni saa kumi
na nusu za alfajiri.Muda huu Elvis
huamka kwa ajili ya kufanya
mazoezi mepesi ya
viungo.Akainuka na kukaa
kitandani akainama akashika
tama.Alihisi kichwa kizito sana.
“ leo siwezi kufanya
mazoezi.Ngoja nipumzike.Jana
nilikunywa sana pombe.Sijui kwa
nini nilikunywa pombe na kulewa
namna ile,si kawaida yangu.”
Akawaza na kujitupa tena
kitandani .Hakuwa na usingizi
akageuka na kumkumbata Doreen
akidhani ni mkewe patricia. jana usiku nakumbuka
Patricia alikuwa ana hamu sana
na mimi lakini nilishindwa hata
kumpatia haki yake kutokanana
kuzidiwa kwa ulevi.Najua atakuwa
aliteseka sana usiku .Ngoja
nijikongoje walau nimpatie hata
mzunguko mmoja kumkata kiu
yake ya jana” akawaza Elvis halafu
akaanza kumpapasa katika
sehemu mbalimbali za mwili
wake.Bado chumbani hakukuwa
kumewashwa taa.Kulikuwa na
mwangaza mdogo uliotoka katika
taa iliyokuwa karibu na dirisha.
Kadiri Elvis alivyoendelea
kumpapasa Doreen ndivyo damu
ilivyozidi kumchemka.Doreen
ambaye tayari alikwisha amka
,akatoa migumo na kuzidi
kumpandisha mzuka
Elvis.Akamvuta kwake na kumkumbatia kwa nguvu akaanza
kumporomoshea mabusu
mfululizo.Ikulu ya Elvis ilikuwa
imechachama na tayari mzee
alikuwa amefura kwa hasira.
“I have to use this
chance.Siwezi kuipata tena nafasi
kama hii” akawaza Doreen na bila
kupoteza muda akaishika na
kuielekeza mahala husika. Alitaka
kuwehuka kwa raha aliyoisikia
pale mzee alipoanza kuzama
taratibu.Akatoa ukulele ambao
ulimstua Elvis.Akajinasua na
kwenda kuiwasha taa.
“ Ouh Mungu wangu
!!!.....akasema Elvis kwa mstuko
huku akihema kwa
nguvu.Hakuamini alichokiona
kitandani.Aliingiwa na hofu
kubwaThis cant be..Doreen
!!..akasema Elvis kwa sauti ndogo
“ How it happened?
Akajiuliza huku bado akiendelea
kumshangaa Doreen aliyekuwa
amekaa kitandani amejifunika
shuka sehemu za kifuani macho
yake yakiwa yamejaa aibu.
“ Usiku wote nimelala na
Doreen.Ouh My God..!! where is
my wife? Patricia yuko wapi?
.jambo hili limetokeaje?
akaendelea kujiuliza
Hakutaka kuendelea kupoteza
muda hadiPatricia atokee ,
akamfuata Doreen pale kitandani
“ Elvis ,I’m sorry…akasema
Doreen alipomuona Elvis
akimfuata pale kitandani huku
uso wake ukionekana kuwa na
hasira kali Doreen why are you here?
Akauliza
“ Hata mimi sifahamu
Elvis,nimejikuta nikiingia humu
chumbani.Nilikuwa nimelewa sana
jana na nikamwamba Patricia
kwamba ninakwenda kulala
akanielekeza chumba cha kulala
.Nilipotea chumba na kujikuta
nikiwa humu.Samahani sana
Elvis.”
“ Doreen kama ulizidiwa na
kilevi na ukapotea chumba Kwa
nini ulitaka kufanya mapenzi na
mimi? Ulimfahamu mtu uliyetaka
kufanya naye mapenzi? Akauliza
Elvis.Doreen akainama chini kwa
aibu
“ Answer me Doreen,kwa nini
ulitaka kufanya nami mapenzi
jana ? Elvis I’m sorry.Haikuwa
dhamira yangu,nilikuwa nimelewa
sana na nilipostuka nikakuta
kuna mtu pembeni yangu
nikapandwa na hisia nikajikuta
nikitamani,I’m so sorry Elvis,
please don’t tell Patricia about
this.” akasema Doreen huku
machozi yakimtoka.Elvis
akamtazama na kusema
“ Ok go now kabla Patricii
hajaingia humu
chumbani.Chumba cha wageni ni
cha tatu mkono wa kulia kutoka
hiki.Go now” akasema Elvis.Kwa
aibu Doreen akainuka.Bado
alikuwa mtupu.Akaichukua nguo
yake na ndani na kuivaa.Mwili
wote wa Elvis ukamsisimka
alipoushuhudia mwili ule
mwororo wa Doreen. she’s so sexy !! akawaza
Elvis akimshuhudia Doreen
akivaa nguo zake.
“ Go now,kuna watu wamelala
hapa wasije wakaamka na
kukushuhudia ukitoka humu
chumbani .” Akasema Elvis huku
akiufungua mlango taratibu na
kuizima taa ya kwenye varanda ili
Doreen asionekane.
“ Its clear,go now” akasema
Elvis.Doreen akatoka na kuingia
katika chumba alichoelekezwa
.Elvis akaenda kukaa kitandani
alikuwa na mawazo mengi sana
“ Sielewi jambo hili
limetokeaje.Ni ulevi gani huo
aliokuwa nao Doreen hadi afikie
hatua ya kupotea na kuja kulala
chumbani kwangu? Tena akadiriki
hata kuniamsha hisia ili tufanye
mapenzi.Hapana siamini kabisa kama kwelialikuwa amelewa.Mtu
aliyelewa na kuhsindwa
kujitambua hadi kupotea mahala
anakokwenda asingeweza
kunifanyia mambo kama
aliyonifanyia jana
Doreen.Inaonekana alikuwa
amedhamiria kufanya vile.Patricia
yuko wapi ? Anafahamu chochote
kuhusiana na alichokifanya rafiki
yake? Akajiuliza na kuikumbuka
picha ya Doreen akivaa nguo yake
ya ndani
“dah ! pamoja na yote lakini
Doreen anasisimua sana .Kila
nikimfikiria nahisi mwili
unanichemka.Ni mwanamke
aliyeumbwa hasa akaumbika.Dah
! nashukuru niliwahi kustuka na
sikuendelea zaidi na mchezo
ule.Nina hakika kwa uziri
aliokuwa nao yule mwanamke kama ningeendelea basi
ningekuwa katika matatizo
makubwa kwani ningetamani
kuendelea tena na tena .Uzuri
wake ni kama ua lenye harufu
nzuri inayowavuta nyuki
kuling’ang’ania .Hili ni jaribu kali
kuwahi kulishinda katika maisha
yangu”akawaza Elvis huku akihisi
ikulu kukiwa hakuna usalama kila
alipoikumbuka picha ile ya Doreen
akiwa mtupu
“ Doreen ananitia majaribuni.
No ! I cant do that.I love my wife so
much.Niliapa kumpenda Patricia
na sintamsaliti hata siku moja
,mbaya zaidi na rafiki yake
mkubwa.” Akawaza Elvis na
kutoka mle chumbani akaelekea
sebuleni kumtafuta mke
wake.Patricia alikuwa amelala sebuleni katika sofa huku kukiwa
na chupa za pombe pembeni yake
“ masikini Patricia unywaji
gani huu wa pombe? akawaza
Elvis huku akimuinamia na
kumbusu
“ nadhani alikunywa pombe
nyingi jana kutokana na furaha
aliyokuwa nayo na vile vile ili
kupunguza mawazo ya jambo
linalomsumbua sana kwa sasa la
kukosa mtoto.Patricia hatakiwi
kuumiza kichwa chake kwa sauala
hili kwani nimekwisha
muhakikishia kwamba hakuna
yeyote mwenye mamlaka ya
kumuuliza chochote kuhusiana na
mtoto.Nilimuoa huku nikijua
kabisa kwamba hana uwezo wa
kupata mtoto na nimekubaliana
na hali hiyo kwa sababu
ninampenda.Kama mimi ambaye ndiye mumewe ninakubaliana na
hali yake ,basi si mama wala mtu
mwingine yeyote ambaye ana
ruhusa ya kuingia katika ndoa
yetu na kuanza kudai
mtoto.Hakuna mahala
tumeandikiana mkataba kwamba
baada tu ya ndoa nitawazawadia
mtoto.”akawaza Elvis huku
akimuamsha mkewe.
“ patricia..!! Patricia.!!!..”
akaita Elvis.Patricia akafumbua
macho.
“ Ouh Elvis ! akasema kwa
sauti ya uchovu.Bado alionekana
kulemewa na ulevi.
“ Wake up Patricia.Wake up
my love,kumepambazuka.Twende
ukalale chumbani” akasema Elvis
huku akimsaidia kuinuka
wakaelekea chumbani “ Elvis kichwa kinaniuma
sana.Nilikunywa pombe nyngi
jana” akasema Patricia
“ Mkewangu ,usirudie tena
kunywa pombe nyingi kiasi
hiki.Hata mimi jana nilikunywa
na kulewa sana na sijui hata
nilifikaje kitandani”
“ Mimi ndiye niliyekuleta
baada ya kukuona umezidiwa na
haujiwezi “ akasema Patricia
“ Ahsante sana mke
wangu.Anyway kunywa maji
kwanza halafu endelee kulala
ujipumzishe.Ngoja nikakuandalie
supu” akasema Elvis na kutoka
akaelekea jikoni.Patricia alijilaza
pale kitandani akiwaza..
“Sijui kama mambo yalienda
kama tulivyokuwa
tumepanga.Natamani kujua kama
mpango wetuulifanikiwa.Natamani kufahamu
nini kilitokea baada ya Elvis
kuamka na kujikuta akiwa
amelala na Doreen? Ingawa uso
wake hauonyesh kama kuna
jambo la tofauti lililotokea lakini
kuna aina Fulani ya wasi wasi
katika sauti yake. Ngoja
nijipumzishe kwanza nitapata jibu
kwa Doreen baadae”
Elvis alikuwa jikoni
akimuandalia supu mkewe lakini
bado tukio la kujikuta akiwa
amelala na Doreen kitanda kimoja
tena wakiwa watupu liliendelea
kumtesa sana.
“ Bado naendelea kujiuliza
kuhusiana na tuko lile .Bado
sielewi nia ya Doreen ilikuwa
nini.Inawezekana Doreen akawa
ananitamani sana na alipomuona
Patricia amezidiwa na kilevi akaamua kuingia chumbani
kwangu kwa lengo la kutaka
kufanya mapenzi nami? .lakini
kwa nin I afanye hivyo wakati
akifahamu kabisa kwamba mimi
ni mume wa rafiki yake kipenzi?
Ingekuwaje iwapo Patricia
angemkuta chumbani kwetu?
Utetezi wake eti kwamba alikuwa
amelewa na akajikuta mle
chumbani hauingiiakilini.Mtu
aliyelewa kiasi cha kutojitambua
aliwezaje kuvua nguo zote na
kufanya juhudi za kutaka
kufanya mapenzi na mtu
aliyemkuta hapo kitandani bila
kufahamu mtu huyo ni nani?
Bado hainiingia akilini
kabsa..Nina imani kabisa Doreen
alidhamiria kufanya vile.Dah !
wanawake” akawaza Ninaanza kuwa na mshaka
kidogo kuhsusiana na tukio
hili.Juzi Patricia aliniambia
kwamba anataka nipate mtoto na
akanipa uhuru wa kuzaa na
mwanamke mwingine yeyote
nitakayeona anafaa.Nina wasi wasi
huu usije ukawa ni mpango wake
nilale na rafiki yake ili nizaie
naye.Kama ni hivyo atakuwa
amekosea sana.Siko tayari
kufanya hivyo.Ninampenda jinsi
alivyo na kama ni mateso yake
basi tutayabeba sote.Siko tayari
kumsaliti mke wangu eti kwa
kigezo cha mtoto.Niliapa siku ile
kanisani kwamba niko tayari
kumpenda katika hali zote,na
ndivyo ninavyofanya.Hata
nikishinikizwa na dunia nzima
siko tayari kumkosea heshima
mke wangu na kwenda kuzaa nje ya ndoa yangu.Kama mwanamke
ninayempenda hana uwezo wa
kupata mtoto huo ni msalaba
wangu na lazima niubebe.Hakuna
njia ya mkato hapa.” Akawaza na
kwa mara nyingine picha ya
Doreen akiwa mtupu ikamjia
“ Nitaifutaje picha hii
kichwani kwangu? naona kama
inajirudia kwa kasi kubwa kila
dakika.Sitaki jambo hili linitie
majaribuni.Sitaki picha ile ya
Doreen akiwa mtupu iendelee
kukitawala kichwa changu na
kunisababishia niwaze mambo
mengine mabaya.Lakini hata
hivyo mwenyezi Mungu anastahili
sifa kwa uumbaji wake.Doreen ni
mwamanke aliyependelewa uzuri
wa kipekee kabisa.Japokuwa
nimeoa na ninaishi kiapo change
cha ndoa na siwezi kutoka nje ya ndoa yangu lakini lazima nikiri
kwamba Doreen ni mwanamke
mwenye mvuto wa ajabu sana na
anayeweza kumfanya mwaume
yeyote afanye jambololote
kumpata.Amenifanya nikasisimka
mno .Dah ! .” akawaza Elvis.
********************
 
I DIED TO SAVE MY PRESDENT

Sehemu 18

Ni saa tano za asubuhi,siku
ya jumapili bado Patricia na Elvis
wako kitandani wakijipumzisha
kutokana na uchovu wa siku
iliyotangulia.Wote walikunywa
pombe nyingi katika sherehe ya
kuzaliwa Patricia.Mlio wa simu
liyokuwa ikiita ndio uliomstua
Elvis akainuka na kwenda
mezani.Ilikuwa ni simu ya Patricia
iliyokuwa ikiita.Katika kioo cha
simu iliandika “ Dharura kaziniElvis akaichukua simu ile na
kumuamsha mke wake
“ mmhh my darling,niache
nilale kidogo .Nimechoka sana”
akasema Patricia huku macho
yake yakionyesha wazi kwamba
alikuwa na uchovu mwingi
“ Pokea simu hii
darling,imepigwa katika namba ya
dharura ya kazini kwako”
akasema Elvis.Neno dharura
likamstua Patricia akainuka
haraka na kuichukua simu
akabonyeza kitufe cha kupokelea
“ Hallow “ akasema
“ Dr Patricia kuna dharura
imetokea”
“ Jambo gani limetokea
Amanda?akauliza
“ Cindy amezinduka”
“ Cindy?!! Patricia
akashangaa Ndiyo amezinduka sasa hivi”
“ Anaweza kuongea?
Anajifahamu?
“ Ndiyo anafahamu zake na
anaweza kuongea japo anasikika
kwa mbali ”
“ Ok nakuja sasa hivi”
akasemaPatricia na kukata simu
.Akavuta pumzi ndefu
“ Kuna nini kimetokea?
Akauliza Elvis
“ Kuna mgonjwa mmoja
ambaye aliletwa pale hospitalini
kwetu akitokea hospitali ya taifa
ya Muhimbili akiwa hana
fahamu.Kwa mujibu wa taarifa
iliyotoka Muhimbili ni kwamba
mwanadada huyo aliokotwa na
wasamaria wema na kupelekwa
pale akiwa hana fahamu .Baada
ya kumchunguza wakaamua
kumleta pale kwetu ili tumfanyie uchunguzi wa kina kuhusianana
nini kinamsumbua kichwani”
“ Nini kilimpelekea apoteze
fahamu? Akauliza Elvis
“ Kwa mujibu wa uchunguzi
tuliomfanyia,alipoteza fahamu kwa
sababu ya kupigwa sana hasa
sehemu za kichwani.Inaonekana
watu waliompiga walikuwa na
lengo la kumuua.”
“ Dah jamani dunia hii imejaa
watu makatili sana”: akasema
Elvis
“ Kwa muda wa miezi miwili
amekaa bila fahamu na katika
muda huo wote hakuna hata
ndugu yake mmoja aliyejitokeza
ndiyo maana nikaamua kumpa
jina la Cindy” akasema Patricia
“ So are you going there?
Akauliza Elvis Yes ! I have to go there”
akasema Patricia
“ I’ll go with you.Umechoka
sana na siwezi kukuacha
ukaendesha gari ukiwa katika
hali hii.Nitakupeleka kazini na
kukurudisha” akasema Elvis
.Wakaingia bafuni kuoga kisha
wakaelekea katika chumba cha
kulia chakula wakapata kifungua
kinywa
“ Sylvie,Doreen bado
hajaamka? Patricia akamuuliza
mtumishi wao wa ndani
“ Aliamka ,akaomba kahawa
kisha akarudi tena kulala” akajibu
Sylvie
“ Ok ngoja nikamuangalie
kabla hatujaondoka.Jana alikuwa
amelewa sana” akasema Patricia
na kuinuka akaelekea katika
chumba cha wageni alikolala Doreen.Bila kubisha hodi Patricia
akaingia chumbani na kumkuta
Doreen amejilaza kitandani
“ Bado umelala? Inaonekana
shughuli ya jana ilikuwa nzito
sana” akasema Patricia huku
akitabasamu.Doreen akainuka na
kunyoosha mikono akamfanyia
ishara Patricia akae kitandani
“ Enhee nipe habari
shoga.Mambo yalikwendaje?
“ Mhhhhh..!!!!” Doreen
akaguna
“ Mbona unaguna?
“ Mambo hayakwenda kama
tulivyopanga” akasema Doreen
“ What happened?
Doreen akainuka na kukaa
kisha akasema
” Nilijitahidi sana kadiri
niwezavyo bila mafanikio.Elvis alikuwa amelala fofofo.Alikuwa
amezidiwa na kilevi”
“ Dah ! So what happened?
Alikuona?
“ Nilijikuta nimepitiwa na
usingizi na nikastuka asubuhi
Elvis akiwa amewasha taa
ananishangaa.Shoga ninasikia
aibu sitaki hata kuonekana huko
nje hadi atakapoondoka.Sijui
nitamtazamaje Elvis usoni “
“ Alisemaje alipokuona?
Akauliza Patricia huku sura yake
ikionyesha wasiwasi mwingi
“ Alistuka sana.Sura yake
ilipata wasiwasi
mkubwa.Hakuamini
kilichotokea.Nilimuomba
samahani nikaondoka haraka kuja
huku.Patricia tumefanya jambo la
aibu sana.Nasikia aibu mno”
akasema Doreen “ samahani sana Doreen kwa
kukuingiza katika jambo hili”
“ Usijali Patricia ,yote hii
ilikuwa ni katika kutafuta
suluhisho la matatizo yako.”
Patricia akakaa kimya akafikiri na
kusema
“ So what are we going to do
now? Akauliza
“ I don’t know Patricia.I’m so
scared to do it again” akasema
Doreen.Patricia akainama
akatafakari na kusema
“ Ahsante Doreen kwa
kujitolea kunisaidia.kwa sasa
naelekea hospitali kuna dharura
imetokea.Nitakuja kukuona jioni
tutaongea zaidi”akasema Patricia
“ Elvis naye anatoka?
Ninaogopa hata kumtazama usoni”
akasema Doreen “ Elvis naye anaondoka.Ndiye
anayenipeleka hospitali.”
“ Ok hata mimi ngoja
nijiandae niondoke niende
nyumbani nikapumzike .Leo
sintatoka kabisa” akasema Doreen
Patricia akatoka mle
chumbani akamuelekeza
mtumishi wake kazi za kufanya
kisha yeye na mumewewakaingia
garini na kuondoka kuelekea
hospitali
‘ Patricia ,hivi Doreen anaishi
na nani?akauliza Elvis.Patricia
akastushwa kidogo kwa swali lile
“ Unauliza Doreen anaishi na
nani..?
“ Ndiyo.Doreen anaishi na
nani? Ana mume?
“ Hana mume anaishi peke
yake.Kwa nini umeuliza? Nilihitaji tu kufahamu kwa
sababu nilishangaa uliponiambia
kwamba alilala pale nyumbani
nikajiuliza angewezaje kufanya
hivyo kama tayari ana mume
wake”
Patricia akacheka kidogo na
kusema
“ Doreen hana mume na
ndiyo maana yuko huru kufanya
jambo lolote”
“ Ok sawa.Uliionaje sherehe
ya jana?
“ Sherehe ilipendeza sana
kiasi kwamba siwezi hata
kuielezea.Japokuwa matatizo
madogo madogo kama ya kulewa
kupitiliza yalikuwepo lakini kwa
ujumla wake shertehe ilikuwa
nzuri sana.”
“ jana ulikunywa pombe
nyingi sana” akasema Elvis Kweli nilikunywa
sana.Baada ya wageni kuondoka
tulibaki tunaendelea kunywa mimi
na Doreen na sikumbuki hata
mwenzangu aliondoka saa ngapi
kwenda kulala.Sitaki tena kurudia
unywaji pombe wa namna ile”
akasema Patricia.Elvis akacheka
kidogo na kusema’
“ Kitugani kilikufanya unywe
pombe namna ile?
“ Ni furaha tu niliyokuwa
nayo jana.Nilitaka nifurahi kwa
sababu kwa siku za hivi karibuni
kichwa changu kimekuwa na
mambo mengi sana kwa hiyo jana
nikaona ni bora niitumie siku ile
kujisahaulisha mambo yote na
kufurahi.” Akasema Patricia.Elvis
akageuza shingo na kumtazama
mkewe Patricia naomba tafadhali
usiwaze chochote kuhusiana na
mambo yale aliyokwambia
mama.Niachie mimi suala hili
nitalishughulikia kama
nilivyokuahidi.” akaema
Elvis.Patricia akatabasamu bila
kusema chochote safari ikaendelea
Walifika hospitali Patricia
akampeleka mumewe sehemu ya
kupumzikia akamuomba amsubiri
pale
“ I must do something”
akawaza Elvis halafu akachukua
simu yake na kuzitafuta namba za
simu za Doreen akampigia
“ Hallow Elvis” akasema
Doreen baada ya kupokea simu
“ Doreen nahitaji kukuona
,umeshaondoka hapo nyumbani? Nimeshaondoka niko njiani
kuelekea nyumbani kwangu.Kuna
tatizo lolote Elvis?
“ Hakuna tatizo ila nahitaji
kukuona.We need to talk”
“ Sawa Elvis,unataka tuonane
wapi? Nielekeze sehemu
unakotaka tukutane”
“ Usisumbuke Doreen
ninakuja nyumbani kwako”
akasema Elvis huku akishuka
ngazi na kuelekea lilipo gari lake.
“ Najua Elvis anataka
kuongelea kuhusiana na lile tukio
la jana.Niliuona uso wake namna
alivyokuwa akinitazama.Patricia
ameniingiza katika mgogoro
mkubwa.I’m so stupid.Nimekubali
kufanya jambo kama lile na
kujidhalilisha namna ile.Ninaona
aibu sana na sijui nitamtazamaje
Elvis”akawaza Doreen lakini maraakatabasamu baada ya
kukumbuka kitu
“ Pamoja na mambo
kutokwenda kama tulivyotaka
lakini kuna jambo nililiona usoni
kwa Elvis.Japokuwa alistuka sana
aliponiona lakini alikuwa
ananitamani.Kuna kila dalili
kwamba Elvis alitamani sana
kufanya nami mapenzi lakini
alikuwa akimuogopa mke
wake.Yawezekana hilo ndilo jambo
linalomleta kwangu.” Akawaza
Doreen na kukumbuka picha ya
tukio la jana
“ Mwili wangu ulipogusana na
Elvis nilipatwa na msisismko wa
aina yake.Nilihisi ni kama
nimelala na mwanaume
wangu.Elvis ni mwanaume
anayesisimua sana.Tayari
tulikwisha anza kufanya mapenzi kama nisingepiga ule ukulele kwa
raha ya ajabu niliyoisikia basi
asingestuka..Sijui nitafanya nini
kumpata Elvis tumalizie pale
tulipoishia .Ouh jamani sijui kwa
nini mawazo kama haya
yananijia.Lakini yote haya
ameyataka Patricia mwenyewe ”
akawaza Doreen na kukumbuka
msisimko alioupata wakati
akizichezea nyeti za Elvis.
“ Ni muda mrefu nilimtamani
Elvis lakini sikuwa na mawazo
yoyote kwamba siku moja mimi na
yeye tunaweza kulala kitanda
kimoja tena katika hali ya
utupu.Elvis ni mume wa rafiki
yangu kipenzi na siku zote
nimeliheshimu hilo..Ni Patricia
mwenyewe ndiye
anayenisbabishia niwaze mawazo
ya namna hii baada ya kunitaka nilale na mumewake.Japokuwa
Elvis ni mwanaume
ninayemtamani sana lakini sikuwa
tayari kulala naye lakini Patricia
alinilazimisha sanahadi nikakubali
na baada ya Elvis kuuona utupu
wangu sina cha kuogopa
tena.Lazima ndoto yangu
itimie.Lazima nitembee naye.”
akawaza Doreen wakati akikata
kona kuingia nyumbani kwake
.Martha mtumishi wake wa ndani
alimfungulia geti akaingiza gari
halafu akaelekea moja kwa moja
chumbani kwake ambako alioga
haraka haraka na kujiandaa kwa
ajili ya kukutana na
Elvis.Alipomaliza kujiandaa
akapanda kitandani na
kujilaza.Picha ya tuko la jana
haikuacha kumjia kichwani. Nina hakika kinachomleta
Elvis ni kuhusianana tukio la
jana tu.yawezekana anataka kuja
kuende………….”alikatishwa
mawazo yake na mtu aliyebisha
hodi katika mlango
wake.Akainukana kwenda
kuufungua Alikuwa ni mtumishi
wake wa ndani
“ Dada yule mgeni uliyesema
akija nimkaribishe sebuleni tayari
amekwisha fika” akasema Martha
mtumishi wa ndani wa Doreen
“ Ok Martha mpeleke katika
chumba cha maongezi” akasema
Doreen kisha akaufunga mlango
wake na kuuegemea.Mapigo ya
moyo wake yalibadilika na kuanza
kwenda kasi
“ Naona aibu sana kukutana
tena ana kwa ana na Elvis.”
Akawaza halafu akaenda katika meza yake ya vipodozi akajitazama
usoni
“lakini kwa nini niogope w
akati ni mke wake ndiye
aliyesababisha haya yote? Sikuwa
nikihitaji jambo kama hili litokee
lakini Patricia amelazimisha hadi
limetokea.Elvis amekwisha uona
utupu wangu na nina hakika
hataacha kunifuata kama nyuki
.Potelea mbali litakalotokea
nalitokee tu siwezi kuendelea
kumuogopa ,kama akitaka penzi
mimi nitampatia tu kwani tayari
nimeruhusiwa na mke wake na
hata hivyo Elvis ni mwanaume
niliyemtamani siku nyingi sana.”
Akawaza Doreen kisha akafungua
mlango akatoka na kuelekea
katika chumba cha maongezi aliko
Elvis Elvis ! karibu sana”
akasema Doreen huku
akijilazimisha kutabasamu
“ Doreen samahani sana kwa
kukusumbua .Najua muda huu
ulikuwa unapumzika”
“ Usijali Elvis,karibu sana.”
Akasema Doreen huku akijitahidi
kuyaficha macho yake yasikutane
na yale ya Elvis.
“ Uhhm Doreen nimelazimika
kuja kukuona ili tuzungumzie
suala lile lililotokea jana
usiku.Bado ni….” Akaanzisha
mazungumzo Elvis lakini Doreen
akamkatisha
“ Elvis utanisamehe sana kwa
tukio lile la aibu.Hata mimi
mwenyewe sielewi
lilitokeaje.Naomba samahani sana
Elvis na tafadhalinaombausimweleze Patricia “ akasema
Doreen
“ Doreen najua ni pombe
mlizokunywa jana ndizo
zilizosababisha jambo lile
litokee.Sote tulikuwa tumelewa
sana jana.Lakini ninachojiuliza ni
kwa nini ukaacha vyumba vingine
vyote na kuingia kwangu? Ni kwa
nini ukanivua hadi nguo yangu ya
ndani na kunipandisha hisia ili
tufanye mapenzi? Kwa nini
ulifanya vile? Doreen ni sisi pekee
tunaofahamu nini kilitokea na
wala sintomueleza mke wangu
kwa hiyo tafadhalinaomba
unieleze ukweli,ni kweli ulikuwa
umelewa au ulidhamiria kufanya
vile? Niambie ukweli nitakuelewa
Doreen “ akasema Elvis
“ Elvis kusema ukweli sikuwa
nikijitambua kutokana na pombe nilizokuwa nimekunywa.Baada ya
sherehe kumalizika na wageni
wote kuondoka nilikuwa nimelewa
sana na kwa hiyo Patricia
akanishauri kwamba nilale pale
pale nyumbani.Tuliendelea
kunywa pombe hadi usiku mwingi
nikamwambia Patricia anionyeshe
chumba nikalale lakini alikuwa
amelewa hajitambui hivyo
nikainuka mwenyewe na kuanza
kutafuta chumba kilipo nikajikuta
nimeingia katika chumba
chenu.Elvis sina maelezo ya
kutosha kulielezea jambo hili kwa
sababu kuna mambo hata mimi
sikumbuki yalitokeaje”akasema
Doreen
“ Natamani sana kukubaliana
nawe Doreen lakini kitu ambacho
hakiniingi akilini ni kwamba kama
ulikuwa umelewa kiasi chakutojitambua kwa nini basi
ukavua nguo zako zote na
kuziweka sofani kisha ukapanda
kitandani mtupu? Pale kitandani
ulimkuta mtu amelala kwa nini
ukaanza kumchezea kwa
madhumuniya kufanya mapenzi?
Akauliia Elvis.Swali lile
likambabaisha Doreen
akashindwa kujibu
“Naomba unijbu Doreen.Ni
kweli ulikuwa umelewa au
ulidhamiria kufanya vile?
Akauliza Elvis
“ Elvis,..” Doreen akataka
kusema kitu lakini akaogopa

“ Tell me please” akasisitiza
Elvis
“ Naomba uniambie
ulijisikiaje uliponiona asubuhi ni mimi ndiye niliyelala nawe na si
mkeo Patricia?
Elvis akamuangalia Doreen kwa
mshangao mkubwa
“ I was angry,very angry….”
Doreen akatabasamu kidogo na
kusema
“ No Elvis,hukuwa
umekasirika.Ulikuwa unamuogopa
mkeo Patricia asijue .I saw your
face.You needed it.You needed me
,right? Akasema Doreen na
kumfanya Elvisi azidi
kumshangaa.
“ Doreen mambo gani hayo
unayasema.Wewe ni rafiki mkuwa
wa mke wangu,unadhani Patricia
angesema nini endapo angekukuta
chumbani kwake tena ukiwa
mtupu? Halafu ulijua kabisa
kwamba umelala kitandani na
mume wa rafikiyako kipenzi na wakati nikijiandaa kufanya tendo
la ndoa nikidhani niko na mke
wangu wala hukuonekana
kustuka.Ni wazi ulikuwa
umedhamiria jambo lile
litokee.Kwa nini Doreen.kwa nini
ulitakakufanya vile? Kwanini
ulitaka kumsaliti rafiki yako
kipenzi? Akauliza Elvis.Doreen
akamtazama na kuuliza
“ Elvis why are you here?
Akauliza Doreen huku
akimsogelea Elvis.
“ I’m here to find answers”
akajibu Elvis
“ No Elvis.You are not here for
answers” akasema Doreen huku
akimkaribia zaidi Elvis na
kukigusisha kifua chake katika
kifua cha Elvis na kuyafanya
mapigo ya moyo ya Elvis
yabadilike You are here because you
need something.Tell me what do
you want Elvis?Usiogope Elvis
tuko hapa peke yetu,mkeo hayupo
wala hakuna anayetuona.So tell
me what do you want?” akasema
Doreen .Elvis aliendelea
kumtazama akashindwa aseme
nini.
“ Why are you doing this
Doreen.” Akauliza Elvis
“ Elvis mbona unauliza
maswali mengi sana.Niambie bila
kunificha ni kitu gani umekifuata
hapa kwangu?Kama hutaki
kuniambia basi nitakwambia .”
Akasema Doreen na taratibu
akafumba macho na kuusogeza
mdomo wake karibu na mdomo wa
Elvis,akambusu na ghafla Elvis
kama mbogo majeruhi akamshika Doreen kwa nguvu na kuanza
kunyonyana nadimi.
Doreen tayari alipandisha
mashetani yake ,alikuwa akihema
haraka haraka.Hakutaka
kupoteza muda akaanza kufungua
vifungo vya shati la Elvis.Ghafla
Elvis akakurupuka na
kumsukuma
“ Elvis,why? What happened?
“ No I cant do this.I real cant”
“ Elvis,usinifanyie hivyo
tafadhali.Nafahamu umekuja
kunifuata mimi.Sasa unaogopa
nini? Hakuna atakayefahamu na
wala mkeo Patricia hatajua
lolote.Please Elvis I need you”
akasema Doreen huku
akimsogelea Elvis
“ No Doreen stop.!..akasema
kwa ukali Elvis huku akihema
kwa nguvu. Walisimama kwa sekunde kadhaa
wakitazamana kila mmoja
akihema kwa nguvu.Vifungo vya
nguo aliyokuwa ameivaa Doreen
vilikuwa vimefunguka na hivyo
kuifanya sehemu ya matiti yake
mazuri kuonekana na kumpa
wakati mgumu sana Elvis
“ Hili ni jaribu kali sana.Sijui
ni kitu gani hasa kilichonileta
huku kwa Doreen.” Akawaza Elvis
huku akiendelea kumtumbulia
macho Doreen
“ Elvis tafadhali naomba
usiogope kitu.Nafahamu
unanitaka lakini
unaogopa.Hakuna atakayefahamu
chochote kuhusiana na jambo
hili.I need you and I’ll give you
everything that you want hata vile
ambavyo umeshindwa kuvipata
kwa mkeo kwangu nitakupa” akasema Doreen .Kauli ile
ikamstua kidogo Elvis akauliza
“ Doreen,kuna jambo lolote
ambalo Patricia amekueleza kwa
siku hizi za karibuni?
“ Jambo gani hilo?
“ Hajakueleza jambo lolote
kuhusiana na mambo ya ndani ya
ndoa yetu?
“ Kuna jambo Fulani
alinieleza”
” Jambo gani? “
“ Ni kuhusiana na yeye
kutopata mtoto”
Elvis akashusha pumzi
akamuangalia Doreen na
kumuuliza
“ Alikueleza sababu za yeye
kutokupata mtoto?
“ Ndiyo alinieleza kila kitu”
Elvis Akakaa kimya kidogo kisha
akasema siku chache zilizopita
,ndugu zangu wakiongozwa na
mama walianza kuhoji kuhusiana
na kwa nini toka tumeoana hadi
leo hii hatujafanikiwa kupata
mtoto.Hakuna anayefahamu ni
kwa nini sisi hatuna mtoto hadi
leo hii.” akanyamaza kidogo
akatazama chini halafu akainua
kichwa na kuendelea
“ Kitendo cha ndugu zangu
kuanza kuulizia kuhusiana na
masuala ya mtoto kimemkosesha
amani mke wangu .Juzi
aliniambia kitu ambacho
kilinishangaza sana.Aliniambia
kwamba yuko tayari mimi nizae na
mwanamke mwingine nje ya
ndoa.Nilimkatalia kuhusiana na
jambo hilo lakini hakuonekana
kuridhika.Tukio lililtokea jana
linanifanya nianze kuhisi kwamba yawezekana mlikuwa mmepanga
litokee.Hiyo ndiyo sababu
nimekuja hapa kwako ili niweze
kuupata ukweli wa tukio lile.Ni
kweli mlikuwa mmepanga na
Patricia kwamba nilale nawe?
Naomba usinifiche Doreen”
akasema Elvis.Doreen alionyesha
wasi wasi mwingi.Alishindwa ajibu
nini.Kwa mbali macho yake
yakaonekana kulengwa na
machozi
“ Elvis naomba nikwambie
ukweli.” Akasema Doreen halafu
akainama akafikiri kwa muda na
kusema
“ Elvis tafadhali naomba
usikasirike lakini ukweli
nikwamba lile lilikuwa ni tukio la
kupangwa..Tulilipanga mimi na
Patricia.” Ouh Mungu wangu
!!akasema Elvis na kusimama
akashika kichwa chake.Doreen
akaendelea
“ Patricia alinifuata akanieleza
matatizo yake na namna
anavyoteseka kwa kukosa
mtoto.Aliniambia kwamba anataka
uwe na furaha maishani mwako
na furaha hiyo ingekamilika
endapo tu ungekuwa na
mtoto.Patricia anaogopa kwamba
siku moja shinikizo toka kwa
ndugu zako litazidi na utaamua
kuzaa na mwanamke ambaye yeye
hamfahamu na hivyo kuhatarisha
ndoa yenu na kwa sababu
anakupenda ndiyo maana akaona
ni vyema kama atakupa nafasi ya
kuweza kuzaa na mwanamke
ambaye yeye anamuamini
.Ulipokataa kufanya hivyo alikuja kwangu na kuniomba nimsaidie
katika tatizo lake hili,.Aliniomba
nizae nawe .Nilimuuliza kama uko
tayari kwa jambo hilo akasema
kwamba alikueleza lakini
haukuwa tayari.Kwa upande
wangu sikuwa tayari kufanya
jambo kama hili hasa kutokana na
namna tunavyoheshimiana lakini
Patricia alinililia sana nikamuonea
huruma na kukubali kumsaidia
ndipo tulipopanga ule mpango na
yakatokea yale yaliyotokea.Elvis
naomba unisamehe sana,nilifanya
vile kwa ajili ya kumsaidia rafiki
yangu “ akasema Doreen.Elvis
akamtazama kwa macho makali
na kusema
“ Siamini kama ni kweli
mmefikia hatua hii.How could you
do this?Mnafahamu madhara
yake? Nilikwisha mwambia Patricia kwamba asiumize kichwa
chake na jambo hili lakini hataki
kunielewa,.What else should I do
to prove to her that I love her with
all my heart? Akasema Elvis kwa
ukali.Jambo lile lilionekana
kumchukiza mno.
“ Elvis tulikuwa tunajaribu
kutafuta suluhu ya tatizo hili.Cant
you see how Patricia is suffering
right now? Akasema Doreen naye
sauti yake ilionekana kuanza
kuwa kali
“ so this is the solution? You
are making things worse than
solving the problem.” Akasema
Elvis
“ Elvis,Patricia loves you so
much na ndiyo maana yuko tayari
kufanya jambo kama hili kwa ajili
ya kukupatia wwewe furaha.Do you think this is easy for her?
Akauliza Doreen
“ Nafahamu mke wangu
ananipenda sana na lengo lake ni
kuniona nikiwa na furaha lakini
njia hii anayotaka kuitumia si
sahihi hata kidogo.Mimi
ninampenda kwa jinsi alivyo na
wala suala la kukosa mtoto
halipunguzi hata chembe moja ya
upendo wangu kwake.Siku zote
nimekuwa nikimuasa kwamba
maneno mengi yatasemwa lakini
anatakiwa awe mvumilivu .Kukosa
mtoto si mwisho wa maisha”
akasema Elvis.Doreen
akamtazama kwa makini na
kusema
“ Hongera kwa msimamo huo
lakini nina hakika moyoni mwako
utakuwa ukiumia sana kwa
kukosa mtoto japokuwa hutaki kuweka wazi.Nina hakika vile vile
kwamba siku moja itafika
utashindwa kuvumilia na
utaamua kuzaa nje ya ndoa
yako.Patricia tayariamekwisha
liona hilo na ndiyo maana
amekubali kwamba uwe na mtoto
wan je ya ndoa lakini toka kwa
mwanamke anayemfahamu na
kumuamini na katika hilo
amenichagua mimi.” akasema
Doreen.Elvis akainama akafikiri
na kusema
“ Iwas there when it
happened.Nilikuwepo na
kushuhudia wakati Patricia
anapoteza uwezo wa
kuzaa.Nilisimama pamoja naye
.Nilimpenda hata kabla ya
matatizo yale kumkutana
nitaendelea kumpenda siku zote
za uhai wangu.Nilimuoa Patricia kwa sababu ninampenda kwa
moyo wangu wote na siumizwi kwa
hali yake ya kukosa mtoto kwa
sababu nililifahamu jambo hili
toka awali na nikawa tayari
kukabiliana nalo.Kuhusu kuzaa
mtoto na mwanamke mwingine
hilo ni jambo ambalo sintaweza
kulifanya.Sijali kama ni yeye
anayetaka ama nani lakini siwezi
kufanya hivyo.”akasema Elvis
“ Kwa nini unafanya hivyo
Elvis? Kwa nini hutaki kumsikiliza
mkeo? Kwa nini hutaki kumuona
Patricia akiwa na furaha? I beg
you, do what she wants you to do
and you can make her happy”
akasema Doreen
“ Ninampenda sana mke
wangu na ndiyo maana sitaki
kufanya hivyo anavyotaka nifanye
kwa sababu ninafahamu lazima ataumia sana moyoni.Halafu ni
kwa nini unanisisitiza sana
kuhusu kufanya jambo hili?
Akauliza Elvis
“ Its because I’m a woman
and I know how a woman feels
pale anapundua kwamba hana
uwezo wa kuzaa mtoto” akasema
Doreen
“ Think about it Elvis and if
you want to do what your wife
wants ,I’ll be right here waiting”
akasema Doreen.Elvis akamtzama
usoni akataka kusema jambo
lakini kabla hajatamka chochote
simu yake ikaita,akaitoa mfukoni
akatazama mpigaji.Alikuwani
Patricia mke wake
“ Hallow Patricia”
“ Elvis uko wapi? Mbona
sikuoni hapa nilipokuacha?
Akauliza Patricia Elvis akamtazama Doreen
halafu akasema
“ Nimetoka kidogo kuna mtu
nimekuja kumtazama mara
moja.Tayari umeshamaliza
shughuli nije nikuchukue?
“ Elvis kuna tatizo
limejitokeza na hakuna mtu
mwingine ninayeweza kumueleza
zaidi yako”
“ Tatizo gani Patricia?
“ Ni kuhusiana na huyu
msichana Cindy niliyekuja
kumtazama.Ni kweli amezinduka
na anaweza kuongea kidogo
.Wakati niko naye nikimuhudumia
kuna jambo amenieleza limenistua
kidogo”
“ amekueleza nini” akauliza
Elvis.
“ Ameninong’oneza kwamba
anataka nimsaidie kumuondoa pale hospitali kwani maisha yake
yako hatarini”
“Maisha yake yako hatarini?
Kivipi?
“ Anadai kwamba kuna watu
wanaotaka kumuua.Anasema
kwamba endapo atagundulika
yuko pale hospitalini basi lazima
atauawa..”
“ Amekueleza nini sababu ya
maisha yake kuwa hatarini na ni
akina nani wanaotaka kumuua?
“ Hapana hajanieleza
chochote.How are we going to help
her?
Elvis akafikiri kidogo na kusema
“Nakuja hapo sasa hivi “
akasema na kukata simu
“ Kuna tatizo limetokea?
Akauliza Doreen
“ Kuna mtu ana tatizo ngoja
nikamuangalie” akasema Elvis Before you go” akasema
Doreen.Elvis akageuka na
kumtazama
“ Nahitaji unijibu kwa nini
umemdanganya mkeo alipokuuliza
uko wapi? Kwa hukumweleza
ukweli kwamba uko na mimi?
“ Sitaki ajue kama nimekuja
kwako na ninaomba Doreen suala
hili Patricia asilifahamu”
“ Usijali Elvis,hakuna
atakayejua .Hata kama tutafanya
Patricia hatajua chochote”
akasema Doreen na kumstua
kidogo Elvis
“ Umesema nini Doreen?
“ Nimesema kwamba muda
wowote ukinihitaji niko hapa
nakusubiri” akasema Doreen
“ stop this Doreen.I have to
go.We’ll talk later” akasema Elvis
na kuondoka Namlaumu sana Patricia
kwa kitu anachotaka
kukifanya.Hakupaswa kufanya
vile kwa sababu ninampenda na
sikuzote atakuwa ni mwanamke
peke e ninayempenda kuliko wote
hapa duniani na siko tayari kuzaa
mtoto na mwanamke
mwingine.Najua alifikia maamuzi
haya kutokana na maneno
yanayoanza kusemwa na
ndugu.Nitasimama imara siku
zote kumtetea na sintakubali mtu
yeyote yule amseme vibaya mke
wangu” akawaza Elvis akiwa
njiani kuelekea hospitalina mara
sura ya Doreen ikamjia
akatabasamu
“ Sielewi ni kwa nini Doreen
alikubali kirahisi namna hii ombi
la Patrica la kutaka kuzaa na
mimi. Si jambo rahisi kwa mwanamke kukubali kuzaa mtoto
na mume wa mtu lakini kwa
Doreen ameonekana kutokuwa na
tatizo lolote kuhusiana na suala
hili .Napata mashaka kama kweli
ana nia ya dhati ya kumsaidia
rafikiyake au ana sababu zake
kwani hata maongeziyake
ukiyasikia unagundua kabisa
kuna kitu anakitafuta.Hata hivyo
dah ! Doreen is so hot.Anasisimua
sana.Kwa mara ya pili leo kama
nisingekuwa jasiri basi ningefanya
naye mapenzi leo kwani tayari
mashetaniyangu yalikwisha
amka.Ananiweka katikamajaribu
makubwa ” Akawaza Elvis halafu
akakumbuka jambo aliloambiwa
na Patricia
“ Huyo msichana ana
matatizo gani? Nani anayetishia
maisha yake? Ngoja nikamsikilizenione kama nitaweza kumsaidia
lakini ninahisi ni suala ambao
linatakiwa kuripotiwa polisi.”
Akawaza Elvis
Alifika hospitali akamtaarifu
mkewe ambaye alfika mara moja
akamchukua na kumpeleka hadi
sehemu Fulani
“ Hii ni sehemu pekee
ambayo hakuna kamera za ulinzi
zilizoelekezwa tofauti na kila kona
ya majengo ya hospitali
hii”akasema Patricia
“ Elvis kuna jambo yule
msichana amenieleza limenistua
kidogo”
“ Jambo gani hilo?
amekwambia nini?
“ Msichana yule ana matatizo
na anahitaji msaada.Amenieleza
kwamba maisha yake yako hatarini na kwamba kuna watu
wanaomtafuta ili kumuua”
“ Ni watu gani hao wanaotaka
kumuua na kwa nini?
“ Hajanieleza kwa undani
kuhusu suala hilo ila ameniomba
nimtoe hapa hospitali kwani
anaogopa wanaomtafuta
wakigundua kwamba yuko hapa
basi watafika na kumuua”
“ Patricia ninapata wasiwasi
kidogo kama huyo msichana tayari
amekwisha rejewa na fahamu
zake kamili.” Akasema Elvis
“ Hakuna tatizo katika
fahamu zake.Anakumbuka kila
kitu na nimemfanyia vipimo yuko
safi.Kumbukumbu zake zote ziko
sawa”
“ Anakumbuka ni kitu gani
kilimsababisha apoteze fahamu
kwa muda wa miezi miwili? Nimejaribu kumuuliza lakini
anaonekana kukumbuka jambo
Fulani halafu huogopa na kuanza
kulia.Anaonekana kuna kitu
ambacho hataki kukiweka wazi”
Elvis akafikiri na kusema
“ Naweza kuruhusiwa
kumuhoji kidogo ili nione ni
namna gani tunavyoweza
kumsaidia?
“ Kwa sasa itakuwa vigumu
kumuhoji kutokana na mazingira
ya hospitali kwanihutaruhusiwa
kuingia mahala aliko kama si
daktari au muhusika wa hospitali
hii.”
“ So what are we going to do?
Akauliza Elvis
“ I don’t know Elvis”
Elvis akainama akafikiri kwa
muda kisha akasema “ Are you sure you want to
help her?akauliza
“ Elvis msichana yule
anaonekana wazi ana tatizo kubwa
na inaonekana kuna kitu kikubwa
anakifahamu na ndiyo maana
amenililia na kuniomba nimsaidie
.Nadhani kuna ulazima wa
kumsaidia”
“ Vizuri kama uko tayari
kumsaidia basi njia pekee ni
kumuondoa hapa hospitali.Hilo
linawezekana ?
“ Anaweza kuruhusiwa lakini
kuna taratibu za kufuata”
“ Hapana hatuwezi kusubiri
hizo taratibu zikamilike
.Yawezekanani kweli anaweza
kuwa katika hatari kubwa.We
have to save her”
“What are we going to do?
Akauliza Patricia Kama kweli tunataka
kumsaidia tunatakiwa tumuondoe
hapa hospitali kimya kimya bila ya
mtu kufahamu “
“ Hilo ni jambo gumu sana
Elvis.Kamera za ulinzi zimefungwa
kila kona ya hospitali hii kwa hiyo
hatuwezi kumtorosha bila ya
kuonekana.I’mso confused”
“ Anaweza kutembea japo
kidogo?
“ nadhani anaweza kutembea
japo bado dhaifu sana”
“ Ok good.Kitu cha kufanya
hapa mvue mavazi yale ya
wagonjwa na umvishe mavazi ya
kawaida.Baada ya hapo mtoe nje
kwa kisingizio kwamba
anakwenda kupunga upepo
.Utampeleka hadi chini ya ule mti
uliopo eneo la megesho.Mimi
nitalitoa gari nje ya geti halafu nitamtuma kijana wa piki piki
ambaye atamfuata na kumtoa nje
kisha nitampakia garini na
kuondoka naye.Hakuna mtu
yeyote ambaye atahisi kwamba
umemtorosha mgonjwa bali
itaonekana ametoroka
mwenyewe”akasema Elvis .Patrcia
akafikiri kidogo kisha akasema
“ Ok ! Ngoja tufanye hivyo ili
kumsaidia yule
msichana.Anaonekana ni kweli
ana tatizo kubwa”
**********************
“ Cindy yuko wapi? Akauliza
Patricia baada ya kuwasili
nyumbani akiwa katika gari ya
kukodi.Gari lao aliondoka nalo
Elvis katika harakati za
kumtorosha Cindy Yuko chumba cha wageni
anapumzika.Vipi hospitali hakuna
tatizo lolote? Akauliza Elvis
“ Hakuna tatizo
lolote.Nimeripoti kwa uongozi
kwamba mgonjwa amepotea.Na
jambo zuri nimeripoti kwamba
mgonjwa aliyepotea ana matatizo
ya akili.Hakuna mtu anayetilia
maanani kupotea kwako hasa
baada ya kusikia kwamba ana
matatizo ya akili” akasema Patricia
na kuvuta pumzi ndefu
‘ Umefanya jambo zuri sana
la kijasiri Patricia.”
“ Ahsante sana Elvis.Ni kweli
tumefanya jambo la kijasiri
japokuwa halikuwa rahisi.Ahsante
kwa kunipa ujasiri wa kulifanya
jambo lile nilikuwa naogopa
sana.Kwa sasa Cindy yuko huru na ni jukumu letu kufahamu
kilichomsibu na kumsaidia”
“ Nadhani ni wakati muafaka
wa kumuhoji na kujua kila kitu
kumuhusu yeye.Tufahamu
ametokea wapi na akina nani
wanaotaka kumuua..” akasema
Elvis kisha wakainuka na
kuelekea katika chumba cha
wageni alimokuwamo Cindy
ambaye alikuwa amekaa kitandani
“ Unajisikiaje hivi sasa?
Akauliza Patricia
“ Ninajisikia afadhali
sana.Kidogo ninajisikia kupata
nguvu.Ahsante sana dokta kwa
msaada wako” akasema Cindy
“ Vizuri sana.Utapona tu
usiwe na wasi wasi” akasema
Patricia .Cindy akamshika mkono
na kusema Dokta ninarudia tena
kukushukuru kwa msaada wako
.Umeyaokoa maisha yangu.Watu
wale wangejua niko pale hospitali
wangenifuata na kuniua” akasema
Cindy .Patricia akageuka na
kumtazama Elvis halafu
akamshika Cindy begani
“ Cindy huyu hapa ni mume
wangu anaitwa Elvis.Kwa pamoja
tumeguswa sana na tatizo lako na
tuko tayari kukusaidia lakini ili
tukupe msaada unaostahili
tunataka tulifahamu tatizo
lako.Tunataka tufahanu nini
kilikutokea na kusababisha
upoteze fahamu kwa muda wa
miezi miwili? Tunataka kufahamu
ni akina nani wanaotaka kukuua
na kwa nini? Tafadhali kuwa
muwazi kwetu na usiogope kitu
hapa uko katika mikono salama.” Akasema Patricia.Cindy akafumba
macho kana kwamba kuna kitu
anakumbuka.Michirizi ya machozi
ikaonekana mashavuni
“ Usilie Cindy.Kuwa
jasiri.Tueleze kitu gani kilikusibu?
Akasema Patricia.Cindy akakohoa
kidogo na kusema
“Jina langu naitwa
Elizabeth.Nilitokea Iringa na kuja
kufanyakazi za ndani jijini Dar e s
salaam.Nilifanya kazi kwa mama
mmoja anaitwa mama Shamim na
alipoondoka kwenda arabuni
akanikabidhi kwa mtu mmoja
anaitwa Pascal Situmwa ambaye
mke wake alikuwa amefariki na
kumuachia watoto wawili
wadogo.Pascal alikuwa akitafuta
mtu wa kuwalea watoto wake.”
“ Hebu ngoja kwanza
Elizabeth.” akasema Elvis huku sura yake ikionyesha mshangao
Fulani
“ Unasema ulikabidhiwa kwa
Pascal Situmwa?
“ Ndiyo .Nilikabidhiwa kwa
Pascal Situmwa.Nilikuwa nafanya
kazi kwake.” Akasema Elizabeth
kwa sauti dhaifu.Elvis akafikiri
kidogo kisha akasema
“ Endelea”
“ Vipi mbona umestuka Elvis
? Do you know him? Akauliza
Patricia
“ hapana simfahamu” akajibu
Elvis.Elizabeth akaendelea
“ Nilianza kufanya kazi kwa
Pascal Situmwa na aliniamini
sana.Niliwalea watoto wake vizuri
bila matatizo.Siku moja Pascal
alikuja na rafiki zake wakanywa
sana pombe sebuleni hadi usiku
mwingi.Asubuhi nilipoamka niliokota pochi ndogo sebuleni
nikaifungua na kuangalia
kilichokuwamo ndani
yake.Kulikuwa na kadi tatu mfano
wa kadi za benki,fedha taslimu
shilingi laki tatu pamoja na dola
mia mbili za marekani.Vile vile
kulikuwa na kitu Fulani kama
memory kadi ya simu halafu
kukawa na flash disc yenye GB
8.Sikuwa na shida na vifaa vile
shida yangu mimi ilikuwa ni zile
fedha tu.Sikutaka kuziweka fedha
zile chumbani kwangu
nikaichukua ile pochi na kwenda
kuifukia chini ya mti nyuma ya
nyumba.Pascal alipoamka asubuhi
alianza kuitafuta ile pochi
akaniuliza lakini nilikana
kuiona.Aliendelea kutafuta pochi
ile kila mahali lakini
hakuipata.Baada ya kuitafuta sana na kuikosa akaniita na
kunionya kwamba niirudishe
pochi ile kwani hakuna mtu
mwingine anayeweza kuichukua
pochi ile zaidi yangu.Alinipa muda
wa dakika thelathini niwe
nimeirudisha pochi
yake.Niliendelea kukataa kwamba
sifahamu mahala iliko hiyo pochi
yake.Baada ya nusu saa akaja
tena na kuniomba nimrudishie
vitu vilivyokuwamo ndani ya ile
pochi ila fedha
nizichukue.Niliendelea kukataa
akanishika na kunipeleka
chumbani kwangu akaanza
kupekua kila mahala lakini
hakuiona pochi wala
hela,akanivua nguo zote na
kunisachi kila mahala hadi
sehemu za siri lakini hakuona
kitu.Hakunisemesha kitu tena.Ilipofika saa tisa alasiri
wakaja watu wanne ambao
sikuwahi kuwaona wakanichukua
na kunipeleka sehemu Fulani
katika shamba moja wakanitesa
sana wakanipiga sana ili
niwaeleze mahala ilipo pochi hiyo
.Walinipiga mno hadi nikapoteza
fahamu na sikujua tena kitu
chochote kilichoendelea hadi
nilipozinduka na kujikuta pale
hospitali.Wale watu walidhamiria
kuna kabisa kwani kabla
sijapoteza fahamu niliwasikia
wakijadiliana mahala
watakapokwenda kunitupa baada
ya kuniua” akasema Elizabeth
.Elvis na Patricia wakatazamana.
“ Pole sana Elizabeth.Kuanzia
sasa usiwe na wasi wasi wowote
kuhusu maisha yako.Hapa uko
sehemu salama na hakuna mtu atakayejua kama uko hapa.Kwa
sasa pumzika tutaongea zaidi
baadae” akasema Elvis halafu
akatoka na kulekea chumbani
akamuacha Patricia akimpa dawa
Elizabeth.Kichwa chake kiliwaza
jina moja tu Pascal Situmwa
“ Pascal Situmwa !..akasema
Elvis kwa sauti ndogo
“ Pascal Situmwa kwa nini
atake kuua Elizabeth kwa sababu
tu ya pochi? Katika pochi hiyo
kulikuwa na nini? Nashawishika
kuamini kwamba katika pochi
hiyo kuna jambo kubwa
.Ninamfahamu Pascal
Situmwa,mpaka afikiri hatua ya
kutaka kumuua huyu msichana
lazima iko sababu
kubwa.Inawezekana kuna jambo
analificha ambalo anahisi pengine
huyu msichana amelifahamu” akawaza Elvis na mara Patricia
akaingia
“ Elvis mbona ulistuka
uliposikia Elizabeth akilitaja jina
la aliyekuwa mwajiri wake? Do you
know him? Akauliza .Elvis
akamshika mkono mkewe na
kumketisha kitandani
“ Ninamfahamu Pascal
Situmwa.Ni mfanyakazi wa idara
ya usalama wa taifa.Ana nafasi
kubwa katika idara ile”
“ Kwa nini basi atake kumuua
Eliza? Hivyo vitu vilivyokuwa
ndani ya hiyo pochi yake vina
thamani gani?
“ I dont know my love but I
need to find out “ akasema Elvis
na kumstua mke wake
“ Find out ? How? akauliza
Patricia
 
Back
Top Bottom