Riwaya: Jina langu ni Pheady

Riwaya: Jina langu ni Pheady

Natumaini unapata picha nzuri ukioanisha mitaa na matukio.
Ni kweli kabisa mfano Umetaja Kilimahewa ni Jirani kabisa na Ghana mitaa yangu pia.. nimeishi Igoma, Igogo, Ghana, kirumba, Bwiru na kuweka makazi ya kudumu Kitangiri.. hivyo naenjoy tu.
 
Ni kweli kabisa mfano Umetaja Kilimahewa ni Jirani kabisa na Ghana mitaa yangu pia.. nimeishi Igoma, Igogo, Ghana, kirumba, Bwiru na kuweka makazi ya kudumu Kitangiri.. hivyo naenjoy tu.
Safi kabisa hii riwaya inachezewa Mwanza hivyo wasomaji wa Mwanza watakuwa wanaona picha ya mji wao katika maandishi.
 
TUENDELEE


iliyokuwa na dhahabu huku ikiwa imefungwa madhubuti kwa namba na finguo.
Aliipokea na kuiweka pembeni yake kwenye kochi nami sikuwa na wasiwasi kwani nilimuamini sana aliwahi kutunza siraha zangu pasipokuchunguza ni nini nilichompa kutunza.
“Inaonekana biashara inachangaya sana kwa sasa maana mwenzetu hutulii sehemu moja, tuwe tunaambizana mdogo wangu ili na sisi tufate nyuki tule asali”. Alisema kwa kutania.
“Unajua dada mimi bado naangaika na maisha kwa hali zote, lakini nina hakika kuna wakati mambo yatakaa sawa nami nitakaa na kustarehe bila miangaiko mingi ya safari zisizoisha.” Baada ya muda tuliagana na nikamtaadhalisha autunze vizuri mzig wangu maana una vitu muhimu naye akaahidi kufanya hivyo.
Nilipotika hapo nilikanyaga mafuta moja kwa moja mpaka Majukano Restaurant ili nikaonane na akina Sonno na kupata kifungua kinywa maana kwa dada nilikataa kunywa chai. Muda nao ulikuwa unakalibia saa tatu tulizoahidiana na wenzangu, wakati naegesha gari maegesho ya Majukano niliona gari wanalotumia akina Sonno ikiwa imeegeshwa nikajua kuwa wameishafika. Nilishuka kwenye gari nikafunga milango na kuongoza sehemu ya hoteli ambapo sikuweza kuaona sehemu hiyo nikaamua nipate kwanza kifungua kinywa ndio niwatazame sehemu ya bar.
Niliagiza supu ya mbuzi, chapati mbili na maziwa ya mgando na kuvishambulia kwa fujo kiasi kwamba baada ya dakika chache nilikuwa nimemaliza suala la tumbo. Nililipa gharama za nilivyotumia na kuingia sehemu ya bar kuwatazama jamaa zangu
Nilipoingia bar niliangaza macho sikuweza kuwaona na bar kulikuwa na watu wachache miongoni mwao walikuwepo wazungu watatu. Nilienda sehemu ya vyumba vya kunywea maalimu kwa watu wasiopenda bugudha na vyumba hivyo hulipiwa, ni baada ya kupita vyumba kama vitatu hivi ndio niliwaona wakiwa wametuliza chupa za konyagi na pembeni yake kukiwa na sahani za nyama choma, waligeuka kuniangalia wakati naingia huku wakitabasamu.
“Salama waungwana” niliwasabahi baada ya kukaa kwenye kiti pembeni yao.
“Sisi salama, hofu kwako” alisema Sonno aliyeonekana ni mwenye furaha sana asubuhi hii.
“Naona watu mnavunja vyupa asubuhi asubuhi” nilisema.
“Kama muda unaruhusu ni lazima ufanye vitu kama hivi ambavyo ni muhimu kwa watu kama sisi vinginevyo unaweza kuchanganyikiwa. Ninaposema muda nina maana ya pesa maana waingereza walisema time is money ama vipi?” alisema Kikakika katika hali ya utani huku naye akionyesha ni mwenye furaha isiyo kifani.
“Basi kama ni hivyo ngoja nami niwemo.” Nilisema huku nikisogeza bilauri aliyokuwa akitumia Kikakika ili nijaze pombe.
“Subiri Mr Pheady, ngoja nikuagizie bilauri yako” alisema Sonno huku akisogeza kiti nyuma.
“Unajua wengine tumezoea ulevi wa gongo kuchangia bilauri” nilisema wakati Sonno akiwa amesimama na wote tkacheka.
“Sawa komredi lakini itabidi sasa uache hayo mazoea” aliongea Sonno huku akielekea mlango wa kutoka nje. Baada ya muda alirudi na bilauri tukaendelea na unywaji na hadithi za hapa na pale.
“Vipi rafiki zangu nyie mna mipango gani? Baada ya kuwa mmemaliza hii shughuli maana sas hivi sisi ni mamilionea” niliongea wakati tkiendelea kukata pombe.
“Mimi nafikiria kuanzisha kampuni ya kukodisha magari nchini Kenya” alisema Kikakika.
“Mimi nina mpango wa kwenda kununua ardhi huko Syria kuishi huko huko nikifanya biashara ya utalii kwani kuna marafiki zangu wengi tulojifunza nao hizi kazi na wameishatajirika.” Hiyo ni mipango iliyotolewa na Sonno.
“Kwa upande wangu nataka kwenda kununua mashamba huko Morogoro, nitachukua kama ekari mia tatu hivi na kuanzisha kilimo cha umwagiliaji na ufugaji wa kisasa, nataka kuwa kabaila wa nguvu.” Niliongea mimi Pheady.
“Du!! Jamaa yangu wewe una wazo matata sana, sijawahi fikiria jambo kama hilo.” Alisema Kikakika.
“Hata mimi amenishangaza” alisema Sonno.
Wazo langu lilionekana kuwashangaza sana, “vipi utaweza kuendana na siasa za Tanzania kwa wazo hilo na vilevile kumbuka huwenda kukatokea wafukua makaburi kutokana na historia yako ya nyuma hivyo kukuweka matatani.” Alisema Sonno.
“Nitatafuta namna ya kubadili kila kitu kinachonihusu na hiyo historia itafutika kwani pesa inaweza kila kitu isitoshe nitakuwa mtu wa shambani mda mwingi.” Nilisema.
“Lakini uwe mwangalifu katika utekelezaji wa wazo lako, kwani ni wazo bora kabisa ila tawala za Tanzania hazieleweki na sera zake hasa kuhusu ardhi anaweza kuja Rais mwingine na kubadiri mambo ambayo yataturudisha enzi za mwalimu na hapo ndugu yangu utakuwa muathirika.” Alisema Kikakika.
“Iwapo itatokea nikahisi mabadiliko ya aina hiyo wakati nikmeishawekeza basi name itabidi niwe mwanasiasa ili kulinda hatima yangu.” Nilisema.
“Tokea lini mshika bunduki akawa mwanasiasa au unamaanisha siasa yako itakuwa ya mlengo wa mtutu.” Alisema Sonno na wote tukacheka.
Tulisha teketeza karibu chupa nne za konyagi wakati naangalia saa yangu ilionyesha saa tano kasoro dakika ishirini. Ni wakati huo nilpowaomba wenzagu niwaache kidogo ili niiende benki kuweka pesa. Kikakika naye alipendelea tuongozane naye akaweke fedha benki na kuna vitu alitaka kununua madukani.
“Sawa nyie nendeni tuonane saa kumi kule Magnum klabu, hata mimi nitatoka hapa sas hivi kuanza mipango yangu ya maisha.” Aliongea Sonno na kuagana mimi na Kikakika tukaongozana na kupanda gari nililokuwa nalo tayari kwa safari yetu. Niliondoa gari mpaka benki ya biashara ya barabara ya Nyerere, tulipofika tulishika na kuingia ndani kuendelea na shughuri zetu.Kikakika alikuwa wa kwanza kumaliza kabla yangu na kuniambia kuwa anaondoka kwenda madukani kwa mguu. Tulikumbushana kuonana kule Magnum klabu saa kumi kama tulivyopanga naye akaondoka. Nikaendelea na mambo yangu hapa benki na kutokana na wingi wa watu ilinichukua muda mrefu kiasi na ilipotimia saa saba kasoro dakika nane nilikuwa tayari nimeishamaliza na kuondoka nikiwa na wazo la kurudisha gari kwa muhuhusika, sikuona sababu ya kuendelea kuwa nalo.
Kwa kuwa ofisi zetu kwa hapa mwanza zipo Kirumba nilonelelea niipeleke ofisini na wao watamkabidhi bosi wao. Nilitia gari moto na kushika barabara ya Nyererere nilielekea mzunguko wa CCM jirani na forodha ya Mwanza, nilipofika benki kuu nilihisi kuna gari lilikuwa limepaki pale benki linanifuata kwa tofauti ya magari mawili kati yetu. Nilibadili mawazo badala ya kuongoza Kirumba nilizunguka mzunguko na kushika njia inayopitia kikosi ha zima moto ikielekea mitaa ya Rufiji. Baada ya kufanya hivyo ile gari nayo ilichukua uelekeo wangu hapo nikajua kua nilikuwa hisia zangu zilikuwa sahihi, nikaamua niwapoteze kwa kuwa nilijua lengo lao ni kunufuata na wapate nafasi nzuri hivyo isingekuwa rahisi kunufukuza kwa kasi kiasi cha kuwashitua wanainchi mchana huu. Nilipachika gia na kuongeza kasi ambayo hata iliwashitua wananchi walioniona, niliongoza mpaka sehemu inayoitwa mlango mmoja alafu nikashika tena barabara ya Nyerere kama natokea Mabatini. Waliokuwa wananifuita walishangaa na kushindwa kuelewa, nilipofika barabara iendayo Bugando Hospitali nilikata kona kuifuata nilikata kona kuona kama bado nafuatiliwa lakini sikukuona kitu. Niliendelea mpaka sehemu ya makaburini na kupaki gari pembeni alafu nikashuka haraka na kwenda kukaa mbali kiasi kuwa mtu awezi fikiria kwamba mimi ndie muhusika wa ile gari.
Nilikaa kwenye kiduka kimoja hapo nikinywa soda kwa muda wa kama dakika kumi lakini sikuona lolote lile la maana nikaiendea gari nhuku nukiwa nikekata shairi kuirudisha moja kawa moja kwa Yule mzee bosi wa ofisi ya mwanza. Nilipofika kwa Yule mzee sikumkuta bali nilimkuta mkewa na kumwachia nikamwachia maagizo na funguo, nilitoka na kutembea kwa miguu kuelekea kituo cha daladala hapa Mwanza huitwa express, bahati nzuri kituoni sikukaa sana nikapata gari moja kwa moja mpaka kitua cha mabasi ya Mwanza mjini. Nilishuka na kukatisha kituo cha polisi hapa stendi nikaelekea stendi ya taxi. Nilikodi taxi na kupelekwa moja kwa moja Kirumba na hapo nilishuka mtaa wa pili kwa kuhofia kuwa dereva asije akajua mpaka ninapokwanda
Baada ya kushuka nilielekea kwa kaka yangu mmoja ambaye ambaye amejenga mtaa wa pili toka niliposhukia, saa yangu ilionyesha ni saa nane na dakika arobaini na mbili. Nilipofika kwa kaka sikumkuta nilimkuta shemeji yangu na wanae wawili wakiangalia rininga, nilisabahiana nao na kukaa, shemeji alimtuma aniletee soda alafu yeye akaamka na kutokomea huko ndani. Haukupita muda nikawa nimeletewa soda na huyo mototo wa kaka ambaye alikuwa na umri wa miaka sita hivi, kabla sijamaliza kunywa soda alitokea shemeji na snia la chakula akanikaribisha nami nikaanza kula huku nikongea na shemeji yangu.
“Shemeji kaka yuko wapi?” niliuliza.
Shemeji aliniambia kuwa alikuwa ametoka kwenda kununua mbao za kukarabati ngarawa yake. Tuliendelea na maongezi ya kawaida huku tukiangalia vipindi vya ITV, ilipotimu saa tisa na nusu niliaga na kuondoka huku nikimwambia shemeji amwambie kaka nitakuja kumuona kesho. Baada ya kutoka hapo nilichukua taxi na kumwambia dereva anipeleke Magnum Klabu, aliponifikisha nilimlipa haki yake nami nikaingia ndani, hapo ndani niliangaza kila sehemu sikuona dalili za kuwepo akina Sonno hivyo nikatafuta kiti kilicho sehemu nzuri ya kukaa mtu kama mimi na kukaa. Nikaagiza kinywaji na kuendelea kunywa taratibu kwani nilikuwa na imani kuwa nimewahi hivyo wakina Sonno wangefika baadae.
Ilipofika saa kumi na dakika saba nilimuona Sonno anaingia huku akiangaza angaza aliponiona alinifuata na kujuliana hali alafu nikamuita muhudumu na kumuambia atuletee konyagi na krest soda mbili. Vinywaji vililetwa tukaendelea kunywa huku tukimsuburi Kikakika, wakati tunaendelea kunywa Sonno alisema amesahau kitu garini hivyo akatoka na aliporudi alikuwa ameshikiria gazeti la Majira la leo. Kwenye ukurasa wa mbele kulikuwa na maandishi yaliyokolezwa wino mweusi nayo yameandikwa “ SITA WAUAWA KWA KIPIGWA RISASI MWANZA” nilisoma habari hiyo ambayo iliandikwa kama ifuatavyo;
“Watu sita wamekutwa wameuawa katika jengo la Pamba Hostel Mwanza, vifo vyao vyao vimetokana na kupigwa risasi. Miongoni akiwemo Inspekta wa polisi na mkirugenzi wa kampuni ya New General African Trades Mr Catto. Wengine hawajatambuliwa kwa majina na polisi wanaendelea na msako mkali wa kuwapata wauaji, na chanzo cha mauaji hayo bado hakijaeleweka.” Huo ndio ulikuwa mwisho wa habari yenyewe.
“Naona hawa watu wamelichukulia hili suala kwa unyeti zaidi ndio maana halikuandikwa kwa kirefu zaidi hapa.” Nilimwambia Sonno baada ya kuwa nimemaliza kusoma hiyo sehemu ya gazeti.
“Hata mimi naona kuna upererezi wa hali ya juu unafanyika ndio maana habari zake imeaandikwa kwa kifupi sana ili zisivume sana na kuharibu uperezi wao.” Sonno aliunga mkono maneno yangu alafu akaendelea. “Kwa hiyo inabidi tuwe makini sana na nyendo zetu.” Alimaliza kuongea.
Tulikuwa tumeendelea na maongezi ya kawaida mpaka ilipofika saa kumi na moja bila kumuona Kikakika tukaanza kuingiwa na wasiwasi. Tulishauliana ikakubalika mimi niende nikamuone hotelini kwake hivyo nilichukua ufunguo wa gari kwa Sonno na kuondoka kuelekea mjini. Niliongoza moja kwa moja mpaka Mwanza guest iliyopo mitaa ya Uhuru kwani ndipo alikuwa amechukua chumba. Niliegesha gari maegesho ya guest hiyo na kuelekea mapokezi ambapo nilimuuliza muhudumu wa mapokezi kuhusu mgeni angu aliyepanga chumba namba kumi na mbili kama yupo. Muhudumu aliniambia toka atoke asubuhi hajaonekana tena pale guest.
Nilitoka nikiwa mwenye mawazo, nilifikiri huyu mtu atakuwa wapi? Ghafla wazo likanijia nikaondoka moja kwa moja mpaka hotelini kwangu. Nilipofika nikaomba funguo mapokezi na kuelekea chumbani kwangu, nilipoingia chumbani kwangu na kuangalia niligundua kuwa kimepekuliwa kwa ustadi wa hali ya juu ila kila kitu kilikuwa sehemu yake. Mapigo ya moyo yalinienda mbio nikifikiri je? Walionikagua ni polisi au ni Patrick na kundi lake, nilishindwa kupata jibu sahihi palepale niliamua kuchukua vitu vyangu na kufunga chumba alafu nikaondoka.
Niliporudisha funguo kwa muhudumu alionekana kuniangalia kwa jicho la udaku, hii ilionyesha kuna kitu anajua lakini sikujali akili yote ilishavurugika niliwaza kuonana na Sonno tu. Ilipofika saa kumi na mbili kasorobo nilifika Magnum Klabu, watu walishaanza kuwa wengi na disco lilishaanza kupigwa, Sonno alikuwa ameelekea ukumbi wa disco nilijaribu kumtafuta mara nikashtukia nashikwa bega kwa nyuma kugeuka alikuwa Sonno. Hapo tukaongozana kwenda sehemu ya bar na kutafuta viti vilivyo mbali na watu na kukaa.
“Nimejaribu kumfuatilia Kikakika sijapata habari zake pale guest zaidi nimeambiwa na muhudumu kuwa toka alipotoka asubuhi hajarudi pale mpaka mida hii, hivyo inaonekana kuna sehemu yupo au kafichwa kwani nimefika katika chumba nilichofikia na kukuta nimepekuliwa.” Nilimuelza Sonno.
“Loo!! Kwa hiyo ni polisi au ni jamaa wa Patrick? Aliuliza kwa taharuki.
“Kutokana na hali ilivyo sitegemei kama watakuwa polisi, kama wangekuwa polisi walingeweka mtego palepale kwani wangenisubiri pale hotelini wangekuwa na nafasi nzuri ya kunikamata. Na kwa kawaida huo ndio utendaji wa polisi pindi wamuonapo mtuhumiwa huwa hawana wazo la kumfatilia zaidi ya kumkamata, labda wawe Usalama wa Taifa.” Nilitoa mawazo yangu kwa Sonno.
“Basi ni dhahiri atakuwa Patrick na kundi lake, sasa tufanyeje ili tumpate maana kwa Patrick hatupafahamu.” Aliongea Sonno huku akionyesha ameghafirika.
Sikiliza Sonno, inabidi wewe uende pale hotelini nilipokuwa Msufini Resaurant na umuwinde Yule kijana aliye mapokezi ukisha mpata mlazimishe akueleze walioenda kupekua chumba nilichokuwa natumia. Sababu sura yake ilionyesha kujua kitu kinachoendelea, mie nitasubiri hapa kwani hapa watu wanacheza disko mpaka asubuhi. Jitahidi kufanya haraka kusudi tumpate Kikakika kabla ya asubuhi. Ikishindika njia hiyo itabidi mimi niwe chambo maana hawawezi kumuua pasipo kufanikiwa kwa kile walichohitaji kutoka kwa marehemu Mr Catto. Baada ya hapo nilimtaadharisha awe makini na akipata fununu za anapoishi Patrick awahi kuja kunipa habari tuzifanyie kazi.
 
Piga kazi kjn people zinapita kimya kimya!
Raha ya Manju ni kuona hadhira inashangilia hapo Manju anaweza madoido mpaka ukimuambia arudie alichofanya anashidwa. Na raha ya mwandishi ni kuona muitikio wa hadhira ( wasomaji). Kadri comments zinapokuwepo nani na kazana.

Kuosoa, kusahihisha na kuongezea maoni ndio kunakomjenga mwandishi .

Nakaribisha Maoni yoyote yale.
 
TWENDE KAZI


7
Nilipoingia ukumbi wa disk nilitafuta sehemu nzuri ya kukaa, viti vingi vilikuwa wazi watu walikuwa ukumbini wakicheza mziki. Nikakaa kwenye kona moja itakayo niwezesha kuona karibu sehemu nzima ya ikumbi wa disko, niliwasha sigara na kuanza kuvuta wakati naangalia watu wakicheza na baada ya muda akapita muhudumu ambaye nilimuita na kumuagiza aniletee chupa ndogo ya pombe aina ya Long John. Aliniletea nikaendelea kunywa huku nikiwaza na kuwazua, nilikuwa nimekaa karibu saa moja na kitu hivi walipoingia wasichana wawili warembo sana na wamevaa mavazi nadhifu. Walipoingia waliongoza moja kwa moja na kuja kukaa kwenye meza iliyokuwa karibu yangu, muda mfupi baadae muhudumu aliwaletea bia za kopo aina ya Stella, nilishangaa kidogo kuona wasichana wawili tu aniletewa katoni nzima kwa mpigo. Walianza kunywa huku wakiongea taratibu na kitambo kidogo walikuwa wameisha kunywa nusu ya katoni na hapo sauti zao zilianza kupanda kiasi cha kuwasikia maongezi yao. Baada ya muda mfupi kidogo waliniomba niwaangalizie bia zao wakacheze disko, kwa kuwa waliona mimi ndio nilikuwa meza ya jirani yao.
Ulikuwa ni muziki wa rhumba uliopigwa na Oliver Ngoma ndio ulikuwa unapigwa nao waliucheza vizuri sana na kwa maringo hasa punde uliunganisha muziki uitwao Azaraki nao wa Oliver. Vimwana waliendelea kucheza name niliwaangalia kwa chati, baada ya kwisha mziki wa Azaraki walirudi kukaa sehemu yao. Walipo rudi sehemu yao walinishukuru huku wakinikaribisha nijiunge nao nami nilishukuru na kuendelea kukaa nilipokuwa wao waliendelea na maongezi yao huku wakizitimba bia.
Ghafla mawazo yalirudi kwa Sonno na Kikakika, nikajihisi vibaya kwa kutokuwa nao wakati huo, nilipoangalia saa yangu ilikuwa ni saa mbili na dakika ishirini na tano na Sonno alikuwa bado hajarudi. Nilitupa macho kwa wale wasichana nikaona mmoja wao akiangalia saa yake alafu nikamsikia akimaka, “Unajua huyu Patrick mshenzi sana”alimueleza mwenzie. Roho ikanishituka kusikia jina, nikatega masikio kunasa sauti zao zaidi.
“Hata mimi huwa namchukia, sijui kwa nini Moddy anamuona wa maana kiasi cha kuniacha nikastare peke yangu na yeye kuongozana naye. Mwenzie alichangia katika maongezi ya rafiki yake.
“Basi mimi ndio usiseme maana namchukia ile mbaya, sasa fikiria kitendo cha kuja kumchuka Zuberi kwangu mchana wakati akisubiri mlo ni uungwana huo”. Aliongea Yule msichana wa kwanza.
“Mimi nashangaa sana kuhusu huyu Patrick, toka wiki hii ianze amekuwa akimfuatafuata sana Moddy, mara ampigie simu aende kwake, wakati mwingine amuijie na gari. Kwa mfano usiku wa jana kampigia simu jioni akaenda na hakurudi mpaka saa tisa usiku ndio anarudi. Nilipomuuliza akanambia alikuwa kwenye mambo ya biashara” aliongea Yule mwingine.
“Kama ni hivyo inashangaza kwani hata mimi Zuberi aliniaga kuwa anakwenda kwa Patrick na sikumuona tena mpaka asubuhi ya leo, tena anakuja ananiambia hata kuwa na nafasi ya kunutoa out leo kwa sababu ana masula nyeti na Patrick.
Nafikiri ndugu msomaji hata kama ni wewe ungekuwa muhusika wa hili suala langu la wizi na kusikia maongezi haya yanayoendelea baina ya hawa mabinti ungegundua kitu kama wewe sio mpungufu wa akili. Nilianza kufikiri haraka nini nifanye ili hawa wasichana wanieleze anakokaa huyo Patrick bila wao kuwa na mashaka na mimi. Hapo likaja wazo kuwa nimsuburi kwanza Sonno maana ilikuwa mapema mno kuchukua muelekeo mwingine, hivyo nilikaa nikiwachunga kwa macho ili wasije wakaondoka bila kufahamu.
Disko lilikuwa linaendelea na watu walizidi kumiminika katika ukumbi huu wa Magnum, ghafla wale wasichana walikuja kwenye meza yangu na vikopo vine vya Stella walivyokuwa wamebakiza na kuviweka mezani huku wakiniomba niwaangalizie wakati wao wakicheza mziki. Walifanya hivyo kutokana na ongezeko la watu, walijua sio rahisi kuziacha mezani kwao na mimi nimudu kuziangalia kwa mbali.
Walicheza kama miziki mitatu hivi alafu wakaja wameshikana mikono mpaka kwenye meza yangu, hawakurudi kwenye meza yao kwani walivuta viti na kukaa huku wakinisogezea kopo moja la Stella na kuniambia ninywe. Ilionekana wazi kuwa pombe zilishawapanda kichwani, niliwashukuru kasha nikawambia kuwa huwa situmii kwani nimezoea pombe kali, walisikitika kwa kukataa kinywaji chao alafu wakaanza mazungumzo yao. Niliwasikiliza huku nikijifanya sina habari nao huku nikiyakata makali polepole, walikuwa wakiongea maongezi ya kawaida tu na tulidumu katika hali hiyo kama dakika tano hivi ndipo nilipowachokoza kwa maneno.
“Akina dada naona tumekaa meza moja lakini hatufahamiani.” Nilitoa kauli ambayo ilikatisha maongezi yao na kuniangalia alafu mmoja wao akasema;
“Unajua kaka tuliona kana kwamba hupendi bugudha ndio maana tukaendelea na maongezi yetu.” Aliongea mmoja wao.
“Sawa dada nafikiri hiyo ilikuwa tafsiri ya kihisia tu” nilisema na kuendelea “sijui wewe unaitwa nani?”
“Naitwa Mtuli.” Alijibu na kunyamaza.
“Na wewe dada unitwa nani?” Nilimuuliza mwingine.
“ Mie naitwa Monica” alijibu.
“Nyie ni wanyeji hapa? Niliuliza.
“Ndio” walijibu kwa pamoja alafu Monica akaunganisha swali, kwani wewe ni mgeni?
“Ndio” nilijibu kwa kudanganya.
“Unatokea wapi?” aliuliza Mtuli.
“Mbeya” niliendelea kudanganya
“Karibu sana Mwanza” alisema Mtuli.
“Nimeishakaribia ila nitashukuru sana nikipata wenyeji kama ninyi” nilijibu na kutupa kijembe.
Sikujibiwa ila niliunganishiwa swali kutoka kwa Monika.
“Unaitwa nani?”
“Naitwa Lyampili Mabagala” nilijibu.
“Hapa Mwanza umekuja kutembea tu au kibiashara” nilitupiwa swali linguine.
“Nimepita tu naenda Ukerewe kumuona mdogo wangu ambaye anafanya kazi huko.”
“Kumbe unaenda Ukerewe, basi mimi ndio kwetu.” Alisema Mtuli.
“Kwenu ni sehemu gani pale ukerewe?” nilimuuliza.
“Wewe unafahamu sehemu gani huko Ukerewe?” Niliulizwa badala ya kujibiwa.
“Nafahamu Muriti, Nansio na Murutunguru.” Nilijibu.
Ahaa!! Hizo sehemu zote umewahi kufika na ukapakariri vizuri?” MTuli aliendelea kunimiminia maswali.
“Sio sana ila nazifahamu.” Nilijibu kwa mkato.
“Basi mie kwetu ni pale Muriti madukani.” Alisemsa na kuendelea. “Baba yangu ni maarufu kidogo pale Muriti kama ulikaa kidogo huenda ikawa ulimufahamu.
“Anaitwa nani?” nilimuuliza.
“Anaitwa Kazobha ndie mwenye bucha la kuchinja nguruwe pale.” Alijibu.
Kwa hakika nilikuwa namfahamu kwani kule Muriti kuna ndugu zangu hata baba yake alikuwa ananifahamu ila huyu binti sikumfahamu kabisa hata yeye hakuonyesha dalili za kunifahamu. Hapo nikavunga. “Huyo mzee niliwahi kumsikia wakati nilipotembelea pale.
Mara Sonno akaingia na kuangaza kwani alikuwa hajaniona, nikampungia mkono naye akaniona na kunihuata. Alifika na kuvuta kiti kimoja kilichosalia ili kuhitimisha mzunguko wa viti vine. Tulijuliana hali kasha akawasalimia waschana wale alionikuta nao;
“Habari zenu akina dada?” alisalimu.
“Nzuri tu, sijui wewe.” Waliongea kwa pamoja.
“ Mie poa kabisa.” Alijibu Sonno.
“Karibu.” Alisema Mtuli huku akumsogezea kopo la Stella.
Sonno alichukua na kukipachua tayari kwa kunywa, alikunywa kama funda tatu hivi na kurudisha kopo kwenye meza huku akiangaza macho ukumbini, alafu akamuita muhudumu na kumuajizia kopo sita za Stella na chupa moja ya Konyagi. Vinywaji vilipoletwa aliwapa wasichana yale makopo ya Stella na kuilaza chupa ya konyagi mezani, ikawa kama unywaji ndio umeanza. Baada ya kuwa nimewatambulisha wote na kufahamiana Sonno alinikonyeza na kutoka hapo tulipokaa, kitambo name niliwaaga hawa wasichana na kuwaambia kuwa naenda maliwatoni na hapo nilimfuata Sonno aliyekuwa ametoka nje ya jingo na kuegamia gari pale maegesho.
“Vipi?” Niliuliza punde nilipofika tu.
“Huyo mtu wako nimemkuta na amenieleza kila kitu ila nimemuachia uhai sijui nimefanya makosa.” Aliongea Sonno.
“Hapana.” Hebu nipe maelezo kwa kifupi.” Nilisema.
“nilipofika nilifanya kama nahitaji chumba hivyo nililipa na akaenda kunionyesha chumba, kulikuwa na watu wanazagaasehemu hizo. Baada ya kuonyeshwa chumba niliingia kuoga na nilipomaliza kuoga alikuwa amebaki peke yake hapo nilimuita kama vile ni shida ya dharura. Alikuja chumbani na alipoingia tu nikafunga mlango na kutoa bastola”
“Hapo nilimshinikiza kujibu maswali yangu huku nikimtishia kuwa akileta ubishi amekwisha na kwa mkwala niliachia risasi moja kwenye sakafu kuonyesha kuwa sitanii kwa kuwa bastola yangu ina kiwambo sauti haikusikika. Alibabaika na kuanza kutetemeka huku akisema. “Usiniue nitajibu.”
“Chumba namba ishirini na saba kinamilikiwa na nan?.” Nilimuhoji.
“Alikuwepo jamaa mmoja hivi ambaye katoka jioni.” Alijibu.
“Ni akina nani waliingia humo zaidi ya huyo jamaa? Alisita kidogo lakini aliponiangalia usoni akaendelea.
“walikuja watu wawili wakanipa pesa alafu wakaenda kukagua humo ndani, tulikuwa nao hawakuchukua kitu chochote.” Aliongea huyo muhudumu kwa uoga.
“Nimekuuliza ni wakina nani? Na je ndio utaratibu wenu kuruhusu wateja kukaguliwa?” niliuliza huku nikisogeza bastola sikioni kwake.
“Namfahamu mmoja tu, anaitwa Patrick Mwisongo anakaa Kigoto kwenye jumba lililo kando ya ziwa.” Alisema
“Hebu nieleze vizuri kabla sijachukia na kusambaza kichwa chako kwa risasi.” Nilizidi kumchimba mkwala.
“Ukivuka pale mwaloni soko la samaki unaendelea mbele baada ya kuacha nyumba za kawaida utakuta jumba la kifahari lenye ua wa michongoma ndio jumba la kwanza la kifahari na liko mbali nyumba nyingine upande wa kushoto kama unatokea mwaloni.” Baada ya hapo nilimwambia atulie asimwambie mtu yeyote juu ya jambo hilo alafu nikampatia sh. Elfu ishirini na kuagana naye bila tatizo. Alimalia kueleza Sonno.
 
TWENDE KAZI


7
Nilipoingia ukumbi wa disk nilitafuta sehemu nzuri ya kukaa, viti vingi vilikuwa wazi watu walikuwa ukumbini wakicheza mziki. Nikakaa kwenye kona moja itakayo niwezesha kuona karibu sehemu nzima ya ikumbi wa disko, niliwasha sigara na kuanza kuvuta wakati naangalia watu wakicheza na baada ya muda akapita muhudumu ambaye nilimuita na kumuagiza aniletee chupa ndogo ya pombe aina ya Long John. Aliniletea nikaendelea kunywa huku nikiwaza na kuwazua, nilikuwa nimekaa karibu saa moja na kitu hivi walipoingia wasichana wawili warembo sana na wamevaa mavazi nadhifu. Walipoingia waliongoza moja kwa moja na kuja kukaa kwenye meza iliyokuwa karibu yangu, muda mfupi baadae muhudumu aliwaletea bia za kopo aina ya Stella, nilishangaa kidogo kuona wasichana wawili tu aniletewa katoni nzima kwa mpigo. Walianza kunywa huku wakiongea taratibu na kitambo kidogo walikuwa wameisha kunywa nusu ya katoni na hapo sauti zao zilianza kupanda kiasi cha kuwasikia maongezi yao. Baada ya muda mfupi kidogo waliniomba niwaangalizie bia zao wakacheze disko, kwa kuwa waliona mimi ndio nilikuwa meza ya jirani yao.
Ulikuwa ni muziki wa rhumba uliopigwa na Oliver Ngoma ndio ulikuwa unapigwa nao waliucheza vizuri sana na kwa maringo hasa punde uliunganisha muziki uitwao Azaraki nao wa Oliver. Vimwana waliendelea kucheza name niliwaangalia kwa chati, baada ya kwisha mziki wa Azaraki walirudi kukaa sehemu yao. Walipo rudi sehemu yao walinishukuru huku wakinikaribisha nijiunge nao nami nilishukuru na kuendelea kukaa nilipokuwa wao waliendelea na maongezi yao huku wakizitimba bia.
Ghafla mawazo yalirudi kwa Sonno na Kikakika, nikajihisi vibaya kwa kutokuwa nao wakati huo, nilipoangalia saa yangu ilikuwa ni saa mbili na dakika ishirini na tano na Sonno alikuwa bado hajarudi. Nilitupa macho kwa wale wasichana nikaona mmoja wao akiangalia saa yake alafu nikamsikia akimaka, “Unajua huyu Patrick mshenzi sana”alimueleza mwenzie. Roho ikanishituka kusikia jina, nikatega masikio kunasa sauti zao zaidi.
“Hata mimi huwa namchukia, sijui kwa nini Moddy anamuona wa maana kiasi cha kuniacha nikastare peke yangu na yeye kuongozana naye. Mwenzie alichangia katika maongezi ya rafiki yake.
“Basi mimi ndio usiseme maana namchukia ile mbaya, sasa fikiria kitendo cha kuja kumchuka Zuberi kwangu mchana wakati akisubiri mlo ni uungwana huo”. Aliongea Yule msichana wa kwanza.
“Mimi nashangaa sana kuhusu huyu Patrick, toka wiki hii ianze amekuwa akimfuatafuata sana Moddy, mara ampigie simu aende kwake, wakati mwingine amuijie na gari. Kwa mfano usiku wa jana kampigia simu jioni akaenda na hakurudi mpaka saa tisa usiku ndio anarudi. Nilipomuuliza akanambia alikuwa kwenye mambo ya biashara” aliongea Yule mwingine.
“Kama ni hivyo inashangaza kwani hata mimi Zuberi aliniaga kuwa anakwenda kwa Patrick na sikumuona tena mpaka asubuhi ya leo, tena anakuja ananiambia hata kuwa na nafasi ya kunutoa out leo kwa sababu ana masula nyeti na Patrick.
Nafikiri ndugu msomaji hata kama ni wewe ungekuwa muhusika wa hili suala langu la wizi na kusikia maongezi haya yanayoendelea baina ya hawa mabinti ungegundua kitu kama wewe sio mpungufu wa akili. Nilianza kufikiri haraka nini nifanye ili hawa wasichana wanieleze anakokaa huyo Patrick bila wao kuwa na mashaka na mimi. Hapo likaja wazo kuwa nimsuburi kwanza Sonno maana ilikuwa mapema mno kuchukua muelekeo mwingine, hivyo nilikaa nikiwachunga kwa macho ili wasije wakaondoka bila kufahamu.
Disko lilikuwa linaendelea na watu walizidi kumiminika katika ukumbi huu wa Magnum, ghafla wale wasichana walikuja kwenye meza yangu na vikopo vine vya Stella walivyokuwa wamebakiza na kuviweka mezani huku wakiniomba niwaangalizie wakati wao wakicheza mziki. Walifanya hivyo kutokana na ongezeko la watu, walijua sio rahisi kuziacha mezani kwao na mimi nimudu kuziangalia kwa mbali.
Walicheza kama miziki mitatu hivi alafu wakaja wameshikana mikono mpaka kwenye meza yangu, hawakurudi kwenye meza yao kwani walivuta viti na kukaa huku wakinisogezea kopo moja la Stella na kuniambia ninywe. Ilionekana wazi kuwa pombe zilishawapanda kichwani, niliwashukuru kasha nikawambia kuwa huwa situmii kwani nimezoea pombe kali, walisikitika kwa kukataa kinywaji chao alafu wakaanza mazungumzo yao. Niliwasikiliza huku nikijifanya sina habari nao huku nikiyakata makali polepole, walikuwa wakiongea maongezi ya kawaida tu na tulidumu katika hali hiyo kama dakika tano hivi ndipo nilipowachokoza kwa maneno.
“Akina dada naona tumekaa meza moja lakini hatufahamiani.” Nilitoa kauli ambayo ilikatisha maongezi yao na kuniangalia alafu mmoja wao akasema;
“Unajua kaka tuliona kana kwamba hupendi bugudha ndio maana tukaendelea na maongezi yetu.” Aliongea mmoja wao.
“Sawa dada nafikiri hiyo ilikuwa tafsiri ya kihisia tu” nilisema na kuendelea “sijui wewe unaitwa nani?”
“Naitwa Mtuli.” Alijibu na kunyamaza.
“Na wewe dada unitwa nani?” Nilimuuliza mwingine.
“ Mie naitwa Monica” alijibu.
“Nyie ni wanyeji hapa? Niliuliza.
“Ndio” walijibu kwa pamoja alafu Monica akaunganisha swali, kwani wewe ni mgeni?
“Ndio” nilijibu kwa kudanganya.
“Unatokea wapi?” aliuliza Mtuli.
“Mbeya” niliendelea kudanganya
“Karibu sana Mwanza” alisema Mtuli.
“Nimeishakaribia ila nitashukuru sana nikipata wenyeji kama ninyi” nilijibu na kutupa kijembe.
Sikujibiwa ila niliunganishiwa swali kutoka kwa Monika.
“Unaitwa nani?”
“Naitwa Lyampili Mabagala” nilijibu.
“Hapa Mwanza umekuja kutembea tu au kibiashara” nilitupiwa swali linguine.
“Nimepita tu naenda Ukerewe kumuona mdogo wangu ambaye anafanya kazi huko.”
“Kumbe unaenda Ukerewe, basi mimi ndio kwetu.” Alisema Mtuli.
“Kwenu ni sehemu gani pale ukerewe?” nilimuuliza.
“Wewe unafahamu sehemu gani huko Ukerewe?” Niliulizwa badala ya kujibiwa.
“Nafahamu Muriti, Nansio na Murutunguru.” Nilijibu.
Ahaa!! Hizo sehemu zote umewahi kufika na ukapakariri vizuri?” MTuli aliendelea kunimiminia maswali.
“Sio sana ila nazifahamu.” Nilijibu kwa mkato.
“Basi mie kwetu ni pale Muriti madukani.” Alisemsa na kuendelea. “Baba yangu ni maarufu kidogo pale Muriti kama ulikaa kidogo huenda ikawa ulimufahamu.
“Anaitwa nani?” nilimuuliza.
“Anaitwa Kazobha ndie mwenye bucha la kuchinja nguruwe pale.” Alijibu.
Kwa hakika nilikuwa namfahamu kwani kule Muriti kuna ndugu zangu hata baba yake alikuwa ananifahamu ila huyu binti sikumfahamu kabisa hata yeye hakuonyesha dalili za kunifahamu. Hapo nikavunga. “Huyo mzee niliwahi kumsikia wakati nilipotembelea pale.
Mara Sonno akaingia na kuangaza kwani alikuwa hajaniona, nikampungia mkono naye akaniona na kunihuata. Alifika na kuvuta kiti kimoja kilichosalia ili kuhitimisha mzunguko wa viti vine. Tulijuliana hali kasha akawasalimia waschana wale alionikuta nao;
“Habari zenu akina dada?” alisalimu.
“Nzuri tu, sijui wewe.” Waliongea kwa pamoja.
“ Mie poa kabisa.” Alijibu Sonno.
“Karibu.” Alisema Mtuli huku akumsogezea kopo la Stella.
Sonno alichukua na kukipachua tayari kwa kunywa, alikunywa kama funda tatu hivi na kurudisha kopo kwenye meza huku akiangaza macho ukumbini, alafu akamuita muhudumu na kumuajizia kopo sita za Stella na chupa moja ya Konyagi. Vinywaji vilipoletwa aliwapa wasichana yale makopo ya Stella na kuilaza chupa ya konyagi mezani, ikawa kama unywaji ndio umeanza. Baada ya kuwa nimewatambulisha wote na kufahamiana Sonno alinikonyeza na kutoka hapo tulipokaa, kitambo name niliwaaga hawa wasichana na kuwaambia kuwa naenda maliwatoni na hapo nilimfuata Sonno aliyekuwa ametoka nje ya jingo na kuegamia gari pale maegesho.
“Vipi?” Niliuliza punde nilipofika tu.
“Huyo mtu wako nimemkuta na amenieleza kila kitu ila nimemuachia uhai sijui nimefanya makosa.” Aliongea Sonno.
“Hapana.” Hebu nipe maelezo kwa kifupi.” Nilisema.
“nilipofika nilifanya kama nahitaji chumba hivyo nililipa na akaenda kunionyesha chumba, kulikuwa na watu wanazagaasehemu hizo. Baada ya kuonyeshwa chumba niliingia kuoga na nilipomaliza kuoga alikuwa amebaki peke yake hapo nilimuita kama vile ni shida ya dharura. Alikuja chumbani na alipoingia tu nikafunga mlango na kutoa bastola”
“Hapo nilimshinikiza kujibu maswali yangu huku nikimtishia kuwa akileta ubishi amekwisha na kwa mkwala niliachia risasi moja kwenye sakafu kuonyesha kuwa sitanii kwa kuwa bastola yangu ina kiwambo sauti haikusikika. Alibabaika na kuanza kutetemeka huku akisema. “Usiniue nitajibu.”
“Chumba namba ishirini na saba kinamilikiwa na nan?.” Nilimuhoji.
“Alikuwepo jamaa mmoja hivi ambaye katoka jioni.” Alijibu.
“Ni akina nani waliingia humo zaidi ya huyo jamaa? Alisita kidogo lakini aliponiangalia usoni akaendelea.
“walikuja watu wawili wakanipa pesa alafu wakaenda kukagua humo ndani, tulikuwa nao hawakuchukua kitu chochote.” Aliongea huyo muhudumu kwa uoga.
“Nimekuuliza ni wakina nani? Na je ndio utaratibu wenu kuruhusu wateja kukaguliwa?” niliuliza huku nikisogeza bastola sikioni kwake.
“Namfahamu mmoja tu, anaitwa Patrick Mwisongo anakaa Kigoto kwenye jumba lililo kando ya ziwa.” Alisema
“Hebu nieleze vizuri kabla sijachukia na kusambaza kichwa chako kwa risasi.” Nilizidi kumchimba mkwala.
“Ukivuka pale mwaloni soko la samaki unaendelea mbele baada ya kuacha nyumba za kawaida utakuta jumba la kifahari lenye ua wa michongoma ndio jumba la kwanza la kifahari na liko mbali nyumba nyingine upande wa kushoto kama unatokea mwaloni.” Baada ya hapo nilimwambia atulie asimwambie mtu yeyote juu ya jambo hilo alafu nikampatia sh. Elfu ishirini na kuagana naye bila tatizo. Alimalia kueleza Sonno.
Nzuri Sana mkuu
 
Back
Top Bottom