Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,985
- 10,840
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 18
“Hapana kosa lo lote kuifanya kazi yako vizuri. Sidhani kama kuna mtu atakayekufukuza hapa na pia sioni sababu kwa nini ufanye kazi kama mnyama!” Mkongwe alimwambia Kijakazi.
“Siku zote nimekuwa hivi! Sasa hata sihisi kama ninafanya kazi kwa sababu nimelemaa kufanya kazi namna hii. “Kijakazi alijibu.
Siku nyingi Mkongwe alifanya kazi pamoja na Kijakazi na hakuacha kusema naye ili afanye kazi kibinaadamu, lakini jawabu lilikuwa lile lile, “Mimi nimeanzia hapa nitamalizikia hapa.”
Mwisho Mkongwe alichoka na alibaki kumtazama tu.
Msimu wa karafuu ulipofika, Fuad aliajiri vibarua wengi shambani kwake kuja kumchumia. Jamaa zake pia walikuja kutoka mjini kwa ajili ya kazi za kuweka hesabu. Kambi za wachumaji karafuu zilipigwa na wafanya kazi wote wa kawaida wa Fuad waliachishwa zile kazi zao ili wajiunge katika kuchuma karafuu. Fuad alishughulika sana kwani hizo ndizo siku za kuchuma pesa. Katika siku hizo alikuwa mkali kupita siku zote na yule aliyezidharau hata chembe mbili tu za karafuu alishika adabu yakc kwa matusi ya Fuad.
Usiku mmoja Kijakazi na Mkongwe walikuwa wamekaa juu ya jamvi wameelekezana nyuso zao na kati yao ipo chungu ya karafuu mbichi wanazichambua.
Mkongwe hakuvunjika moyo katika kufanya kazi. Mara alianza kumpamba kwa maneno.
“Hivyo Bi Kijakazi utaendelea kufanya kazi namna hii mpaka lini?” Mkongwe aliuliza.
Kijakazi alishtuka kwani hakupata kuitwa bibi hata siku moja maishani mwake. Bibi aliyemjua yeye duniani ni Bibi Maimuna tu ambaye alifariki zamani.
“Umesemaje vile? Umeniita Bibi? Tafadhali usiniite hivyo; mimi na Kijakazi tu.”
“Mimi nimekwita bibi kwa ajili ya kukuheshtmu, kwa ajili ya umri wako, nakuona sawa sawa na mama yangu aliyenizaa. Nakuuliza tena kama hukusikia Bi Kijakazi, utafanya kazi namna hii mpaka lini?” Mkongwe aliuliza.
“Mpaka mwisho wa maisha yangu yote.”
Mara Mkongwe alianza kumweleza kwa urefu na kumwambia “Sikiliza Bi Kijakazi, na lazima ufanye kazi kidesturi, ufanye kazi huku ukijifikiria kama wewe ni binaadamu. Ukiendelea kufanya kazi namna hiyo utatuharibia sisi sote kwani mara kwa mara humsikia Bwana Fuad akisema “Unamwona Kijakazi namna anavyofanya kazi?” Kwa sababu yako wewe ndiyo ikawa Fuad anatutaabisha sisi sote hapa. Wewe ndiwe umekuwa mfano katika kila kazi na katika kustahamili mateso. Mimi sitakubali kutumwa kama wewe!”
Kijakazi alistushwa na maneno hayo na aliyasikia kama sauti zilizokuwa zikisema naye akiwa katika ndoto kwani hapana hata siku moja aliyopata kuambiwa yeye mwenyewe na Fuad kuwa anafanya kazi vizuri. Sifa zote alizopewa Kijakazi alipewa wakati hayupo kwani akiwa uso kwa uso na Fuad, yalikuwa ni yale yale tu ya Fuad kuukunja uso wake na kumtolea maneno ya usafihi na matusi kama alivyofanya marehemu Bwana Malik.
“Ah! Kweli Bwana Fuad anasema hivyo?” Kijakazi aliuliza kwa sauti ya furaba kubwa.
“Bi Kijakazi mimi sipendi kukutukana lakini sina budi kukwambia uache upumbavu wako! Sisi ni lazima tupumzike kwani ni binaadamn sawa sawa na Fuad! Huoni kuwa huyo Bwana Fuad wako ni mtu asiye na fadhila na mwizi wa nguvu za watu?” Mkongwe alisema huku akiwa amekasirlka sana.
Maneno yote aliyoyasema Mkongwe yalipita kwenye masikio ya Kijakazi kama upepo. Fikra yake yote ilikuwa katika kuwaza kwamba ijapokuwa siyo mbele yake yeye mwenyewe, baada ya muda mrefu, tena mrefu sana, Fuad amemtaja kuwa anamfurahisha kwa kazi yake nzuri.
Kijakazi alijiuliza mwenyewe kwa nini hakusifiwa na Fuad mbele ya uso vvake? Kwa nini hata siku moja hakuambiwa neno zuri kutoka kinywani mwa Fuad?
“Hapana kosa lo lote kuifanya kazi yako vizuri. Sidhani kama kuna mtu atakayekufukuza hapa na pia sioni sababu kwa nini ufanye kazi kama mnyama!” Mkongwe alimwambia Kijakazi.
“Siku zote nimekuwa hivi! Sasa hata sihisi kama ninafanya kazi kwa sababu nimelemaa kufanya kazi namna hii. “Kijakazi alijibu.
Siku nyingi Mkongwe alifanya kazi pamoja na Kijakazi na hakuacha kusema naye ili afanye kazi kibinaadamu, lakini jawabu lilikuwa lile lile, “Mimi nimeanzia hapa nitamalizikia hapa.”
Mwisho Mkongwe alichoka na alibaki kumtazama tu.
Msimu wa karafuu ulipofika, Fuad aliajiri vibarua wengi shambani kwake kuja kumchumia. Jamaa zake pia walikuja kutoka mjini kwa ajili ya kazi za kuweka hesabu. Kambi za wachumaji karafuu zilipigwa na wafanya kazi wote wa kawaida wa Fuad waliachishwa zile kazi zao ili wajiunge katika kuchuma karafuu. Fuad alishughulika sana kwani hizo ndizo siku za kuchuma pesa. Katika siku hizo alikuwa mkali kupita siku zote na yule aliyezidharau hata chembe mbili tu za karafuu alishika adabu yakc kwa matusi ya Fuad.
Usiku mmoja Kijakazi na Mkongwe walikuwa wamekaa juu ya jamvi wameelekezana nyuso zao na kati yao ipo chungu ya karafuu mbichi wanazichambua.
Mkongwe hakuvunjika moyo katika kufanya kazi. Mara alianza kumpamba kwa maneno.
“Hivyo Bi Kijakazi utaendelea kufanya kazi namna hii mpaka lini?” Mkongwe aliuliza.
Kijakazi alishtuka kwani hakupata kuitwa bibi hata siku moja maishani mwake. Bibi aliyemjua yeye duniani ni Bibi Maimuna tu ambaye alifariki zamani.
“Umesemaje vile? Umeniita Bibi? Tafadhali usiniite hivyo; mimi na Kijakazi tu.”
“Mimi nimekwita bibi kwa ajili ya kukuheshtmu, kwa ajili ya umri wako, nakuona sawa sawa na mama yangu aliyenizaa. Nakuuliza tena kama hukusikia Bi Kijakazi, utafanya kazi namna hii mpaka lini?” Mkongwe aliuliza.
“Mpaka mwisho wa maisha yangu yote.”
Mara Mkongwe alianza kumweleza kwa urefu na kumwambia “Sikiliza Bi Kijakazi, na lazima ufanye kazi kidesturi, ufanye kazi huku ukijifikiria kama wewe ni binaadamu. Ukiendelea kufanya kazi namna hiyo utatuharibia sisi sote kwani mara kwa mara humsikia Bwana Fuad akisema “Unamwona Kijakazi namna anavyofanya kazi?” Kwa sababu yako wewe ndiyo ikawa Fuad anatutaabisha sisi sote hapa. Wewe ndiwe umekuwa mfano katika kila kazi na katika kustahamili mateso. Mimi sitakubali kutumwa kama wewe!”
Kijakazi alistushwa na maneno hayo na aliyasikia kama sauti zilizokuwa zikisema naye akiwa katika ndoto kwani hapana hata siku moja aliyopata kuambiwa yeye mwenyewe na Fuad kuwa anafanya kazi vizuri. Sifa zote alizopewa Kijakazi alipewa wakati hayupo kwani akiwa uso kwa uso na Fuad, yalikuwa ni yale yale tu ya Fuad kuukunja uso wake na kumtolea maneno ya usafihi na matusi kama alivyofanya marehemu Bwana Malik.
“Ah! Kweli Bwana Fuad anasema hivyo?” Kijakazi aliuliza kwa sauti ya furaba kubwa.
“Bi Kijakazi mimi sipendi kukutukana lakini sina budi kukwambia uache upumbavu wako! Sisi ni lazima tupumzike kwani ni binaadamn sawa sawa na Fuad! Huoni kuwa huyo Bwana Fuad wako ni mtu asiye na fadhila na mwizi wa nguvu za watu?” Mkongwe alisema huku akiwa amekasirlka sana.
Maneno yote aliyoyasema Mkongwe yalipita kwenye masikio ya Kijakazi kama upepo. Fikra yake yote ilikuwa katika kuwaza kwamba ijapokuwa siyo mbele yake yeye mwenyewe, baada ya muda mrefu, tena mrefu sana, Fuad amemtaja kuwa anamfurahisha kwa kazi yake nzuri.
Kijakazi alijiuliza mwenyewe kwa nini hakusifiwa na Fuad mbele ya uso vvake? Kwa nini hata siku moja hakuambiwa neno zuri kutoka kinywani mwa Fuad?